Spika sitta jiandae na hili wakikuchoka!!!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Thursday, April 29, 2010 1:34 AM
Ilimbidi spika wa bunge la Ukraine aombe hifadhi chini ya miamvuli kujikinga na mayai aliyokuwa akivurumishiwa na wabunge kabla ya wabunge wa chama tawala na cha upinzani hawaajaanza kurushiana makonde ndani ya bunge.
Wabunge wa bunge la Ukraine waliweka pembeni kazi ya kutunga sheria na kuanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe huku wengine wakimvurumishia spika wa bunge mvua ya mayai na nyanya.

Ngumi na vurugu hizo zilizuka ndani ya bunge la Ukraine wakati bunge lilipoidhinisha mkataba na Urusi wa kutumia bandari ya Ukraine kama bezi yake ya kijeshi hadi mwaka 2042. Mkataba huo utaifanya Ukraine iuziwe gesi na Urusi kwa bei nafuu.

Wabunge wanaopinga mkataba huo walianzisha vurugu ambayo iliisha baada ya mabomu ya moshi kurushwa ndani ya bunge.
 
ndugu mbona hujampa ujumbe wowote Spika wetu....u know this can never happen in our parliament....
 
ndugu mbona hujampa ujumbe wowote Spika wetu....u know this can never happen in our parliament....
hakuna lisilowezekana kijana kama wabunge wetu wakiendelea na mfumo wao wa kuwapuuza wananchi hili litatokea muda si mrefu
 
hakuna lisilowezekana kijana kama wabunge wetu wakiendelea na mfumo wao wa kuwapuuza wananchi hili litatokea muda si mrefu

Sidhani kwamba Wabunge wanawapuuza wananchi kiasi hicho. Kinachoendelea ni kwamba Bunge limegawanywa na wajanja (mafisadi) wachache kiasi cha kufanya lionekane halifanya kazi ipasavyo.

Sita achokwe na nani Wabunge? Na achokwe kwa kipi cha mno atakachowaudhi Wabunge hata waanze kutafuta maya viza ya kumrushia? Huo mwamko na umoja wa kuweza kufanya hivyo wabunge wetu wanao? Ndani ya mjengo ule wa Bunge ni asilimia ndogo sana ya Wabunge wanaojali Spika anafanya nini. Pale idadi kubwa wanajali nafsi zao na kipi wafanye ili wapigakura waweze kuwapa tena ubunge.
 
Mimi ningekuwepo Bungeni ile siku PM alipohoji ati kwa nini watanzania wasiende kufanya kazi kenya,mimi ningeweza kurusha hata ngumi.I hate it
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom