Spika Sitta: Kelele za Kingunge hazininyimi usingizi

Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.

Chief,

With due respect. You better revisit your constitutional law class!

Otherwise, ukiamua kufanya uchambuzi wa issues kama hizi itabidi uwe makini. Si kwamba wote humu ni vilaza wa hilo darasa la Westminster. By far, our parliament in Tanzania is no where in exercising the powers of the parliament as espoused by the Westminister model. Kifupi ni kwamba Sitta is doing ambacho Msekwa na waliomtangulia ingebidi wawe wamefanya. Lakini kwa vile Msekwa na waliomtangulia walikuwa stalwarts wa CCM, ndo leo tunamuona Sitta kwamba anaingilia uhuru wa mihimili mingine. HE IS SIMPLY DOING WHAT HE SUPPOSED TO DO. KULIWEZESHA BUNGE KUISIMAMIA SERIKALI.Kitu ambacho kiko kwenye katiba yetu.

Hivi kweli Mkuu Pasco, kwa akili yako mkuu..unaweza kushika computer yako na kuandika kwamba Serikali haikutekeleza maamuzi ya bunge kwa vile "iliona hawana hatia wahusika". Really? kwa lugha nyingine kutekeleza yale maazimio ilikuwa ni OPTION YA serikali? C`on brother. Surely you can do better. Maana nakuaminia kichwa chako.

In all, Kingunge et al..wanakimbia vivuli vyao. Wanataka status quo. Maana hawajazoea kuwajibishwa. And precisely hicho ndo kinatuumiza nchi zetu za dunia ya nne. Viongozi wamezoea kuendesha nchi kama kampuni binafsi..akitokea mtu akataka kufuata sheria-tena zilizokwenye vitabu vyetu. Mwanzo wengi tunakuwa hostile kwa watu kama hao.
again I say, Kingunge, perhaps hajui nini maana ya Westmnister model. After all alisoma elimu ya ukomunisti, kwa hiyo simlaumu.

Tuendelee kuelimishana,

Masanja
 
Ndugu yuo got it very wrong, Speaker hawezi kupingana na mahakama?
hilo lazima ulielewe tena saana, hukumu yoyote inayotolewa na mahakama ni halali mpaka itakapotenguliwa na mahakama au mamlaka ya juu zaidi wenye mandate ya kufanya hivyo. mfano hili la Zombe hata Raisi kaliongelea lakini haimanishi anapingana na mahakama bali ni mtu kuona au kuzania haki haijatendeka.
Sasa ukija mazungumzo yaani vitu vilivyo nje ya ukumbi wa bunge au mahakama havina authority yoyote. Mfano Dr Sengondo Mvungi anapoongelea kitu, mimi au wewe au hata Jaji mkuu ikiwa ni nje ya eneo la mahakama litabaki ni neno au ushauri nk ambao yoyote yule anaweza kukubaliana nao au kutokubaliana nao. na ndio maana hata leo hii Raisi anaweza sema kitu, lakini wengine wakakipinga. Au AG anaweza kuwa na muono tofauti wa jambo la kisheria na mwanasheria mwingine hata awe Jaji Mkuu, lakini wakiingia mahakamani final say ni ya Judge.
Inabidi utofautishe mambo yanayo ongeleawa na watu kwenye semina, barabarani, warsha, kongamano, kwenye forums, blog nk na kile kinachoongelewa kwenye sehemu mahususi.
Mfano watu wanaona kwenye kesi ya Zombe haki haikutendeke, hizo zitaitwa kelele mpaka pale mahakama ya Juu au mamlaka zingine zitakapo liongelea suala hilo ndani ya mipaka yao.
Hili la serikali na Bunge bado serikali haijapeleka utekelezaji wake, hivyo huwezi kupinga kitu ambacho hakipo, ndio maana hata unapotaka kukata rufaa ni lazima uwe na uamuzi wa mahakama sau mwenendo wa kesi .
na zaidi ya hapo si suala la Sitta kupinga au kukubali, bali hiyo report inatakiwa iwasilishwe na serikali kwa kamati husika na kusomwa bunge ili wabunge waridhie au la.

Let me put in the right perspective kumsaidia Pasco

Jaji Mkuu alilalamika mbele ya Spika Sitta na Rais Kikwete kuwa Bunge limekuwa likiingilia uhuru wa mahakama kwa kuamua mambo kimahakama na hata kutumia Bunge kulalamikia maamuzi ya mahakama (kesi ya mafuta Morogoro). Sitta akaja Bungeni na kutoa jibu rasmi kwa Jaji Mkuu na kuisigina vibaya sana Mahakama. Jaji Mkuu alisemea kwenye sherehe, Spika akajibia kwenye mimbari ya Bunge!!!!!!!

Hata hivyo Pasco, zingatia jambo moja. Kuna vacuum. Palipo na vacuum lazima pajazwe. Sitta anajaza hilo ombwe. Ili azijaze mihimili mingine ifanye kazi yake sawa sawa
 
Chief,

With due respect. You better revisit your constitutional law class!

Otherwise, ukiamua kufanya uchambuzi wa issues kama hizi itabidi uwe makini. Si kwamba wote humu ni vilaza wa hilo darasa la Westminster. By far, our parliament in Tanzania is no where in exercising the powers of the parliament as espoused by the Westminister model. Kifupi ni kwamba Sitta is doing ambacho Msekwa na waliomtangulia ingebidi wawe wamefanya. Lakini kwa vile Msekwa na waliomtangulia walikuwa stalwarts wa CCM, ndo leo tunamuona Sitta kwamba anaingilia uhuru wa mihimili mingine. HE IS SIMPLY DOING WHAT HE SUPPOSED TO DO. KULIWEZESHA BUNGE KUISIMAMIA SERIKALI.Kitu ambacho kiko kwenye katiba yetu.

Hivi kweli Mkuu Pasco, kwa akili yako mkuu..unaweza kushika computer yako na kuandika kwamba Serikali haikutekeleza maamuzi ya bunge kwa vile "iliona hawana hatia wahusika". Really? kwa lugha nyingine kutekeleza yale maazimio ilikuwa ni OPTION YA serikali? C`on brother. Surely you can do better. Maana nakuaminia kichwa chako.

In all, Kingunge et al..wanakimbia vivuli vyao. Wanataka status quo. Maana hawajazoea kuwajibishwa. And precisely hicho ndo kinatuumiza nchi zetu za dunia ya nne. Viongozi wamezoea kuendesha nchi kama kampuni binafsi..akitokea mtu akataka kufuata sheria-tena zilizokwenye vitabu vyetu. Mwanzo wengi tunakuwa hostile kwa watu kama hao.
again I say, Kingunge, perhaps hajui nini maana ya Westmnister model. After all alisoma elimu ya ukomunisti, kwa hiyo simlaumu.

Tuendelee kuelimishana,

Masanja

Masanja nawe unakosea kabisa. Kumbuka Serikali inaundwa na Rais (kwa kushauriana na Waziri Mkuu ambaye naye huteuliwa na Rais). Mtu pekee aliyepata mandate ya wananchi wote ni Rais peke yake na siyo wabunge (mmoja mmoja) wala huyo Waziri Mkuu mwenye ambaye kachaguliwa na watu chini ya 40,000. Waziri Mkuu wanapata nguvu kwa kuwa wabunge wengi ni wa chama chake (Katiba - Waziri Mkuu atatoka chama chenye wabunge wengi au Mbunge mwenye kuungwa mkono na wabunge wengi).

Bunge likitioa maazimio sio amri kwa Serikali. Serikali inaweza kusema sitekelezi na Bunge linachoweza kufanya na kura ya kutokua na imani. BASI.

Sisi tunavyoenda na commentaries ni kana kwamba Bunge linaweza kuilazimisha serikali itende itakacho. Hapana. Mwenye mandate ya kwenda nchi nzima kusema niliwaahidi hili na nimefanya au sikufanya ni Rais peke yake. Spika atarudi Urambo, Zitto Kigoma Kaskazini, Hamad Rashid Wawi etc.

Hii ni serikali dhaifu tu, Mkapa angesema hapana na ingekuwa HAPANA.

Role ya Bunge katika Richmond ilipaswa kuisha pale Serikali ilipoanguka. Kitendo cha sisi wabunge kuendelea kufuatilia kita backlash lazima maana ukisoma tena ile ripoti kuna siasa nyingi sana mle na kazi haikwisha.

Mfano - kwa nini leo Mwakyembe anasema gazeti la Matanzania watwambie Richmond ni nani. Tulimlipa 438m tshs ili atwambie hivyo.

Kwa nini Mwakyembe alisema kuna mambo hawakusema ili kuficha aibu ya serikali?

Kwa nini kwenye vikao vya CCM na wabunge mwakyembe anasema wanaomtetea Lowasa waache maana yakifunuka mengine Lowasa atafungwa jela!

Kama Lowasa aliiba mahala pake ni Jela tu na sio pengine. Kwa nini kina mwakyembe walificha na katika ripoti yao walisema "PM APIME"

Ukitulia na kuangalia mambo ya nchi yetu kwa jicho la 'objectivity', utachanganyikiwa tu! hatuchanganyikiwi kwa sababu hivi sasa uchambuzi wetu umeegemea makambi na prejudices. When we come back to senses, tutasema ahaaa
 
Hawa wazee wameongea mambo yao huko ndani ya vikao vyao, kwa nini wanajibizana kwenye magazeti? Hekima imewaishia kabisa?

Ukiona hivyo maana yake ni kwamba vikao haviheshimiwi tena ama havina maana yoyote. Pia inaweza kuwa ni dalili kwamba watu wakisemea kwenye vikao vya ndani kuna wengine hoja zao hazisikilizwi, the best option ni kufyatukia kwenye magzeti.

Hiyo ni dalili tosha kwamba Chama hakina uongozi, ama uongozi uliopo ni weak, hivyo umeshindwa kusimamia taratibu/kanuni/sheria za Chama. Kila mtu anafyatuka kivyake kupitia vyombo vya habari.

Mpaka hapo sioni umuhimu wa kuwafukuza waandishi wa habari kwenye hivyo vikao vya CCM. Maana kila kilichojadiliwa kinakuwa reported kana kwamba mwandishi alikuwa ni mmoja wa waliohudhuria kikao hicho. Kinachobadilika ni namna wanavyoripoti chanzo cha habari.
 
Ukiona hivyo maana yake ni kwamba vikao haviheshimiwi tena ama havina maana yoyote. Pia inaweza kuwa ni dalili kwamba watu wakisemea kwenye vikao vya ndani kuna wengine hoja zao hazisikilizwi, the best option ni kufyatukia kwenye magzeti.

Hiyo ni dalili tosha kwamba Chama hakina uongozi, ama uongozi uliopo ni weak, hivyo umeshindwa kusimamia taratibu/kanuni/sheria za Chama. Kila mtu anafyatuka kivyake kupitia vyombo vya habari.

Mpaka hapo sioni umuhimu wa kuwafukuza waandishi wa habari kwenye hivyo vikao vya CCM. Maana kila kilichojadiliwa kinakuwa reported kana kwamba mwandishi alikuwa ni mmoja wa waliohudhuria kikao hicho. Kinachobadilika ni namna wanavyoripoti chanzo cha habari.

Nikumegee kidogo.

Kinachotokea ni kwamba hawa jamaa hawaaminiani kabisa kabisa. Hivyo, kila kundi lina magazeti yake kutokana na wamiliki. wakiwa ndani ya kikao wanapiga simu kwa wahariri wa magazeti yao au waandishi wao na simu zinakuwa wazi wanasikia kila kitu kisha ndio hizo habari tunazosoma. Wenyewe wanasema wanawahiana ili kila kundi liwe na mwono wake kwa umma.

Tunachosoma kimsingi kinategemea gazeti lipo upande gani na nani chanzo cha habari. Na sisi kwa kiu ya habari tunaamini. Ukweli ni kwamba tunalishwa spin za orientation ya gazeti na chanzo cha habari.

Suluhisho ni wao kupasuka maana kila kundi lina sifa ya kuwa chama

CCM - Sitta

Mwenyekiti: Samwel Sitta
Katibu Mkuu: Harrison Mwakyembe
MKT-UWT: Beatrice Shelukindo
Mfadhili: Reginald Mengi (nyangumi)
Media: IPP Media - Nipashe, ITV etc na Majira (NICOL owns Majira)

CCM - Lowasa

Mwenyekiti: Edward Lowasa
Katibu Mkuu: Makongoro Mahanga
MKT-UWT: Sophia Simba
Mfadhili: Rostam Aziz (papa)
Media: Habari Corp - Mtanzania, Channel ten
 
Masanja,

Mimi sio mwanasheria lakini kwa model ya UK, serikali kupuuza maazimio ya bunge ni kitu kinachowezekana na kuna mifano mingi.

Sisemi serikali ya TZ ilikuwa sahihi kupuuza maazimio ya bunge kuhusu Richmond, ninachosema kama wanatumia model ya UK kama ulivyosema basi wana uwezo huo.

Wakipuuza ushauri wa wabaunge, serikali kwa maana ya chama tawala kinawajibika kwa wananchi. Wananchi ndio watawauliza mbona mlikiuka hili na lile? Vinginevyo bunge linaweza kupiga kura ya kumwondoa waziri mkuu.

Mara nyingi tu kamati za bunge zimependekeza kiongozi fulani awe fired lakini serikali ikaamua kufanya tofauti.

Kama nilivyosema sio mwanasheria lakini ninajua na kuona jinsi seperation of power inavyofanya kazi hapa UK na jinsi ambavyo hivyo vyombo vitatu haviingiliani.


Chief,

With due respect. You better revisit your constitutional law class!

Otherwise, ukiamua kufanya uchambuzi wa issues kama hizi itabidi uwe makini. Si kwamba wote humu ni vilaza wa hilo darasa la Westminster. By far, our parliament in Tanzania is no where in exercising the powers of the parliament as espoused by the Westminister model. Kifupi ni kwamba Sitta is doing ambacho Msekwa na waliomtangulia ingebidi wawe wamefanya. Lakini kwa vile Msekwa na waliomtangulia walikuwa stalwarts wa CCM, ndo leo tunamuona Sitta kwamba anaingilia uhuru wa mihimili mingine. HE IS SIMPLY DOING WHAT HE SUPPOSED TO DO. KULIWEZESHA BUNGE KUISIMAMIA SERIKALI.Kitu ambacho kiko kwenye katiba yetu.

Hivi kweli Mkuu Pasco, kwa akili yako mkuu..unaweza kushika computer yako na kuandika kwamba Serikali haikutekeleza maamuzi ya bunge kwa vile "iliona hawana hatia wahusika". Really? kwa lugha nyingine kutekeleza yale maazimio ilikuwa ni OPTION YA serikali? C`on brother. Surely you can do better. Maana nakuaminia kichwa chako.

In all, Kingunge et al..wanakimbia vivuli vyao. Wanataka status quo. Maana hawajazoea kuwajibishwa. And precisely hicho ndo kinatuumiza nchi zetu za dunia ya nne. Viongozi wamezoea kuendesha nchi kama kampuni binafsi..akitokea mtu akataka kufuata sheria-tena zilizokwenye vitabu vyetu. Mwanzo wengi tunakuwa hostile kwa watu kama hao.
again I say, Kingunge, perhaps hajui nini maana ya Westmnister model. After all alisoma elimu ya ukomunisti, kwa hiyo simlaumu.

Tuendelee kuelimishana,

Masanja
 
Masanja nawe unakosea kabisa. Kumbuka Serikali inaundwa na Rais (kwa kushauriana na Waziri Mkuu ambaye naye huteuliwa na Rais). Mtu pekee aliyepata mandate ya wananchi wote ni Rais peke yake na siyo wabunge (mmoja mmoja) wala huyo Waziri Mkuu mwenye ambaye kachaguliwa na watu chini ya 40,000. Waziri Mkuu wanapata nguvu kwa kuwa wabunge wengi ni wa chama chake (Katiba - Waziri Mkuu atatoka chama chenye wabunge wengi au Mbunge mwenye kuungwa mkono na wabunge wengi).

Bunge likitioa maazimio sio amri kwa Serikali. Serikali inaweza kusema sitekelezi na Bunge linachoweza kufanya na kura ya kutokua na imani. BASI.

Sisi tunavyoenda na commentaries ni kana kwamba Bunge linaweza kuilazimisha serikali itende itakacho. Hapana. Mwenye mandate ya kwenda nchi nzima kusema niliwaahidi hili na nimefanya au sikufanya ni Rais peke yake. Spika atarudi Urambo, Zitto Kigoma Kaskazini, Hamad Rashid Wawi etc.

Hii ni serikali dhaifu tu, Mkapa angesema hapana na ingekuwa HAPANA.

Role ya Bunge katika Richmond ilipaswa kuisha pale Serikali ilipoanguka. Kitendo cha sisi wabunge kuendelea kufuatilia kita backlash lazima maana ukisoma tena ile ripoti kuna siasa nyingi sana mle na kazi haikwisha.

Mfano - kwa nini leo Mwakyembe anasema gazeti la Matanzania watwambie Richmond ni nani. Tulimlipa 438m tshs ili atwambie hivyo.

Kwa nini Mwakyembe alisema kuna mambo hawakusema ili kuficha aibu ya serikali?

Kwa nini kwenye vikao vya CCM na wabunge mwakyembe anasema wanaomtetea Lowasa waache maana yakifunuka mengine Lowasa atafungwa jela!

Kama Lowasa aliiba mahala pake ni Jela tu na sio pengine. Kwa nini kina mwakyembe walificha na katika ripoti yao walisema "PM APIME"

Ukitulia na kuangalia mambo ya nchi yetu kwa jicho la 'objectivity', utachanganyikiwa tu! hatuchanganyikiwi kwa sababu hivi sasa uchambuzi wetu umeegemea makambi na prejudices. When we come back to senses, tutasema ahaaa

Mheshimiwa Zitto,

We are on the same wevelength. Ninachojaribu kupingana na mkuu Pasco na Kingunge ni hii ya kufanya madude mabovu harafu kujificha kwenye Westminsiter model. Mkuu sina mda lakini hapa ningejaribu kui-construe hiyo model kukuonyesha kwamba akina Kingunge et al. hawana hoja. Tatizo la mabunge yetu..yameshakuwa reduced kuwa kamati za chama. NDO MAANA MBUNGE ANAOGOPA KUULIZWA SWALI..KWA SABABU ANAJUA HATA KAMA YUKO POPULAR..CHAMA KINAWEZA KUMKATAA. Sasa mkuu hii demokrasia tuliiga wapi?

Umeongea swala makini kwamba Raisi ana mandate ya wananchi wote. alkini hebu nikukumbushe kitu. Ni kwa kujua dhahiri kwamba wananchi wote hatuwezi kumuwajibisha Kikwete ndo maana tukachagua na wabunge kusudi tuwape madaraka ya kumuwajibisha rais pale atakapokosea. Thats exactly the role of parliament in any democratic society. Sasa leo huwezi sema kwamba kama bunge limeiamrisha serikali kufanya kitu..Rais atakataa simply because na yeye ana mandate ya wananchi. Perhapas tusiende mbali..chukulia mfano wa katiba ya Uganda (nina imani umeisha isoma). Na ile katiba ni hiyo hiyo..iliyorithiwa pale Westminster. Lakini uiangalia harafu uniambie kwamba bunge letu linafikia hata nusu ya lile bunge kwa kuisimamia serikali. (perennial problem inakuwa pale bunge linapobadilika na kuwa NRM Committee).

Sasa issue yako mkuu, inapingana na hii dhana kwa sababu una assume kwamba kwa vile Rais ana mandate ya wananchi..akikosea tutamuwajibisha kwenye sanduku la kura. This is wrong and no where it has ever worked. Itakuwaje asipogombea tena? As MP you know better. Sasa kama wabunge wameiambia serikali ifanye kitu. Ni kama sisi wananchi tumemwambia Kikwete afanye hivyo. Yes, unaweza kusema kwamba na yeye ana mandate, alkini ndo maana tunasheria na tumeweka wazi kwamba bunge litaisimimamia serikali. Because we know kwamba RAISA HAYUKO INFALLIBLE. He can always make wrong decisions.

Again, I agree na wewe kwamba over all, kwenye nchi yetu kuna madudu mengi sana ambayo yanakwenda deep kuliko tunavyoona hapa.

Kikubwa tunahitaji watu kama wakina Sitta (despite their dirty linens in their closet) waulize some hard questions. Tutaanzia hapo na si kujificha kwenye model za wakoloni za miaka hiyo...eti Westminister.


Masanja
 
Mheshimiwa Zitto,

We are on the same wevelength. Ninachojaribu kupingana na mkuu Pasco na Kingunge ni hii ya kufanya madude mabovu harafu kujificha kwenye Westminsiter model. Mkuu sina mda lakini hapa ningejaribu kui-construe hiyo model kukuonyesha kwamba akina Kingunge et al. hawana hoja. Tatizo la mabunge yetu..yameshakuwa reduced kuwa kamati za chama. NDO MAANA MBUNGE ANAOGOPA KUULIZWA SWALI..KWA SABABU ANAJUA HATA KAMA YUKO POPULAR..CHAMA KINAWEZA KUMKATAA. Sasa mkuu hii demokrasia tuliiga wapi?

Umeongea swala makini kwamba Raisi ana mandate ya wananchi wote. alkini hebu nikukumbushe kitu. Ni kwa kujua dhahiri kwamba wananchi wote hatuwezi kumuwajibisha Kikwete ndo maana tukachagua na wabunge kusudi tuwape madaraka ya kumuwajibisha rais pale atakapokosea. Thats exactly the role of parliament in any democratic society. Sasa leo huwezi sema kwamba kama bunge limeiamrisha serikali kufanya kitu..Rais atakataa simply because na yeye ana mandate ya wananchi. Perhapas tusiende mbali..chukulia mfano wa katiba ya Uganda (nina imani umeisha isoma). Na ile katiba ni hiyo hiyo..iliyorithiwa pale Westminster. Lakini uiangalia harafu uniambie kwamba bunge letu linafikia hata nusu ya lile bunge kwa kuisimamia serikali. (perennial problem inakuwa pale bunge linapobadilika na kuwa NRM Committee).

Sasa issue yako mkuu, inapingana na hii dhana kwa sababu una assume kwamba kwa vile Rais ana mandate ya wananchi..akikosea tutamuwajibisha kwenye sanduku la kura. This is wrong and no where it has ever worked. Itakuwaje asipogombea tena? As MP you know better. Sasa kama wabunge wameiambia serikali ifanye kitu. Ni kama sisi wananchi tumemwambia Kikwete afanye hivyo. Yes, unaweza kusema kwamba na yeye ana mandate, alkini ndo maana tunasheria na tumeweka wazi kwamba bunge litaisimimamia serikali. Because we know kwamba RAISA HAYUKO INFALLIBLE. He can always make wrong decisions.

Again, I agree na wewe kwamba over all, kwenye nchi yetu kuna madudu mengi sana ambayo yanakwenda deep kuliko tunavyoona hapa.

Kikubwa tunahitaji watu kama wakina Sitta (despite their dirty linens in their closet) waulize some hard questions. Tutaanzia hapo na si kujificha kwenye model za wakoloni za miaka hiyo...eti Westminister.


Masanja


Kaka nakuelewa kabisa. Tujadili hoja hii kwa kumtoa Sitta na Kingunge ili tuwe objective.

Ibara ya 63 ya katiba - kushauri na kusimamia! Ushauri ukikataliwa na unayemshauri na unaamini kuwa ni ushauri bora, unatangaza kuwa huyu hashauriki. Hivyo, unamtoa na kwenda kwenye uchaguzi mwingine. Kama hutaki kumtoa, unaendelea naye mpaka uchaguzi ulio kwenye ratiba kwa mujibu wa katiba na kelele zinaishia hapo.

Bunge kama mwakilishi wa wananchi kwa kupitia mbunge mmoja mmoja nguvu yetu ni kura ya kutokuwa na imani na Rais.

Jambo kubwa la kuzingatia hapa ni kwamba KATIBA ndio ipo juu ya kila kitu (constitutional supremacy) na hakuna mhimili ulio juu ya mhimili mwingine. Sisi wabunge tuna hangover ya Parliamentary supremacy!

Kina Kingunge wao wanahangover ya Party supremacy
 
Suluhisho ni wao kupasuka maana kila kundi lina sifa ya kuwa chama

CCM - Sitta

Mwenyekiti: Samwel Sitta
Katibu Mkuu: Harrison Mwakyembe
MKT-UWT: Beatrice Shelukindo
Mfadhili: Reginald Mengi (nyangumi)
Media: IPP Media - Nipashe, ITV etc na Majira (NICOL owns Majira)

CCM - Lowasa

Mwenyekiti: Edward Lowasa
Katibu Mkuu: Makongoro Mahanga
MKT-UWT: Sophia Simba
Mfadhili: Rostam Aziz (papa)
Media: Habari Corp - Mtanzania, Channel ten

Poor JK! Maana sijui hata anaangukia kundi gani?
 
Mheshimiwa Zitto,


Kikubwa tunahitaji watu kama wakina Sitta (despite their dirty linens in their closet) waulize some hard questions. Tutaanzia hapo na si kujificha kwenye model za wakoloni za miaka hiyo...eti Westminister.


Masanja

Wanauliza hizo hard questions?

Tunahitaji Bunge ambalo hakuna chama kinakuwa na zaidi ya theluthi mbili ya wabunge. Hapo utaona true wesminster model. Westminster model katika hali ya sasa ya single party dominance ni kurudi chama kimoja.
 
Jamani hasira za kingunge ni pamoja na kunjang'anywa hiyo stend ya ubungo. hivi kwa nini wananchi wasiandamane kupinga uongozi wa Rais kikwete kama wafanyavyo nchi nyingine?


Tumia neno kwa nini wananchi tusiandamane nasi kwa nini wasiandamane kwani wewe si mwananchi ?
 
Masanja nawe unakosea kabisa. Kumbuka Serikali inaundwa na Rais (kwa kushauriana na Waziri Mkuu ambaye naye huteuliwa na Rais). Mtu pekee aliyepata mandate ya wananchi wote ni Rais peke yake na siyo wabunge (mmoja mmoja) wala huyo Waziri Mkuu mwenye ambaye kachaguliwa na watu chini ya 40,000. Waziri Mkuu wanapata nguvu kwa kuwa wabunge wengi ni wa chama chake (Katiba - Waziri Mkuu atatoka chama chenye wabunge wengi au Mbunge mwenye kuungwa mkono na wabunge wengi).

Bunge likitioa maazimio sio amri kwa Serikali. Serikali inaweza kusema sitekelezi na Bunge linachoweza kufanya na kura ya kutokua na imani. BASI.

Sisi tunavyoenda na commentaries ni kana kwamba Bunge linaweza kuilazimisha serikali itende itakacho. Hapana. Mwenye mandate ya kwenda nchi nzima kusema niliwaahidi hili na nimefanya au sikufanya ni Rais peke yake. Spika atarudi Urambo, Zitto Kigoma Kaskazini, Hamad Rashid Wawi etc.

Hii ni serikali dhaifu tu, Mkapa angesema hapana na ingekuwa HAPANA.

Role ya Bunge katika Richmond ilipaswa kuisha pale Serikali ilipoanguka. Kitendo cha sisi wabunge kuendelea kufuatilia kita backlash lazima maana ukisoma tena ile ripoti kuna siasa nyingi sana mle na kazi haikwisha.

Mfano - kwa nini leo Mwakyembe anasema gazeti la Matanzania watwambie Richmond ni nani. Tulimlipa 438m tshs ili atwambie hivyo.

Kwa nini Mwakyembe alisema kuna mambo hawakusema ili kuficha aibu ya serikali?

Kwa nini kwenye vikao vya CCM na wabunge mwakyembe anasema wanaomtetea Lowasa waache maana yakifunuka mengine Lowasa atafungwa jela!

Kama Lowasa aliiba mahala pake ni Jela tu na sio pengine. Kwa nini kina mwakyembe walificha na katika ripoti yao walisema "PM APIME"

Ukitulia na kuangalia mambo ya nchi yetu kwa jicho la 'objectivity', utachanganyikiwa tu! hatuchanganyikiwi kwa sababu hivi sasa uchambuzi wetu umeegemea makambi na prejudices. When we come back to senses, tutasema ahaaa
.
Mh.zito,
Tunakushukuru sana kwa ufafanuzi wako mzee.
Tatizo kubwa hapa ndani ni ushabiki.
Mwanakijiji ni mshabiki sana wa akina mwakyembe pasipokuwajua wao ni akina nan.Ukiangalia post zake kwa Lowasa ni majembe tu.Lakini hajawahi kusema kuwa ile kamati ya Mwayembe ilijaa siasa na wivu na uroho wa madaraka.

Halafu kitu kingine hapa.Ni kwamba kila anachoandika mwanakijiji basi wana jf wanaona ni sawa ata kama ni pumba.
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.
I guess, kama huna kifafa wewe basi una kifafa cha ukoo ila kwako kiko dormant,maneno yako kuattack bunge la sasa hivi wakati linafanya kazi inayokubaliwa na wengi,ni ya kijinga tu!!!

Wewe unafurahi spika kushambuliwa kwa kufanya kazi zake vzr?? wala huoneshi kujua lolote kuhusu separation of powers!! kama ni mwandishi wa habari basi ni mwandishi koko!!! you better keep quite.
 
I guess, kama huna kifafa wewe basi una kifafa cha ukoo ila kwako kiko dormant,maneno yako kuattack bunge la sasa hivi wakati linafanya kazi inayokubaliwa na wengi,ni ya kijinga tu!!!

Wewe unafurahi spika kushambuliwa kwa kufanya kazi zake vzr?? wala huoneshi kujua lolote kuhusu separation of powers!! kama ni mwandishi wa habari basi ni mwandishi koko!!! you better keep quite.

Acheni watu wawe na uhuru wa mawazo. Mtakimbiza watu humu halafu mbaki kama chama kimoja - zidumu fikra za mwenyekiti.

Pasco anao uhuru wa mawazo yake na wala hajashambulia Bunge. Kwa nini mnakosa ngozi ngumu ya kusoma usichopenda?

Tulianzisha JF ili watanzania wapate pa kusemea bila kuogopa. Huu mwenendo wa kutovumilia mawazo ya wengine unaota mizizi sasa hapa.

Jibu hoja kwa hoja. Kama huna jibu na hoja huipendi kajifungie msalani ulieeeeeeeeeeeee, ujifute machozi urudi kukata ishu na sio kuanza kutukanana hapa.
 
hivi mechi ya the blues na mashetani ni saa ngapi?

hizi habari za siasa zinakula unit zangu!!!!
 
Acheni watu wawe na uhuru wa mawazo. Mtakimbiza watu humu halafu mbaki kama chama kimoja - zidumu fikra za mwenyekiti.

Pasco anao uhuru wa mawazo yake na wala hajashambulia Bunge. Kwa nini mnakosa ngozi ngumu ya kusoma usichopenda?

Tulianzisha JF ili watanzania wapate pa kusemea bila kuogopa. Huu mwenendo wa kutovumilia mawazo ya wengine unaota mizizi sasa hapa.

Jibu hoja kwa hoja. Kama huna jibu na hoja huipendi kajifungie msalani ulieeeeeeeeeeeee, ujifute machozi urudi kukata ishu na sio kuanza kutukanana hapa.
.
Mh.Zito hapa umesema .
hapa wanataka kila kitu ndiyo mzee.
Kila analosema sita,Ndiyo mzee.Kila akiandika Mwanakijiji ndiyo mzee?.ujinga gani huu bila kupima hoja ya mtu
 
Masanja,

Mimi sio mwanasheria lakini kwa model ya UK, serikali kupuuza maazimio ya bunge ni kitu kinachowezekana na kuna mifano mingi.

Sisemi serikali ya TZ ilikuwa sahihi kupuuza maazimio ya bunge kuhusu Richmond, ninachosema kama wanatumia model ya UK kama ulivyosema basi wana uwezo huo.

Wakipuuza ushauri wa wabaunge, serikali kwa maana ya chama tawala kinawajibika kwa wananchi. Wananchi ndio watawauliza mbona mlikiuka hili na lile? Vinginevyo bunge linaweza kupiga kura ya kumwondoa waziri mkuu.

Mara nyingi tu kamati za bunge zimependekeza kiongozi fulani awe fired lakini serikali ikaamua kufanya tofauti.

Kama nilivyosema sio mwanasheria lakini ninajua na kuona jinsi seperation of power inavyofanya kazi hapa UK na jinsi ambavyo hivyo vyombo vitatu haviingiliani.

Mkuu heshima mbele,

Mi nadhani ni vyema tuielewe hii separation of powers in context. UK nadhani ndo mfano mbovu kuliko yote when it comes to separation of powers. Mbunge ni waziri..wakati House of Lords ambao ndo chombo cha juu cha sheria kimechanganyika na wanasiasa. Infact sasa ndo mapendekezo yametolewa kui-overhaul system nzima ya siasa na mfumo wa bunge huko UK. Kwa hiyo separation of powers iko more in theoretical context kuliko reality ambayo tunaiona.

Infact tuongelee mfano wa USA ambao wao notion ya separation of powers waliikataa since the founding of their country. RATHER wanatumia checks and balance. Hutakuta mbunge ni waziri au vice versa. Ingawa hata USA nao ni common law country. LAKINI wametengeneza mfumo ambao unawasuit mazingira yao.

SASA basi kwa nchi zetu Africa, tunapenda kutumia mfumo wa UK (at least in theory)..si kwa sababu ndo tunaona unatufaa, bali kwa sababu kuna loopholes nyingi za wanasiasa kufanya wayatakayo. kama kuappoint marafiki zao na kuhakikisha wanakaa madarakani kwa kutumia mfumo wa chama ambao una reward incompetence na loyalty kuliko ufanisi wakazi. Tunaposema kwamba serikali inawajibu wa kutekeleza maamuzi ya bunge...we simply mean that the government inayofuata utawala bora inabidi ifanye hivyo. Kama Zitto alivyoelezea..serikali ikishindwa wabunge wanaweza piga kura ya kutokuwa na imani na serikali.

tatizo ni kwamba mabunge mengi epecially Africa...yamekuwa dominated na ruling parties, ambapo the governement of the day can virtually go away with any wrong. Huwezi ukafanya the same kama USA ambako kuna ushindani wa kweli.


In all, separation of powers is so much theoretical than reality reveals. Not even in Mediaval Europe ambapo wakina Mentesque waliipigania sana ikawa article of faith kwa serikali za western Europe.
 
Let me put in the right perspective kumsaidia Pasco

Jaji Mkuu alilalamika mbele ya Spika Sitta na Rais Kikwete kuwa Bunge limekuwa likiingilia uhuru wa mahakama kwa kuamua mambo kimahakama na hata kutumia Bunge kulalamikia maamuzi ya mahakama (kesi ya mafuta Morogoro). Sitta akaja Bungeni na kutoa jibu rasmi kwa Jaji Mkuu na kuisigina vibaya sana Mahakama. Jaji Mkuu alisemea kwenye sherehe, Spika akajibia kwenye mimbari ya Bunge!!!!!!!

Hata hivyo Pasco, zingatia jambo moja. Kuna vacuum. Palipo na vacuum lazima pajazwe. Sitta anajaza hilo ombwe. Ili azijaze mihimili mingine ifanye kazi yake sawa sawa

Mheshimiwa Zitto, I am very skeptical that we have anything like separation of powers in Tanzania. Three pillars that we keep on mentioning namely Bunge, Mahakama na serikali, all seem to me that are under JK, only separate in theory. Nadhani kuna kipengele kinachosema wazi kabisa kuwa Bunge linaundwa na Rais na wabunge.
NI obvious kuwa mawaziri wote ni wabunge, hapo huwezi kuwa separate.

It is only recent Bunge limeanza kuwa Bunge, na Sitta anakua mklai anapoona Mahakama haiwi mahakama na inakuwa kama ni mtekelezaji wa amri za Executive.

Kama Bunge lingekuwa independent, issue ya Richmond isingekuwa kama ilivyo sasa. Kama Mahakama ingekuwa huru, Zombe angekuwa ndani. Kama Mahakama ingekuwa huru Ditto angefika anakostahili kabla ya kifo chake, kama kungekuwa na separation of powers kusingekuwa na kitu kama IPTL, Dowans, EPA na wahalifu wote kuendelea kupeta barabarani.

We will be fooling ourselves in believing that kuna separation of powers wakati tunaona wazi kabisa kuwa individuals wanao tawala by proxy na executive wameconsolidate powers. Wabunge wengi ni kama waliingizwa kwenye viti vyao kwa hela za mtu mmoja, na huyu mtu mmoja ndio ana remote control ya wabunge, mahakimu na executives.

Pamoja na kuwa unaona kama kuna parliamentary supremacy, that is just a dream or just a wishful thinking, there is no such a thing wakati kwa muda mrefu CCM ndio imekuwa supreme, CCM ina nguvu kuliko hata bunge ndio maana hata Mzee Kingunge na hangover ya party supremacy, we all see it everyday, thanks to uelewa mdogo tulionao watanzania wengi.
 
Kwenye siasa hakuna anayeweza kuwa wa kwanza kumrushia jiwe mwanamke mwasherati. Kwa kuwa ina one way or the other huyo mwanamke mwasherati uasherati wake aliufanya na hao wanaotaka kumpiga mawe.

Sitta is no saint, Zitto is no saint, so was Nyerere, so was Mzee Karume. Lakinissue ni kuwa kuna walio evil hao ndio tatizo, hakuna anayesema kuwa Sitta ni malaika msafi asiye na doa, kama ameishi kwenye siasa za Tanzania lazima atakuwa na madoa yake, lakini hayo hayawezi kuwa kigezo cha kusema anayofanya sasa ni mabaya, au anayofanya sasa tuyapuuze kwa kuwa alimfukuza Mzee Mwinyi kwenye nyumba aliyokuwa anakaa miaka ya 80, that is ridiculous.
 
Back
Top Bottom