Star tv na itv kuzindundua kingamuzi na matangazo ya digital September 2012

Kurunzi

JF-Expert Member
Jul 31, 2009
9,277
9,912
Serikali kupitia Tume ya Mawasiliano nchini imesema kuwa ifikapo Disemba 31 mwaka 2012 ndiyo itakuwa mwisho kwa vituo vyote vya televisheni kurusha mawasiliano yake katika mfumo wa analogy na kujiunga na mfumo wa digitali, hivyo basi kwa msingi huo kampuni ya Sahara Media Group na wadau shirika wako kwenye mchakato kuharakisha zoezi la kusimika minara na mitambo kwaajili ya kuingia kwenye masafa bora ya kisasa.

attachment.php


Mkurugenzi wa Sahara Media Group bw. Anthony Dialo akiongea na waandishi wa (habari wataonekana katika picha nyingine) ambapo amesema kuwa kuanzia mwezi Septemba 2012 minara na mitambo ya king'amuzi kipya itawashwa rasmi kwaajili ya kuanza kufanya kazi. Star Tv pamoja na televisheni zote za IPP zitaingia katika mfumo wa digitali kupitia king'amuzi hicho.

attachment.php


"Uzuri wa mfumo wa digitali kupitia kingamuzi unakupa fursa ya kupata chanel nyingi zaidi katika frequency moja, Inakupa afya ya macho kupata picha safi kwa matukio na taarifa mbalimbali" says Mr. Dialo.

"Jumla ya leseni tatu zilitolewa na TCRA kwa ajili ya kurusha matangazo ndani ya mfumo wa digitali, TBC wakishirikiana na Star Media wanakingamuzi chao kiitwacho Startimes, Makanisa wakishirikiana na Agape wanaking'amuzi chao kiitwacho Ting, na leseni ya tatu ilitolewa kwa Sahara Media Group wakishirikiana na IPP, hivyo kaa tayari kujionea mapinduzi mapya ndani ya mfumo wa Digitali" Aliongeza Mkurugenzi huyo wakati wa mahojiano yaliyofanyika kwenye minara ya urushaji wa matangazo iliyopo katika vilima vya Nyanshana wilaya ya Ilemela jijini Mwanza..
 

Attachments

  • sahara media group 2.jpg
    sahara media group 2.jpg
    66.5 KB · Views: 824
  • sahara media group 10.jpg
    sahara media group 10.jpg
    47.7 KB · Views: 788
Ningewashauri hao TCRA watoe kingamuzi 1 cha ziada ambacho mtumiaji anauwezo kutumia kadi 1 wa kuona chanel zote, mfano kuwe na kingamuzi chenye ITV na tv zake zote(EATV,CAPITAL),Star Tv,Mlimani,TBC,Chanel10 na tv zake zote(C2C na DTV) na nyinginezo za ziada kama walivyo Star times na Ting hii itasaidia kiasi fulani, hebu pata picha unaingia sebuleni kwa mtu unakuta deki za vingamuzi zaidi ya 3 havileti picha nzuri kwanza ni mzigo na manynya mengi sebuleni hayapendei hadhi ya sebule inageuka karakana maan manyaya kila kona...
 
Jumla ya leseni tatu zilitolewa na TCRA kwa ajili ya kurusha matangazo ndani ya mfumo wa digitali, TBC wakishirikiana na Star Media wanakingamuzi chao kiitwacho Startimes, Makanisa wakishirikiana na Agape wanaking'amuzi chao kiitwacho Ting, na leseni ya tatu ilitolewa kwa Sahara Media Group wakishirikiana na IPP, hivyo kaa tayari kujionea mapinduzi mapya ndani ya mfumo wa Digitali" Aliongeza Mkurugenzi huyo wakati wa mahojiano yaliyofanyika kwenye minara ya urushaji wa matangazo iliyopo katika vilima vya Nyanshana wilaya ya Ilemela jijini Mwanza..
Kampuni ya tatu si Sahara ni ZUKU labda kama tcra wameongeza na sahara imekuwa ya nne.
 
According to TCRA ambayo imetoa leseni kwa makampuni matatu (Startimes, Ting na hao Basic transmision) mara mfumo wa digitali utakapoanza rasmi basi ili kuondoa usumbufu wa kuwa na ving'amuzi vyote vitatu, hawa service provider itawalazimu kuingiza local chanel zote katika ving'amuzi vyao na hizi local chanels zitakuwa ni free to air channels.

kwa hiyo watanzania wasiwa na wasiwasi, local chanel zote zitapatikana katika ving'amuzi vyote vitatu na zitakuwa free to air]

 
he he he he he hii ishu ya ving'amuzi nayo du noma kwahiyo sasa na TV zitakuwa kama simu maana kbla ya mchina kuja na double line lazima mtu utembee na simu kadhaa sasa na TV naona kama tunaelekea huko he he he he he
 
Nahisi kuchanganyikiwa.

Sisi wenye Dstv inakuwaje? Tutapata hizo local channels au ni lazima kuongeza ving'amuzi?
 
According to TCRA ambayo imetoa leseni kwa makampuni matatu (Startimes, Ting na hao Basic transmision) mara mfumo wa digitali utakapoanza rasmi basi ili kuondoa usumbufu wa kuwa na ving'amuzi vyote vitatu, hawa service provider itawalazimu kuingiza local chanel zote katika ving'amuzi vyao na hizi local chanels zitakuwa ni free to air channels.

kwa hiyo watanzania wasiwa na wasiwasi, local chanel zote zitapatikana katika ving'amuzi vyote vitatu na zitakuwa free to air]

Mkuu kama hivi ndivyo for the first time Tanzania tutakuwa tumefanya maamuzi yenye akili maana kila unaposoma na kuangalia maamuzi ya serekali yetu kwenye Multilateral contracts unabaki kujiuliza tuna laana au?? yaani tunajikana as if hao wanaosaini hiyo mikataba watahamia kwenye sayari nyingine wao na ndg zao right after hyo mikataba kuanza kutumika.
 
Hapo kwenye bluu naomba ufafanuzi mkuu twatwatwa, maana mimi sielewi nazidi kuchanganyikiwa tu.

kwa uelewa wangu mdogo ni hivi DVB S wao wanatumia mainly SATELITE katika transmission zao na hizi DVB T wao mainly wanatumia tower (sijui nisemeja hapa) but kwa hizi DVB S ambazo wanatumia satelite moja kwa moja karusha kwa wateja wao haiwalazimu kufunga mitambo tena kwani whenever you are ukifunga satelite dish utapata access na ndo maaana DSTV hata ukiwa very interior unaweza kuiaccess.

tofauti na hawa wanaotumia DVB T ambao wao inawalazimu kufunga towers (transmitters) pale wanapotaka kutoa accessbility ya huduma zao na ndo maana STARTIMES wao wanatumia mitambo ambayo kwa sasa wamefunga DAR, ARUSHA, MWANZA, DODOMA, TANGA NA MOSHI na ukiwa nje ya mikoa hiyo huwezi pata huduma zao

na ndo maana tunasema ZUKU sio competitor kwa startimes na zuku, kwani system zao ni tofauti wao ZUKU na DSTV naweza sema ni competitors though Kind of service zinazotolewa na makampuni yote haya zinafanana.
 
kwa uelewa wangu mdogo ni hivi DVB S wao wanatumia mainly SATELITE katika transmission zao na hizi DVB T wao mainly wanatumia tower (sijui nisemeja hapa) but kwa hizi DVB S ambazo wanatumia satelite moja kwa moja karusha kwa wateja wao haiwalazimu kufunga mitambo tena kwani whenever you are ukifunga satelite dish utapata access na ndo maaana DSTV hata ukiwa very interior unaweza kuiaccess.

tofauti na hawa wanaotumia DVB T ambao wao inawalazimu kufunga towers (transmitters) pale wanapotaka kutoa accessbility ya huduma zao na ndo maana STARTIMES wao wanatumia mitambo ambayo kwa sasa wamefunga DAR, ARUSHA, MWANZA, DODOMA, TANGA NA MOSHI na ukiwa nje ya mikoa hiyo huwezi pata huduma zao

na ndo maana tunasema ZUKU sio competitor kwa startimes na zuku, kwani system zao ni tofauti wao ZUKU na DSTV naweza sema ni competitors though Kind of service zinazotolewa na makampuni yote haya zinafanana.

Asante nimekupata......
 
Back
Top Bottom