IshaLubuva
JF-Expert Member
- Dec 4, 2008
- 250
- 11
Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Runinga cha ITV cha usalama barabarani ambapo walikuwa wanahojiwa abiria na madereva kuhusu speed za mabasi. Baadhi ya abiria waliohojiwa walikuwa wanakubaliana na kikomo cha speed ya km 80 kwa saa kilichopo sasa, lakini kukawa na aina fulani ya kuchomekea kuiomba serikali iangalie uwezekano wa kuongeza ukomo huo ili ufikie km 100 kwa saa kwa msingi kwamba kukaa kwenye basi kwa muda mrefu nako kunachosha abiria.
Ni nini maoni yenu wanaJF juu ya hili? kuna haja ya kuongeza ukomo huo au tubakie na uliopo wa km 80 kwa saa?
Ni nini maoni yenu wanaJF juu ya hili? kuna haja ya kuongeza ukomo huo au tubakie na uliopo wa km 80 kwa saa?