Spika wa bunge (Anne Makinda) akiri posho kuongezwa!

Zitto ameshauri watanzania wawanunie viongozi wanaoshabikia posho akiwemo spika makinda kuonesha kwamba haturidhiki na mtindo wa kujilimbikizia. Wewe unadhani kununa kutawapa ujumbe kwamba watanzania hawawaungi mkono?

Source: Zitto twitter account

Tuwanunie wabunge wote hadi wazikane hizo posho na kuzirudisha na kupitisha zifanye kazi nyingine za jamii. Hivi hizi posho zinaweza kuongezwa bila kupitishwa kwenye budget? Jamani wabunge si ndio wanapitisha budget na hakuna pesa ya serikali inayotumika bila kupitishwa kwenye budget! kwa hiyo ina maana wabunge walipitisha nyongeza ya posho zao kwenye budget iliyopita. Sikusikia hata mbunge mmoja akitoa shilingi ili posho zisipite zikiwa na nyongeza. Spika ametekeleza tu maamuzi ya wabunge wenzake.

Wabunge wa nchi kweli wanatufanya sisi hamnazo kweli!!
 
Baada ya piga nikupige,sintofahamu na sarakasi nyingi hatimaye spika wa bunge,Anne Makinda a.k.a Mama wa Yutong ametangaza rasmi kuongezeka kwa posho za wabunge.Kiasi kilichoongezeka ni 130000 na kufanya posho kwa kila kikao kufikia 200000 kutoka 70000.Sababu alizotoa Mama wa Yutong ni kupanda gharama za nyumba za kulala wageni mjini dodoma.
 
Ni hivi majuzi tu magazeti yaliandika kwamba malipo ya vikao kwa wabunge yamepanda kutoka sh 70,000 mpaka sh 200,000. Mara baada ya taarifa hiyo kulitokea kauli za kujichanganya kwa viongozi mbalimbali.

Kwa bahati nzuri leo spika kaamua kulitolea ufafanuzi na kathibitisha ni kweli nyongeza hiyo imefanyika kwa nyongza ya sh 130,000 na sasa ni sh 200,000. Kilichonifurahisha kama sio kunitoa machozi ni sababu ya nyongeza hiyo.. mh spika yeye anasema gharama za maisha zimepanda sana hivyo kufanya wabunge kuishi kwa tabu, Je
- Gharama hizi hupanda kwa maisha ya wabunge tu au?
- Kama bunge limeweza kuona kupanda huko kwa maisha kwanini asitetee mishahara ipande kwa asilimia hizo hizo?
- Kama mbunge anashindwa kuishi kwa 70,000 kwa siku, vipi anayelipwa sh 100,000 kwa mwezi?

Wana jamvi nawakilisha
 
Mh Anne Makinda,Spika wa Bunge La Tanzania ameweka wazi kwamba Posho za wabunge zimepanda,analalamika upotoshwaji wa makusudi kwamba posho zimepanda toka Tsh 70,000 hadi Tshs 200,000.Hata hivyo hajaweka wazi zimepanda hadi Shs ngapi.Makinda ametoa maelezo haya ikiwa si zaidi ya siku mbili tangu Kashilila aseme kwamba posho hazijapanda.

Source: Clouds Radio 1800 hours News

TBC wamemuonesha pia bibi akitangaza ongezeko hilo,toka elfu 70 mpaka laki mbili ni ongezeko la zaidi ya asilimia 170! Ni sawa na Mshahara wa wafanyakazi wengi wa serikali kwa mwezi,MBONA VIJANA UDSM WALIAMBIWA SERIKALI HAINA PESA?
 
Hivi kwanini hawatumii wingi na umuhimu wao effectively? Say wagome for a month!

By the way hivi wabunge wakigoma kuna hasara yoyote?
Kwa njia bora za mawasiliano zilizopo sasa hii inawezekana sana. Hivyo walimu tuondokane na dhana ya kutegemea CWT pekee wakati imeshindwa kazi. Wenye kulijua hili tutaendelea kupiga kelele mpaka na wengine watuelewe. Saa ya ukombozi bila shaka yaja. Walimu mpo? Tuungane basi jamani! Hamwoni wenzetu hapo Kenya wameanza mgomo (wauguzi) mpaka kitaeleweka! Eti
 
Ubinafsi ndo unawasumbua hawa wabunge. Mshahara milioni 12 kwa mwezi, Posho ya kikao 200,000 posho ya mafuta 50,000, posho ya kuwa nje ya jimbo 80,000.. Almost laki 330,000 kwa siku.
 
Hivi kwanini hawatumii wingi na umuhimu wao effectively? Say wagome for a month!

By the way hivi wabunge wakigoma kuna hasara yoyote?
wagome hata mwezi hatuwahitaji watu kwenda kutunga sheria za kuzuia kukonyezana huku wakiacha mahoteli yanakula tax holiday tu.sheraton-royal palm-movenpick-na sasa Serena!
 
Halafu amewasemea wabunge kuwa mshahara wanaopokea ni mdogo sana ukilinganisha na majukumu wanayofanya. Hivi huyu mama ana ndugu nyumbani kwao au ndiyo wale waliokimbia kijijini kwa kukataa kuolewa?

Mwita 25, Dr. kwa sasa amefanikisha matibabu yako!
 
spika anna makinda amekiri kuwa posho za wabunge zimepanda kutoka 70,000/= hadi 200,000/= ila hawatazichukua mpaka wasaini sasa je wale wabunge wanaoingia bungeni wanasaini tu halafu wanatoka itakuwaje
 
Hivi kuna msemo unaosema mwenye nacho huongezewa au Maji hutiririkia baharini. Sijui ndo wanaoutumia hawa wabunge kwani kama kuhusu hali ngumu, walimu, maaskari polisi na manesi wanahali ngumu zaidi achilia mbali wale wasiokuwa na kazi.
 
Nampongeza sana zito, uyu anaelewa machungu yetu, nadhani kununa hakutasaidia, hawa dawa yao ni kuwazomea, lazima tuwazomee huku tukiwaita walooo. Pia napendekeza tususie hizi sherehe kwani ni mabilioni mengi ya ela yametumika katika maandalizi yake badala ya kwenda kuwasaidia mama pia dada zetu wanaojifungulia sakafuni uko m'nyamala, temeke, muhimbili, m'mmoja nk, tususie sherehe hizi, tutumie uo mda kwenda kjitafutia riziki
 
Spika katema cheche, ni kweli posho za wabunge zimepanda, kisa? Gharama za maisha zimepanda mjini Dodoma. Hivi hizi gharama za maisha zimepanda dodoma tu, huku kwetu uswahilini hazijapanda eeh? Anne mnalipwa mshahara sijui milioni ngapi kwa mwezi, mnapewa hela ya mafuta, bado marupurupu kibao, leo mnajiongezea posho eti gharama za maisha zimepanda, haya maisha yamepanda kwenu tu, mimi ninaelipwa sh 135,000
kwa mwezi nisemeje? Shame on you.... I wish ningekuwa karibu hapo wkt unaongea ningekunasa kibao
 
Hawa watu wanatuchanganya! Jana, katibu wa bunge alieleza kwamba hakuna kitu kama hicho, yaani nyongeza ya posho kwa Wabunge, leo nimemsikia kupitia TBC1 Bi Kiroboto kwa masikio yangu akidai kwamba wamelazimika kuwaongezea posho hizo Wabunge eti kwa sababu gharama za maisha Dodoma zimepanda!

Swali: Hivi ni lini Dodoma ilijitenga na Tanzania! Je wafanyakazi wa kawaida wanaoishi Dodoma, posho na Mishahara yao nao imeongezwa!

Nilitaka kujua tu wajomba.
 
Back
Top Bottom