Suala la kuwa na imani tofauti linapotatiza taasisi ya ndoa

Hili jambo linawezekana, kukiwa na kitu kuchukuliana, kuheshimu imani ya mwenzio, dini moja bila mapenzi ni ptuuuuuuuuuuuuu
 
muslim-family-at-eid.jpg


Kujadili dini ni mojawapo ya mijadala inayokwepwa na baadhi ya wanajamii ili kuepusha shari na kudumisha amani. Lakini linapokuja swala mahusiano hususan pale watu wawili wenye imani tofauti za kidini wanapotaka kuoana, unaweza kuzuka mjadala mzito miongoni mwa ndugu na jamaa wa wapenzi hao na wakati mwingine hata marafiki hutokea kupinga muunganiko huo.

Ninao mfano unaonihusu. Mdogo wangu anayenifuatia kuzaliwa alipata mchumba (mume) mwenye imani tofauti na imani yetu, jambo hilo lilizusha mtafaruku katika familia yetu kila mmoja akisema lake. Ilitokea tu mimi na baadhi ya ndugu zangu akiwemo baba tuliafiki ule muunganiko wao na ndoa ikafungwa na sasa ndoa yao ni imara na imetimiza miaka tisa mwaka huu wakiwa na watoto watatu.

Ukweli ni kwamba jambo hili limekuwa likileta mtafaruku katika baadhi ya familia na wakati mwingine familia hujikuta ikisambaratika hasa pale ambapo familia moja inashindwa kukubali utashi wa mtoto wao kuolewa au kuoa mtu mwenye imani tofauti na mara nyingi hii hutokea katika familia zenye msimamo mkali wa kidini. Kama inavyofahamika mapenzi ni kitu cha ajabu sana. Pale ambapo penzi linapochipua hufunika imani zetu kiasi cha kujikuta wakati mwingine tunazisaliti imani hizo ambazo hata hivyo baadhi yetu hazikuwa utashi wetu bali tu tumejikuta tukiwa humo kwa sababu ni imani ambazo tumezaliwa na kukuta wazazi wetu wakiwa ni wafuasi wa imani hizo.

family-praying.jpg


Huu ni mtihani mgumu sana kwetu na mara nyingi waathirika wa mtihani huu wengi wao ni wanawake na watoto ukilinganisha na wanaume. Wakati mwingine huwa najiuliza inakuwaje mtu anampata mpenzi anayempeda sana na mwenye sifa azitakazo lakini anashindwa kufunga naye ndoa kwa sababu ya kuwa na imani tofauti? Lakini pia wapo ambao wanalazimika kufunga ndoa na wapenzi wao sio kwa sababu wamependana, bali ni kwa sababu tu imani zao zinafanana…………!

Kuna wanawake wengi sana wa kiasi cha kutosha wanalazimika kuishi katika ndoa ngumu kwa sababu ya imani zao, kilichowavuta kuingia katika muunganiko huo ni imani zao lakini sio upendo. Lazima tukubali kwamba mapenzi ni kitu kingine na imani ni kitu kingine. Kuingia katika ndoa kwa kigezo cha imani kunakuwa na changamoto zake ambazo mara nyingi hazina matokeao mazuri.

Naamini hata humu JF wapo ambao wamewahi kukabiliana na mtihani huu au wako katika hati hati ya kukabiliana na mtihani huu. Hebu tupeane uzoefu juu ya jambo hili linalowatatiza wengi.

Swali: Iwapo wewe ni single, Je uko tayari kufunga ndoa na mtu mwenye imani tofauti na imani yako? Je umejiandaaje kukabiliana na changamoto za wazazi, ndugu, marafiki na jamii kwa ujumla watakapopinga muunganiko wenu ?

Nisingependa mjadala huu uwe ni wa kidini.

Nadhani mmenielewa.........


Zamani zile watu walikuwa wanaowana kwa kufuata kabila. Bahati nzuri hilo limefifia hasa sehemu za mjini. Tumekuwa Watanzania zaidi kuliko watu wa makabila fulani. Limebaki suala la dini. Nalo litachukua njia ile ile ya ukabila. Ni suala la muda tu. Ndiyo hizo ndoa za bomani. Wanakubaliana kila mtu abaki na dini yake au mmoja abadili dini yake kumfuata mwenzie (nani abadili ni mjadala mpana kabisa).

Kijana mmoja aliwekewa zengwe la dini akasema abadili kumfuata mke. Wakasema mbona kabila tofauti akasema kama nitabadili dini siwezi kushindwa kubadili kabila - nalo nabadili ! Akapata mke. Determination!
 
Mkuu baba yako angekua mdini angeoa Mkristo? Au una maanisha ni mshika dini? Maneno mengine angalia mkuu ukikosea kidogo tu unaleta tafsiri nyingine.

Tatizo hamsomi maandiko, Quran iko very clear kwamba unaweza kuolewa nakuoa watu wa vitabu yaani Wayahudi na Wakiristo, kwa sababu ni believers kinachokatazwa ni kuoa au kuolewa na mpagani, yaani mtu asiye amini uwepo wa Mungu. Soma Quran 2:221 na Quran 5.5.
 
mi sikubaliani na wewe hata kidogo,hizo ni hadithi tu za kufikirika,mi baba yangu ni muislam na mama yangu ni mkristo na ni mdini kweli kweli na wapo kwenye ndoa yao zaidi ya miaka 40....kwa ushahidi huu wa wazazi wangu unafikiri mi ntakuunga mkono?
Wote ni makafiri, hakuna mwenye dini hapo. Ndoa ilifungwa msikitini au kanisani? Najua haikufungwa popote pengine ni ya kiserikali. Wanapohitaji msaada au ushauri wa kiroho wanaenda wapi?
 
Mkuu hapa hakunaga shida hata chembe...haya madhehebu ni ndg kabisa haya.
Sometimes kuna shida..labda kama wote wazazi ni watu wa dini rasharasha. Lakini ukikuta mlutheri kweli kweli itakuwa ugomvi maana hatataka watoto wake wakabusu sanamu. Na mkatoliki atalazimisha mwanae akabusu masanamu.
 
Dada yetu mkubwa alipata mchumba mwislamu wakiwa chuoni. Walipendana sana na jamaa alikuwa anakuja nyumbani na alijua msimamo wa dini ulivyo. Walifunga ndoa ya bomani baada ya mjadala mrefu sana.

Kusema ukweli shemeji alimpenda sana mkewe na pesa ilikubali. Waliweza kununua nyumba Nairobi wakawa wanazipangisha kwa Kshs lakini kila mara shemeji alimuomba dada abadili dini waozwe ki-Islam, dada alipataa.

Kumbe shemeji alipata mchepuko mkristo pia. Alimuahidi, kama atakubali kubadilisha dini amuoe atamjengea nyumba. Bi dada alikubali, nyumba ili jengwa na ndoa ya ubani ilifugwa.

Baada ya kuoa ndiyo shemeji anamwambia dada kuwa ameoa. Dada alisema uke wenza hauwezi. Wote wawili walilia sana ma ilibidi waachane. Dada aligaiwa nyumba moja ya Nairobi. Kila mtu aka endelea na maisha.
 
Hili swala katika dini ya uislamu limeruhusiwa mwanamume kuoa mwanamke wa dini ya kikristo au ya kiyahudi na hali yuopo na dini yake, na imekatazwa kwa mwanamke kuolewa na dini hizo amma akiwa hana dini muislamu haruhusiwi kumuoa
 
Swala Dini kwenye ndoa ni suala muhimu sana, katokana mambo yafuatayo

1. Kuwalea watoto katika mstari na kuwahimiza kumpenda Mungu.

Watoto wanaplekwa Msikini wana ambiwa "Mkristo ni kafili," na wengine wanaplekwa kanisani wana ambiwa "Yesu ni njia ya kweli na uzima" Wote wakirudi nyumbani ,Wana wauliza wazazi wao upi ni ukweli? kulingana na mafundisho kila mtu aliyoyapata.Wazazi wanabaki kuangliana . Hii inaleta picha mbaya kwa watoto.
2.Kuepuka migogoro ya ndoa hasa pale Mzee yupo kwenye Mfungo wa Ramadhani na mama yupo kwenye Mambo ya Kiinjili (kanisani)
3.Mafundisho ya Dini ni tofauti kila fundisho la dini moja,linakashifu dini nyingine.

Mfano. Waislam wanasema Wakristo ni makafili, na mafundisho ya kiislamu yanasema Muhislamu safi hawezi kushare vitu na Kafili hasa .Tendo la ndoa na some times Chakula.NB. Baadhi ya mafundisho ya Dini fulani yanakataza kula baadhi ya vyakula e.g kitimoto.
Na Baadhi ya Dini inasemekana kwamba Wanafuga Majini, Ibada za kikristo zinafukuza Majini.
kwa Mtaji huo nyumba Haiwezi kusettle.

Muhimu: Watu watakaa kwenye ndoa wakiwa na dini tofauti if and only if.Watahamua wote kuweka Dini zao pembeni na kuamua kujiunga na Dini nyingine ya Upagani(fiftyfifty uisilamu na aukristo) lakini huwezi ukuwa Mkristo Deep au Muhislamu Deep, ukiishi kwenye ndoa kama hiyo.

Kwa hiyo natoa ushauri, ndoa iwe za watu wenye imani moja!! unless kila mtu aache misingi ya Dini yake. waamue kuwa Wapagani.

Regards,

jangakuu
Uko sahihi kabisa!

Lzm tuwe kitu kimoja,mnasali pamoja km familia na mambo mengine!
 
Mtimti, ebu chunguza vizuri maisha ya wazazi wako, itakuwa lazima kuna mmoja si muumini wa kweli yaani hayuko serious sana na dini, kama mmojawapo anazingatia imani yake.

Lakini kama wote ni waumini watiifu ki kweli kweli kwa dini zao, shida ipo sana tu!

Kutojali kwa mmojawapo wa wazazi wako ndo kumesaidia katika hilo!

Umeongea pointi nzuri sana sana.
 
Mie mrutery, mchumba RC, yeye tunapendana sana, ila wakati huo hataki kwenda kinyume na matakwa ya wazazi wake. tumejaliwa mtoto, ila ndoa imekwama kwa sababu ya msimamo huo wa matakwa ya wazazi. najua nawa confuse kwa kusema tunapendana ila dini zinatutenganisha, kuna mengine ya ndani yanayoashiria hayo ila kwa kusimulia uta conclude kuwa hakuna upendo hapo!
Huyo ni mjinga anatafuta kisingizio,kwani kuna shida gani wote ni wa Yesu?
Hajaelewa bado imani ni nn!
 
Mie mrutery, mchumba RC, yeye tunapendana sana, ila wakati huo hataki kwenda kinyume na matakwa ya wazazi wake. tumejaliwa mtoto, ila ndoa imekwama kwa sababu ya msimamo huo wa matakwa ya wazazi. najua nawa confuse kwa kusema tunapendana ila dini zinatutenganisha, kuna mengine ya ndani yanayoashiria hayo ila kwa kusimulia uta conclude kuwa hakuna upendo hapo!
Hivi ni Dini ndizo zikakazowafanya muone Mbingu? Au ni Yesu ambaye wote wawili mnamtumikia na kumuabudu kuwa ni Mkombozi wa maisha yenu? Sijaelewa hapa.
 
mi sikubaliani na wewe hata kidogo,hizo ni hadithi tu za kufikirika,mi baba yangu ni muislam na mama yangu ni mkristo na ni mdini kweli kweli na wapo kwenye ndoa yao zaidi ya miaka 40....kwa ushahidi huu wa wazazi wangu unafikiri mi ntakuunga mkono?
Uko sahihi kabisa. Imani gani inayozungumziwa? Kama imani ya dini basi ukiona kuna mgawanyiko, elewa uelewa ni mdogo kwa mmoja wao. Kama uelewa ni mkubwa, Dini haitakiwi kuwa jambo la kumhusu mwingine tofauti na wewe.

Tunaona sasa hivi Pakistan wanaharibu serikali eti kwa sababu ya dini, Rubbish. Kuna wachungaji hapa TZ wanaharibu ndoa za watu kwa sababu ya dini, Rubbish. Familia haiendi mbinguni, ni wewe, wewe peke yako. Usimsumbue mwenzako.
 
mi sikubaliani na wewe hata kidogo,hizo ni hadithi tu za kufikirika,mi baba yangu ni muislam na mama yangu ni mkristo na ni mdini kweli kweli na wapo kwenye ndoa yao zaidi ya miaka 40....kwa ushahidi huu wa wazazi wangu unafikiri mi ntakuunga mkono?
very true, i have the same experience, so mm sioni shida watu wakipendana, dini si kigezo cha kuachana km wawili wanapendana.
 
very true, i have the same experience, so mm sioni shida watu wakipendana, dini si kigezo cha kuachana km wawili wanapendana.

muslim-family-at-eid.jpg


Kujadili dini ni mojawapo ya mijadala inayokwepwa na baadhi ya wanajamii ili kuepusha shari na kudumisha amani. Lakini linapokuja swala mahusiano hususan pale watu wawili wenye imani tofauti za kidini wanapotaka kuoana, unaweza kuzuka mjadala mzito miongoni mwa ndugu na jamaa wa wapenzi hao na wakati mwingine hata marafiki hutokea kupinga muunganiko huo.

Ninao mfano unaonihusu. Mdogo wangu anayenifuatia kuzaliwa alipata mchumba (mume) mwenye imani tofauti na imani yetu, jambo hilo lilizusha mtafaruku katika familia yetu kila mmoja akisema lake. Ilitokea tu mimi na baadhi ya ndugu zangu akiwemo baba tuliafiki ule muunganiko wao na ndoa ikafungwa na sasa ndoa yao ni imara na imetimiza miaka tisa mwaka huu wakiwa na watoto watatu.

Ukweli ni kwamba jambo hili limekuwa likileta mtafaruku katika baadhi ya familia na wakati mwingine familia hujikuta ikisambaratika hasa pale ambapo familia moja inashindwa kukubali utashi wa mtoto wao kuolewa au kuoa mtu mwenye imani tofauti na mara nyingi hii hutokea katika familia zenye msimamo mkali wa kidini. Kama inavyofahamika mapenzi ni kitu cha ajabu sana. Pale ambapo penzi linapochipua hufunika imani zetu kiasi cha kujikuta wakati mwingine tunazisaliti imani hizo ambazo hata hivyo baadhi yetu hazikuwa utashi wetu bali tu tumejikuta tukiwa humo kwa sababu ni imani ambazo tumezaliwa na kukuta wazazi wetu wakiwa ni wafuasi wa imani hizo.

family-praying.jpg


Huu ni mtihani mgumu sana kwetu na mara nyingi waathirika wa mtihani huu wengi wao ni wanawake na watoto ukilinganisha na wanaume. Wakati mwingine huwa najiuliza inakuwaje mtu anampata mpenzi anayempeda sana na mwenye sifa azitakazo lakini anashindwa kufunga naye ndoa kwa sababu ya kuwa na imani tofauti? Lakini pia wapo ambao wanalazimika kufunga ndoa na wapenzi wao sio kwa sababu wamependana, bali ni kwa sababu tu imani zao zinafanana…………!

Kuna wanawake wengi sana wa kiasi cha kutosha wanalazimika kuishi katika ndoa ngumu kwa sababu ya imani zao, kilichowavuta kuingia katika muunganiko huo ni imani zao lakini sio upendo. Lazima tukubali kwamba mapenzi ni kitu kingine na imani ni kitu kingine. Kuingia katika ndoa kwa kigezo cha imani kunakuwa na changamoto zake ambazo mara nyingi hazina matokeao mazuri.

Naamini hata humu JF wapo ambao wamewahi kukabiliana na mtihani huu au wako katika hati hati ya kukabiliana na mtihani huu. Hebu tupeane uzoefu juu ya jambo hili linalowatatiza wengi.

Swali: Iwapo wewe ni single, Je uko tayari kufunga ndoa na mtu mwenye imani tofauti na imani yako? Je umejiandaaje kukabiliana na changamoto za wazazi, ndugu, marafiki na jamii kwa ujumla watakapopinga muunganiko wenu ?

Nisingependa mjadala huu uwe ni wa kidini.

Nadhani mmenielewa.........
dini or dhehebusi sababu ya kufunja mapanzi ya dhati, ni jins ya kufanya chaguo lako sahihi tuu vile unataka . kama mtu aona ana msimamo mkal na dini or dhehebu lake, fanya kumtafuta yule unaedhani atafata ule upande ulioko wewe, so in the future wasije kutulilia hapa JF -MMU, au siyo jaman.
 
Back
Top Bottom