Spika Sitta, Pinda wametupotosha

Asha Abdala

JF-Expert Member
Mar 21, 2007
1,130
44
JANA Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akijibu swali bungeni lililotaka kujua ni lini viongozi wa kiserikali kama rais wataacha kutumia ziara za kiserikali kufanya shughuli za kichama, kama alivyofanya Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni huko Pemba, alisema rais ni mkubwa wake wa kazi na yeye asingeweza kutoa kauli ya kile kinachodaiwa kuwa alikisema, kwa sababu hakuwepo, na hajui ni nini rais alisema, zaidi ya kusoma tu kwenye vyombo vya habari.

Zaidi ya majibu hayo ya Pinda, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, aliingilia kati kumsaidia waziri mkuu na kusema kwamba hakukuwa na haja ya swali hilo kujibiwa, kwani liko wazi.

Kwamba haiwezekani kutenganisha kofia mbili alizonazo rais, yaani ile ya urais na ile ya kuwa mwenyekiti wa chama chake, na kusisitiza kuwa hata katika nchi zilizoendelea sana kama Marekani, rais wao hutumia ndege ya serikali ‘Air Force One’ kufanya ziara ya kichama.

Kwanza, sisi tunasisitiza tena kuwa si sahihi kwa rais wala kiongozi yeyote wa serikali kutumia ziara za kiserikali ambazo kimsingi zimegharamiwa na kodi za Watanzania wote kutoa hotuba, kauli, kufanya shughuli au jambo lolote kwa masilahi ya chama chake cha siasa.

Si sahihi, kwa sababu mtu anapokuwa kiongozi wa kiserikali, wajibu wake ni kuwatumikia Watanzania wote bila kujali chama chake.

Pili, kiongozi wa kiserikali kufanya shughuli kwa masilahi ya chama chake cha siasa wakati akiwa kwenye ziara ya kiserikali, ni kuruhusu mgongano wa kimasilahi kati ya masilahi ya chama chake na masilahi ya taifa, ambayo ndiyo hasa anayopaswa kuyasimamia wakati huo akiwa kwenye ziara hizo za kiserikali.

Tatu, hatukubaliani na upotoshaji wa Spika Sitta kuwa haiwezekani kwa rais kutenganisha majukumu yake kama rais na kama mwenyekiti wa CCM, kwani sisi tunaamini kuwa inawezekana, kinachotakiwa ni kwa mhusika (Rais Kikwete) kuwa na utashi na utayari wa kutodharau misingi ya utawala bora wala kuwa mwepesi wa kubagua wafuasi wa vyama vingine vya siasa pindi awapo kwenye ziara za kiserikali.

Nne, Rais Kikwete anapaswa kupanga muda wa kufanya ziara za kichama ambao utakuwa ni tofauti na ule wa ziara za kiserikali, na anapaswa kutumia ruzuku ya CCM kwa ziara za kichama, badala ya kudoea usafiri wa kiserikali halafu anakwenda kuzungumzia mambo ya CCM kama alivyofanya Pemba hivi karibuni.

Akiona ni vigumu, basi aache ziara zake za kichama zifanywe na Makamu Mwenyekiti wake, Pius Msekwa, au Katibu Mkuu wake, Yusufu Makamba, pale inapolazimu.

Tano, kauli ya Pinda kuwa hawezi kutoa kauli kuhusu kile alichokisema Rais Kikwete, eti kwa sababu ni mkuu wake wa kazi, ni ya upotoshaji.

Pinda kwa nafasi yake kama Waziri Mkuu, ndiye mtu wa mwisho anayepaswa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo lolote linalohusu serikali na maadili ya viongozi wake, akiwemo rais.

Kwanini Pinda anasema hakuwepo na hajui alichokisema rais? Kama vyombo vya habari viliandika uongo kuhusu kile alichokisema Kikwete kule Pemba, serikali iliyo chini ya Pinda kama Waziri Mkuu, ilishindwa vipi kutoa taarifa ya kukanusha kile kilichoripotiwa kupitia mwandishi wake, Salva Rweyemamu?

Kwanini Pinda anaviamini tu vyombo vya habari pale vinaporipoti mambo mazuri ya viongozi lakini haviamini pale vinaporipoti kauli zisizofaa za rais?

Tunautaka umma wa Watanzania uelewe kuwa majibu yaliyotolewa bungeni na viongozi hawa ni ya upotoshaji, ni wajibu wa kila mwananchi kutochoka kuwarudisha kwenye mstari viongozi wetu pale wanapofanya ndivyo sivyo.

Chanzo: Tanzania Daima

Tafakari yangu:

Pongezi kwa mhariri kwa kuwazodoa. Ukweli ni kuwa kikwete alivunja katiba kwa kufanya ubaguzi wa kisiasa, lakini kubwa zaidi ni kuwa amekiuka sheria ya utumishi wa umma ambayo inawataka watumishi wa umma kufanya kazi bila kubagua au kuwanyanyasa wananchi kutokana na tofauti za kivyama kwa kutumia ofisi zao za umma. Sheria inawataka pia kutotumia ofisi za umma kwa manufaa ya vyama vyao. Rais ni mtumishi wa umma, ni wazi kwamba katika ziara hiyo ya Zanzibar ametumia fedha za ofisi ya umma na mikutano ya hadhara iliitishwa kwa kofia yake kama Rais lakini akafika na kuitumia kichama. Hii si mara ya kwanza, mtakumbuka Kikwete na mawaziri wake walipokwenda Kigoma na Rukwa wakafanya uharibifu mwingi kwa kofia ya umma ikiwemo kuwarubuni wenyeviti wa vijijini na vitongoji kutoka CHADEMA. Kwa hiyo Rais akaenda kuzivunja serikali ambazo alipaswa kushirikiana nazo katika ziara hiyo. Halafu Pinda na Sitta wanatetea huo uvunjaji wa sheria na wapinzani bungeni nao wanawaachia tu. Huu mjadala haupaswi kufungwa mpaka kieleweke. Kama executive imeshindwa kuitafsiri na kuheshimu hii sheria. Na legislature kwa maana ya spika na bunge lake wanachekelea tu. Inabidi sasa kupata judicial directives. Wakome kabisa hawa! Ni vizuri Tanzania tukaheshimu maadili ya siasa za vyama vingi na utawala wa sheria.

Asha
 
Hayo yote sawa,kwani tumesahau kwamba hakuna chama kinaitwa CCM? Nijuavyo mimi, kuna kitengo cha dola kinachoitwa CCM. Kama CCM kingekuwa chama cha siasa basi kingechukua mkondo ule ule uliochukuliwa na vyama vingine kuomba usajili kwa Liundi (aliyekuwa msajili wa vyama vya siasa) mwaka 1992. Lakini CCM haikufanya hivyo na ndio maana kimeendelea kuwa kitengo cha dola (au chama dola) kama wakati wa mfumo wa chama kimoja. Kwa hiyo, sishangai kwa JK na Mh Sitta kushindwa kuona kwamba kutumia pesa za umma kwa manufaa ya chama ni makosa na uvunjanji wa sheria. Hata watangulizi wao walifanya hivyo (Sumaye na Mkapa) kwa hiyo hawaoni tatizo labda tuwalazimeshe kuyaona makosa yao kwa kutumia mahakama au nguvu ya umma. Hii pia ihusishe CCM kurudisha mali zilizochangiwa na wananchi wote wakati wa mfumo wa chama kimoja.
 
Kwanza, sisi tunasisitiza tena kuwa si sahihi kwa rais wala kiongozi yeyote wa serikali kutumia ziara za kiserikali ambazo kimsingi zimegharamiwa na kodi za Watanzania wote kutoa hotuba, kauli, kufanya shughuli au jambo lolote kwa masilahi ya chama chake cha siasa.

Si sahihi, kwa sababu mtu anapokuwa kiongozi wa kiserikali, wajibu wake ni kuwatumikia Watanzania wote bila kujali chama chake.

Nini itakuwa maana ya kushinda uchaguzi kama viongozi/wanachama wa chama tawala watakuwa sawa na wale walioshindwa uchaguzi? Kama suala ni kauli zake, wanaoona kauli hizo zinapotosha wanayo haki ya kuelezea wananchi jinsi kauli hizo zinavyopotosha ama zilivyo mbaya. Na labda hilo likawaongezea mtaji wa kisiasa.

Pili, kiongozi wa kiserikali kufanya shughuli kwa masilahi ya chama chake cha siasa wakati akiwa kwenye ziara ya kiserikali, ni kuruhusu mgongano wa kimasilahi kati ya masilahi ya chama chake na masilahi ya taifa, ambayo ndiyo hasa anayopaswa kuyasimamia wakati huo akiwa kwenye ziara hizo za kiserikali.

Sioni mgongano wowote katika lililosemwa hapo. Naomba ufafanuzi. Nijuavyo mimi, hakuna sheria, wala agizo lolote linalomzuia mwanachama wa chama chochote amabae ni kiongozi wa serikali kufanya shughuli za kichama kila inapobidi.

Tatu, hatukubaliani na upotoshaji wa Spika Sitta kuwa haiwezekani kwa rais kutenganisha majukumu yake kama rais na kama mwenyekiti wa CCM, kwani sisi tunaamini kuwa inawezekana, kinachotakiwa ni kwa mhusika (Rais Kikwete) kuwa na utashi na utayari wa kutodharau misingi ya utawala bora wala kuwa mwepesi wa kubagua wafuasi wa vyama vingine vya siasa pindi awapo kwenye ziara za kiserikali.

Rais wa Tanzania atatokana na chama cha siasa kilichomteua kukiwakilisha katika uchaguzi, na kushinda uchaguzi huo. Sioni jinsi majukumu yake yanavyoweza kutenganishwa. Chama chake kinategemea Mwenyekiti wake afanye kazi za chama pia (wakati huo huo atakuwa ni Rais). Labda kama ikikubalika kiKatiba kuwa Rais asiwe na cheo chochote katika uongozi wa chama chake. Vinginevyo, haitakuwa rahisi kwa Rais kuwa Mwenyekiti leo (na si Rais) na kuwa Rais kesho (bila kuwa Mwenyekiti). Nadhani sio logical.

Nne, Rais Kikwete anapaswa kupanga muda wa kufanya ziara za kichama ambao utakuwa ni tofauti na ule wa ziara za kiserikali, na anapaswa kutumia ruzuku ya CCM kwa ziara za kichama, badala ya kudoea usafiri wa kiserikali halafu anakwenda kuzungumzia mambo ya CCM kama alivyofanya Pemba hivi karibuni.

Sijui kama kuna uhakika wa ruzuku inayotumika na Rais kutoka katika chama ama serikali wakati wowote anapofanya ziara zake. Vile vile, muda wote Rais atakaoutumia katika kipindi chote cha uongozi wake atakuwa ameutumia kama Rais pamoja na kofia nyingine yoyote atakayokuwa nayo. Sioni uwezekano wowote wa Rais kuwa katika majukumu yake bila kuwa Rais. Serikali ni ya chama chake (kilichoshinda uchaguzi) na hakuna linaloweza kubadilisha hilo hadi uchaguzi mwingine utakapofanyika, ama kwa mapenzi ya Mungu.

Tano, kauli ya Pinda kuwa hawezi kutoa kauli kuhusu kile alichokisema Rais Kikwete, eti kwa sababu ni mkuu wake wa kazi, ni ya upotoshaji.

Pinda kwa nafasi yake kama Waziri Mkuu, ndiye mtu wa mwisho anayepaswa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo lolote linalohusu serikali na maadili ya viongozi wake, akiwemo rais.

Nadhani kauli iliyotolewa na Rais ni Rais mwenyewe anaetakiwa kuielezea (hasa kama inaonekana kuwa na utata). Sidhani kuwa Pinda kama Waziri Mkuu anatakiwa aitolee ufafafanuzi wowote. Kama kuna swali lolote linalohusiana na kauli za Rais, nadhani ni vyema maswali yoyote yakaelekezwa kwake binafsi ama kwa ofisi yake. Sio jambo rahisi kwa PM kutoa ufafanuzi wa kauli ya Rais (kupinga ama kukubali lolote alilolisema). Nadhani hii iko wazi sana tu.
 
Miongoni mwa yalioandikwa kuwa aliwaambia Wazanzibari ni haya:

"Nasema mwaka 2010 tutatesa" "hatuna sababu ya kushindwa", maendeleo yaliofikiwa ni makubwa ninafurahi kuwa tulioyaahidi tumeyatimiza na mengine tutayatekeleza bado tunaendelea," alisema.

"Nasema mwaka 2010 tutatesa"
Si dhani kuwa neno "kutesa" ni lenye kwendana na kanuni (sharia).
Hivyo Waziri Mkuu Pinda ameonja joto la jazba akiwa kama Waziri Mkuu wa Tanzania hivi upo uwezekano wa Mh.Kikwete nae kutumia lugha ambayo haiendani na utawala wa kisheria.
 
Halafu Air Force One kwa taarifa tu kwa Sitta, mpaka press Pool wanalipia kila safari wakipanda.

Obama akienda kwenye mambo ya Democrats ni kweli atatumia Air force One lakini serikali italipwa gharama halisi ya safari na chama cha Democrats kwa safari hizo.
 
Back
Top Bottom