Stock taking....

Jan 27, 2012
80
70
Naomba tu kujua , baada ya hii ajali ya ATCL Kigoma, je Shirika hili jadidi, lina ndege yoyote /ngapi sasa zina zo operate?

N.B: Scenario 1: Ndege zero ( Hakuna ndege) : Ratio ya zero income to idadi ya wafanyakazi na operating expenses

Scenario 2: Labda ndege moja- Vs operating expenses... na vyeo vilivyopo.
 
Hawana ndege iliyobaki inaruka, hata hivo mimi nimefurahi kuona hiyo ndege imeharibika bila kuleta madhara maana kuna siku niliipanda kutokea Dar kwenda Kigoma via Tabora.Tulivofika uwanjani muda wa kuondoka ukafika lakini hakuna hata update ya kinachoendelea tulikaa kama masaa mawili ndo tukaambiwa ipo tayari twende kuboard. Ndani ya ndege tukaambiwa eti ilikua maintenance,sitanii chezea vitu vingine lkn sio kukaa angani kwa muda wa masaa matatu na kitu ambacho huna uhakika nacho ni hatari sana bora imekufa tujue hakuna ndege ya kwenda Kigoma kuliko kurisk maisha yetu na mafisadi ambao wanajali matumbo yao tu
 
Shirika limeshafulia rasmi halina kitu tena.

Bora sasa wauze assets wawaachishe kazi wafanyakazi wawalipe mafao.

I am sure hata ma Pilot wao watakuwa ni kiwango cha chini, maana kama Pilot mzuri kwa nini asiende Precision au kwengingineko abakie hapo anaendesha ndege kutoka Dar kwenda Kigoma sijui.

Wanaopanda ATC nao wana moyo
 
Halafu nimecheka leo maana katika gazeti la Mwananchi wamezungumzia pia juu ya hii 'ishu a.k.a Inshu' katika Maoni na Uchambuzi na pia katika makala.
Ila kilichonichekesha zaidi ni kumkwoti Kaimu Mkurugenzi , someone Chizi akisema kuwa shirika hilo linatarajia kupata mshirika wa kibiashara atakayekuwa akitoa huduma katika mikoa ya Kigoma na Mwanza.
Kiukweli, tunachekesha kwa mengi, as a country!
ATCL haifufuliki!
 
Back
Top Bottom