Abunwasi
JF-Expert Member
- Jun 25, 2009
- 5,486
- 3,468
Sijui kama wana jamii walitafakari kauli ya spika jana akilalamika kuwa kuna watu wanajaribu kumchafua kupitia kwenye mitandao, magazeti na wengine kuingia jimboni kwake na kutoa zawadi kwa wapiga kura wake.
Mtanisamehe wana jamii kama ninawakwaza lakini mimi huota sana njozi za mchana na katika njozi hizi nilikuwa ninajiuliza huyu mwenye kigoda juzi juzi tu aliwaambia wanabunge kuwa katika zama hizi za demokrasia inabidi wawe na ngonzi ngumu kuweza kuhimili mikimiki ya siasa. Jee yeye hivi sasa bado ana ngozi laini?
Afadhali wenzetu hao wana jukwaa la kusikika Jee wale ambao hawanga jukwaa lakini husemwa katika jumba kuu la dodoma inakuwaje?
Hivi kusemwa kwenye mitandao na magazeti inatosha kuomba ulinzi uimarishwe kumlinda mzee?
Halafu hawa wanasiasa wetu ambao ni wabunge hivi hayo majimbo ni mali yao? Katika dahari hizi za demoghasia kila mtu ana haki ya kujiuza kwa wananchi sasa hawa wazee wanaogopa nini kama kweli wanaamini kuwa bado wanauzika kwa wananchi?
Mbona kuna mbunge amejitokeza waziwazi na kusema kwamba anatarajia kugombea urahisi mwakani lakini mzee JK ambaye kwa hivi sasa ndiyo mwenyenchi wala hakuonesha kupanick na kuweka mikwara?
Wanajamii kwa vile nilikurupushwa na mnyapara wa kazi ilibidi niamke lakini hata baada ya kuamka bado sijapata majibu pengine tafakuri zenu zinaweza kusaidia kueongeza uelewa wangu.
Mtanisamehe wana jamii kama ninawakwaza lakini mimi huota sana njozi za mchana na katika njozi hizi nilikuwa ninajiuliza huyu mwenye kigoda juzi juzi tu aliwaambia wanabunge kuwa katika zama hizi za demokrasia inabidi wawe na ngonzi ngumu kuweza kuhimili mikimiki ya siasa. Jee yeye hivi sasa bado ana ngozi laini?
Afadhali wenzetu hao wana jukwaa la kusikika Jee wale ambao hawanga jukwaa lakini husemwa katika jumba kuu la dodoma inakuwaje?
Hivi kusemwa kwenye mitandao na magazeti inatosha kuomba ulinzi uimarishwe kumlinda mzee?
Halafu hawa wanasiasa wetu ambao ni wabunge hivi hayo majimbo ni mali yao? Katika dahari hizi za demoghasia kila mtu ana haki ya kujiuza kwa wananchi sasa hawa wazee wanaogopa nini kama kweli wanaamini kuwa bado wanauzika kwa wananchi?
Mbona kuna mbunge amejitokeza waziwazi na kusema kwamba anatarajia kugombea urahisi mwakani lakini mzee JK ambaye kwa hivi sasa ndiyo mwenyenchi wala hakuonesha kupanick na kuweka mikwara?
Wanajamii kwa vile nilikurupushwa na mnyapara wa kazi ilibidi niamke lakini hata baada ya kuamka bado sijapata majibu pengine tafakuri zenu zinaweza kusaidia kueongeza uelewa wangu.