AK-47
JF-Expert Member
- Nov 12, 2009
- 1,373
- 199
Inasikitisha sana dada zetu wamekuwa wakipata ushauri unaochanganya kiasi cha kufanya vitu vya ajabu ili kuwavutia wanaume. Kibaya zaidi ushauri huo unatolewa na wanawake wenzao kwenye majarida eti utakuta jike limeandika makala Mambo 100 ya kumridhisha mwanaume. Hivi kweli mwanamke anajua nini kinachomridhisha mwanaume kuliko mwanaume mwenyewe. Hakuna mambo 100 ya kumridhisha mwanaume, mwanaume anamambo machache mno ya kumridhisha na hayazidi hata matano lakini wenzenu wanawapotosha kiasi cha kujihisi si wazuri lakini mie napenda kuwaambi wanawake nyie ni wazuri mno hivyo mlivyozaliwa. Msichanganywe na ma-columnist wanaojifanya wataalam wa mapenzi wanacheza na akili zenu na kuathirika kisaikolojia na kiafya na hata kushindwa kujua nini hasa cha kufanya ili kudumisha mahusiano yenu. Ushauri huu ni maalum katika kuonyesha upendo wangu kwenu wakati huu tukielekea kwenye Valentine Day.