Sanda Matuta
JF-Expert Member
- May 9, 2007
- 949
- 134
Wakuu,
Naombeni msaada wenu kwenye hili na ikiwezekana toeni ushauri wenu kwa huyu Bwn. Shigongo, kwangu kama nimepituka na Watunzi wengine wa hadithi na sinema za Kitanzania na kuzipa majina ya kiingereza.
Mimi binafsi sio mtaalam wa lugha hiyo ya kiingereza ila kwa kiasi fulani naweza kugundua kosa.
Juzi hapa nilisoma katika gazeti la Risasi kama sikosei huyo Bw Shigongo ameandika hadithi humo na kuipa Jina la SPRING OF SADNESS na kuitafsiri kwa kiswahili kwa KISIMA CHA HUZUNI.
Kwa maana halisi ya hicho kingereza hapo yaani SPRING ni tofauti kabisa na maana mgeuzo ya KISIMA kwa kingeleza.
Kisima ni maji yaliyo tulia tofauti kabisa na spring,spring ni maji yaliyo katika kububujika au kutiririka.
Nadhani Bwn.Shigongo angetafuta watu wanao jua lugha hizo vizuri akawapa kazi ya edit hadithi zake na kuzirekebisha pale inapo bidi,na si tu kuziweka kwenye kurasa.
Magazeti yake yanasomwa na watu wengi, wengine wapo katika kujifunza, sasa unapomwambia spring ni kisima na kubeba hiyo maana, then atabisha hata kwenye ukweli akiaambiwa spring si kisima.
Na kama mimi ndio nisiye elewa hapa basi tafadhali nielimisheni
Naombeni msaada wenu kwenye hili na ikiwezekana toeni ushauri wenu kwa huyu Bwn. Shigongo, kwangu kama nimepituka na Watunzi wengine wa hadithi na sinema za Kitanzania na kuzipa majina ya kiingereza.
Mimi binafsi sio mtaalam wa lugha hiyo ya kiingereza ila kwa kiasi fulani naweza kugundua kosa.
Juzi hapa nilisoma katika gazeti la Risasi kama sikosei huyo Bw Shigongo ameandika hadithi humo na kuipa Jina la SPRING OF SADNESS na kuitafsiri kwa kiswahili kwa KISIMA CHA HUZUNI.
Kwa maana halisi ya hicho kingereza hapo yaani SPRING ni tofauti kabisa na maana mgeuzo ya KISIMA kwa kingeleza.
Kisima ni maji yaliyo tulia tofauti kabisa na spring,spring ni maji yaliyo katika kububujika au kutiririka.
Nadhani Bwn.Shigongo angetafuta watu wanao jua lugha hizo vizuri akawapa kazi ya edit hadithi zake na kuzirekebisha pale inapo bidi,na si tu kuziweka kwenye kurasa.
Magazeti yake yanasomwa na watu wengi, wengine wapo katika kujifunza, sasa unapomwambia spring ni kisima na kubeba hiyo maana, then atabisha hata kwenye ukweli akiaambiwa spring si kisima.
Na kama mimi ndio nisiye elewa hapa basi tafadhali nielimisheni