Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
na Mwanne Mashugu, Zanzibar
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, amesema tofauti za mitazamo kuhusiana na suala la uhuru wa Zanzibar, limekuwa kikwazo kikubwa na kusababisha kushindwa kufikiwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.
Spika Kificho alisema hayo jana katika kikao cha mazungumzo kilichowakutanisha viongozi wa CCM na ujumbe wa Jumuiya ya Ulaya, ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Saleh Ramadhan Ferouz, Makao Makuu ya chama hicho, Kisiwandui jana Zanzibar.
Kificho, ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alisema wakati viongozi wa CCM, wanaamini Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ndiyo yaliyoleta uhuru wa kweli kwa wananchi wanyonge wa visiwani, huku CUF wakiamini uhuru wa mwaka 1963, ambao CCM wameuona kama ni uhuru bandia katika historia ya Zanzibar.
Spika Kificho alisema hali hiyo inasababishwa na kutoaminiana na hata kama Serikali ya Umoja wa Kitaifa itafikiwa mawaziri wake watakuwa katika wakati mgumu katika utekelezaji wa majukumu yao.
Alieleza ugumu wa utekelezaji wa suala hilo, utakuwa hauna tofauti na hali ilivyojitokeza katika serikali ya umoja wa kitaifa ulioafikiwa nchini Kenya, kutokana na kutoaminiana na kuathiri ufanisi wake.
Mpango wa kuundwa serikali ya mseto Zanzibar, ulikwama baada ya viongozi wa CUF kugoma kuingia katika kura ya maoni kama ilivyokuwa imeamuliwa katika kikao cha Halmasahuri Kuu ya CCM, kilichokutana Butiama chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake, Rais Amani Abeid Karume.
Katika mazungumzo hayo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Saleh Ramadhan Ferouz, alisema nia ya CCM ni njema, ndiyo maana ikaingia katika mazungumzo na CUF, lakini mpango wa kuundwa serikali ya pamoja umekwamishwa na viongozi wa CUF.
Aliueleza ujumbe huo wa Jumuiya ya Ulaya, kutokana na uzito wa suala hilo NEC ya CCM iliamua ajenda ya suala hilo iamuliwe kwa kura ya maoni, itakayowashirikisha Wazanzibari wote ili kulinda misingi ya demokrasia na katiba ya nchi.
Hata hivyo, Ferouz alisema CCM imeridhishwa na maandalizi ya uchaguzi mdogo katika Jimbo la Magogoni na maandalizi ya kuelekea uchaguzi mkuu lakini alisema uvumilivu wa kisiasa lazima uzingatiwe na viongozi wa vyama vyote vya siasa Zanzibar, kwa kuweka masilahi mbele ya umoja wa kitaifa.
Kiongozi wa ujumbe wa EU, Tim Clarke, alisema ujumbe huo umefika Zanzibar kuangalia ustawi wa demokrasia katika kuelekea uchaguzi mkuu na tayari uchaguzi mdogo wa Jimbo la Magogoni unaotarajiwa kufanyika Mei 23, mwaka huu.
Alisema pamoja na kuwa jumuiya hiyo imeamua kuadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake hapa Zanzibar, lakini alisema wanapenda kuona maendeleo ya demokrasia yanapatikana kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, amesema tofauti za mitazamo kuhusiana na suala la uhuru wa Zanzibar, limekuwa kikwazo kikubwa na kusababisha kushindwa kufikiwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.
Spika Kificho alisema hayo jana katika kikao cha mazungumzo kilichowakutanisha viongozi wa CCM na ujumbe wa Jumuiya ya Ulaya, ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Saleh Ramadhan Ferouz, Makao Makuu ya chama hicho, Kisiwandui jana Zanzibar.
Kificho, ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alisema wakati viongozi wa CCM, wanaamini Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ndiyo yaliyoleta uhuru wa kweli kwa wananchi wanyonge wa visiwani, huku CUF wakiamini uhuru wa mwaka 1963, ambao CCM wameuona kama ni uhuru bandia katika historia ya Zanzibar.
Spika Kificho alisema hali hiyo inasababishwa na kutoaminiana na hata kama Serikali ya Umoja wa Kitaifa itafikiwa mawaziri wake watakuwa katika wakati mgumu katika utekelezaji wa majukumu yao.
Alieleza ugumu wa utekelezaji wa suala hilo, utakuwa hauna tofauti na hali ilivyojitokeza katika serikali ya umoja wa kitaifa ulioafikiwa nchini Kenya, kutokana na kutoaminiana na kuathiri ufanisi wake.
Mpango wa kuundwa serikali ya mseto Zanzibar, ulikwama baada ya viongozi wa CUF kugoma kuingia katika kura ya maoni kama ilivyokuwa imeamuliwa katika kikao cha Halmasahuri Kuu ya CCM, kilichokutana Butiama chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake, Rais Amani Abeid Karume.
Katika mazungumzo hayo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Saleh Ramadhan Ferouz, alisema nia ya CCM ni njema, ndiyo maana ikaingia katika mazungumzo na CUF, lakini mpango wa kuundwa serikali ya pamoja umekwamishwa na viongozi wa CUF.
Aliueleza ujumbe huo wa Jumuiya ya Ulaya, kutokana na uzito wa suala hilo NEC ya CCM iliamua ajenda ya suala hilo iamuliwe kwa kura ya maoni, itakayowashirikisha Wazanzibari wote ili kulinda misingi ya demokrasia na katiba ya nchi.
Hata hivyo, Ferouz alisema CCM imeridhishwa na maandalizi ya uchaguzi mdogo katika Jimbo la Magogoni na maandalizi ya kuelekea uchaguzi mkuu lakini alisema uvumilivu wa kisiasa lazima uzingatiwe na viongozi wa vyama vyote vya siasa Zanzibar, kwa kuweka masilahi mbele ya umoja wa kitaifa.
Kiongozi wa ujumbe wa EU, Tim Clarke, alisema ujumbe huo umefika Zanzibar kuangalia ustawi wa demokrasia katika kuelekea uchaguzi mkuu na tayari uchaguzi mdogo wa Jimbo la Magogoni unaotarajiwa kufanyika Mei 23, mwaka huu.
Alisema pamoja na kuwa jumuiya hiyo imeamua kuadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake hapa Zanzibar, lakini alisema wanapenda kuona maendeleo ya demokrasia yanapatikana kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.