Spika Anne Makinda, something is wrong...

Jethro

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
2,219
370
Wana JF,

Leo Jioni kutoka BUNGENI Speaker ANNA MAKINDA katika hitimisho lake akiwaambia wabunge kuwa wasipende sana kuwatajka watu wakati wakichangia hoja zao na akadai kuna mashitaka mengi sana toka humo bungeni na nje ya bunge yako kwa kamati ya maadili,

Alipo niacha hoi sana ni pale alipo sema ati wabunge wengine esp wale walio kuwa wakitaja majina ya watu ati hawatoi hata hoja "ati hawa wabunge wana wataja watu tuu hata hoja zao hatuzionii"

Nachukulia mfano mbunge wa Viti maalumu CHADEMA wa wisho kuongea alitaja wavuvi wa ziwa Tanganyika kuwa hawana usalama mzuri wanapo enda kuvu kuwa hakuna vyombo vya kulinda majini kwa kuwa ziwa hilo pia lina tumika na nchini jirani kama DRC Congo,Burundi na kuna uharamia wa hatari watu wana tekwa, Mbali na hilo mbunge huyo akasifia kazi nzuri ya Police Mkoa wa Dodoma.

Sasa sielewi Speaker anapo amka na kusema haoni hoja zinazo tolewa esp anaonyesha kabisa kuwa haipendi upinzani inapo toa hoja na kichwani kwake amejiwekea mind set kuwa upinzani always wao hoja zao ni za fujo tuuu.

Je nasi huku raia tukija na kusema speaker anna makinda huchukulia hoja za upinzani kama ni fujo na mzaha na anadhika juu ya hoja za upinzani?

My Take:

Imefika wakati Speaker wa Bunge Anna Makinda kupigia mistari maneno yake anayo lopoka humo ndani ya bunge na kama anakuwa off mood basi asiwe anaingia bungeni.

Wana JF: Ati tuna sema Nchi yetu ina mihimili 3 Serikali , Mahakama na Bunge kwa hali hii inavyoendelea kwa kutizama tuu kwa upeo wa macho kwa fikra hizi tulizo nazo tuu haiitaji uwe na Bachelor of Law toka UDSM,Mzumbe,UDOM ukweli ni kwamba muhimili ni Serikali tuu hivi vingine vitatu vipo tuu kiitetea serikali kila kukicha wabunge wanaitetea serikali mahakama wanaitetea serikali serikali inajitetea yenyewe hapo kuna kitu kweli?
 
Nimekuwa Nikimsikiliza Mama Anna Makinda akisema kwamba Watanzania Wengi wanawalaumu Wabumge "Eti" Hawazingatii Sheria. Mama Nakushangaa sana tena Sana.

Unawazungumzia Watanzania Gani?
Unawazungumzia Wana CCM ambao hawawezi Kuhoji Chochote kinachozungumzwa na Ninyi wana CCM

Leo Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu AMEKUFANYA UMEONEKANA KITUKO MBELA YA JAMII na WATANZANIA WAMEONA

Nikuulize Anne

1. Hivi Kwa Akili zako unafikiri Watanzania Jana Hawakuona Wabunge wa CCM wakizungmzia Mauaji ya Singida ( Ambayo Kesi yake Iko Mahakamani)?

2. Hivi Unafikiri kwamba Watanzania hawakukuona wewe na Mwanasheria Mkuu Mkikenua Meno wakati Mbunge wa CCM akilizungumzia Suala lililoko Mahakamani?

3. Mama Anna Naomba uwe Mkweli Naamini Kabisa Hizo SMS unazopata Nyingi ni za Kukulalamikia.

4. Wabunge wa CDM ni Watu wazima. Usitegee hata siku Moja Waheshimu Kanuni Ambazo wewe Umeshindwa Kuzimamia kwa Haki

5. Hivi Unafikri Watanzania Hawakuona Pale Mh. Lukuvi alipoomba Mwongozo juu ya Mwongozo lakini Ikawa Dhambi kwa Mheshimiwa Machali?

Wito kwa Makamanda wa Upinzani

1. Mkikubali Bunge liendeshwe Kama Akina Anna Makinda na Lukuvi na akina Mabumba wanavyotaka MMWKWISHA.

2. Kama Mheshimiwa Spika au Mwenyekiti anakosea Ni Vyema Kumweleza Wazi maana Watanzania Wanaangalia

3. Kama Spika au Naibu Spika akikutukana (Kama alivyofanya Ndugai kwa Mdee na Mnyika) Na Nyinyi Mtukaneni kwa tusi lile lile Alilowatukana. Akisema Uombe Radhi Aanze kuomba radhi yeye

Kwa Kweli Huwa Nafurahia sana Pale Mwenyekiti au Spika anapoona Kiti cha Moto (Kitu Ambacho CCM hawapendi kabisa)

Mama Anna Makinda kama Unataka Uheshimike Basi zitumie Kanuni Bila Upendeleo
 
Ingekuwa amri yake asingekubali bunge lionyeshwe live kwenye tv. Ukiona MCCM anachangia hata kama ni pumba anaachwa aseme hadi mwisho lakini kama ni wa upinzani unakuta anaanza kukatizwa hata kama hajamalizia sentensi. Mama badala ya kupata heshima unayodai unajiongezea aibu na dharau kwa wengi wanaoangalia mwenendo wa bunge. Jaribu kuwa fair katika kuongoza mojadala kuthibitisha vinginevyo.
 
CCM ilifanya makosa makubwa kumuacha Samuel Sitta (Speed and Standard!) na kutuwekea "Kituko" hiki! Kinalalamika ovyo bila kujua kinalalamikia nini, ilimradi kikwaze wapinzani.
 
Mwana Huyo mamam sasa anapoelekea ni kuzimu nawaambieni

Lukuvi na Warema leo hii nchi ikaingia machafukoni nyie ndio mtakuwa wakwanza kukama diplomatic Passport na kukimbia nchi hii wa kwanza hata kabla ya JK na Pinda maana mume kaa hapo kuwapotosha watanzania mkijua fika kuwa jahazi la CCM ndio kabisaaaa limetokota

My Take:

Kweli Samwel Sitta was threat to CCM walilijua hilo maana ingekuwa leo JK ni Chali kabisaaa hasinge tobozaa nchi inakwenda kiholela holela tuuuu.

Kweli Upeo wa kufikili hata wewe Warema AG wa serikali na kusomea sheria unashindwa kujenga hoja kweli kwelii. Hivi katika sheria hukufundishwa haki za binadamu na usawa? Au AG wewe huna ubinadamu na uzalendo wa Taifa hili mwalitaka Taifa hili liwe na mazezeta tuuu every year
 
Huyu Mama simpendi sababu moja amekubali kutumika na mafisadi kwa manufaa ya mafisadi!!ana roho mbaya sana anadhani nyinyiem itadumu milele!atashangaa watakimbia wote hao subiri tu muda waja!!!vijana wote wajipange ajili ya ubunge 2015 kutoa uozo wote uliopo mjengoni!!
 
Huyu mama ili bunge lilishamshinda Sika nyingi angekuwa na busara ange handover tuu iyo post
 
Mh sungura alitoa tuhuma za uuaji wa mwigulu labda hukuona hiyo segment! Lakini hata wa ccm hutaja watu! Bila hatua yyt
 
Spika alikuwa Mzee Sitta. Makinda na timu yake wako pale kuizika CCM. Wanafikiri wanachofanya ni kuibeba CCM lakini wasichojua ni kuwa wanawasukuma wananchi upande wa upinzani.
 
Mwigul anaharibu utulivu wa nchi hii, ccm hawaoni watakigundua itakuwa too late! He is so selfish! The boy dead comeon!
 
And some of the ccm drs kebwe and the like seems myopic! Cant figureout what is happening! Mwig is disastrous!
 
Huyu mama anatamani yani wabunge wachadema wote awatoe nje!
 
Yani wabunge wa CHADEMA ni wavumilivu sana aisee.. mi ningekua nshazabua makofi watu mle ndani! wabunge wa ccm wako kama zombies
 
Nimempa Ushauri Kama Mama Yangu, Kama Bibi yangu, kama Shangazi yangu. Najua hata kama si Memba lazima atakuwa anapitipitia

Mama Leo Umetia Hasira, Umetia Kinyaa, Umekubali Kutumika na Lukuvi na Werema kwa Mambo ambayo hata Mtoto Aliyeangalia Bunge jana atakuwa AMEKUSHANGAA
 
CCM ilifanya makosa makubwa kumuacha Samuel Sitta (Speed and Standard!) na kutuwekea "Kituko" hiki! Kinalalamika ovyo bila kujua kinalalamikia nini, ilimradi kikwaze wapinzani.

Sasa hili ndio linaonyesha wazi kuwa bungeni watu wamekuja wapya na huko tuendako kwa speed hii huyu mama atakuja kimbia hicho kiti maana Sitta hapo alipamudu kabisaaa kwani alikuwa nae ni mtaalamu wa Sheria sasa mama anapambana na Lisu atamweza wapi Nchi nzima tunajua fika JK aliki kuwa ni bora akose Urais kulikoni Tindu Lisu kuwa mbunge sasa mwaona joto lake hata AG warema anapatwa na kigugumizi sana lukuvi ndo mnafi mkubwa anadhani atafarijiwa na wna Iringa ng'oooo anajidanganya kabisa kwa hilo


 
kebwe n the like bcause of their shortsitednes r cheering the devil himself! Killer Mwig is the devil! Kills 4 hs glory
 
Katika mpangilio wa kiutawala wajinga hawapaswi kupewa nafasi ya kutawala, wakipewa matokeo yake huwa kama unayoyaona ivi leo! chama kinachoongozwa na raisi dhaifu, mawaziri wajinga wajinga, wabunge wehuwehu wasiojua nini maana ya kuwa mbunge!
ni aibu na ni hasara sana, ona leo mpaka Masele anawaza kuwa raisi,makamba anawaza kuwa raisi, membe nae walewale.
hii inatokana na kuona kuwa inawezekana maana top aliepo ni mwenye akili zinazofanana na zao
 
Back
Top Bottom