Spring of Sadness - Eric Shigongo

Sanda Matuta

JF-Expert Member
May 9, 2007
949
134
Wakuu,

Naombeni msaada wenu kwenye hili na ikiwezekana toeni ushauri wenu kwa huyu Bwn. Shigongo, kwangu kama nimepituka na Watunzi wengine wa hadithi na sinema za Kitanzania na kuzipa majina ya kiingereza.

Mimi binafsi sio mtaalam wa lugha hiyo ya kiingereza ila kwa kiasi fulani naweza kugundua kosa.

Juzi hapa nilisoma katika gazeti la Risasi kama sikosei huyo Bw Shigongo ameandika hadithi humo na kuipa Jina la SPRING OF SADNESS na kuitafsiri kwa kiswahili kwa KISIMA CHA HUZUNI.

Kwa maana halisi ya hicho kingereza hapo yaani SPRING ni tofauti kabisa na maana mgeuzo ya KISIMA kwa kingeleza.

Kisima ni maji yaliyo tulia tofauti kabisa na spring,spring ni maji yaliyo katika kububujika au kutiririka.

Nadhani Bwn.Shigongo angetafuta watu wanao jua lugha hizo vizuri akawapa kazi ya edit hadithi zake na kuzirekebisha pale inapo bidi,na si tu kuziweka kwenye kurasa.

Magazeti yake yanasomwa na watu wengi, wengine wapo katika kujifunza, sasa unapomwambia spring ni kisima na kubeba hiyo maana, then atabisha hata kwenye ukweli akiaambiwa spring si kisima.

Na kama mimi ndio nisiye elewa hapa basi tafadhali nielimisheni
 
To be precise spring ni chemchemi more than kisima.

Unaweza kuchimba ardhi na kutengeneza kisima kwa kuipata water table iliyo chini.Hiki ni kisima.Well.

Spring ni maji yanayokuja juu yenyewe na kububujika.Chemchemi.

Shigongo mbona michemsho yake ni major tu, yaani hili ukilingnisha na michemko mingine utaona wala si issue kabisa.
 
Wakuu,

Naombeni msaada wenu kwenye hili na ikiwezekana toeni ushauri wenu kwa huyu Bwn. Shigongo, kwangu kama nimepituka na Watunzi wengine wa hadithi na sinema za Kitanzania na kuzipa majina ya kiingereza.

Mimi binafsi sio mtaalam wa lugha hiyo ya kiingereza ila kwa kiasi fulani naweza kugundua kosa.

Juzi hapa nilisoma katika gazeti la Risasi kama sikosei huyo Bw Shigongo ameandika hadithi humo na kuipa Jina la SPRING OF SADNESS na kuitafsiri kwa kiswahili kwa KISIMA CHA HUZUNI.

Kwa maana halisi ya hicho kingereza hapo yaani SPRING ni tofauti kabisa na maana mgeuzo ya KISIMA kwa kingeleza.

Kisima ni maji yaliyo tulia tofauti kabisa na spring,spring ni maji yaliyo katika kububujika au kutiririka.

Nadhani Bwn.Shigongo angetafuta watu wanao jua lugha hizo vizuri akawapa kazi ya edit hadithi zake na kuzirekebisha pale inapo bidi,na si tu kuziweka kwenye kurasa.

Magazeti yake yanasomwa na watu wengi, wengine wapo katika kujifunza, sasa unapomwambia spring ni kisima na kubeba hiyo maana, then atabisha hata kwenye ukweli akiaambiwa spring si kisima.

Na kama mimi ndio nisiye elewa hapa basi tafadhali nielimisheni
kwa hiyo ulitaka tafsiri ya SPRING OF SADNESS IWEJE?...ulitaka iwe ni

maji yaliyo katika kububujika au kutiririka YA HUZUNI..! au vipi?:eek::D
 
kwa hiyo ulitaka tafsiri ya SPRING OF SADNESS IWEJE?...ulitaka iwe ni

maji yaliyo katika kububujika au kutiririka YA HUZUNI..! au vipi?:eek::D

Mimi sikuta iwe vyovyote ila kwa maana HARISI.
Angeweza kuandika tu 'KISIMA CHA HUZUNI' na ikaleta maana inayo jitosheleza,hakukua na haja ya KINGEREZA kwani walengwa wa hizo hadithi walio wengi hawajui hiyo lugha au wapo katika kujifunza hiyo lugha.
Kwa kuwapa maana ya maneno zisizo sahihi ni kuwapotosha katika kijifunza.
Sasa labda wewe uwe na mawazo mengine?!
 
kwa hiyo ulitaka tafsiri ya SPRING OF SADNESS IWEJE?...ulitaka iwe ni

maji yaliyo katika kububujika au kutiririka YA HUZUNI..! au vipi?
:eek::D


"MTIRIRIKO WA HUZUNI" ......ingefaa zaidi.

Lakini sisi si Shigongo yeye mwenyewe ndio mwenye haki ya kuamua.
Tunachoweza kufanya ni kushauri kile kilicho sahihi tu!
 
"MTIRIRIKO WA HUZUNI" ......ingefaa zaidi.

Lakini sisi si Shigongo yeye mwenyewe ndio mwenye haki ya kuamua.
Tunachoweza kufanya ni kushauri kile kilicho sahihi tu!

Nadhani na wewe una uhusiano na Shigongo wa kutafsiri ndovyo sivyo..spring of sadness=chemchemi ya huzuni!
Nawakilisha..
 
Je, tuna hakika kwamba kichwa cha maneno hakimaanishi/hakihusu kipindi cha mwaka cha kuchipua? Kwa Kingereza husemwa mara nyingi kwa mfano "Winter of Sorrow/Discontent" bila kuwepo kwa nia ya kugusia mambo ya hali ya hewa hata kidogo. Matumizi haya ni ya kitamathali.
 
Hii ni zamani ila leo nimekuwa nikipekua kila linalotokea mbele yangu na kuliwekea komenti ikiwezekana.

Kwa hapa, phrase ya "Spring of Sadness" bila kuanza na "the" ina maana kuwa kipindi cha kuchipua, kinachofuata mara tu baada ya kipupwe, hakikuwa cha furaha. The Spring ina maana ya spiringi kama tunavyozijua za kwenye gari, na Sadness siyo maombolezo, bali ni kukosa furaha. Matumizi ya neno spring kwa maana ya kisima au chem chem ni makosa kwani chem chem inaitwa springs. Kama mheshimiwa Shigongo alitaka kusema "kisima cha maombolezo" angesema "The well of mourns (au mourning)" (-ambayo haisikiki vizuri katika kiingereza) au kama alitaka kusema chemchem ya maombolezo basie angesema "The springs of mourns (au mourning)." Vinginevyo angejiepusha kabisa na kutafsiri neno kwa neno (jambo linalowasumbua sana watu wanaofikiri kwa kiswahili na kuandika/kuzungumza kwa kiingereza) na badala yake akatumia phrase nyingine tofauti kabisa inayochukua maana ya kile alihotaka wasomaji wafahamu.
 
Hii ni zamani ila leo nimekuwa nikipekua kila linalotokea mbele yangu na kuliwekea komenti ikiwezekana.

Kwa hapa, phrase ya "Spring of Sadness" bila kuanza na "the" ina maana kuwa kipindi cha kuchipua, kinachofuata mara tu baada ya kipupwe, hakikuwa cha furaha. The Spring ina maana ya spiringi kama tunavyozijua za kwenye gari, na Sadness siyo maombolezo, bali ni kukosa furaha. Matumizi ya neno spring kwa maana ya kisima au chem chem ni makosa kwani chem chem inaitwa springs. Kama mheshimiwa Shigongo alitaka kusema "kisima cha maombolezo" angesema "The well of mourns (au mourning)" (-ambayo haisikiki vizuri katika kiingereza) au kama alitaka kusema chemchem ya maombolezo basie angesema "The springs of mourns (au mourning)." Vinginevyo angejiepusha kabisa na kutafsiri neno kwa neno (jambo linalowasumbua sana watu wanaofikiri kwa kiswahili na kuandika/kuzungumza kwa kiingereza) na badala yake akatumia phrase nyingine tofauti kabisa inayochukua maana ya kile alihotaka wasomaji wafahamu.

Mkulu umeeleweka/nimekuelewa
 
Huyu bwana kama mtu ulipitapita shule ukasoma vitabu vya kawaida sana kama vile zaka la damu, kijiji chetu, hawala ya fedha, this time tomorrow, mine boy, willy Gamba's (mhusika), Joram Kiango's (mtunzi), Cain and Abel, Sydney sheldon (mtunzi), james hardley chase (e.g. there is always a price tag), ...., etc etc etc, huwezi kuthubutu kusoma vitabu vya shigongo, kwanza title ya novel yenyewe tu inakuboa unaona huyu mtu kama hii profession amesomea, basi hakuiva na hataiva ila ataendelea kulazimisha tu! Sivipendi vitabu vyake kwanza sababu tu ya title na wala huwa sitamani hata nimnunulie mdogo wangu asome!
 
Wakuu,

Naombeni msaada wenu kwenye hili na ikiwezekana toeni ushauri wenu kwa huyu Bwn. Shigongo, kwangu kama nimepituka na Watunzi wengine wa hadithi na sinema za Kitanzania na kuzipa majina ya kiingereza.

Mimi binafsi sio mtaalam wa lugha hiyo ya kiingereza ila kwa kiasi fulani naweza kugundua kosa.

Juzi hapa nilisoma katika gazeti la Risasi kama sikosei huyo Bw Shigongo ameandika hadithi humo na kuipa Jina la SPRING OF SADNESS na kuitafsiri kwa kiswahili kwa KISIMA CHA HUZUNI.

Kwa maana halisi ya hicho kingereza hapo yaani SPRING ni tofauti kabisa na maana mgeuzo ya KISIMA kwa kingeleza.

Kisima ni maji yaliyo tulia tofauti kabisa na spring,spring ni maji yaliyo katika kububujika au kutiririka.

Nadhani Bwn.Shigongo angetafuta watu wanao jua lugha hizo vizuri akawapa kazi ya edit hadithi zake na kuzirekebisha pale inapo bidi,na si tu kuziweka kwenye kurasa.

Magazeti yake yanasomwa na watu wengi, wengine wapo katika kujifunza, sasa unapomwambia spring ni kisima na kubeba hiyo maana, then atabisha hata kwenye ukweli akiaambiwa spring si kisima.

Na kama mimi ndio nisiye elewa hapa basi tafadhali nielimisheni

Huyu bwana kama mtu ulipitapita shule ukasoma vitabu vya kawaida sana kama vile zaka la damu, kijiji chetu, hawala ya fedha, this time tomorrow, mine boy, willy Gamba's (mhusika), Joram Kiango's (mtunzi), Cain and Abel, Sydney sheldon (mtunzi), james hardley chase (e.g. there is always a price tag), ...., etc etc etc, huwezi kuthubutu kusoma vitabu vya shigongo, kwanza title ya novel yenyewe tu inakuboa unaona huyu mtu kama hii profession amesomea, basi hakuiva na hataiva ila ataendelea kulazimisha tu! Sivipendi vitabu vyake kwanza sababu tu ya title na wala huwa sitamani hata nimnunulie mdogo wangu asome!
 
Hata sababu ya huyo ndugu kutafsiri kila mara mimi siielewi. Sijui ndio kutujulisha kiingereza kimemkolea? Makosa ni mengi tu huwa anayafanya mwenye tafsiri zake. Bora abaki na kiswahili tu - kwa ushauri.
 
Labda hadithi au riwaya zinakuwa ni za kiingereza na yeye anacho fanya ni kuzitafasiri kwa kiswahili na kudai kuwa yeye ndiye mtunzi.
 
Huyu bwana kama mtu ulipitapita shule ukasoma vitabu vya kawaida sana kama vile zaka la damu, kijiji chetu, hawala ya fedha, this time tomorrow, mine boy, willy Gamba's (mhusika), Joram Kiango's (mtunzi),
Joram Kiango hakuwa mtunzi, alikuwa ni mhusika wa kwenye riwaya... Mtunzi alikuwa ni Ben R. Mtobwa
 
Huyu bwana kama mtu ulipitapita shule ukasoma vitabu vya kawaida sana kama vile zaka la damu, kijiji chetu, hawala ya fedha, this time tomorrow, mine boy, willy Gamba's (mhusika), Joram Kiango's (mtunzi), Cain and Abel, Sydney sheldon (mtunzi), james hardley chase (e.g. there is always a price tag), ...., etc etc etc, huwezi kuthubutu kusoma vitabu vya shigongo, kwanza title ya novel yenyewe tu inakuboa unaona huyu mtu kama hii profession amesomea, basi hakuiva na hataiva ila ataendelea kulazimisha tu! Sivipendi vitabu vyake kwanza sababu tu ya title na wala huwa sitamani hata nimnunulie mdogo wangu asome!

Ah, nyinyi mwaona sasa.Lakini sisi ambao tumeanza kusoma hadithi za Shaigongo tanga miaka ile tulishagundua kuwa si lolote wala si chochote.Nadhani tatizo lake kubwa ni ukiritimba wa utunzi.Magazeti yake yote anataka atunge yeye na wala hawapi nafasi watunzi wengine wazuri ambao wamejaa tele nchini.Anatakiwa kubadilika sasa
 
chemichemi au chemchem :confused2: ! swali zuri nakupa heko mtoa MADA
 
Back
Top Bottom