mzee wa mawe
Senior Member
- Aug 2, 2011
- 151
- 15
WANACHAMA 395 wa chama cha mapinduzi (ccm) wilayani Kilwa, mkoani Lindi wamejiunga na CUF baada ya kuchukizwa na mfumo wa stakabadhi ghalani katika ununuzi wa zao la ufuta. Akizungumza jana jijini Dar es salaam, Naibu mkurugenzi wa mipango, uchaguzi na Bunge wa CUF, Shaweji mketo, alisema zoezi hilo lilifanyika wakati wa ziara yake wilayani humo kuanzia julai 23 hadi 29, mwaka huu.
Mketo alisema jumla ya waliojiunga na chama hicho ni 1,108, huku 395 wakitokea CCM na ambao amewakabidhi za chama hicho. Alisema wanachama 675 hawakuwa na chama na 38 kutoka CHADEMA.
Mketo alisema wanachama wengi waliojiunga na chama hicho walisema kuwa walikasirishwa na mfumo wa stakabadhi ghalani ambao umekuwa ukiwanyonya wakulima. Alisema kuwa kilio cha wakulima hao ni kutaka uhuru wa kuuza ufuta kwa wafanyabiashara ambao hununua kwa sh 1,700 kwa kilo badala ya vyama vya ushirika vinavyonunua kwa sh 1,000 kama vilivyo agizwa na serikali.
Mketo alisema jumla ya waliojiunga na chama hicho ni 1,108, huku 395 wakitokea CCM na ambao amewakabidhi za chama hicho. Alisema wanachama 675 hawakuwa na chama na 38 kutoka CHADEMA.
Mketo alisema wanachama wengi waliojiunga na chama hicho walisema kuwa walikasirishwa na mfumo wa stakabadhi ghalani ambao umekuwa ukiwanyonya wakulima. Alisema kuwa kilio cha wakulima hao ni kutaka uhuru wa kuuza ufuta kwa wafanyabiashara ambao hununua kwa sh 1,700 kwa kilo badala ya vyama vya ushirika vinavyonunua kwa sh 1,000 kama vilivyo agizwa na serikali.