Stephen Hawking on Religion: Science will Win!!!

Science inaishinda religion katika kufanya uchunguzi, religion haina uchunguzi na in fact ukifanya uchunguzi katika conventional religion utaambiwa unafanya blasphemy. Religion, for the most part represent a closed conservative system with some fantastic and dogmatic ideas that are suppose to be taken by fiat.No proofs, no skepticism and no room for questioning authority.

Dini haitaki maswali, lakini inajidai kuwa na majibu karibu yote.

Science on the other hand, encourages the pursuit of knowledge, skepticim, questioning of authority.

Sayansi siyo tu inakubali maswali, inasisitiza uchunguzi na kuuliza maswali na ina maarifa ya kukubali kwamba haina majibu yote.

Labda kwa tafsiri hii ya "science vs Religion" inaweza kutoa upotofu wa moja kwa moja na kuifanya Sayansi ionekane ni zaidi ya Dini.

There is this quote from Albert Einstein ( a scientist):


"After religious teachers accomplish the refining process indicated, they will surely recognize with joy that true religion has been ennobled and made more profound by scientific knowledge."

Kwa tafsiri ninayoipata ni kuwa sayansi ni aina nyingine moja wapo ya dini kwani kiini na chimbuko la dini ni imani katika jambo fulani (hapa tukizungumzia uwepo au kutokuwepo kwa mambo fulani fulani ambayo wengine wanayaamni na wengine hawayaamini). Sayansi nayo kwa staili yake ya weza kuwa ndio dini ya kweli kwa wale wanaoiamini/wafuasi wake.

Sayansi kwa mapana yake ni ina jaribu kuwafanya waamini wa dini fulani waweze kufikiri zaidi katika mambo yanayowazunguka kwa kutumia utashi na pia uchnguzi wa kina, Sio kwamba dini haina uchunguzi wa kama ambavyo sayansi inafanya.

Ukichukua tafsiri ya dini kama "religion" na sio "religions" unaweza kuzuia upeo wa hoja. Kwani kwa mfani ndani ya dini ya Kikristu (Christianity), unaweza kuona wapo wafuasi wa dini wa milengo miwili (conservatives & liberal/traditionalists and progressives ). Kuna wale wanaoamini kuwa maneno katika Biblia ni vile yalivyo tokea mwanzo wa kund ikwa kwake, sasa na hata milele hayawezi kubadilika na kwamba Biblia haina makosa kwa kuwa imeandikwa kwa nguvu za Mungu.

Lakini kwa upande mwingine, wapo wale ambao wana amini uwepo wa Mungu na neno lake kwa kuchochewa pia na utafiti na uchunguzi wa kisayansi na ndio hao wanaoleta mapinduzi katika dini kwa kuamini kuwa hata maandiko ya Mungu walihusisha binadamu ambao kimsingi yangeweza kuwa na upotofu kulingana na mwandishi na mazingira ya wakati (historia, jiografia, sayansi) na kadhalika.

Kwa suala la uchunguzi pia, ukichukulia dini kwa mapana yake, unaweza kuona pia kuwa chimbuko la sayansi ni dini ambapo sayansi inaweza kutofautisha yale ambayo yanawezekana na yasiyowezekana kwa hitimisho la kidunia zaidi kwa kusema yapo nje ya uwezo wa mwanadamu (beyond/human being or universe) kwa mfano kuweza kuumba mtu na kumfanya aishi.

Lakini kwa upande mwingine, aina hiyo hiyo kushindwa kwa uchunguzi/ utafiti wa kujua ukweli katika dini kama ilivyo kwenye sayansi kunaweza kupelekea ya hitimisho kwa wafuasi wake hususan kwa yale wasiyoweza kwa kwa akili zao wenyewe na kusema hayo ni ya "Mungu".

Wanasayansi wanashindwa kusema/kutaja "very specific" ni nani anaweza kufanya yale yasiyowezekana na binadamu wa kawaida ili hali wafuasi wa dini wao wanaona kuwa hayo wasiyoyaweza yapo hivyo kutokana na kuwa kwenye mamlaka ya mtu mwingine mwenye uwezo zaidi yao na ambaye hawawezi kumuona kwa macho na akili zao (Mungu).
 
Umeuliza Science inaishinda dini nini, ukajibiwa kirefu, in a nutshell umeambiwa uchunguzi. Kama huna uchunguzi unafanya mambo kwa tradition tu institution yako inakufa.

Hapa ndipo Science inapoipida bao religion.

Uliza jingine.

Sasa mbona unarejea kwene square one? Nimeuliza hivi ni wapi imesemwa kuwa kazi ya dini ni kufanya uchunguzi..(Rejea majibu yako..sina muda wa kudurufu upuuzi.)

Nikaekwambia huezi ukasimamisha kulinganisha vitu viwili bila ya kuwa na scale moja, kwamba kama dini haina jukumu la uchunguzi kwanini uilinganishe na science, huu si ndio ukichaa?..Halafu unajibu tena kulekule kwenye square one.
 
Science inaishinda religion katika kufanya uchunguzi, religion haina uchunguzi na in fact ukifanya uchunguzi katika conventional religion utaambiwa unafanya blasphemy. Religion, for the most part represent a closed conservative system with some fantastic and dogmatic ideas that are suppose to be taken by fiat.No proofs, no skepticism and no room for questioning authority.

Dini haitaki maswali, lakini inajidai kuwa na majibu karibu yote.

Science on the other hand, encourages the pursuit of knowledge, skepticim, questioning of authority.

Sayansi siyo tu inakubali maswali, inasisitiza uchunguzi na kuuliza maswali na ina maarifa ya kukubali kwamba haina majibu yote.


Kiranga, you need to know that SCIENCE is also a religion based on visible and experimented proof AND RELIGION is based on believing with faith without experimenting anything.

If you do not believe in religion, your religion is Science. And if you dont believe in science your religion is RELIGION. period!!. You can develop many theories trying to run from the truth and pleasing yourself, but that is the truth and fact.
 
Labda kwa tafsiri hii ya "science vs Religion" inaweza kutoa upotofu wa moja kwa moja na kuifanya Sayansi ionekane ni zaidi ya Dini.

There is this quote from Albert Einstein ( a scientist):


"After religious teachers accomplish the refining process indicated, they will surely recognize with joy that true religion has been ennobled and made more profound by scientific knowledge."

Kwa tafsiri ninayoipata ni kuwa sayansi ni aina nyingine moja wapo ya dini kwani kiini na chimbuko la dini ni imani katika jambo fulani (hapa tukizungumzia uwepo au kutokuwepo kwa mambo fulani fulani ambayo wengine wanayaamni na wengine hawayaamini). Sayansi nayo kwa staili yake ya weza kuwa ndio dini ya kweli kwa wale wanaoiamini/wafuasi wake.

Sayansi kwa mapana yake ni ina jaribu kuwafanya waamini wa dini fulani waweze kufikiri zaidi katika mambo yanayowazunguka kwa kutumia utashi na pia uchnguzi wa kina, Sio kwamba dini haina uchunguzi wa kama ambavyo sayansi inafanya.

Ukichukua tafsiri ya dini kama "religion" na sio "religions" unaweza kuzuia upeo wa hoja. Kwani kwa mfani ndani ya dini ya Kikristu (Christianity), unaweza kuona wapo wafuasi wa dini wa milengo miwili (conservatives & liberal/traditionalists and progressives ). Kuna wale wanaoamini kuwa maneno katika Biblia ni vile yalivyo tokea mwanzo wa kund ikwa kwake, sasa na hata milele hayawezi kubadilika na kwamba Biblia haina makosa kwa kuwa imeandikwa kwa nguvu za Mungu.

Lakini kwa upande mwingine, wapo wale ambao wana amini uwepo wa Mungu na neno lake kwa kuchochewa pia na utafiti na uchunguzi wa kisayansi na ndio hao wanaoleta mapinduzi katika dini kwa kuamini kuwa hata maandiko ya Mungu walihusisha binadamu ambao kimsingi yangeweza kuwa na upotofu kulingana na mwandishi na mazingira ya wakati (historia, jiografia, sayansi) na kadhalika.

Kwa suala la uchunguzi pia, ukichukulia dini kwa mapana yake, unaweza kuona pia kuwa chimbuko la sayansi ni dini ambapo sayansi inaweza kutofautisha yale ambayo yanawezekana na yasiyowezekana kwa hitimisho la kidunia zaidi kwa kusema yapo nje ya uwezo wa mwanadamu (beyond/human being or universe) kwa mfano kuweza kuumba mtu na kumfanya aishi.

Lakini kwa upande mwingine, aina hiyo hiyo kushindwa kwa uchunguzi/ utafiti wa kujua ukweli katika dini kama ilivyo kwenye sayansi kunaweza kupelekea ya hitimisho kwa wafuasi wake hususan kwa yale wasiyoweza kwa kwa akili zao wenyewe na kusema hayo ni ya "Mungu".

Wanasayansi wanashindwa kusema/kutaja "very specific" ni nani anaweza kufanya yale yasiyowezekana na binadamu wa kawaida ili hali wafuasi wa dini wao wanaona kuwa hayo wasiyoyaweza yapo hivyo kutokana na kuwa kwenye mamlaka ya mtu mwingine mwenye uwezo zaidi yao na ambaye hawawezi kumuona kwa macho na akili zao (Mungu).

Tofauti ya sayansi na dini.

Dini inakwenda kwa imani, unaambiwa mungu ni muumba wa yote na aliumba mbingu na nchi, kwa misingi ya kidini unatakiwa kuamini tu, ukianza kuuliza mungu alitoka wapi unaonekana unafanya kufuru na St. Augustine anasema kabla ya kuumba mbingu na nchi mungu alikuwa anaumba moto kwa ajili ya kuwaweka watu wote watakaouliza alikuwa anafanya nini kabla ya kuumba mbingu na nchi. Dini haitaki uchunguzi.

Sayansi on the other end, haiendi bila uchunguzi.Ukisema kitu bila kukifanyia experiments, observation na ma peer review hufanyi sayansi.

Kwa hiyo kutaka kusema sayansi ni dini kwa maana ya kwamba inafuata imani tu, si kuitendea haki, hiyo itakuwa under the realm of pseudoscience. Sayansi halisi ni lazima iwe testable, ndiyo maana mpaka leo kuna wanasayansi kibao wanasema vitu vilivyo katika some of the most intriguing aspects of string theory si sayansi, ni pseudoscience, kwa sababu testability yake haiko katika our immediate future - some accounts has it that we need a particle accelerator the size of the Milky Way Galaxy to test-

Sayansi inaenda beyond imani, inaenda na uchunguzi na facts. Kui reduce sayansi iwe sawa na dini kwa msingi wa imani ni upotofu.
 
Kiranga, you need to know that SCIENCE is also a religion based on visible and experimented proof AND RELIGION is based on believing with faith without experimenting anything.

If you do not believe in religion, your religion is Science. And if you dont believe in science your religion is RELIGION. period!!. You can develop many theories trying to run from the truth and pleasing yourself, but that is the truth and fact.

Kwangu mimi swala hili ni rahisi, na sayansi si religion.

Ukishaanza kuongelea "experimented proofs" unaondoka katika uwanja wa dini tayari.Yesu alivyokuwa anawahubiria watu alikuwa anawambia "Amin, amin nawaambia......." hakuwa anawaambia "experiment and test this...." In fact alikuwa ana discourage kutokuwa na imani, dini zote worth their name zinakwenda na imani, si kwa experimentation (The Buddha deviated a little bit from this but some can debate if Buddhism is even a religion, in any case modern day Buddhism is largely traditionalism)

Religion inaendana na faith, belief, kuamini vitu bila ku verify.

Science inaendana na knowledge, experiments, observation, kutoamini kitu bila ku verify.

Utasemaje science ni religion ?
 
Sasa mbona unarejea kwene square one? Nimeuliza hivi ni wapi imesemwa kuwa kazi ya dini ni kufanya uchunguzi..(Rejea majibu yako..sina muda wa kudurufu upuuzi.)

Nikaekwambia huezi ukasimamisha kulinganisha vitu viwili bila ya kuwa na scale moja, kwamba kama dini haina jukumu la uchunguzi kwanini uilinganishe na science, huu si ndio ukichaa?..Halafu unajibu tena kulekule kwenye square one.

Nimekueleza kwamba, scale yangu ya ukweli, kujua kipi kinafaa na kipi haifai, ni uchunguzi.

Institution yenye utamaduni wa uchunguzi naiona inafaa zaidi ukiilinganisha na institution isiyo na utamaduni wa uchunguzi. Kama unabishia hili niambie.

Sasa basi, swali lako lilikuwa sayansi inaishinda dini katika nini? Nikakwambia katika uchunguzi.

Na kwa sababu sayansi inaishinda dini katika uchunguzi, sayansi kwangu mimi ni bora kuliko dini.

Naweza kulinganisha mtiririko huu na huu hapa chini.

Abdulhalim: : Hivi Sayansi inaizidi nini dini?

Kiranga: Dhahabu, Sayansi ina tani mia na dini ina tani mbili za dhahabu

Abdulhalim: : Kwani wapi wamesema kazi ya dini ni kukusanya dhahabu?

Kiranga: Sijasema kwamba kuna sehemu yoyote wamesema kazi ya dini ni kukusanya dhahabu, najibu swali lako tu.

Abdulhalim: : Ili ujibu swali langu ni lazima uchague kitu ambacho dini na sayansi vinakutana. Lazima uwe na kipimo kimoja.

Kiranga: Kipimo changu ni dhahabu.Kwangu mimi ili uwe na maana inabidi uwe na dhahabu, kama huna dhahabu huna maana, hata kama umeamua kwa makusudi kuitokuwa na dhahabu, hii si excuse.
 
Tofauti ya sayansi na dini.

Dini inakwenda kwa imani, unaambiwa mungu ni muumba wa yote na aliumba mbingu na nchi, kwa misingi ya kidini unatakiwa kuamini tu, ukianza kuuliza mungu alitoka wapi unaonekana unafanya kufuru na St. Augustine anasema kabla ya kuumba mbingu na nchi mungu alikuwa anaumba moto kwa ajili ya kuwaweka watu wote watakaouliza alikuwa anafanya nini kabla ya kuumba mbingu na nchi. Dini haitaki uchunguzi ambapo unatoa matokeo kama ilivyo kwa sayansi
Sayansi on the other end, haiendi bila uchunguzi.Ukisema kitu bila kukifanyia experiments, observation na ma peer review hufanyi sayansi.

Kwa hiyo kutaka kusema sayansi ni dini kwa maana ya kwamba inafuata imani tu, si kuitendea haki, hiyo itakuwa under the realm of pseudoscience. Sayansi halisi ni lazima iwe testable, ndiyo maana mpaka leo kuna wanasayansi kibao wanasema vitu vilivyo katika some of the most intriguing aspects of string theory si sayansi, ni pseudoscience, kwa sababu testability yake haiko katika our immediate future - some accounts has it that we need a particle accelerator the size of the Milky Way Galaxy to test-

Sayansi inaenda beyond imani, inaenda na uchunguzi na facts. Kui reduce sayansi iwe sawa na dini kwa msingi wa imani ni upotofu.

Kuitofautisha dini na sayansi kwa misingi ya "uchunguzi na matokeo ya uchunguzi wake" pengine nami naona ni kupotoka. Kwani hata katika dini pia kuna maeneo yanayohusu uchunguzi ( kwa mfano wali waliopata kufanya matendo ya miujiza kama kutembea juu ya maji, kufufu wafu nk). Ni aina ya sayansi ktk dini ambayo wengine hawawezi kuiamini pia!!.

Kumbuka kuwa hata kupitia sayansi hiyo hiyo, wafuasi wa sayansi wana amani kuwa kuna asili ya kila kitu ikiwemo dunia na vile vilivyomo na kupitia hiyo imani pia wanaweza kujenga misingi ya kutetea matokeo ya utafiti na uchunguzi wanaofanya. Hakuna mwanasayansi hata moja ambae anaweza kufanya utafiti pasipo kuwa na imani kuwa matokeo ya utafiti wake yatampeleka wapi na kama anataka kuthibitisha hilo kwa watu, ni lazima pia ajenge hoja za kuwafanya hao wanaomfuatilia wamwamini katika matokeo yake.

Kwa mfano, kupitia sayansi, mgunduzi wa kanuni au nadharia fulani ya kisayansi ni lazima ajenge hoja yake katika imani ya kuwezesha utafiti kufanyika ili kuthibitisha kile anachotaka kufanya. sayansi pia kama ilivyo kwenye dini inazingatia kanuni fulani ambayo inaweza kuwa ya kinadharia au vitendo. katika hilo ndio maana unaweza kuona kuna kutofautiana au kukubalina pia kwa nadharia na kanuni (theories & principles) katika kundi moja la wana sayansi na hapo unapata wa mlengo wa kulia na kushoto kama ilivyo dini.
Dini si lazima uamini uwep wa mungu, na ndio maana zipi pia dini za mashetani (labda haziamini kama mungu yupo). Sayansi inafikia wakati nayo inagengwa katika nadharia ambazo nyingine si rahisi kuthibitisha kwa macho ya mtu wa kawaida mapaka uwe na upeo tofauti kwa mfano kanuni ya akina kuelewa, kanuni za kupaa angani, kanuni za mvutano, kanuni za mrejesho nyuma nk.

Si rahisi kwa mtu wa kawaida ambae hajui somo la sayansi kuweza kuelezwa na kuelewa hata kama matokeo yake yanaonekana wazi pasipo kuwepo kwa imani ya kuyaona matokeo hayo kwa jicho jingine la zaidi ya binadamu wa kawaida. Kwa kushindwa kuweza kupatia ufumbuzi baadhi ya matatizo katika hii dunia, sayansi haiwezi kusimama sawa na dini.

Kigezo cha kutofautisha dini na sayansi kisiwe ni uwepo au uwepo wa Mungu tu, ni zaidi ya hapo. na kukosekana kwa tafsiri iliyokubalika ya "religion" miongoni mwa wanazuoni labda kunaweza kuifanya sayansi nayo kuwa ni aina fulani ya dini kwani waanzilishi wake upata wafuasi kama kanisa/misikiti ambapo mambo hayo yanayofanyika katika ulimwengu wa sayansi utegemea zaidi nguvu za asili zisizoonekana kwa macho ya kawaida (natural forces) ambazo hizo utumainiwa kuwa ndio nguvu za Mungu (awe anaishi au asiwe anaishi).

Nguvu za asili pia zinatambulika katika jamii ya wanasayansi ambapo kwao hutafakari na kuona "zipo kwa kuwa zipo tokea kuwepo kwa dunia (lakini hawawezi kueleza kwa uthibitisho kuwa dunia imekuwepo tokea lini na kwa nini imekuwepo kwa hali hii iliyopo!!)". Hiyo dhana ya ukomo wa upeo wa kufikiria na kuyaona yale yajayo iwe katika sayansi au kwa wafuasi wa dini zinazoamini uwepo wa Mungu ndio inayotthihirisha "uwepo wa ngumu nyingine tofauti ndani yetu ambayo wengine wanaiamni na kuita Mungu lakini hawaiamini hivyo kuona yote wanayofanya ni kwa uwezo na utashi wao binafsi" .
 
Kuitofautisha dini na sayansi kwa misingi ya "uchunguzi na matokeo ya uchunguzi wake" pengine nami naona ni kupotoka. Kwani hata katika dini pia kuna maeneo yanayohusu uchunguzi ( kwa mfano wali waliopata kufanya matendo ya miujiza kama kutembea juu ya maji, kufufu wafu nk). Ni aina ya sayansi ktk dini ambayo wengine hawawezi kuiamini pia!!.


Hujaeleza uchunguzi umefanyikaje kuhusu miujiza hii.Kwa kadiri ninavyofahamu misahafu inaeleza tu kwamba miujiza ilitokea, na wala misahafu haijaeleza Musa alivyopasua bahari alichunguza vipi, alitumia formula gani, na sisi tukitaka kurudia tutumie formula gani.Kitu pekee wanachokwambia ni kuamini katika mungu na kumfuatisha amri zake.Huu si uchunguzi.By uchunguzi namaanisha system inayo entertain questioning na kupata natural explanations of seemingly supernatural phenomena.Huwezi kuniambia miujiza ya katika misahafu ina constitute uchunguzi.If anything una prove point yangu kwamba dini na misahafu yake havina uchunguzi, vimejaa imani tu.

Kumbuka kuwa hata kupitia sayansi hiyo hiyo, wafuasi wa sayansi wana amani kuwa kuna asili ya kila kitu ikiwemo dunia na vile vilivyomo na kupitia hiyo imani pia wanaweza kujenga misingi ya kutetea matokeo ya utafiti na uchunguzi wanaofanya. Hakuna mwanasayansi hata moja ambae anaweza kufanya utafiti pasipo kuwa na imani kuwa matokeo ya utafiti wake yatampeleka wapi na kama anataka kuthibitisha hilo kwa watu, ni lazima pia ajenge hoja za kuwafanya hao wanaomfuatilia wamwamini katika matokeo yake.

Sayansi haiendi na imani, ukisema kitu chochote kinachohusu imani katika mkutano wa wanasayansi watu watakuona umepotea njia.Sayansi inaenda na vitu vinavyothibitishika na kupimika.Hebu tutajie imani moja ya kisayansi. Imani na sayansi havichangamani.Sayansi inaenda na ujuzi, na ukiwa na ujuzi, umepita imani.Imani ni kwa watu wasiojua vitu tu. Sayansi inaenda na facts, haiendi na imani. Newtons laws hazina imani, relativity equations hazina imani, thermodynamics laws hazina imani, hizi ni proven facts according to the rigors of all logical, reasonable and scientific standards.

Kwa mfano, kupitia sayansi, mgunduzi wa kanuni au nadharia fulani ya kisayansi ni lazima ajenge hoja yake katika imani ya kuwezesha utafiti kufanyika ili kuthibitisha kile anachotaka kufanya. sayansi pia kama ilivyo kwenye dini inazingatia kanuni fulani ambayo inaweza kuwa ya kinadharia au vitendo. katika hilo ndio maana unaweza kuona kuna kutofautiana au kukubalina pia kwa nadharia na kanuni (theories & principles) katika kundi moja la wana sayansi na hapo unapata wa mlengo wa kulia na kushoto kama ilivyo dini.
Dini si lazima uamini uwep wa mungu, na ndio maana zipi pia dini za mashetani (labda haziamini kama mungu yupo). Sayansi inafikia wakati nayo inagengwa katika nadharia ambazo nyingine si rahisi kuthibitisha kwa macho ya mtu wa kawaida mapaka uwe na upeo tofauti kwa mfano kanuni ya akina kuelewa, kanuni za kupaa angani, kanuni za mvutano, kanuni za mrejesho nyuma nk.

Mgunduzi anaweza kuanza kwa imani, akaweka hypothethis yake, akaweka equations zake, lakini sayansi itaikubali hii hypothethis kama hypothethis tu.Hapo ndipo wanasayansi wengine wataanza kuitest hypothethis/ theory.

Einstein alivyoleta nadharia yake ya relativity, watu waliikubali kwa sababu ili make sense, lakini ikawa bado haijawa established scientifically kwa sababu ilikuwa bado haijawa tested, haijaweza ku predict phenomena.

Sir Arthur Eddington aliongoza team iliyoitest nadharia ya relativity ya Einstein wakati jua lilipopatwa mwaka 1919.Mpaka mwaka 1919 general theory of relativity ili make sense lakini wanasayansi walikataa kuikubali moja kwa moja kwa sababu moja, ilikuwa bado haijaweza kuwa tested kwa kufanya accurate and measurable predictions. Kutokana na a higher precision katika theory ya relativity, iliweza ku predict sayari ya Mercury kuwa pembeni kidogo ya pale ilipotakiwa kuwa kwa mujibu wa Newtonian physics, na kweli jua lilipopatwa watu walipoangalia kwa umakini wakaona Einstein yuko right. Hii aspect ya uchunguzi na verification ndiyo ninayoisema kwamba haipo katika dini, kwa mfano ukianza kusema tuanze kuchunguza mungu alianza anzaje utaondoka katika uwanja wa dini na kuingia uwanja wa falsafa, kwa sababu dini haitaki uchunguzi, inataka mtu aamini tu bila kuuliza.Tofauti na sayansi.

Si rahisi kwa mtu wa kawaida ambae hajui somo la sayansi kuweza kuelezwa na kuelewa hata kama matokeo yake yanaonekana wazi pasipo kuwepo kwa imani ya kuyaona matokeo hayo kwa jicho jingine la zaidi ya binadamu wa kawaida. Kwa kushindwa kuweza kupatia ufumbuzi baadhi ya matatizo katika hii dunia, sayansi haiwezi kusimama sawa na dini.

Kama nilivyosema mwanzo, sayansi haiendi kwa imani, inaenda kwa knowledge.Imani na ujuzi havichanganyiki.Ukishakuwa na ujuzi umepita imani, huna imani.Nikiwa nakuja kwako kukutembelea, halafu sina uhakika kama upo nyumbani huko ninakokuja ama la, lakini nafikiri utakuwepo maana baada ya mida ya kazi huna tabia ya kutoka sana, nitasema naenda kumtembelea Ngoshwe, naamini yupo nyumbani.Kwa nini nasema naamini? Kwa sababu sina hakika, unaweza kuwepo nyumbani, ama unaweza kwa siku hii ukawa umebadilisha mipango yako ya kawaida, umeenda kuangalia mechi ya Kombe la Dunia. Lakini nikifika nyumbani, nikakuona, nikahakiki kwamba ni wewe, nikakuamkua, tukatafakari mambo, kamwe siwezi tena kusema "naamini Ngoshwe yupo nyumbani kwake" nitaonekana punguani, naamini nini wakati mtu yupo mbele ya macho yangu?.Hapo nitasema najua Ngoshwe yuko nyumbani kwake. Hii ndiyo tofauti ya kuamini na kujua. Kujua ni zaidi ya kuamini. Wanasayansi wanataka kujua, hawataki kuamini. Kuamini si sayansi, ni dini.Sayansi ni zaidi ya kuamini.

Sayansi haiwezi kusimama sawa na dini, sayansi imeipita dini katika ukweli, uchunguzi na uwazi.Mambo gani sayansi imeshindwa kuyapatia ufumbuzi ambayo dini imeyaweza? Sanasana mimi naona sayansi inavutia zaidi kwa sababu inaposhindwa inasema, na naiona dini inaleta uongo kwa sababu kila kitu tusichoweza kukieleza binadamu dini inataka kutupa jibu rahisi lisilothibitishika linalolalia kwenye nyanja za supernatural forces na mungu.

Kigezo cha kutofautisha dini na sayansi kisiwe ni uwepo au uwepo wa Mungu tu, ni zaidi ya hapo. na kukosekana kwa tafsiri iliyokubalika ya "religion" miongoni mwa wanazuoni labda kunaweza kuifanya sayansi nayo kuwa ni aina fulani ya dini kwani waanzilishi wake upata wafuasi kama kanisa/misikiti ambapo mambo hayo yanayofanyika katika ulimwengu wa sayansi utegemea zaidi nguvu za asili zisizoonekana kwa macho ya kawaida (natural forces) ambazo hizo utumainiwa kuwa ndio nguvu za Mungu (awe anaishi au asiwe anaishi).

Mungu ni mfano mmoja tu.Nimeongea pia kuhusu uchunguzi na dini isivyokumbatia uchunguzi.Nimeongea kuhusu dini kama Buddhism ambayo essentially haiamini katika mungu, lakini inafuata traditions fulani dogmatic na kuifanya i fall short of scientific beauty and rigors of verification. Kwa hiyo usitake kusema kwamba nimemtumia mungu kama litmus test, sijafanya hivyo.

Kwangu mimi ukiamini explanation zilizo supernatural kwa natural phenomena, tayari umeingia kwenye dini.Kwa hiyo anayeamini mungu, malaika, shetani, majini, mizimu ya mababu, roho etc wote hao ni waumini wa dini. Sayansi haifuatishi vyote hivi na inataka tutafute natural explanations za seemingly supernatural phenomena.Na kadiri miaka inavyozidi na sayansi kuongeza ujuzi wetu, tunazidi kuona kwamba mengi tuliyofikiri kuwa ni supernatural na kazi ya mungu yanaweza kuelezeka vizuri tu katika natural world. Zamani watu waliamini radi na kupatwa kwa jua ni mungu kakasirika anataka kuwajulisha binadamu.Leo tunajua radi inatokana na umeme kwenye mawingu na kupatwa kwa jua kunatokana na alignment ya jua mwezi na dunia.Kwa hiyo hata haya mengine ambayo leo hatujayajua na tunamsingizia mungu asiyekuwepo, siku moja tunaweza kugundua kumbe hata hayamhitaji mungu.

Nguvu za asili pia zinatambulika katika jamii ya wanasayansi ambapo kwao hutafakari na kuona "zipo kwa kuwa zipo tokea kuwepo kwa dunia (lakini hawawezi kueleza kwa uthibitisho kuwa dunia imekuwepo tokea lini na kwa nini imekuwepo kwa hali hii iliyopo!!)". Hiyo dhana ya ukomo wa upeo wa kufikiria na kuyaona yale yajayo iwe katika sayansi au kwa wafuasi wa dini zinazoamini uwepo wa Mungu ndio inayotthihirisha "uwepo wa ngumu nyingine tofauti ndani yetu ambayo wengine wanaiamni na kuita Mungu lakini hawaiamini hivyo kuona yote wanayofanya ni kwa uwezo na utashi wao binafsi" .

Nguvu za asili kama zipi?

Wanasayansi wanaweza kuthibitisha dunia imekuwapo tokea lini, na kwa nini imekuwepo kwa hali hii iliyopo, labda wewe hujafanya homework yako kutafuta haya mambo tu.

Kuwa na upeo wa kufikiri kwa mwanadamu - kama kweli kuna upeo- hakuthibitishi kuwapo kwa kitu kingine chochote ambacho hakithibitishiki.
 
Nimekueleza kwamba, scale yangu ya ukweli, kujua kipi kinafaa na kipi haifai, ni uchunguzi.

Institution yenye utamaduni wa uchunguzi naiona inafaa zaidi ukiilinganisha na institution isiyo na utamaduni wa uchunguzi. Kama unabishia hili niambie.

Sasa basi, swali lako lilikuwa sayansi inaishinda dini katika nini? Nikakwambia katika uchunguzi.

Na kwa sababu sayansi inaishinda dini katika uchunguzi, sayansi kwangu mimi ni bora kuliko dini.

Naweza kulinganisha mtiririko huu na huu hapa chini.

Abdulhalim: : Hivi Sayansi inaizidi nini dini?

Kiranga: Dhahabu, Sayansi ina tani mia na dini ina tani mbili za dhahabu

Abdulhalim: : Kwani wapi wamesema kazi ya dini ni kukusanya dhahabu?

Kiranga: Sijasema kwamba kuna sehemu yoyote wamesema kazi ya dini ni kukusanya dhahabu, najibu swali lako tu.

Abdulhalim: : Ili ujibu swali langu ni lazima uchague kitu ambacho dini na sayansi vinakutana. Lazima uwe na kipimo kimoja.

Kiranga: Kipimo changu ni dhahabu.Kwangu mimi ili uwe na maana inabidi uwe na dhahabu, kama huna dhahabu huna maana, hata kama umeamua kwa makusudi kuitokuwa na dhahabu, hii si excuse.

A failed argument.
 
Imeandikwa, wapumbavu husema hakuna Mungu...

Wajanja wamewaandikia wapumbavu kwamba "wapumbavu husema hakuna mungu" kwa kujua kwamba wapumbavu wanaogopa sana kujulikana kwamba wao ni wapumbavu, kwa hiyo katika jitihada za kuficha upumbavu wao bila kufikiri, wanakubali kuwepo kwa mungu bila uchunguzi, ili mradi wasionekane kwamba wao ni wapumbavu.

Wapumbavu wa kweli ni wale wanaomuamini mungu asiyekubali uchunguzi.

Na wale wasiomuamini mungu bila kuogopa kuitwa wapumbavu wanavaa a badge of honor.

Kitabu chenyewe kilichoandika wapumbavu husema hakuna mungu ndiyo hicho hicho kilichoandika jua linaizunguka dunia. That tells you so much about the credibility of that book.

Nani mpumbavu wa kweli hapo sasa?
 
A failed argument.

An even worse assertion is the one trying to brand another as a failed argument without explanation, it does not even try therefore it doesn't even have a chance of failing.

You are not even wrong, you are worse than wrong. At least with a wrong/ failed argument we can see where it went wrong/ failed.

You = nada !
 
Hii ni mada inayohitaji umakini sana kuijadili. Kwa kiasi fulani napenda ainisho lililotolewa na Einstein. Nionavyo sayansi, kama elimu kwa ujumla wake, ni NYENZO tu ya kutuwezesha kufahamu complexity (sijui neno zuri la kiswahili) ya mifumo ya vitu vilivyomo duniani na katika universe na sheria za asili zinazoviongoza. Sayansi hutumia tu sheria za asili katika kufafanua mifumo na jinsi za vitu vilivyopo. Haina uwezo wa kubadili sheria hizo au kuumba visivyokuweko (from nothing). Na complexity hiyo naiona si katika vitu tu bali hata katika tabia za viumbe ikiwa ni pamoJa na binadamu katika harakati za maisha (survival) hapa duniani na kwingineko.

Nikijumlisha vyote hivi ndipo Ukuu wa Mwenyenzi Mungu unapozidi kunidhihirikia. (Niseme kabisa mimi ni Mkristo na kwangu mimi kuwepo kwa Mwenyenzi Mungu na Kristo ni masuala yasiyo na mjadala). Kwangu mimi dini ni mfumo mzima wa uhai na nafsi ya binadamu ambao huwezi kuutenga na Muumba wake. Hivyo, kwangu mimi sayansi na elimu ni kama tochi tu ya kunionyesha maajabu ambayo Mwenyenzi Mungu katuwekea. Kila nikiwa ndani ya ndege huwa naendelea kustaajabu jinsi akili za viumbe wa Mwenyenzi Mungu walivyoweza kuchambua na kutumia vitu na sheria za asili kuunda chombo kizito kinachopaa angani (lakini wasivyoweza kubadili asili za madini yanayotumika kuunda ndege au sheria za anga).

Wakati mwingine nimekuwa napambana na wahubiri na wakristo wenzangu wanaojaribu kuonyesha kwamba elimu, maarifa na sayansi ni vitu vinanvyopingana na imani; wengine wanavihusisha na shetani! Nimekuwa nikiwaambia kuwa vyote hivyo vyatoka kwa Bwana na vimekuwepo kwa makusudi kabisa kutudhihirishia Ukuu wake. Nadhani wengine wanapambana na sayansi visivyo kwa ajili ya inferiority complex zao tu. Huku wengine sayansi inawatia kiburi kufikiri wamemaliza ilhali imetuwezesha kujua mengi kuhusu vitu vichache sana katika maajabu yasiyomithilika yaliyoumbwa na Mwenyenzi Mungu. Kwa kifupi, dini si sayansi na sayansi si dini. Sayansi ni nyenzo na dini ni msingi mzima wa uwepo wetu na vyote vinavyotuzunguka ambapo sayansi inatusaidia tu kuelewa na kutuongezea uwezo wa kuishi duniani katika muda mfupi tuliopewa.

Natumaini kuna hoja nimejenga hapo.
 
Niseme kabisa mimi ni Mkristo na kwangu mimi kuwepo kwa Mwenyenzi Mungu na Kristo ni masuala yasiyo na mjadala

Ahsante,

Hapo (maandishi niliyonukuu kutoka kwa drifter) ndipo utakapoona tofauti ya muumini wa dini na mfuasi wa sayansi.

Kwa muumini wa dini, kuna vitu havina mjadala. Kwa mfuasi wa sayansi, hakuna kitu kisichokuwa na mjadala.Kwa muumini wa dini, vile visivyothibitishwa au kuthibitishika (mungu, mbingu, moto, malaika etc) vinaaminika.Kwa mfuasi wa sayansi, hata vile vilivyokwisha thibitishika bado vinajaribiwa ili kuona kama bado vinaweza ku stand the test of rigorous and constant review, kuna watu mpaka leo wanataka ku disprove Einstein's theory of Relativity, hata baada tha Eddington kutoa an experimental verification.

Halafu kuna watu wanasema sayansi ni dini ?

Sijui unakusudia nani kwenye inferiority complex, lakini binafsi siwezi kupata inferiority complex kutokana na sayansi kwa sababu najua sayansi ukiifanyia kazi itakuzawadia ujuzi. Na kwa upande mwingine siwezi kutiwa kiburi na sayansi kwa sababu najua kwamba tunayojua ni kama tone dogo tu la maji wakati tusiyoyajua ni kama bahari nzima, kwa hiyo kiburi kitoke wapi wakati hatujaweza hata kui harness vilivyo nguvu ya jua, achilia mbali ile ya black hole lililopo katikati ya galaxy ya Milky Way ?

Swali,

Kwa nini unafikiri vitu vyenye complexity ni lazima viwe vimeumbwa na mungu ?
 
...hawa watu wa dini na scriptures zao ndo wameturudisha nyuma zaidi ya mika 1000,na si ndio hawa waliowafundisha watu wao Earth is the centre of the universe na galileo alipo wachallenge na kuwaambia dunia inazunguka jua wakataka kumuua na kumweka house arrest the rest of his life na kuharibu his scientific work ambazo zingeachwa may be life ingekuwa tofauti na sasa(who knows),wakipewa nafasi hawa wataturudisha dark ages,seriously hawa watu wanaojilipua kwa ahadi ya bikira saba na wale wanaokesha wakisubiri mwokozi na kuimba nyimbo za kulaani utajiri hata kama ni wa halali ni wa kuogopa sana.
 
By religion here they mean belief in GOD. Well...this is a very 'cut and deal' debate for me.

GOD first
Science second. End of story.
I have seen the hand of God in many incidences and things that science cannot prove.
SO I stick with my belief that GOD is supreme and infact GOD Himself created that science, HE knew the nature of man so He gave them science, Insisting on proving this and that.

To each their own opinion. Stephen Hawking is entitled to his.
 
...hawa watu wa dini na scriptures zao ndo wametudisha nyuma zaidi ya mika 1000,na si ndio hawa waliowafundisha watu wao Earth is the centre of the universe na galileo alipo wachallenge na kuwaambia dunia inazunguka jua wakataka kumuua na kumweka house arrest the rest of his life na kuharibu his scientific work ambazo zingeachwa may be life ingekuwa tofauti na sasa(who knows),wakipewa nafasi hawa wataturudisha dark ages,seriously hawa watu wanaojilipua kwa ahadi ya bikira saba na wale wanaokesha wakisubiri mwokozi na kuimba nyimbo za kulaani utajiri hata kama ni wa halali ni wa kuogopa sana.

Koba Koba Koba,

Inahitaji ujasiri kuacha tradition na kufuata ukweli.Dini haiwezi kutafuta ukweli, inaweza kufuata tradition tu, ndiyo maana hairuhusu maswali mengi yatakayoiumbua.

Hiyo story ya Galileo ni classic example ya jinsi gani conservatism na tradition zinaweza kuzuia maendeleo.

Kabla ya hapo Galileo alionyesha ni jinsi gani Aristotle aliupotosha ulimwengu kwa miaka karibu 2000 kwa kuhubiri na kuandika kwamba kila kitu kinaweza kupatiwa jibu kwa fikra na nadharia tu, Galileo, in the immortalized experiment of falling bodies rolling down slopes (in some places corrupted as balls dropping down the leaning tower of Pisa). Kwa hiyo kwangu Galileo ndiye father of modern experimental science.

Kwa hiyo nashukuru sana umeleta huo mfano wa Galileo. Galileo alionyesha umuhimu wa uchunguzi, kutokubali kitu kwa sababu tu kimekubalika kwa miaka mingi na kukifanyia experiment ili kupata personal verification.

You are right, wanaojilipua kwa bikira saba na wale wanaokesha kumsubiri mwokozi wote wako equally deluded, kwa sababu wanasubiri na kuota vitu visivyothibitishika.
 
By religion here they mean belief in GOD. Well...this is a very 'cut and deal' debate for me.

GOD first
Science second. End of story.
I have seen the hand of God in many incidences and things that science cannot prove.
SO I stick with my belief that GOD is supreme and infact GOD Himself created that science, HE knew the nature of man so He gave them science, Insisting on proving this and that.

To each their own opinion. Stephen Hawking is entitled to his.

What was the color of the hand of god? What approximate measurements was it? When did god create science? What nature of man did god know?

Opinions are like asses, everybody has one, facts on the other hand, are sacred.

And god is not a matter of fact, god is a matter of faith. Unprovable, unverifiable entity. Right up there with Father Christmas, Santa Claus, The Easter Bunny, Snow White and The Seven Dwarfs. Tinkerbell and all the fairies, The Loch Ness Monster, Popobawa, the genies, the angels, the devil and all the other fictional characters.
 
...at the end of the day people hear what they want to hear from who they want to hear it from whether it make sense or not.

My theory is, watu wanapenda kuji identify na kitu kilicho kikubwa kuliko wao, hivyo wanataka kuamini hata mambo yasiyopo ilimradi tu wayape maisha yao maana kwa mtizamo wao.

Na maisha bila mungu atakayejibu sala za wazembe wasiotaka kufanya homework yao, wanaongojea miujiza na kujibiwa sala rather than kufanya kazi, yanakuwa too cold, too scary.Kwa hiyo ili kujifariji wana mu invent mungu ambaye hata hayupo, ili tu wajisikie comfortable kwamba if worst comes to worst the big man will take care of everything.

Partly ni kama saikolojia ya mtoto anayekua huku akiona wazazi wake wapo wanam protect, akikua anataka kuamini kwamba kuna mzazi mkubwa zaidi, mzazi wa binadamu wote, atakayeweza kujibu sala za watu.

I hate to break it down to you, ushahidi wote, ma earthquake yanayoua watoto wasio hatia huko Haiti, vita, uovu etc, vinaonesha hakuna mungu, na kama yupo hatujali kwa hiyo you might as well assume hayupo.

Hata mimi ningekuwa mungu nina uwezo wote na upendo wote, ningeweza kutengeneza dunia bora kuliko hii.
 
Back
Top Bottom