Stan Katabalo: Tunauhitaji mzimu wako wa habari za Uchunguzi!

Kamongo

JF-Expert Member
Mar 20, 2009
1,957
2,068
Nafikiri watu wengi mnakumbuka yule mwandishi wa habari miaka ya themanini na tisini marehemu stan Katabaro,alikuwa ni mwandishi mahiri kwa miaka ya leo hana tofauti na Saed Kubenea,Johnson Mbwambo,nauliza kifo chake kilisababishwa na nini hasa?wanaokumbuka watujuze

Nakumbuka wakati niko mdogo ingawa nilikuwa najua kusoma na kuandika wakati huo,kulikuwa na kashfa moja kubwa sana iliyoitingisha nchi,kashfa ya loliondo,kipindi hicho kuna mwandishi mmoja alikuwa anaitwa Stan Katabalo,nadhani alikuwa anaandikia gazeti la Mfanyakazi au.., huyu jamaa mwandishi alikuwa anapambana na system na mbaya zaidi alikuwa peke yake katika kutetea masilahi ya nchi yetu, nakumbuka watu kama Ndolanga na wenzake.

Pamoja na Rais wa kipindi kile walikuwa wanahusika sana kwenye ile kashfa ya Loliondo, huyu jamaa mwandishi shujaa huyu alikuja kufa katika mazingira ya ajabu sana na mpaka leo sijasikia hata akienziwa,inauma sana...

Huyu jamaa alikuwa si tu shujaa bali alifungua njia kwenye tasnia nzima ya investigative journalism hapa nchini,hivi kwanini isianzishwe hata tuzo kwa jina lake?

Huyu mtu anadeserve heshima ya pekee sana katika suala hili,kwa sababu hizi kashfa zote mnazoziona leo zikiwemo Richmond, IPTL, ESCROW sio kwamba zimeanza jana au juzi katika nchi hii.

Ni tangu kipindi hichoo cha Mwinyi sema tu watu hawakuwa makini kama ilivyo sasa na matokeo yake kwa wale waliokuwa conscious kama Stan Katabalo waliishia kupotezwa kusikojulikana, REST IN PEACE STAN KATABALO, HAKIKA WEWE ULIKUWA JABALI NA MZALENDO HALISI WA NCHI HII.
 
Alikufa ghafla!

Kumfananisha Kubenea na Stan, ni kumpandisha tuu chati Kubenea, Stan alikuwa akiandika investigative journalism kwenye developing story, Kubenea anaandika udaku kwenye medani za siasa, sio uchunguzi in a really sense ya uchuguzi.

Waliotaka kufuata nyanyo za Katabalo, ni This Day na Kulikoni, walioanza, wakati wakifuatilia story ya Rada.
 
Masikini_Jeuri

Gazeti lake liliitwa Mfanyakazi, kila wiki nilihakikisha napata nakala yangu. Humo ndani pia kulikuwa na hadithi za mtunzi maarufu Agoro Anduru, sijui kaishia wapi siku hizi. Na column fulani ndogo ya vichekesho iliyokuwa ikiitwa Nipashe, yenye picha ya sikio kuubwa.

Nilisikitishwa sana na kifo cha Stan Katabaro, Mungu amweke pema na aisaidie familia yake, Amen.
 
Last edited by a moderator:
Alikufa ghafla!.
Kumfananisha Kubenea na Stan, ni kumpandisha tuu chati Kubenea, Stan alikuwa akiandika investigative journalism kwenye developing story, Kubenea anaandika udaku kwenye medani za siasa, sio uchunguzi in a really sense ya uchuguzi. Waliotaka kufuata nyanyo za Katabalo, ni This Day na Kulikoni, walioanza, wakati wakifuatilia story ya Rada.
ni kweli kabisa pasco...

Tatizo kubwa la kubenea ni ku-personalize uandishi wake na hivyo kuwa na agenda moja tu,
 
Siamini sana uchawi lakini kifo chake kinasemekana kulikuwa na mkono wa mtu.

Aliwasumbua sana jamaa na kashfa ya Loliondo na mpaka walitishia kumuua lakini hakuacha kuandika. Tulikuja kushtukia amekufa tayari lakini alikuwa ni mwandishi mahari ambaye akianza kuriporti tukio ni mwanzo mpaka mwisho. Lakini Ndolanga (mkurugenzi wa wanyama pori wakati ule na Rais Mstaafu Mwinyi) wanaweza kueleza kilichomkuta!!! Inawezekana alilishwa sumu bila kujua.

RIP Stan Katabaro. Hivi alikufa na gazeti lake la mfanyakazi? Mbona silioni wala kulisikia siku hizi?

Tiba
 
Hawezikulinganishwa na waandishi uchwala wa sasa huyu bwana alikuwa na team nyingine ya madongo.

Mnamkumbuka Stanley KAMANA wa Family Mirror (RIP) hawa wote walikufa vifo vya ajabu ila ikumbukwe pia wakati hule lile janga la UKIMWI lilikuwa halijulikani na mtu aliyeugua dalili zake zilikuwa zinaelekezwa kwa Prof. Maji Marefu naye hakuwa na hiyana ya kubadilisha kibao mpaka pale walipomshutukia na kumfukuza Dar ila alichafua hali ya hewa mitaa ya Kariakoo na Ilala.
 
Gazeti lake liliitwa Mfanyakazi, kila wiki nilihakikisha napata nakala yangu. Humo ndani pia kulikuwa na hadithi za mtunzi maarufu Agoro Anduru, sijui kaishia wapi siku hizi. Na column fulani ndogo ya vichekesho iliyokuwa ikiitwa Nipashe, yenye picha ya sikio kuubwa.

Nilisikitishwa sana na kifo cha Stan Katabaro, Mungu amweke pema na aisaidie familia yake, Amen.

Agoro Anduru (The Temptation) ni Marehemu pia (RIP)

Stan hawezi kulinganishwa na mwandishi yeyote katika hii decade 2000 - 2010! Kubenea, Mbwambo, e.t.c they are no where near - kumbuka kuwa wakati the so called "uhuru wa vyombo vya habari" ulikuwa mdogo sana!

RIP Stan K.
 
Gazeti lake liliitwa Mfanyakazi, kila wiki nilihakikisha napata nakala yangu. Humo ndani pia kulikuwa na hadithi za mtunzi maarufu Agoro Anduru, sijui kaishia wapi siku hizi.

Ulipomtaja marehemu Agoro Anduru umenikumbusha vipaji vya uandishi wa huyu mwana riwaya mahiri.............jamani walikuwepo watanzania wenye vipaji ambao taifa hili halitaki hata kuwaenzi............Sijui kwa nini....
 
Alikufa ghafla!.
Kumfananisha Kubenea na Stan, ni kumpandisha tuu chati Kubenea, Stan alikuwa akiandika investigative journalism kwenye developing story, Kubenea anaandika udaku kwenye medani za siasa, sio uchunguzi in a really sense ya uchuguzi. Waliotaka kufuata nyanyo za Katabalo, ni This Day na Kulikoni, walioanza, wakati wakifuatilia story ya Rada.

Kama kawaida yako mzee unajiamini sana na unaweza kusema lolote lile. Kumbuka kuwa hata KGB ilisambaratika!
 
Je, mnakumbuka na ile kashfa ya RIO? Kwenye mkutano wa Mazingira Duniani ulifanyika BRAZIL (Rio de Janeiro)

Kwahakika hakuna kama STAN KATABALO.

Kashfa ya LOLIONDO ilimhusu sana sana ABUBAKAR MGUMIA......

Huyo bwana ndiye aliyekuwa mhimiri wa kashfa ya Loliondo kabla ya kutolewa Wizara ya Utalii na kupelekwa kuwa RC Singida. Hivi siku hizi yuko wapi huyo Mgumia?


RIP Katabaro.....Namkumbuka sana jinsi alivyokuwa mwandishi mzuri sana na asiye na woga.

Wadau naomba pia mkumbuke jamaa mmoja anaitwa Anthony Ngaiza ambaye aliwahi kuwa editor wa Family Mirror kwenye miaka ya 1992/93 kabla ya kuhamia MCT. Tunahitaji kweli kuwakumbuka hawa jamaa!
 
Back
Top Bottom