Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,435
- 113,444
Wanabodi,
Nimekuwa nikifuatilia kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu Pinda Bungeni leo asubuhi.
Kumeulizwa jumla ya maswali 5 tuu badala ya 10, na yote ni kutoka wabunge wa kambi ya upinzani, hivyo baada ya dakika 15 tuu, kipindi hicho cha maswali ya papo kwa papo kilimalizika kwa spika Sitta kutangaza maswali yamekwisha!.
Hivyo kikao cha bunge kiliendelea kwa kipindi cha maswali na majibu ya kawaida.
Baada ya maswali mawili matatu, Spika Sitta aliintervene na kutoa ufafanuzi ufuatao, nimeparaphrase, " Najua wengi mtashangazwa na maswali kwa Waziri Mkuu leo kuwa yote yametoka upinzani!, hili sio bunge la wapinzani ni bunge la vyama vyote. Hali kama hii haiwezi kuachwa iendelee, lazima tutafanya uchunguzi nini kilitokea maana najua Wapinzani wana hila, wanaweza kuwa wamefanya manuva fulani"!
Mhe. Sitta aliyazungumza hayo in a jocking manner, lakini ni maneno serious, kama kina Zitto, Dr. Slaa na wapinzani wengine wataiacha joke hiyo ipite tuu bila kuikemea,
huko kutakuwa ni kumdekeza spika kuendelea kuliendesha Bunge kwa manufaa ya CCM.
Kwa maoni yangu Spika amepotoka kwa kusema Wapinzani wana hila.
Kitendo pekee cha kuwepo waulizaji 5 tuu tuka upinzani, ni uthibitisho toka, waliojitokeza ndio hao tuu, ndio maana maswali yaliisha baada ya dakika 15 tuu!.
Kama kulikuwa hakuna swali toka CCM kuna ubaya gani?. Kama bunge wa CCM hawakuwa na swali, hiyo ni walakin?.
Mhe Spika anasema hili sio bunge la wapinzani, nadhani status ya wabunge ndani ya bunge ni equal regardles parties affiliation, itakuja tokea siku pia kipindi hicho hicho cha maswali na majibu, kutakuwa hakuna swali toka upinzani, its ok.
Kulikuwa na maswali mawili kutoka CUF na Matatu kutoka Chadema, eti kwa vile hakukuwa na swali toka CCM, basi ndio kuna hila, hivyo atafanya uchunguzi!
Huu ni upotokaji!.
"
Nimekuwa nikifuatilia kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu Pinda Bungeni leo asubuhi.
Kumeulizwa jumla ya maswali 5 tuu badala ya 10, na yote ni kutoka wabunge wa kambi ya upinzani, hivyo baada ya dakika 15 tuu, kipindi hicho cha maswali ya papo kwa papo kilimalizika kwa spika Sitta kutangaza maswali yamekwisha!.
Hivyo kikao cha bunge kiliendelea kwa kipindi cha maswali na majibu ya kawaida.
Baada ya maswali mawili matatu, Spika Sitta aliintervene na kutoa ufafanuzi ufuatao, nimeparaphrase, " Najua wengi mtashangazwa na maswali kwa Waziri Mkuu leo kuwa yote yametoka upinzani!, hili sio bunge la wapinzani ni bunge la vyama vyote. Hali kama hii haiwezi kuachwa iendelee, lazima tutafanya uchunguzi nini kilitokea maana najua Wapinzani wana hila, wanaweza kuwa wamefanya manuva fulani"!
Mhe. Sitta aliyazungumza hayo in a jocking manner, lakini ni maneno serious, kama kina Zitto, Dr. Slaa na wapinzani wengine wataiacha joke hiyo ipite tuu bila kuikemea,
huko kutakuwa ni kumdekeza spika kuendelea kuliendesha Bunge kwa manufaa ya CCM.
Kwa maoni yangu Spika amepotoka kwa kusema Wapinzani wana hila.
Kitendo pekee cha kuwepo waulizaji 5 tuu tuka upinzani, ni uthibitisho toka, waliojitokeza ndio hao tuu, ndio maana maswali yaliisha baada ya dakika 15 tuu!.
Kama kulikuwa hakuna swali toka CCM kuna ubaya gani?. Kama bunge wa CCM hawakuwa na swali, hiyo ni walakin?.
Mhe Spika anasema hili sio bunge la wapinzani, nadhani status ya wabunge ndani ya bunge ni equal regardles parties affiliation, itakuja tokea siku pia kipindi hicho hicho cha maswali na majibu, kutakuwa hakuna swali toka upinzani, its ok.
Kulikuwa na maswali mawili kutoka CUF na Matatu kutoka Chadema, eti kwa vile hakukuwa na swali toka CCM, basi ndio kuna hila, hivyo atafanya uchunguzi!
Huu ni upotokaji!.
"