Upepo wa Pesa
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 21,251
- 34,198
Habari wana jamvi!
Leo nimeona si vibaya kushare nanyi kidogo nnachojua kuhusu kilimo cha umwagiliaji, na katika uzi huu nitajaribu kuelezea kile nnachojua na pia kupata mawazo kutoka kwa wadau mbali mbali hasa wakulima ambao kwa namna moja au nyingine ndio main actors katika sector ya umwagiliaji!
Kwa miaka kadhaa iliyopita mashirika mbali mbali na serikali vimekua vikiweka mkazo sana katika kilimo cha umwagiliaji, nadhani wote tunakumbuka kilichotokea mwaka huu na mwaka jana ambapo wakulima wengi walipata hasara kwa kulima alafu mvua ikakatika mazao yakiwa katika critical stage, stage ambayo maji ni lazima yawepo kwa ajili ya mimea shambani!
Kwa kifupi katika ulimwengu wa sasa hakuna kilimo cha kibiashara kitafanikiwa bila kuwa na mfumo sahihi na mathubuti kwa ajili ya umwagiliaji!!
Kwa kuanza, leo nitaomba tujifunze/tujikumbushe aina mbali mbali za umwagiliaji au njia ambazo mkulima anaweza kufikisha maji kwenye mmea.
1. Umwagiliaji wa maji kwa kutumia mifereji (furrow/surface irrigation method)
Huu ni umwagiliaji ambao mkulima anatumia mifereji kufikisha maji shambani, umwagiliaji huu unaaminika kutumiwa miaka mingi sana iliyopita, kwa kifupi ndio umwagiliaji mkongongwe (oldest) kushinda njia nyingine za umwagiliaji! Pamoja na faida zake ila umwagiliaji huu unahitaji maji mengi sana na pia unapelekea upotezaji mwingi sana wa maji shambani na uharibifu wa ardhi. Kwa kifupi sio bora ukilnganisha na njia nyingine za umwagiliaji. Katika kundi hili pia kuna border irrigation method
2. Umwagiliaji wa matone (drip irrigation)
Huu ni umwagiliaji wa kisasa kabisa ambao unatumia maji machache na katika njia ambayo ni fanisi. Umwagiliaji huu unaingina katika kundi la “pressurized irrigation” ambapo mara nyingi mtumiaji anahitaji pump kama mechanism ya kulift/kupush/kusukuma maji. Lakini pia umwagiliaji huu unaweza kutumia njia ya “gravitation” ambapo mmwagiliaji anaweka maji kwenye pipa lililo juu (la simtank) na kuruhusu maji yashuke kwa kani mvutano kwenda kwenye drip pipes!
3. Sprinkler irrigation
Hii inatumia njia ambayo maji yanarushwa hewani kama mvua na kushuka kwenye mimea, hii njia pia inaangukia kwenye kundi la “pressurized irrigation” kama ilivyo drip irrigation. Katika njia hii ni lazima mmwagiliaji awe na pump au mechanism yoyote itayotoa pressure!
Ziko njia nyingi za umwagiliaji lakini hizi ndio common kwa maeneo mengi hapa kwetu Tanzania na duniani kwa ujumla!! Katika uzi huu tutajifunza umwagiliaji kwa ujumla, mahitaji ili kuanzisha kilimo cha umwagiliaji, changamoto zake kupitia kwa members wengine humu ambao pia watakua na mawazo au mchango kwenye hii sector na zaidi ya yote tutapitia njia moja baada ya nyingine na kujifunza kwa undani zaidi!
Kama una nia ya kufanya kilimo biashara, basi hakuna jinsi utakwepa kilimo cha umwagiliaji hasa ukizingatia mabadiliko ya hali ya hewa katika miaka ya hivi karibuni
Karibuni sana wanajamvi kwa maswali, mawazo katika hii sector ya kilimo hasa cha umwagiliaji!
SEHEMU YA KWANZA Link: Things to consider before you start to irrigate
SEHEMU YA PILI : Madumuni ya umwagiliaji, post namba 75
Leo nimeona si vibaya kushare nanyi kidogo nnachojua kuhusu kilimo cha umwagiliaji, na katika uzi huu nitajaribu kuelezea kile nnachojua na pia kupata mawazo kutoka kwa wadau mbali mbali hasa wakulima ambao kwa namna moja au nyingine ndio main actors katika sector ya umwagiliaji!
Kwa miaka kadhaa iliyopita mashirika mbali mbali na serikali vimekua vikiweka mkazo sana katika kilimo cha umwagiliaji, nadhani wote tunakumbuka kilichotokea mwaka huu na mwaka jana ambapo wakulima wengi walipata hasara kwa kulima alafu mvua ikakatika mazao yakiwa katika critical stage, stage ambayo maji ni lazima yawepo kwa ajili ya mimea shambani!
Kwa kifupi katika ulimwengu wa sasa hakuna kilimo cha kibiashara kitafanikiwa bila kuwa na mfumo sahihi na mathubuti kwa ajili ya umwagiliaji!!
Kwa kuanza, leo nitaomba tujifunze/tujikumbushe aina mbali mbali za umwagiliaji au njia ambazo mkulima anaweza kufikisha maji kwenye mmea.
1. Umwagiliaji wa maji kwa kutumia mifereji (furrow/surface irrigation method)
Huu ni umwagiliaji ambao mkulima anatumia mifereji kufikisha maji shambani, umwagiliaji huu unaaminika kutumiwa miaka mingi sana iliyopita, kwa kifupi ndio umwagiliaji mkongongwe (oldest) kushinda njia nyingine za umwagiliaji! Pamoja na faida zake ila umwagiliaji huu unahitaji maji mengi sana na pia unapelekea upotezaji mwingi sana wa maji shambani na uharibifu wa ardhi. Kwa kifupi sio bora ukilnganisha na njia nyingine za umwagiliaji. Katika kundi hili pia kuna border irrigation method
2. Umwagiliaji wa matone (drip irrigation)
Huu ni umwagiliaji wa kisasa kabisa ambao unatumia maji machache na katika njia ambayo ni fanisi. Umwagiliaji huu unaingina katika kundi la “pressurized irrigation” ambapo mara nyingi mtumiaji anahitaji pump kama mechanism ya kulift/kupush/kusukuma maji. Lakini pia umwagiliaji huu unaweza kutumia njia ya “gravitation” ambapo mmwagiliaji anaweka maji kwenye pipa lililo juu (la simtank) na kuruhusu maji yashuke kwa kani mvutano kwenda kwenye drip pipes!
3. Sprinkler irrigation
Hii inatumia njia ambayo maji yanarushwa hewani kama mvua na kushuka kwenye mimea, hii njia pia inaangukia kwenye kundi la “pressurized irrigation” kama ilivyo drip irrigation. Katika njia hii ni lazima mmwagiliaji awe na pump au mechanism yoyote itayotoa pressure!
Ziko njia nyingi za umwagiliaji lakini hizi ndio common kwa maeneo mengi hapa kwetu Tanzania na duniani kwa ujumla!! Katika uzi huu tutajifunza umwagiliaji kwa ujumla, mahitaji ili kuanzisha kilimo cha umwagiliaji, changamoto zake kupitia kwa members wengine humu ambao pia watakua na mawazo au mchango kwenye hii sector na zaidi ya yote tutapitia njia moja baada ya nyingine na kujifunza kwa undani zaidi!
Kama una nia ya kufanya kilimo biashara, basi hakuna jinsi utakwepa kilimo cha umwagiliaji hasa ukizingatia mabadiliko ya hali ya hewa katika miaka ya hivi karibuni
Karibuni sana wanajamvi kwa maswali, mawazo katika hii sector ya kilimo hasa cha umwagiliaji!
SEHEMU YA KWANZA Link: Things to consider before you start to irrigate
SEHEMU YA PILI : Madumuni ya umwagiliaji, post namba 75