Suala la ajira ni tatizo kubwa sana

mwankuga

JF-Expert Member
Aug 30, 2010
334
120
Kuna tatizo kubwa sana la ajira katika nchi yetu.Vijana wengi wapo mitaani huku serikali ikiwa haina nia ya dhati ya kutatua tatizo hilo.Zaidi suala la ajira limekuwa kama jambo la kupatia kura wakati wa uchaguzi.Mfano katika uchaguzi wa mwaka 2005,CCM na mgombea wao waliahidi kuwa watawapatia ajira milioni 1 ndani ya miaka 5.Leo hii pasipo ushahidi wa kutosha kuwa eti lengo limevuka.

Sina uhakika sana na sina data za kutosha,inasemekana sekta ya umma ina uwezo wa kuajiri watu 40000,wakati katika soko la ajira kuna watu wasio na ajira zaidi ya 600000.
Tuna ongea sana,lakini tufike hatua tusimame tudai haki zetu hata kama watu watasema kuna suala la kujiajiri.Kazi ya serikali ni kuweka mazingira mazuri ya kuwaajiri na kujiajiri kwa watanzania.

Hebu wadau jitokezeni tujadili suala hili kwa uwazi zaidi na kama mtu una data za uhakika mwaaga hapa,halafu tuweke mikakati ya kukabiliana na suala hili.Ukimya wetu unaonyesha kana kwamba hili si tatizo kubwa sana.
 
ajira imekuwa ni tatizo kubwa hapa nchini na hizo ajira za kikwete ni uzushi mtupu sana sana watakuambia wameongeza ajira kwenye sekta isiyo rasmi
 
Back
Top Bottom