Spika Sitta: Kelele za Kingunge hazininyimi usingizi

Mwanakijiji,

(natumia katiba toleo la mwaka 2000, lile la mwaka 2005 ambalo lina mabadiliko makubwa sina)

Ukisoma ibara ya 38(2) unapata hoja yako ya kwamba akivunja na yeye habaki.

Ukisoma ibara ya 42(3) unaona kuwa akivunja anabaki kuendelea na kazi.

Ibara ya 42 - 3 ipo juu ya ibara ya 38-2 kwa sababu hii ya 38 imeanza na maneno bila kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii............ Masharti yanayotajwa ni yale ya 42-3.

Akivunja anabaki

Ndiyo maana tunahitaji Katiba Mpya ili kuondoa hizo contradictions, na inawezekana wameziweka makusudi ili kutuchanganya na kutudanganya sisi ambao ni layman wa sheria.
 
Masanja nawe unakosea kabisa. Kumbuka Serikali inaundwa na Rais (kwa kushauriana na Waziri Mkuu ambaye naye huteuliwa na Rais). Mtu pekee aliyepata mandate ya wananchi wote ni Rais peke yake na siyo wabunge (mmoja mmoja) wala huyo Waziri Mkuu mwenye ambaye kachaguliwa na watu chini ya 40,000. Waziri Mkuu wanapata nguvu kwa kuwa wabunge wengi ni wa chama chake (Katiba - Waziri Mkuu atatoka chama chenye wabunge wengi au Mbunge mwenye kuungwa mkono na wabunge wengi).

Hili lina ukweli kwa kiasi fulani. Lakini wote wawili (Rais na Wabunge) wanachaguliwa wakiwa na mandate tofauti kabisa na hivyo si sawa kuona kwamba mwingine mwenye mandate moja yuko juu ya mwingine kwa vile ana mandate tofauti. Rais anachaguliwa kuwa kiongozi na mtendaji mkuu wa Taifa letu na anateuliwa kusimamia na kutekeleza ilani ya chama chake kama Rais wa Jamhuri. Na pamoja na hayo anatekeleza majukumu yake anayopewa Kikatiba (siyo kichama). Hiyo ndio mandate yake.

Wabunge wanachaguliwa kuwa wawakilishi wa wananchi siyo katika kusikiliza malalamiko na matatizo yao tu au kushughulikia mambo ya kwenye majimbo yao tu bali kufanya kile ambacho pia wanapewa kikatiba kama mandate yao, yaani "kuishauri na kuisimamia serikali". Kwa maneno mengine wabunge ndio sauti ya wananchi wengi zaidi na siyo Rais!

Wananchi wanapoona mambo hayaendi wanavyotaka au matatizo kwenye uendeshaji wa serikali yao wanapomlilia Rais wanafikiria Rais ni kama Mfalme fulani hivi; Wananchi wanapaswa kuwalilia wabunge wao kwani ni wao ndio wanaweza kuihoji serikali na waziri yoyote juu ya jambo lolote lilimo ndani ya serikali, ni wao wanapitisha fedha za matumizi mbalimbali (bajeti) na ni wao ndio wanatunga sheria za kusimamia au kufuatwa na vyombo vingine. Mandate yao basi ni kubwa mno lakini ni tofauti na ile ya Rais. Na tofauti hii haifanyi mhimili mmoja kuwa juu ya mwingine; bali vyote vikifanya kazi zao sawasawa ndio nchi hujengwa na kazi hutekelezwa.


Bunge likitioa maazimio sio amri kwa Serikali. Serikali inaweza kusema sitekelezi na Bunge linachoweza kufanya na kura ya kutokua na imani. BASI.

Bunge likitoa amri kwa serikali au maagizo kwa serikali; serikali inatakiwa kukataa au kukubali. Ikikataa Bunge linapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali hiyo kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani Waziri Mkuu na kumlazimisha kujiuzulu (na kuvunja baraza la mawaziri). Kama serikali haitaki kutekeleza yanayoamriwa na Bunge basi serikali inapoteza uhalali wake kwani hatuwezi kuwa na serikali isiyowatii wananchi wake (kumbuke Bunge ndio wawakilishi wa wananchi na madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi)!

Tukikubali kuwa serikali inaweza kusema "sitekelezi" tunakubali jambo hatari sana. Leo Bunge linapitisha bajeti ya kutenga bilioni 100 kwa ajili ya mradi wa nishati. Serikali inasema "hatutaki" tutatumia bilioni hizo 100 kujenga madampo ya kuoeshea mifugo. Bunge linakubali kuwa serikali imekataa maagizo ya Bunge, basi Bunge nalo linapoteza uhalali wake kwani linakuwa limeshindwa "kuisimamia" serikali.

Hivyo, sikubali kabisa hii dhana kuwa serikali inaweza kulikatalia Bunge madaraka yake na ikabakia kuwa serikali halali kwani siku serikali ikikataa kusimamiwa na Bunge basi tumeruhusu utawala wa Kiimla.

Sisi tunavyoenda na commentaries ni kana kwamba Bunge linaweza kuilazimisha serikali itende itakacho. Hapana.

Absolutely! Na limepewa njia za kufanya hivyo.

a. Serikali ikikataa wanaweza kupigiwa kura ya kutokuwa na imani, WAziri Mkuu na baraza wanavunjika lakini Bunge na Rais bado wapo

b. Wanaweza kumuita Waziri yeyote na kumhoji jambo lolote lililo chini yake

c. Kujadilii utekelezaji wa kila Wizara wakati wa kikao cha bajeti; kumbuka Bunge ndio wawakilishi wa wananchi hivyo sisi wananchi kupitia wawakilishi wetu tunauliza, vipi kuhusu barabara fulani, vipi kuhusu mpango fulani n.k Serikali haiwezi kukataa kutoa maelezo. Tukikubali hilo tumekwisha!

d. Kujadili na kuidhinisha (yaani sisi wananchi ndio tunakubali) mpango "wowote" wa serikali na siyo tu hilo bali pia kuutengea fedha na kuundia sheria. Rais hana madaraka hayo; hayo ni madaraka yetu wananchi. Tukikubali kuwa serikali inaweza kujitekelezea mpango wake au kuendelea na mpango uliokataliwa na Bunge halafu ikabakia kuwa serikali tukwishnei!

e. Kuridhia mikataba yote ya serikali na hapo ina maana "mapatano yoyote ya mkataba ambayo mmojawapo wa walioshiriki ni Serikali ya
Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi Zanzibar au Idara
yoyote ya Serikali hiyo au mtumishi yeyote wa Serikali aliyeshiriki
kwa niaba ya Serikali."

Hii ina maana Bunge lilikuwa na haki ya kupitia Mikataba ya Richmond, kama vile lilivyo na haki ya kupitia wa Dowans, Rites, n.k na kuiridhia ikibidi. Na Bunge likisema "serikali vunjeni mkataba huu" serikali haiwezi kusema "hatuvunji" na ikabakia madarakani! Ikifanya hivyo, the parliament has become obsolete and inherently irrelevant.

Mwenye mandate ya kwenda nchi nzima kusema niliwaahidi hili na nimefanya au sikufanya ni Rais peke yake.

Si kweli. Lipo Bunge moja tu nalo linaitwa "Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" hakuna Bunge la Urambo, Bunge la Kigoma Kaskazini au Bunge la Igunga. Hivyo, Bunge nalo lina mandate ya kitaifa kama vile Rais alivyo na mandate yake. Kufikiria kuwa Rais ndiye mwenye mandate ya kitaifa na nyinyi wengine you have parochial mandate ni hatari kwa demokrasia. Wabunge wetu japo wanatoka katika vyama, majimbo na wanaingia tofauti wanaitwa ni "Wabunge wa Jamhuri ya Muungano"!
Spika atarudi Urambo, Zitto Kigoma Kaskazini, Hamad Rashid Wawi etc.

Ndio lakini hawarudi kwenye vibunge vyao huko; na wakirudi bila ya kupigania haki yao ya kusimamia serikali na kuilazimisha serikali kwa njia za kikatiba, wanastahili kubakia huko huko Urambo, Kigoma Kaskazini na Wawi, wasirudi tena Dodoma; hawastahiili.
Hii ni serikali dhaifu tu, Mkapa angesema hapana na ingekuwa HAPANA.

Kama Mkapa naye angeruhusiwa kusema "hapana" kwa vile ni "Mkapa" basi tumekwisha! Madaraka na haki ya Bunge hayategemei nani Rais. Rais angeweza kuwa Malaika Jibrili lakini akiapa kulinda na kuhifadhi Katiba yetu atapimwa kwa kipimo kile kile!

Role ya Bunge katika Richmond ilipaswa kuisha pale Serikali ilipoanguka.

Hapana. Bunge lilitoa melekezo ya Kamati yake (soma haki, madaraka na kinga ya Bunge).. na serikali ilitakiwa kutii. Kilichotakiwa baada ya Lowassa kujiuzulu ni kutekelezwa maazimio yote na wala tusingefika hapa. Pinda ndiye aliyekoroga alipofikiri anaisaidia nchi kwa kuanzisha uchunguzi wake mwenyewe na kufanya vitu ambavyo Bunge halikuagiza. Kwa maneno mengine aliamua kulidharau Bunge (sisi wananchi!). Serikali haiwezi kutudharau wananchi na ikabakia madarakani.

Whenever there is a showdown between the rulers and the people; the people must always rule supreme. Because sovereignty belongs to the people not to the president or prime minister.


Kitendo cha sisi wabunge kuendelea kufuatilia kita backlash lazima maana ukisoma tena ile ripoti kuna siasa nyingi sana mle na kazi haikwisha.

then jadilini Bungeni, toaneni ngeu, na mrarueni; msiogopane. Kama kazi haijaisha au kina Mwakyembe waliboronga ni Bunge tu lina uwezo wa kutengua maamuzi yake siyo? so.. go ahead tengueni yaliyofanywa na kina Mwakyembe, pigeni kura kumrestore Lowassa na kuipa Richmond haki yake. Tutaheshimu uamuzi wenu.


Mfano - kwa nini leo Mwakyembe anasema gazeti la Matanzania watwambie Richmond ni nani. Tulimlipa 438m tshs ili atwambie hivyo.

well.. mkabeni Koo Mwakyembe juu ya hilo.. ndio maana ya kuwa wawakilishi wetu. Jenga hoja Bungeni, pigeni kura hata ikibidi kumng'oa spika lakini Katiba lazima iheshimiwa hata kama ina matobo kuliko ya mapakacha.

Kwa nini Mwakyembe alisema kuna mambo hawakusema ili kuficha aibu ya serikali?

Kama haya waliyoyasema yameshaiabisha hivi hayo mengine si tutaitisha mapinduzi. Lakini, kama wabunge mnaweza kupitia tena maamuzi ya Richmond na kutengeneza kilichoharibiwa na kama kina Mwakyembe walivunja taratibu au sheria ya Bunge, Bunge linaweza kuwaadhibu. Sielewi kinachongojewa ni nini? mnawaogopa hawa kina Mwakyembe?


Kwa nini kwenye vikao vya CCM na wabunge mwakyembe anasema wanaomtetea Lowasa waache maana yakifunuka mengine Lowasa atafungwa jela!

Labda kuna ukweli; Na believe me wanaopush kumsafisha Lowassa they have no idea what is in store for them. Siku moja yatakapotokea kuna watu watawashukuru kina Mwakyembe kwa kutokusababisha wao kuishia Jela. Lakini kama watu wanaamini kuwa Mwakyembe na timu yake wana vitu hawajavisema basi wawalazimishe hata mahakamani au Bungeni kufanya hivyo au wao ndio wapelekwe jela!


Kama Lowasa aliiba mahala pake ni Jela tu na sio pengine. Kwa nini kina mwakyembe walificha na katika ripoti yao walisema "PM APIME"

oh well.. walimpa ushauri wa kuamua kujitetea au kuondoka. Yeye baada ya kupima akaona haya maji mazito akajiuzulu. Well.. siyo kosa la Kamati Teule kuwa Lowassa aliamua kujiuzulu kwa kashfa.

Ukitulia na kuangalia mambo ya nchi yetu kwa jicho la 'objectivity', utachanganyikiwa tu! hatuchanganyikiwi kwa sababu hivi sasa uchambuzi wetu umeegemea makambi na prejudices. When we come back to senses, tutasema ahaaa

Kuna ukweli mkubwa sana hapo.
 
Hivi ni nani ambaye ana uwezo wa kuanzisha mjadala wa mabadiliko ya katiba, ni Bunge au Serikali? Je, ni kitu gani kinaweza kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba? Ni ipi nafasi ya wananchi katika mchakato huu?
 
Jamani hasira za kingunge ni pamoja na kunjang'anywa hiyo stend ya ubungo. hivi kwa nini wananchi wasiandamane kupinga uongozi wa Rais kikwete kama wafanyavyo nchi nyingine?

Mkuu Major,

Mbona unasema wananchi wasiandamane? Wewe unajiweka wapi? Si wewe nawe ni mwananchi?!!!! Mimi nafikiri ungesema kwa nini wananchi tusiandamane!!!!! Hint: Polisi haitatoa kibali cha hayo maandamano!!!

Tiba
 
Katiba inasemaje hapo? Katika sifa za kupoteza Urais kuna kuvuliwa uanachama wa chama?

Well, Katiba inasema kuwa mgombea Urais atakuwa ni mtu aliyependekezwa na chama cha siasa. Na 38:2(c) inasema kuwa nafasi yake itakuwa wazi kwa sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni "baada ya Rais kupoteza sifa za kushika nafasi madaraka ya kuchaguliwa;" which in this case ni kuwa mwanachama. So akipoteza unachama wa chama chake hawezi kuendelea kuwa Rais!
 

- Mkulu Bongolander, maneno mazito sana hayo, Tanzania hatujawahi kuwa na separation of power, Msekwa alijaribu sana kulitenganisha bunge na Ikulu, lakini walipomgundua wakaanza kumpa nafasi kamati kuu, wakamfanya kuwa watatu on the line kwenye urais, na wakampa sana kukaimu urais enzi zile Mkapa na Shein wanapishana Airport wakibadili ndege za kwenda nje na kabla hajashituka wakamtupa nje ya uspika,

- Akaingia Sitta, ambaye kwanza walikuwa pamoja na Mtandao baadaye akaona upuuuzi wao umezidi kipimo, akaanza kutaka kutenganisha bunge na Ikulu ndio huyu sasa wamemkaba kooni, Judicila naomba hiyo msiitaje kabisa maana ni kama haipo, huwa tunaisikia pale tu jaji mkuu ana-retire, anarusha maneno mengi ya ki-coward of how much alikuwa kiingiliwa na Bunge na Ikulu, blah! blah! wanampa kamati ya kula na pensheni nzito basi yameisha, hakuna cha separation of power wala nothing.

- Tukishaona wazungu wamekuja toka nje kufuatilia hela zao wanazotupa za misaada ndio tunaanza kujidai na sisi tuna three branches of government, three branches my foot!


FMeS!


Mkulu, Yaani hata kukupa Thanks haitoshi.

Haya ni mawe tupu!

Yaani mkuu, I dont think anybody could say it better than this!

Ubarikiwe sana.
 
Hivi ni nani ambaye ana uwezo wa kuanzisha mjadala wa mabadiliko ya katiba, ni Bunge au Serikali? Je, ni kitu gani kinaweza kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba? Ni ipi nafasi ya wananchi katika mchakato huu?


Mkuu wenye huo uwezo ni sisi wananchi. Period.

Hivi mnafikiria mabadiliko yataletwa na nani? Unategemea serikali iondoe status quo wakati ndo inafaidi?

Narudi..wananchi tusipoamka, basi we should get ready for the long night! Na ndo dhana tuliyonayo...kudhani kwamba CCM itafanya hiki wala kile...duh!

Kikwete anasema kilimo kwanza. Masanja nasema hivi: Mapinduzi ya fikra kwanza!!
 
Hili lina ukweli kwa kiasi fulani. Lakini wote wawili (Rais na Wabunge) wanachaguliwa wakiwa na mandate tofauti kabisa na hivyo si sawa kuona kwamba mwingine mwenye mandate moja yuko juu ya mwingine kwa vile ana mandate tofauti. Rais anachaguliwa kuwa kiongozi na mtendaji mkuu wa Taifa letu na anateuliwa kusimamia na kutekeleza ilani ya chama chake kama Rais wa Jamhuri. Na pamoja na hayo anatekeleza majukumu yake anayopewa Kikatiba (siyo kichama). Hiyo ndio mandate yake.

Wabunge wanachaguliwa kuwa wawakilishi wa wananchi siyo katika kusikiliza malalamiko na matatizo yao tu au kushughulikia mambo ya kwenye majimbo yao tu bali kufanya kile ambacho pia wanapewa kikatiba kama mandate yao, yaani "kuishauri na kuisimamia serikali". Kwa maneno mengine wabunge ndio sauti ya wananchi wengi zaidi na siyo Rais!

Wananchi wanapoona mambo hayaendi wanavyotaka au matatizo kwenye uendeshaji wa serikali yao wanapomlilia Rais wanafikiria Rais ni kama Mfalme fulani hivi; Wananchi wanapaswa kuwalilia wabunge wao kwani ni wao ndio wanaweza kuihoji serikali na waziri yoyote juu ya jambo lolote lilimo ndani ya serikali, ni wao wanapitisha fedha za matumizi mbalimbali (bajeti) na ni wao ndio wanatunga sheria za kusimamia au kufuatwa na vyombo vingine. Mandate yao basi ni kubwa mno lakini ni tofauti na ile ya Rais. Na tofauti hii haifanyi mhimili mmoja kuwa juu ya mwingine; bali vyote vikifanya kazi zao sawasawa ndio nchi hujengwa na kazi hutekelezwa.




Bunge likitoa amri kwa serikali au maagizo kwa serikali; serikali inatakiwa kukataa au kukubali. Ikikataa Bunge linapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali hiyo kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani Waziri Mkuu na kumlazimisha kujiuzulu (na kuvunja baraza la mawaziri). Kama serikali haitaki kutekeleza yanayoamriwa na Bunge basi serikali inapoteza uhalali wake kwani hatuwezi kuwa na serikali isiyowatii wananchi wake (kumbuke Bunge ndio wawakilishi wa wananchi na madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi)!

Tukikubali kuwa serikali inaweza kusema "sitekelezi" tunakubali jambo hatari sana. Leo Bunge linapitisha bajeti ya kutenga bilioni 100 kwa ajili ya mradi wa nishati. Serikali inasema "hatutaki" tutatumia bilioni hizo 100 kujenga madampo ya kuoeshea mifugo. Bunge linakubali kuwa serikali imekataa maagizo ya Bunge, basi Bunge nalo linapoteza uhalali wake kwani linakuwa limeshindwa "kuisimamia" serikali.

Hivyo, sikubali kabisa hii dhana kuwa serikali inaweza kulikatalia Bunge madaraka yake na ikabakia kuwa serikali halali kwani siku serikali ikikataa kusimamiwa na Bunge basi tumeruhusu utawala wa Kiimla.



Absolutely! Na limepewa njia za kufanya hivyo.

a. Serikali ikikataa wanaweza kupigiwa kura ya kutokuwa na imani, WAziri Mkuu na baraza wanavunjika lakini Bunge na Rais bado wapo

b. Wanaweza kumuita Waziri yeyote na kumhoji jambo lolote lililo chini yake

c. Kujadilii utekelezaji wa kila Wizara wakati wa kikao cha bajeti; kumbuka Bunge ndio wawakilishi wa wananchi hivyo sisi wananchi kupitia wawakilishi wetu tunauliza, vipi kuhusu barabara fulani, vipi kuhusu mpango fulani n.k Serikali haiwezi kukataa kutoa maelezo. Tukikubali hilo tumekwisha!

d. Kujadili na kuidhinisha (yaani sisi wananchi ndio tunakubali) mpango "wowote" wa serikali na siyo tu hilo bali pia kuutengea fedha na kuundia sheria. Rais hana madaraka hayo; hayo ni madaraka yetu wananchi. Tukikubali kuwa serikali inaweza kujitekelezea mpango wake au kuendelea na mpango uliokataliwa na Bunge halafu ikabakia kuwa serikali tukwishnei!

e. Kuridhia mikataba yote ya serikali na hapo ina maana "mapatano yoyote ya mkataba ambayo mmojawapo wa walioshiriki ni Serikali ya
Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi Zanzibar au Idara
yoyote ya Serikali hiyo au mtumishi yeyote wa Serikali aliyeshiriki
kwa niaba ya Serikali."

Hii ina maana Bunge lilikuwa na haki ya kupitia Mikataba ya Richmond, kama vile lilivyo na haki ya kupitia wa Dowans, Rites, n.k na kuiridhia ikibidi. Na Bunge likisema "serikali vunjeni mkataba huu" serikali haiwezi kusema "hatuvunji" na ikabakia madarakani! Ikifanya hivyo, the parliament has become obsolete and inherently irrelevant.



Si kweli. Lipo Bunge moja tu nalo linaitwa "Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" hakuna Bunge la Urambo, Bunge la Kigoma Kaskazini au Bunge la Igunga. Hivyo, Bunge nalo lina mandate ya kitaifa kama vile Rais alivyo na mandate yake. Kufikiria kuwa Rais ndiye mwenye mandate ya kitaifa na nyinyi wengine you have parochial mandate ni hatari kwa demokrasia. Wabunge wetu japo wanatoka katika vyama, majimbo na wanaingia tofauti wanaitwa ni "Wabunge wa Jamhuri ya Muungano"!


Ndio lakini hawarudi kwenye vibunge vyao huko; na wakirudi bila ya kupigania haki yao ya kusimamia serikali na kuilazimisha serikali kwa njia za kikatiba, wanastahili kubakia huko huko Urambo, Kigoma Kaskazini na Wawi, wasirudi tena Dodoma; hawastahiili.


Kama Mkapa naye angeruhusiwa kusema "hapana" kwa vile ni "Mkapa" basi tumekwisha! Madaraka na haki ya Bunge hayategemei nani Rais. Rais angeweza kuwa Malaika Jibrili lakini akiapa kulinda na kuhifadhi Katiba yetu atapimwa kwa kipimo kile kile!



Hapana. Bunge lilitoa melekezo ya Kamati yake (soma haki, madaraka na kinga ya Bunge).. na serikali ilitakiwa kutii. Kilichotakiwa baada ya Lowassa kujiuzulu ni kutekelezwa maazimio yote na wala tusingefika hapa. Pinda ndiye aliyekoroga alipofikiri anaisaidia nchi kwa kuanzisha uchunguzi wake mwenyewe na kufanya vitu ambavyo Bunge halikuagiza. Kwa maneno mengine aliamua kulidharau Bunge (sisi wananchi!). Serikali haiwezi kutudharau wananchi na ikabakia madarakani.

Whenever there is a showdown between the rulers and the people; the people must always rule supreme. Because sovereignty belongs to the people not to the president or prime minister.




then jadilini Bungeni, toaneni ngeu, na mrarueni; msiogopane. Kama kazi haijaisha au kina Mwakyembe waliboronga ni Bunge tu lina uwezo wa kutengua maamuzi yake siyo? so.. go ahead tengueni yaliyofanywa na kina Mwakyembe, pigeni kura kumrestore Lowassa na kuipa Richmond haki yake. Tutaheshimu uamuzi wenu.




well.. mkabeni Koo Mwakyembe juu ya hilo.. ndio maana ya kuwa wawakilishi wetu. Jenga hoja Bungeni, pigeni kura hata ikibidi kumng'oa spika lakini Katiba lazima iheshimiwa hata kama ina matobo kuliko ya mapakacha.



Kama haya waliyoyasema yameshaiabisha hivi hayo mengine si tutaitisha mapinduzi. Lakini, kama wabunge mnaweza kupitia tena maamuzi ya Richmond na kutengeneza kilichoharibiwa na kama kina Mwakyembe walivunja taratibu au sheria ya Bunge, Bunge linaweza kuwaadhibu. Sielewi kinachongojewa ni nini? mnawaogopa hawa kina Mwakyembe?




Labda kuna ukweli; Na believe me wanaopush kumsafisha Lowassa they have no idea what is in store for them. Siku moja yatakapotokea kuna watu watawashukuru kina Mwakyembe kwa kutokusababisha wao kuishia Jela. Lakini kama watu wanaamini kuwa Mwakyembe na timu yake wana vitu hawajavisema basi wawalazimishe hata mahakamani au Bungeni kufanya hivyo au wao ndio wapelekwe jela!




oh well.. walimpa ushauri wa kuamua kujitetea au kuondoka. Yeye baada ya kupima akaona haya maji mazito akajiuzulu. Well.. siyo kosa la Kamati Teule kuwa Lowassa aliamua kujiuzulu kwa kashfa.



Kuna ukweli mkubwa sana hapo.

Great!

Kuna masuala kadhaa sikubaliani nayo. Hii inatokana na approach tofauti ambazo tumechukua. Wewe unajibu swali la 'what ought to be' na mimi najibu swali la 'what is'
 
Hawa wazee wameongea mambo yao huko ndani ya vikao vyao, kwa nini wanajibizana kwenye magazeti? Hekima imewaishia kabisa?

Mkuu Zitto,

Waswahili usema, penye udhia penyeza rupia. Busara wameweka kando kila mtu sasa anapigana kivyake na huo ndio mwanzo wa kusambaratika kwa CCM. Na kama JK aliunda kamati ya Mwinyi akitarajia imsaidie, amegonga mwamba kwani maelezo yanayotolewa kwenye hiyo kamati halafu yanawekwa hadharani namna hii, yanaongeza ukubwa wa ufa badala ya kuupunguza. Tutarajie mengi zaidi.

Tiba
 
Kaka, chukua katika soma sura ya Bunge. Halafu soma sura ya Rais. Tanzania kikatiba haina Rais wa mpito. Akivunja Bunge anabaki kuwa Rais mpaka Rais mpya atakapoapishwa. Anabaki na mamlaka yale yale kana kwamba hakuna lililotokea.

Naelewa hilo lakini maana yake ni kwamba uchaguzi mkuu unapoitwa nafasi ya Urais nayo inagombewa pia na yeye asipogombea haina maana ataendelea kuwa na nafasi yake kwa sababu kiufundi aliipoteza Bunge lilipovunjwa. Bunge likivunjika Rais anaendelea kuwa madarakani kwa masharti yale yale ya kawaida ya uvunjaji wa Bunge kwamba ataendelea kuwa Rais hadi RAis mpya atakapoapishwa. Lakini haina maana Bunge litakapokutana aliyekuwa Rais ambaye hakugombea Uchaguzi naye anaendelea kuwa RAis!


Watungaji wa katiba yetu waliitunga katika hali ya kuhakikisha kuwa hakutakuwa na ombwe. Mfano chukua Rais anapofariki, hatangazwi mpaka atangazwe na Rais (unaipata hiyo? Makamu anaapa kwanza kuwa Rais kisha ndiyo anatangaza kuwa Rais (aliyekuwapo kafariki).

I'm not sure about this one. Where did you get this?


Niliwahi kuandika humu JF kuwa Rais ana kofia mbili tofauti zenye majukumu mawili tofauti na yamefafanuliwa na katiba.

  1. Rais kama Mkuu wa nchi
  2. Rais kama Mkuu wa Serikali
Kama Mkuu wa Serikali hayupo juu ya Bunge.
Kama Mkuu wa nchi, yupo juu ya Bunge.

Sijaona mahali popote kwenye Katiba yetu ambapo Mkuu wa Nchi amewekwa kuwa ni juu ya Bunge. Naomba unisaidie. I'm probably missing something here.

I'm attaching Katiba toleo la 2005.
 

Attachments

  • Tanzaniaconst-eng.pdf
    345.7 KB · Views: 45
Great!

Kuna masuala kadhaa sikubaliani nayo. Hii inatokana na approach tofauti ambazo tumechukua. Wewe unajibu swali la 'what ought to be' na mimi najibu swali la 'what is'

I beg to differ.. I know I'm writing what actually is, and you are writing what seems to be! LOL
 
Naona ndot za m'kijiji zinaanza kutimia moja baada ya lingine...mungu akutie nguvu kaka utonyeshe utabiri zaidi ya huu unaoendelea..
 
.
Mh.zito,
Tunakushukuru sana kwa ufafanuzi wako mzee.
Tatizo kubwa hapa ndani ni ushabiki.
Mwanakijiji ni mshabiki sana wa akina mwakyembe pasipokuwajua wao ni akina nan.Ukiangalia post zake kwa Lowasa ni majembe tu.Lakini hajawahi kusema kuwa ile kamati ya Mwayembe ilijaa siasa na wivu na uroho wa madaraka.

Halafu kitu kingine hapa.Ni kwamba kila anachoandika mwanakijiji basi wana jf wanaona ni sawa ata kama ni pumba.

Mkuu Samwel,

Si kweli kwamba kila anachoandika MMKJ watu wanaona ni sawa. Mara ngapi watu wametofautiana naye kimawazo? Lakini tufike mahali tukubali kwamba MMKJ huwa aandiki bila kufanya utafiti wa kutosha na ndio maana anaweza kuandika article ukashindwa umkosoe wapi!!!

Tiba
 
mkuu samwel,

si kweli kwamba kila anachoandika mmkj watu wanaona ni sawa. Mara ngapi watu wametofautiana naye kimawazo? Lakini tufike mahali tukubali kwamba mmkj huwa aandiki bila kufanya utafiti wa kutosha na ndio maana anaweza kuandika article ukashindwa umkosoe wapi!!!

Tiba

mkuu tiba

si swala la kushangaza hata yesu alisema nabii aaheshimiki nyumbani kwake...na ndio maana hutomwona m'kijiji akijibizana na hoja kama hizi
 
Mkuu Samwel,

Si kweli kwamba kila anachoandika MMKJ watu wanaona ni sawa. Mara ngapi watu wametofautiana naye kimawazo? Lakini tufike mahali tukubali kwamba MMKJ huwa aandiki bila kufanya utafiti wa kutosha na ndio maana anaweza kuandika article ukashindwa umkosoe wapi!!!

Tiba

Huyo Samwel bado ana hasira kibao dhidi ya wote waliosababisha Lowasa ateme U-PM (akiwemo mwanakijiji).
 
Mkuu Samwel,

Si kweli kwamba kila anachoandika MMKJ watu wanaona ni sawa. Mara ngapi watu wametofautiana naye kimawazo? Lakini tufike mahali tukubali kwamba MMKJ huwa aandiki bila kufanya utafiti wa kutosha na ndio maana anaweza kuandika article ukashindwa umkosoe wapi!!!

Tiba


Baelezee mkuu!

Kama kuna kitu Mwanakijiji ameki-master katika maisha yake....He (sorry kama ni she) knows how to build arguments. Haweki hoj kama hajaifanyia utafiti.

Kwa hili tujifunze, tusione aibu. Elimu haina mwisho.
 
Hili lina ukweli kwa kiasi fulani. Lakini wote wawili (Rais na Wabunge) wanachaguliwa wakiwa na mandate tofauti kabisa na hivyo si sawa kuona kwamba mwingine mwenye mandate moja yuko juu ya mwingine kwa vile ana mandate tofauti. Rais anachaguliwa kuwa kiongozi na mtendaji mkuu wa Taifa letu na anateuliwa kusimamia na kutekeleza ilani ya chama chake kama Rais wa Jamhuri. Na pamoja na hayo anatekeleza majukumu yake anayopewa Kikatiba (siyo kichama). Hiyo ndio mandate yake.

Wabunge wanachaguliwa kuwa wawakilishi wa wananchi siyo katika kusikiliza malalamiko na matatizo yao tu au kushughulikia mambo ya kwenye majimbo yao tu bali kufanya kile ambacho pia wanapewa kikatiba kama mandate yao, yaani "kuishauri na kuisimamia serikali". Kwa maneno mengine wabunge ndio sauti ya wananchi wengi zaidi na siyo Rais!

Wananchi wanapoona mambo hayaendi wanavyotaka au matatizo kwenye uendeshaji wa serikali yao wanapomlilia Rais wanafikiria Rais ni kama Mfalme fulani hivi; Wananchi wanapaswa kuwalilia wabunge wao kwani ni wao ndio wanaweza kuihoji serikali na waziri yoyote juu ya jambo lolote lilimo ndani ya serikali, ni wao wanapitisha fedha za matumizi mbalimbali (bajeti) na ni wao ndio wanatunga sheria za kusimamia au kufuatwa na vyombo vingine. Mandate yao basi ni kubwa mno lakini ni tofauti na ile ya Rais. Na tofauti hii haifanyi mhimili mmoja kuwa juu ya mwingine; bali vyote vikifanya kazi zao sawasawa ndio nchi hujengwa na kazi hutekelezwa.

Rais anapotekeleza mamlaka yake kama mkuu wa nchi ni DOLA na sio mhimili wa dola. Yeye mwenyewe Rais ni dola. Rais anakuwa mhimili pale tu anapotekeleza mamlaka yake kama Mkuu wa Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu.

Bunge likitoa amri kwa serikali au maagizo kwa serikali; serikali inatakiwa kukataa au kukubali. Ikikataa Bunge linapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali hiyo kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani Waziri Mkuu na kumlazimisha kujiuzulu (na kuvunja baraza la mawaziri). Kama serikali haitaki kutekeleza yanayoamriwa na Bunge basi serikali inapoteza uhalali wake kwani hatuwezi kuwa na serikali isiyowatii wananchi wake (kumbuke Bunge ndio wawakilishi wa wananchi na madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi)!

This is what ought to....... Bunge letu halina mamlaka ya kutoa amri wala kuiagiza Serikali (what is). Bunge limepewa mamlaka ya kikatiba kuishauri Serikali (ibara ya 63) na KUISIMAMIA serikali. Katika katiba ya Kiingereza neno hili limeandikwa 'to oversee'. Hivyo Bunge halina mamlaka yeyote ya kutoa amri, kuagiza wala kuelekeza.

Tukikubali kuwa serikali inaweza kusema "sitekelezi" tunakubali jambo hatari sana. Leo Bunge linapitisha bajeti ya kutenga bilioni 100 kwa ajili ya mradi wa nishati. Serikali inasema "hatutaki" tutatumia bilioni hizo 100 kujenga madampo ya kuoeshea mifugo. Bunge linakubali kuwa serikali imekataa maagizo ya Bunge, basi Bunge nalo linapoteza uhalali wake kwani linakuwa limeshindwa "kuisimamia" serikali.

Mfano huu hauendani na mjadala. Bajeti imewekewa taratibu za kisheria za utekelezaji wake (public finance act and appropriation acts). hivyo mfano wako hapa sio penyewe.

Serikali inaweza kukataa agizo la Bunge iwapo Bunge likisema toa 100bn kwenye dampo na weka kwenye nishati. Serikali inaweza kusema sitaki na Bunge halitafanya kitu. Katika mchezo wa siasa, Bunge litasubiri shughuli za serikali nalo kusema hatutekelezi shughuli zenu. Huu ndio utaratibu ambao ulikuwa unatumika sana Ulaya ambapo mabunge yalikuwa yanagomea miswada ya Serikali mpaka serikali itekeleze mambo yao.

Bunge la Tanzania hutumia njia hii kwenye masuala ya maslahi ya wabunge tu. Njia hii ingetumika katika Richmond tungekuwa tumemaliza sinema hii mapema sana.

Hivyo, sikubali kabisa hii dhana kuwa serikali inaweza kulikatalia Bunge madaraka yake na ikabakia kuwa serikali halali kwani siku serikali ikikataa kusimamiwa na Bunge basi tumeruhusu utawala wa Kiimla.

Unatafsiri vibaya neno kusimamiwa. Hakuna serikali inayoweza kukataa kusimamiwa kwani ni jukumu la Bunge kikatiba. Kusimamia sio kuamrisha wala kuagiza. Ninaamini walioandika katiba walichagua sana maneno maana neno hili ni dhaifu sana (the weakest - oversee?). Serikali ya Tanzania inaweza kulikatalia Bunge ushauri wake na Bunge lisiwe na la kufanya maana hata kura ya kutokuwa na imani ina taratibu zake na lazima iwe hoja mahususi. Hoja mahususi haiwezi kuwa ' wamekataa ushauri wetu, basi hatuna imani. Itagonga mwamba maana lazima AG atataka tafsiri ya mahakama.

Absolutely! Na limepewa njia za kufanya hivyo.

a. Serikali ikikataa wanaweza kupigiwa kura ya kutokuwa na imani, WAziri Mkuu na baraza wanavunjika lakini Bunge na Rais bado wapo

b. Wanaweza kumuita Waziri yeyote na kumhoji jambo lolote lililo chini yake

c. Kujadilii utekelezaji wa kila Wizara wakati wa kikao cha bajeti; kumbuka Bunge ndio wawakilishi wa wananchi hivyo sisi wananchi kupitia wawakilishi wetu tunauliza, vipi kuhusu barabara fulani, vipi kuhusu mpango fulani n.k Serikali haiwezi kukataa kutoa maelezo. Tukikubali hilo tumekwisha!

d. Kujadili na kuidhinisha (yaani sisi wananchi ndio tunakubali) mpango "wowote" wa serikali na siyo tu hilo bali pia kuutengea fedha na kuundia sheria. Rais hana madaraka hayo; hayo ni madaraka yetu wananchi. Tukikubali kuwa serikali inaweza kujitekelezea mpango wake au kuendelea na mpango uliokataliwa na Bunge halafu ikabakia kuwa serikali tukwishnei!

e. Kuridhia mikataba yote ya serikali na hapo ina maana "mapatano yoyote ya mkataba ambayo mmojawapo wa walioshiriki ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi Zanzibar au Idara yoyote ya Serikali hiyo au mtumishi yeyote wa Serikali aliyeshiriki kwa niaba ya Serikali."

Hii ina maana Bunge lilikuwa na haki ya kupitia Mikataba ya Richmond, kama vile lilivyo na haki ya kupitia wa Dowans, Rites, n.k na kuiridhia ikibidi. Na Bunge likisema "serikali vunjeni mkataba huu" serikali haiwezi kusema "hatuvunji" na ikabakia madarakani! Ikifanya hivyo, the parliament has become obsolete and inherently irrelevant.

Katika eneo la mikataba uhalisia ni kwamba mikataba inayosemwa hapa ni mikataba kati ya nchi na nchi na sio nchi na makampuni binafsi. Serikali inapoingia mikataba na makampuni binafsi, kwa mujibu wa sheria za kimataifa haingii kama dola bali kama kampuni binafsi na unapotokea mgogoro unashughulikiwa hivyo hivyo. Ni Tanzania inc. na Barrick inc etc. Tunapenda iwe vinginevyo, lakini hali halisi ndiyo hii.

Tunapojifariji kwa kutafsiri Katiba tupendavyo sisi, tunajishoot wenyewe maana lazima tutakosea mkakati. Bunge kikatiba haliwezi kuiambia serikali vunja mkataba huu na serikali ikaufyata. Hakuna mandate hiyo katika katiba ya sasa.

Mikataba ambayo Bunge lina mandate nayo ni ile inayohusu dola nyingine na inahitaji kuridhiwa na Bunge. Kenya hata Bunge haliridhii kwani ratification mwisho wake ni Baraza la Mawaziri.

Si kweli. Lipo Bunge moja tu nalo linaitwa "Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" hakuna Bunge la Urambo, Bunge la Kigoma Kaskazini au Bunge la Igunga. Hivyo, Bunge nalo lina mandate ya kitaifa kama vile Rais alivyo na mandate yake. Kufikiria kuwa Rais ndiye mwenye mandate ya kitaifa na nyinyi wengine you have parochial mandate ni hatari kwa demokrasia. Wabunge wetu japo wanatoka katika vyama, majimbo na wanaingia tofauti wanaitwa ni "Wabunge wa Jamhuri ya Muungano"!


Nakubaliana nawe kuwa Bunge ni Moja tu isipokuwa wabunge wanatoka majimbo tofauti tofauti. Kwa mfumo wetu wa utawala kuna kitu kinaitwa three line whip - Binafsi, Jimbo na Chama kilichokuingiza Bungeni. Ajenda ya Taifa inabebwa na chama chako na kwa Tanzania inabebwa na Rais aliyechaguliwa na chama chako. Mengine yote ni nadharia.

Watanzania wanapopiga kura, tofauti na Uingereza au Canada kwa mfano, hawachagui Serikali bali wanachagua mtu mmoja kulibeba Taifa (Rais) na mtu mmoja mmoja kutoka kila jimbo kwenda katika Baraza la kutunga sheria na kumsimamia Rais. Humo ndio Rais anaunda Serikali. Ni mtu mmoja tu kwa mujibu wa katiba yetu mwenye mandate ya Watanzania wote - RAIS. Mengine yote nadharia!

Ndio lakini hawarudi kwenye vibunge vyao huko; na wakirudi bila ya kupigania haki yao ya kusimamia serikali na kuilazimisha serikali kwa njia za kikatiba, wanastahili kubakia huko huko Urambo, Kigoma Kaskazini na Wawi, wasirudi tena Dodoma; hawastahiili.

Majimbo ni mfumo tu ujue, ni mahala pa kupitia tu ili kwenda Dodoma. Tungeweza kuamua kutumia mfumo wa Uwiano wala usingekuwa na majimbo. Tunaingiza vipi kina Slaa, Mwakyembe, Killimbah, Sijapata Nkayamba Bungeni ni suala la mfumo tu na ndio maana nchi tofauti zina mifumo tofauti. Fundamentally kwa mfumo wetu tulionao sasa jimbo ni chama cha siasa!

Kama Mkapa naye angeruhusiwa kusema "hapana" kwa vile ni "Mkapa" basi tumekwisha! Madaraka na haki ya Bunge hayategemei nani Rais. Rais angeweza kuwa Malaika Jibrili lakini akiapa kulinda na kuhifadhi Katiba yetu atapimwa kwa kipimo kile kile!

Agreed.

Hapana. Bunge lilitoa melekezo ya Kamati yake (soma haki, madaraka na kinga ya Bunge).. na serikali ilitakiwa kutii. Kilichotakiwa baada ya Lowassa kujiuzulu ni kutekelezwa maazimio yote na wala tusingefika hapa. Pinda ndiye aliyekoroga alipofikiri anaisaidia nchi kwa kuanzisha uchunguzi wake mwenyewe na kufanya vitu ambavyo Bunge halikuagiza. Kwa maneno mengine aliamua kulidharau Bunge (sisi wananchi!). Serikali haiwezi kutudharau wananchi na ikabakia madarakani.

Whenever there is a showdown between the rulers and the people; the people must always rule supreme. Because sovereignty belongs to the people not to the president or prime minister.


Narudia Bunge letu halina mandate ya kutoa maelekezo kwa serikali.


Nimejaribu kujibu ndani ya maelezo yako. Mjadala uendelee
 
Rais ni sehemu ya Bunge kwa kusaini miswada kuwa sheria. Akikataa kusaini, amekataa. Nchi nyingine Bunge laweza kupitisha na kum over rule Rais. Kwetu hapana. Bado yupo juu ya Bunge constitutionally
Zitto sijakuelewa hapa, labda umeeleza kwenye post zingine. Ninavyoelewa ni kuwa kama Mswadaumekataliwa kuasiniwa na Rais utarudihwa tena bungeni kujadiliwa na kufanyiwa marekebisho, na kama wabunge wa tabaki na msimamo wao ule ule wa kutokuubadirisha mswaada wakaupeleka tena kwa rais kusianiwa ili iwe sheria na rais akaukataa kama itatokea Rais akaukataa mswaada mara mbili basi hakuna mjadala either of the two inatakiwa vitokee, Rais ajiuzuru na serikali yake, au Bunge kuvunjwa na uchaguzi mkuu kufanywa.

Kwa hiyo kusema kuwa Rais akikataa mswada then Bunge halina namna nadhani sio sahihi, labda kama sijakuelewa.
 
Back
Top Bottom