Spika Samuel Sitta adai kutumiwa Ujumbe wa Vitisho

Kipanga

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
676
34
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel Sitta amedai kuwa kuna mtu/watu wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho kupitia simu yake ya mkononi. Akizungumza na TBC Taifa, Spika Sitta alidai kuwa ameshatoa taarifa ya jambo hilo polisi kwani hawezi kupuuzia vitisho hivyo ingawa alidai pia kuwa hao ni watu wanaokerwa na utendaji wake mzuri wa kazi.
 
Vyombo vyetu vya usalam vitapoteza muda mrefu sana kutafuta jinsi kukabiliana na suala hilo...vitisho vya sms na hata simu pia....nafikria wakajifunze kwa wenzetu na pia suala la msingi hapa ki kusajili line zote za simu ziendane na kitambulisho cha uraia.......kila kitu kiwe wazi kwenye kitambulisho....hata kama una namba 3 zote ziwekwe baada ya hapo hutakiwi kuongeza ingine.....hadi ufuate utaratibu sahiihi uliokwekwa...kuongeza au kubadili namba.........itasaidia sana
 
Skill4ever,
Nakubaliana na wewe nadhani hali iliyopo sasa ya ushindani wa kibiashara kati ya Kampuni za simu imesababisha kutokuwa na udhibiti wa utoaji wa line za simu. Siku hizi line zinauzwa kwa mafungu line 5 Sh.1,000 mtu ananunua anaweka kwenye simu anakutukana anatoa line anatupa. Kwa kweli ni hatari sana na inashangaza hata TCRA wako kimya sijui hawajui au wanashindwa nini kuzibana hizi kampuni za Simu.
 
Lakini wanao mtisha ni mafisadi hili liko wazi! Kwakeli hawa fisadi wasipopelekwa wanako stahili yaani kule segerea wata hatarisha amani ya nchi yetu!
 
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel Sitta amedai kuwa kuna mtu/watu wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho kupitia simu yake ya mkononi. Akizungumza na TBC Taifa, Spika Sitta alidai kuwa ameshatoa taarifa ya jambo hilo polisi kwani hawezi kupuuzia vitisho hivyo ingawa alidai pia kuwa hao ni watu wanaokerwa na utendaji wake mzuri wa kazi.

Nani kamwambia utendaji wake wa kazi mzuri? Hizi SMS anajitumia mwenyewe mzugaji tu huyu mzee...
 
Nani kamwambia utendaji wake wa kazi mzuri? Hizi SMS anajitumia mwenyewe mzugaji tu huyu mzee...
Masatu huna maana! Huwezi kuja na statement kama hiyo bila kufanya utafiti, tunaigeuza JF kuwa kijiwe cha waropokaji! Atajitumiaje sms hizo mwenyewe, ili iweje? Sitta ni tegemeo letu wengi tunaoipenda nchi na kuamini katika UTAWALA WA SHERIA. Waswahili hunena, aisifuye mvua, imemnyea! Naamini Masatu ana tabia hiyo ya kujiandikia mwenyewe sms, ya "kujinanihii" mwenyewe! Sitta soldier on!
 
Lakini wanao mtisha ni mafisadi hili liko wazi! Kwakeli hawa fisadi wasipopelekwa wanako stahili yaani kule segerea wata hatarisha amani ya nchi yetu!

Ninasubiri kuona nini wanategemea kumfanya huyu mzee. Hawa mafisadi tunawajua wote, tunawajua watoto wao, mali zao na mienendo yao.
Kama wataanza kufanya upumbavu wa kuwatisha watu wenye uchungu na nchi yao, basi wawe tayari kukabiliana na maafa ya hali ya juu toka kwa wananchi wenye hasira. Mafisadi wasijione wako juu ya kila kitu. Serikali inawalinda lakini nguvu za wananchi ni zaidi ya serikali. Wananchi wanaweza kujichukulia sheria mikononi na mtaona dunia chungu.
 
Nani kamwambia utendaji wake wa kazi mzuri? Hizi SMS anajitumia mwenyewe mzugaji tu huyu mzee...

Anajipigia debe mwenyewe. Kuna watu kila siku ni kulalamika wanaonewa na huenda hata hizo sms zinatumwa na wapambe wao ili kupata huruma ya wananchi, siasa mchezo mbaya.

Kama mtu ametumiwa hizo sms si apeleke polisi na kuwaachia wao? Hii ya kwenda kwenye TV kuongelea sms naona kama ni kutaka kuonewa huruma.
 
Masatu huna maana! Huwezi kuja na statement kama hiyo bila kufanya utafiti, tunaigeuza JF kuwa kijiwe cha waropokaji! Atajitumiaje sms hizo mwenyewe, ili iweje? Sitta ni tegemeo letu wengi tunaoipenda nchi na kuamini katika UTAWALA WA SHERIA. Waswahili hunena, aisifuye mvua, imemnyea! Naamini Masatu ana tabia hiyo ya kujiandikia mwenyewe sms, ya "kujinanihii" mwenyewe! Sitta soldier on!

mtindi,

Kama jina lako linavyo suggest, Huyu mzee wako ni fisadi tena fisadi kiwembe soma hii hapa chini;

Ama kweli, ukistaajabu ya Mussa, utayaona ya Firauni! Kama unadhani vigogo wa EPA ni mafisadi peke yao, basi ulikuwa hujamfahamu Spika wa Bunge SAMUEL JOHN TEGEZA SITTA ! Ukimsikiliza anapoongea unaweza kuamini kwamba kiongozi huyo wa Bunge ni msafi kutokana na umahiri wake wa kujivalisha sifa kemkem – Mr Misifa. Unakumbuka hivi karibuni alivyomtukana Naibu Spika eti hawezi kusimamia mambo nyeti mpaka awepo yeye mwenye Bunge? ! Kisa nini? Kupenda sifa na kumdhalilisha mwenzake mbele ya umma, halafu bado anaendelea kuliita Bunge eti ni chombo cha kidemokrasia!

Tumebaini kwamba Sitta amekuwa akijimiminia sifa nyingi ili kulinda ufisadi anaoufanya usigundulike katika jamii yetu. Ngoja nikupe tone tu la madhambi yake kwa umma ili uone ni hatua gani utachukua, na ili na yeye ajipime kwa nafasi yake. Angalia uchafu huu:-

- Anatumia vibaya fedha za umma. Amekuwa akitumia msaidizi wake kuchota mapesa kwa kisingizio kuwa ni masurufu ya safari za ndani na nje ya nchi. Kila safari ya siku moja ndani ya nchi huchukua shilingi Milioni tano (5,000,000/=), na kila safari ya siku moja nje ya nchi huchukua shilingi Milioni Kumi na Tano (15,000,0000/=). Ameshindwa kufanya marejesho ya masurufu (imprest) hayo, licha ya kupeleka risiti kadhaa za kughushi/za uongo kwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Bunge. Mpaka sasa anadaiwa jumla ya shilingi Milioni sitini (60,000,000/=) za masurufu.

- SITTA hupeleka risiti za uongo kwa Mhasibu Mkuu, zikionesha madai kutoka Oysterbay Pharmacy ya Shilingi Milioni Mbili ( 2,000,000/= ) aliyotumia kwa tiba kila wiki.

- Amekuwa akilazimisha hawara yake wa Hospitali ya Aga Khan naye alipwe posho kama wabunge anapokwenda naye Dodoma. Kwa mfano, hawara huyo alilipwa ‘per diem’ kuanzia tarehe 13/12/2007 hadi tarehe 31/01/2008 ( Siku 50). Huo ni Ufisadi mkubwa!

- Anaye kimada wake mwingine anayekwenda kwa jina la ASIA ambaye anaishi nyumba Na. 111 karibu na Mahakama ya Ardhi Upanga na amezaa naye. Huko mtaani kwao kimada huyo hujiita mama SITTA, na ni dada yake aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa iliyokuwa Tume ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC). Mwanamke huyo muda wote hutumia gari la Ofisi ya Bunge STK 232 Toyota RAV 4.

- Pia anaye kimada mwingine (jina limehifadhiwa) ambaye anaishi kinondoni ( Livingstone), mtaa wa Honolulu katika nyumba ya kupanga inayomilikiwa na dada yake Kawawa. Nyumba hiyo inatazamana na Nyumba Na. KH.MK/No. 337 katika mtaa huo huo. Kimada huyo hutumia gari ya kiofisi ya Spika mwenyewe STK 3002.

- Vimada wote hao hupata huduma za maji na umeme kwa gharama za Ofisi ya Bunge. Kuna kipindi mke halali wa Spika, aliwahi kulalamikia hali hiyo. Kuna siku maji yalikatika nyumbani, mke wa Spika akaomba apelekewe ‘ bowser’ la maji na Ofisi ya Bunge. Ohooo! Watekelezaji wakapeleka maji kimakosa kwa kimada. Mama Sitta akashtukia dili.

- Kuna taarifa kwamba mnamo Mwezi Oktoba 2007, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iligundua mapungufu makubwa katika matumizi ya fedha yaliyofanywa na Spika SITTA. nimedokezwa kuwa Spika aliwanyamazisha wajumbe wa kamati hiyo, ambapo aliwatishia kutowapatia posho na safari za nje kama wangeyafumua mapungufu yake hadharani! Hapo inaonesha kuwa wajumbe hao walipewa rushwa!!

- Kama JK anataka viongozi wa kisiasa na wa serikali watenganishe biashara na uongozi wa ku – ‘sacrifice’ kimojawapo, hilo litakuwa gumu kwa sababu Sitta alipokuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha cha Uwekezaji nchini (TIC) alitumia nafasi hiyo kuingia ubia na wafanyabiashara wengi wa Kigeni. Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inatambua kuwa Spika ana hisa kwenye kampuni moja ya Kichina inayosafirisha nagogo licha ya marufuku yaliyowekwa?!

- Nililokupa hapo ni tone tu.
 
mtindi,

Kama jina lako linavyo suggest, Huyu mzee wako ni fisadi tena fisadi kiwembe soma hii hapa chini;

Ama kweli, ukistaajabu ya Mussa, utayaona ya Firauni! Kama unadhani vigogo wa EPA ni mafisadi peke yao, basi ulikuwa hujamfahamu Spika wa Bunge SAMUEL JOHN TEGEZA SITTA ! Ukimsikiliza anapoongea unaweza kuamini kwamba kiongozi huyo wa Bunge ni msafi kutokana na umahiri wake wa kujivalisha sifa kemkem – Mr Misifa. Unakumbuka hivi karibuni alivyomtukana Naibu Spika eti hawezi kusimamia mambo nyeti mpaka awepo yeye mwenye Bunge? ! Kisa nini? Kupenda sifa na kumdhalilisha mwenzake mbele ya umma, halafu bado anaendelea kuliita Bunge eti ni chombo cha kidemokrasia!

- Nililokupa hapo ni tone tu.
Sita kuwa na vimada wewe inakuuma nini?, ulitaka amchukue dada yako?.
 
mtindi,

Kama jina lako linavyo suggest, Huyu mzee wako ni fisadi tena fisadi kiwembe soma hii hapa chini;

Ama kweli, ukistaajabu ya Mussa, utayaona ya Firauni! Kama unadhani vigogo wa EPA ni mafisadi peke yao, basi ulikuwa hujamfahamu Spika wa Bunge SAMUEL JOHN TEGEZA SITTA ! Ukimsikiliza anapoongea unaweza kuamini kwamba kiongozi huyo wa Bunge ni msafi kutokana na umahiri wake wa kujivalisha sifa kemkem – Mr Misifa. Unakumbuka hivi karibuni alivyomtukana Naibu Spika eti hawezi kusimamia mambo nyeti mpaka awepo yeye mwenye Bunge? ! Kisa nini? Kupenda sifa na kumdhalilisha mwenzake mbele ya umma, halafu bado anaendelea kuliita Bunge eti ni chombo cha kidemokrasia!


- Nililokupa hapo ni tone tu.
Masatu,
Hiyo makala imeandikwa na nani? Siyo fisadi mwingine?
 
Masatu,
Hiyo makala imeandikwa na nani? Siyo fisadi mwingine?

Mkuu,

Hii imekuwa katika circulation kwa miezi sasa.... author simjui mimi nimeikuta humu humu jf kulikuwa na thread ya suala hili...
 
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel Sitta amedai kuwa kuna mtu/watu wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho kupitia simu yake ya mkononi. Akizungumza na TBC Taifa, Spika Sitta alidai kuwa ameshatoa taarifa ya jambo hilo polisi kwani hawezi kupuuzia vitisho hivyo ingawa alidai pia kuwa hao ni watu wanaokerwa na utendaji wake mzuri wa kazi.

1. Ni aibu kubwa sana kwa taifa, inapofikia mahali Spika wa bunge, anakuwa reduced to this level yaani ya kulalamika kama sisi wengine wananchi wa kawaida, kwa sababu ungetegemea kiongozi wa nafasi kama yake kua analindwa vizuri sana na system yetu, sasa kama Spika analalamika kua anatishwa, sisi wananchi wa kawaida itakuwaje na hivyo vitisho, maana nilitegemea kwua simu zkae zinakuwa connected na security system kwamba ukimtumia wanaweza kuku-trace within some few minutes wakajua wewe uliyemtumia ni nani, au?

2. Six alikuwa ni mmoja wa the rock wa kundi la Mtandao, the dataz ni aliahidiwa u-Waziri Mkuu, lakini kwenye process za kampeni Lowasssa, akaibuka kuwa the most effective wa kampeni chafu na hivyo kumpiku ukaribu na muungwana na hata kupewa u-PM, ni Lowassa na Rostam ndio walioamua apewe u-Spika, ni Rostam ndiye aliyemuambia achukue fomu ya u-Spika, na ni Rostam ndiye aliyemtuma Amina RIP, kumpelea ujumbe Msekwa kuwa hatakiwi na Mtandao asichukue fomu, lakini Msekwa hakukubali akaishia kuaibika.

3. Six na Mtandao, walitumia mbinu chafu sana kumuondoa Msekwa, kwa kumtumia Mtandao mwingine Marehemu Akukweti, aliyekua naibu wake kwa muda mrefu sana, kwamba aliiba hela nyingi sana kwenye ujenzi wa bunge jipya, ambao the dataz ni kuwa Msekwa, Sumaye na Lukuvi wametengeneza hela nzuri sana na ile kampuni moja ya Ireland.

- My point hapa ni kwamba Six sio mgeni wa michezo michafu ya siasa, wakati anatumia uhuni kumtoa Msekwa, hatukusikia Msekwa akipiga kelele za wolf! wolf! kama anazopiga yeye sasa, wakati akiwatukana sana wagombea wengine behind magazeti yote ya Mtandao kwenye kampoeni za urais wengine hawakupiga kelele kama anazopiga yeye sasa.

4. Sio siri kwamba yeye sasa yuko upande wa pili wa Mtandao, kwa sababu ya kushindwa kuwalinda kama walivyotegemea wakati wanampa ile nafasi, na tayari Mtandao wameshapeleka watu wawili wa kugombea naye ubunge ili wamtoe, pia kule kwa Mwakyembe tayari hawa mafisadi wamesham-recruit dada wa RC Mwakipesile, ili amuondoe Mwakyembe, nako kwa naibu Spika pia wamesha-recruit mtu wao wa kumuondoa, the dataz ni kwamba kuna wabunge 36 ambao Mtandao waliamua kwenye kikao chao cha siri huko Morogoro ambacho kiliongozwa na Nchimbi, kwamba ni lazima waondolewe at any cost Membe pia ni included kwenye hiyo list ya 36, kwa sababu na yeye ni threat kwa urais wa 2015.

5. The dataz ni kwamba katika kikao hicho the mtarajiwa wao Mtandao wa 2010/2015 Mkulu Masha, alionywa vikali sana na wajumbe kwamba hawategemei kuja kua betrayed tena kama Muungwana alivyowafanya sasa, na akithubutu basi yatamkuta makubwa sana.

Six, aaache kupiga kelele za mbweha kila wakati katika kutafuta umaarufu na wananchi, umaarufu na wananchi ambao anautafuta sana kwa sababu za kutaka urais ataupata kwa kuchapa kazi ya wananchi. Kwanza ni lazima tuamini kwamba amejitoa completely na Mtandao, na kwamba sasa tunaweza kumuamini, lakini sio kutuchezea akili na mbinu za kitoto kama this one.
 
5. The dataz ni kwamba katika kikao hicho the mtarajiwa wa 2010/2015 Masha, alionywa vikali sana na wajumbe kwamba hawategemei kuja kwua betrayed kama Muungwana alivyowafanya sasa, na akithubutu basi yatamkuta makubwa sana.

.

Hii ni kali sana mkuu, kama anapata huyu huo urais basi huko baadae tukiyakumbukia ya muungwana JK itabidi tu tumsifu na kumwomba radhi kwa jinsi anavyosemwa sasa. Nakumbuka ule msemo wa "kila kukicha afadhali ya jana!"
 
hakuna sms wala nini. hii ni njia anatumia kujiongezea umaarufu!!!
 
But I have two questions which I would to be answered before giving out my comments,
Why these insulting messages have been sent to Sita?
Is these foolish mgs are political related or family related matter?
 
But I have two questions which I would to be answered before giving out my comments,
Why these insulting messages have been sent to Sita?
Is these foolish mgs are political related or family related matter?
 
Yangu Mimacho!!

ukistaajabu ya Sita utayajua zaidi ya Mtandao.

hadi siku wananchi tutakapotoka tulipokaa na kutetea wahalifu, tukaandamana kwa kuwapinga ndio watajua akili, lakini najiuliza ni lini? ni sisi sisi wananchi waoga tutakaoweza? maana tunawaogopa hao fisaid as if wao ni "Mungu Watu"

Tanzania weeee!
 
Nani kamwambia utendaji wake wa kazi mzuri? Hizi SMS anajitumia mwenyewe mzugaji tu huyu mzee...


Masatu,
Nakubaliana na wewe kabsaa. Mh. Sitta utendaji wake mzuri ni upi huo? Zaidi ya kusoma majina ya wageni kama vile Bunge ni send off party kuna lipi alilofanya kuiondoa nchi kwenye umasikini? EPA kimya, Richmond kimya, ziara za raisi kimya, uzembe serikalini kimya. Hivi bunge si linahitajika kuihakiki na kuishauri serikali? Ni lini walifanya hayo? Mh. Sitta ni mbabaishaji na aache kujipandishia chati.
 
Back
Top Bottom