Leo asubuhi nimepitia pale Ubungo stand ya mkoa na kukuta hali ya giza ambayo sikuamini kabisa kwani kama nchi iliyopata uhuru miaka 50 iliyopita leo stand yetu kuu inakosa hata taa (Umeme) na tena tumeweka agent wa kuendesha stand ile (kama sikosei) hatuna hata standby generator!!! sielewi watawala wa nchi hii wanafanya nini juu ya wananchi wake!!! Usalama wa abiria na mizigo yao haupo tena kama hali ilivyo kuwa leo hii kwani kulisikika tu kelele na vilio vya watoto. CCM na serikali mnatupeleka wapi jamani hili ni swala dogo sana kwa uwezo wa serikali!!!