Muhimu: Nani kati ya hawa unamwona anafaa kupeperusha bendera yetu Igunga toa pia sababu.
1. Kajua Sebastiani 2. Marco Amos 3. Kahema John, 4. Buzinza Magego, 5. Dickson Samsoni, 6. Anwari Luhumbi, 7. Erasto Tumbo, 8. Joseph Mwandu, 9. Juma Katigula, 10.Frank Matto, 11.Joseph Mapalala 12.Juma Chaha.
Pamoja Tutaweza, Nimerudi kuwashika............mapambano ndiyo yanaanza..... People's Power.
1. Kajua Sebastiani 2. Marco Amos 3. Kahema John, 4. Buzinza Magego, 5. Dickson Samsoni, 6. Anwari Luhumbi, 7. Erasto Tumbo, 8. Joseph Mwandu, 9. Juma Katigula, 10.Frank Matto, 11.Joseph Mapalala 12.Juma Chaha.
Pamoja Tutaweza, Nimerudi kuwashika............mapambano ndiyo yanaanza..... People's Power.
Wana Chadema nimeona niwatoe wasiwasi kuhusu matokeo yaliyopita ya jimbo la Igunga ieleweke Chadema hatukuweka mgombea wagombea walikuwa wawili tu RA wa CCM aliyepata kura 34,090 na Leopard Mahona wa CUF aliyepata kura 11,321 unaweza kuona kabisa ni kiasi gani kuna mtaji wa kura za upinzani huko, hiyo ni mbali na matokeo ya kura za urais.
Kwa taarifa yenu Chadema Igunga ina mizizi kuliko watu wanavyodhani, CCM imechokwa watu wanataka mabadiliko hizo kura za CUF zisiwababaishe wananchi walikuwa hawana alternative nyingine zaidi ya kukipigia chama hicho nafikiri Chadema kingeweka mgombea mambo yangekuwa tofauti, kura zinaonyesha mbali ya RA kugawa pesa kila kaya lakini bado watu walimkataa.
Ngoja niwakumbushe historia ya uchaguzi mdogo wa Busanda 2009, matokeo ya ubunge Busanda ya mwaka
2005: CCM= 61,868, CUF=13,094 na Chadema= 3,109 lakini kwenye uchaguzi mdogo uliofuata mambo yakabadilika...
2009: CCM= 29,242, CUF= 977 tu na Chadema ikapata kura 22,799 what happened to CUF?
Kilichoifanya Chadema iipiku CUF kwa kura nyingi kiasi hicho ndicho hicho hicho kitaifanya Chadema kuibuka kidedea kwenye uchaguzi huu. Kwa hilo sina wasiwasi kabisa kwasababu zifuatazo, kwanza Igunga tuna mtaji wa kura za upinzani pili tuna nyongeza kutoka CCM waliokatishwa tamaa na utawala wa CCM na tatu wapenzi wa mbunge wao kipenzi RA waliochukizwa na maamuzi ya kumfukuza mbunge wao tuko nao pamoja. Nne CCM imechoka haina mtu kitaifa wa kwenda Igunga na kukiuza chama Nape na Chiligati kwa hali ya kawaida hawawezi kukanyaga kule labda kama wanataka kuzomewa.
Pamoja na hayo Chadema ina kikosi kazi kilichokamili kuanzia mzee wa anga hadi askari wa miamvuli, NEC ikiacha haki itendeke kwenye uchaguzi huu na Chadema tukijipanga vizuri kuzilinda kura kwa sababu zipo tuna kila haja ya kutembea kifua mbele kuwa jimbo hilo ni letu.