Suala la kuwa na imani tofauti linapotatiza taasisi ya ndoa

iNATEGEMEANA jinsi ulivyo-deep kwenye dini yako. kama wewe ni muumini wa kweli basi inawezekana DINI ikawa kikwazo kikubwa katika si ndoa ila kuanzisha mahusiano na mtu yeyote. Wapo watu huanza kwa kuuliza wewe dini gani na akipata uhakika si mlengwa wake basi hata ufanye nini humpati ng'oo.

Wabaguzi tu hao. Hata kwenye group discussion ya kusoma wanabagua. Nikiwa sekondari kulikuwa na chama moja lilikuwa limejitenga kabisa, ati wasichanganyike na 'mataifa', sa bahati yao mbaya katika kundi hilo nondo zilikuwa hazipandi, wote waliishia na division za kuning'inia karibu na zero.
 
Hivi hiyo hadithi umetunaga ama ni habari ambayo ipo kwenye kitabu cha dini ?.na kama ndiyo ni kitabu gani?.nina maana ni cha dini gani kinakataza kuoana dini tofauti?.
 
mi sikubaliani na wewe hata kidogo,hizo ni hadithi tu za kufikirika,mi baba yangu ni muislam na mama yangu ni mkristo na ni mdini kweli kweli na wapo kwenye ndoa yao zaidi ya miaka 40....kwa ushahidi huu wa wazazi wangu unafikiri mi ntakuunga mkono?

kuwa dini moja ni bora kuliko dini tofauti
 
Kama kweli unamuamini Mungu,na Mungu wako ndio kama Mungu wa ELIYA anayejibu kwa moto basi atakusaidia hata kupata mwenzi sahihi awe wa dini yako au asiye wa dini yako.Maandiko yanasema kuwa WANADAMU hutizama sura lakini YEYE MUNGU hutizama moyo wa mwanadamu na kuvichunguza viuno.Tatizo kwenye hizi dini tumekuwa Wkristo/waislamu wa KICHINA yani hatuelewi nini tunaamini na kwa nini tunaamini.Tunaendeshwa kwa hofu na kufuata mkumbo.
 
Kama kweli unamuamini Mungu,na Mungu wako ndio kama Mungu wa ELIYA anayejibu kwa moto basi atakusaidia hata kupata mwenzi sahihi awe wa dini yako au asiye wa dini yako.Maandiko yanasema kuwa WANADAMU hutizama sura lakini YEYE MUNGU hutizama moyo wa mwanadamu na kuvichunguza viuno.Tatizo kwenye hizi dini tumekuwa Wkristo/waislamu wa KICHINA yani hatuelewi nini tunaamini na kwa nini tunaamini.Tunaendeshwa kwa hofu na kufuata mkumbo.
Oww Gosh blame the chinese funny huh?.... but I liked what u have said up there absolutely right...

Back to topic our religion made it easy for us women... Muzlim woman can't marry non-Muzlim guy... we dont have many options..do we now? However many ppl have religions but they either do not follow what their religion ask them or they do not understand it and dont even bother to learn...

One of the things I have been looking in a man, was that he fears God... not just a Muzlim man.
 
No Name nimeipenda signature yako!

Swali ni moja kwa mtoa hoja Wakristo tunaamini katika kuwahubiria wengine habari za upendo wa Masihi na wokuvu wake! naamini kupitia kwangu nimemleta mwenzi wangu kwa Bwana Yesu! Nitarudi na data za kusupport hili.
 
Biblia inatufundisha kuwa Mke anaweza kutakaswa ndani ya Mume hali kadhalika mume ndani ya mke! Huyo asiyeamini akisha kuamini anakuwa kafunguliwa vifungo na nira za mwovu zinakuwa zimevunjwa!

Labda ikiwa hapa tunalenga ndoa kati waaminio na wasioamini!
 
Pdidy alichosema ni kweli hasa. Mlokole hawezi kumwoa mwislamu! nk. Ndoa ni ushirika. Mnakua mwili mmoja...Maana yake mnafanana kila kitu, kuanzia mnavyoabudu nk. Kuweni makini jamani kwani wasichana wapo wengi saaana. Kama ni mkristo utapata kanisani nk. Huo ndio ukweli hasa.

Mungu akubariki Pd.
 
Pdidy alichosema ni kweli hasa. Mlokole hawezi kumwoa mwislamu! nk. Ndoa ni ushirika. Mnakua mwili mmoja...Maana yake mnafanana kila kitu, kuanzia mnavyoabudu nk. Kuweni makini jamani kwani wasichana wapo wengi saaana. Kama ni mkristo utapata kanisani nk. Huo ndio ukweli hasa.

Mungu akubariki Pd.

I beg to differ Red Pepper; hapa unahubiri dhambi ya ubaguzi: You can't choose to fall in LOVe! Mimi wangu sikumpata kwenye nyumba yoyote ya ibada! Tukakubaliana na pamoja na yote tukaamua kuwa nyumba yetu ijengwe tukiwa na imani moja tu UKRISTO; Niki kuambia hivi leo yeye ndiye mwalimu wangu kwenye suala la imani utashangaa! Lakini ndio ukweli na namshukuru Mungu kwa hilo! Shukrani na sifa zimwendee yeye! Huwezi jua WAKRISTO wa kanisani kwangu wangenifikisha wapi ukichukulia tulianza kumegana tangu tuko Sunday school!

Lets be realistic!
 
Pdidy alichosema ni kweli hasa. Mlokole hawezi kumwoa mwislamu! nk. Ndoa ni ushirika. Mnakua mwili mmoja...Maana yake mnafanana kila kitu, kuanzia mnavyoabudu nk. Kuweni makini jamani kwani wasichana wapo wengi saaana. Kama ni mkristo utapata kanisani nk. Huo ndio ukweli hasa.

Mungu akubariki Pd.

N huko Kanisani wakina dada ambao hawajaolewa ni wengi kuliko wakina kaka wasiooa.wanaambiwa hakuna kuolewa na mtu asiye wa kanisani(kumbuka hata makanisa imani zimetofautiana) hivyo waendelee kuvumilia na kumuomba Mungu.Na kama tujuavyo Mungu hana formula moja ya kujibu.What if ukappewa mtu wa imani tofauti na una Mungu halafu ukakataa?
 
Swala la dini ni muhimu ila kukubaliana ni muhimu zaidi.Mfano kwa msichana wa kikatoliki kuolewa na dini nyingine yoyote ni lazima apate kibali toka kwa askofu wake na mumewe lazima akubali watoto wote wawe wakatoliki.Hiyo kidogo ni shida hivyo ni vizuri sana wapenzi kuliangalia hili swala kwa umakini.Kwa wanaume si ngumu sana sababu mara nyingi msichana ndiye hufuata dini ya mwanaume.
 
mi sikubaliani na wewe hata kidogo,hizo ni hadithi tu za kufikirika,mi baba yangu ni muislam na mama yangu ni mkristo na ni mdini kweli kweli na wapo kwenye ndoa yao zaidi ya miaka 40....kwa ushahidi huu wa wazazi wangu unafikiri mi ntakuunga mkono?

na wewe we ni dini gani? na kwa nini usiwe na dini zote mbili? au ni mkristo nusu na mwislamu nusu? au wewe na wenzio (watoto) MMEGAWANYIKA? wengine mna majina ya Kikristo na wengine kiislam?
 
na wewe we ni dini gani? na kwa nini usiwe na dini zote mbili? au ni mkristo nusu na mwislamu nusu? au wewe na wenzio (watoto) MMEGAWANYIKA? wengine mna majina ya Kikristo na wengine kiislam?

Unajua hapa mnachokigombania ni njia yakumfikia Mungu!

DINI ni Njia tu! hivyo sio lazima wote tupite iliyo moja tu!

Unaweza kabisa kuwa dini au dhehebu fulanai wakati wa uchanga wako na si lazima uwe dini au thehebu hilo wakati ukifa! Mbona hatujiulizi babu zetu wa kwanza walikuwa dini gani? Isifike mahala hiki ndio kiwe kigezo cha utu wetu!

Nasema huu ni ubaguzi!
 
No Name nimeipenda signature yako!

Swali ni moja kwa mtoa hoja Wakristo tunaamini katika kuwahubiria wengine habari za upendo wa Masihi na wokuvu wake! naamini kupitia kwangu nimemleta mwenzi wangu kwa Bwana Yesu! Nitarudi na data za kusupport hili.
Ni kweli usemayo Masikini_Jeuri but ikumbukwe pia kwako wewe inawezekana ikawa rahisi kumleta mwenzi wako kwa Yesu kwa vile ni mwanamke (yaani mkeo) so kitaratibu ni rahisi kwa mwanamke kuibadili dini yake na kukufuata wewe. lakini hali inawezakuwa tofauti iwapo mwanamke mwenye dini kama yako akiolewa na mwanaume mwenye dini kama ya / aliyokuwa nayo mkeo kwani hata yeye huyo mwanaume anaamini katika dini yake kuwa akifanikiwa kumwokoa mkewe atapata baraka. So kwa kuwa mke anatakiwa kumtii mumewe ni wazi atakwenda kwa mumewe na atashindwa kumleta mumewe kwa Yesu kirahisi.

So I still believe kuwa dini ndani ya ndoa ni moja wapo ya vitu vya kuzingatia kama unajiamini ni mfuasi mzuri wa dini yako na uangalie na uwezo wako wa kumbadilisha mtu mwingine na kumkaribisha katika dini yako
 
So I still believe kuwa dini ndani ya ndoa ni moja wapo ya vitu vya kuzingatia kama unajiamini ni mfuasi mzuri wa dini yako na uangalie na uwezo wako wa kumbadilisha mtu mwingine na kumkaribisha katika dini yako

Naam; ila palipo na upendo na nia thabiti kati yenu wachia mbali u-extremism; mnaweza kupata njia
 
hivi kweli wapenzi ambao dini tofauti wanaweza kuoana kwasababu mimi nilikua na rafiki wa kike baadaye tuliachana kwa kisingizio cha dini. nawasilisha maada
 
Inawezekana/haiwezekani...ni vyema ukampenda wa dini yako ili kuepusha usumbufu,kamwe usikubali hisia zako zichukuliwe na wa dini tofauti.Kumbuka ndoa ni jambo la kifamilia na mara nyingi ndoa hufungwa kidini,sasa kama dini tofauti ni nani yuko tayari kufuata dini ya mwenzie?Kitendo cha kubadili dini sio kitu rahisi,huleta mgogoro wa kudumu dhidi ya familia/ndugu.Angalao madhehebu kubadili ni rahisi.Jitahidi kutafuta wa dini yako,huyo aliyekuacha sababu ya dini yuko sahihi sababu hamna fiucha kati yenu zaidi ya kuchezeana tu..
 
No comment maana mada imenigusa mpaka rohoni...coz am deeply in love with a christian catholic man...
 
Back
Top Bottom