Reli itajengwaje wakati malori ya wazito yamejaa barabarani? Watawala hawataki kusikia kitu reli.
Mtawala gani Tz anafikiria maendeleo yetu!
Jambo moja la hakika ni kuwa mwisho wao ni mbaya. Wapo kama wale wa Sodoma na Gomora. Ole wao.
Ningelitamani kusikia kauli kama hii yako ya kutaka mabadiliko ikitoka kwa vinywa vya Watanzania walio wengi. Na sio kusikia wakisema tu bali kutenda, kutenda kwenye visanduku vya kura. Najua CCM wataendelea kutisha watu, wataendelea kuhonga na kurubuni lakini ikiwa Watanzania tuko tayari kwa mabadiliko, hatutatishika wakitutisha, tutakula vyao wakituhonga na kuturubuni na ikifika siku ya kuamua, tutaamua mabadiliko. Miaka 50 ni mingi sana kuongozwa na magamba.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.