Jimmy hayaelewa ule utafiti ulilenga kitu gani, lengo la utafiti ule ilikua kuangalia uwezo viongozi kusimamia mijadala bungeni, ndio maana ulilenga kwa spika, naibu wa spika na wenyeviti.
Mjadala bungeni sio kielelezo cha kukomaa demokrasia, kanuni zilizopo spika anao uwezo wa kulazimisha nini kijadiliwe na nini kisijadiliwe, Pia spika anao uwezo wa kuamua nani ampe nafasi na nani amnyime nafasi.
Wabunge pia wamekua wakijadili kwa maslahi ya chama, ni mpaka maslahi ya umma yatapoanza kuwekwa mbele kabla ya maslahi ya chama tunaweza kusema demokrasia inakomaa
Bunge letu sasa hivi limekuwa kama tamthilia mijadala mingi imejikita katika ushabiki mkubwa wa kisiasa sio kwa maslahi ya Taifa, nalikumbuka bunge la mwaka 2010 chini ya spika Sitta, bunge likuwa na changamoto nyingi wabunge walikuwa wanachangia kwa hoja, ili bunge la sasa limekuwa bunge la muongozo spika...unashangaa mtu kama Tundu Lissu anasimama na kutumia data za magazeti ya udaku kama reference.
Bunge la sasa hivi limekuwa dhaifu kutoka na uongozi wa bunge kuwa dhaifu..wanaegemea sana chama tawala..limekuwa bunge la vijembe..binafsi namkubali Tundu Lissu kwa sababu anaongea facts..Ndungai kubali kiti chenu kimepwaya tofauti na bunge la kipindi cha mh. Sita.
nashukuru kwa kukumbuka uwezo mkubwa wa Mh.Sita sasa umeonyesha kuwa huyu mama anayeongoza bunge pamoja na Jenister Mhagama hawana lolote wako dhaifu sana ktk kuliongoza bunge hili, bora Ndugai kwa kiasi flan kuliko hawa akina mama wawili. Wewe una ushabiki wa ukada kwa kuwa yale wanayoyaongea akina Mwigulu, komba, na wengine unawaacha ila umemwona Tundu lissu, acha ukada na majungu hayatakusaidia kitu.