Source Mwananchi 28/10/2011 - Sudan ilifadhili Mauaji ya Muammar Gaddafi

Diehard

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
467
347
Rais wa Sudan, Omar Al Bashir amesema nchi yake ilitoa msaada wa wapinzani wa Libya waliomuondoa madarakani Kanali Muammar Gaddafi.

Katika hotuba kupitia televisheni, Bashir alisema hatua hiyo ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa Gaddafi kutokana na yeye kuwaunga mkono waasi wa sudan miaka mitatu iliyopita.

Sudan na Libya hawajawa na uhusiano mzuri kwa miaka mingi. Rais Al Bashir alisema kundi la JUSTICE AND EQUALITY MOVEMENT (JEM) ambalo ni la waasi kutoka Dafur lilivamia Khartoum miaka mitatu iliyopita wakitumia magari ya jeshi la libya, vifaa, silaha, na pesa kutoka serikali ya Muammar Gaddafi. Alisema Mungu amewapa Sudan fursa ya kulipiza mashambul;io kwa kutuma silaha na msaada kwa raia kwa utawala uliofanya mapinduzi.

Tafsiri yangu:

Kumekuwa na takwimu nyingi zisemazo Gaddafi alikuwa mtu mwema na kutolewa mtiririko wa mengi aliyowafanyia raia wake na wengine kujaribu kukataa maovu yake wakisema kuwa ni propaganda za kimagharibi lakini wanasahau kuwa Gaddafi alileta jeshi lake kupigana na Tanzania katika vita isiyomuhusu ambayo inasemekana wanajeshi wake wapatao 600 walikufa leo unasema alipenda raia wake.

Ikumbukwe Gaddafi amewahi kuwasaidia waasi Chad na Sudan miaka ya nyuma, alihusika na kupotea kwa mwandishi wa habari wa Lebanon Shia imam Musa al-Sadr , ni huyu huyu Gaddafi aliyekuwa na shule ya kijeshi na moja ya graduates wake na ambao waliokuwa wanasapotiwa na Gaddafi ni hawa hapa Charles Taylor - Liberia, Foday Sankoh - mwanzilishi wa Revolutioneray United Front, Jean Bedel Bokassa dictactor wa Afrika ya kati, Blaise Compaore wa Burkina Faso aliyechukua nchi kwa kumuua Rais Thomas Sankara, Ni Gaddafi huyuhuyu aliye kuwa akilifinance kikundi cha waasi wa Ethiopia cha Mengistu Haile Mariam moja ya vikosi vibaya kuwahi kutokea Afrika katika mauaji.

Kifupi Gaddafi aliwafadhiri waasi wa nchi nyingine ili tawala za nchi hizo zianguke alifanikiwa kwa kiwango chake na kwa kuwa aliishi kwa upanga na yeye kaondoka kwa upanga GAME ON NGOMA DRAW, Aliwafadhili waasi na waasi waliomuondoa walifadhiliwa na wengine kumbe mpaka Sudan labda na T+Z maana mauaji ya Gadafi yanapingwa kwa nguvu
 
Vyombo vyetu vya habari na kudesa,kopy and pesiti.Hii habari ilijurikana siku ameuwawa gadafi alafu hawa ndo wanaileta,wamekosa habari au?
 
Aliwafukuza wapalestine 30,000 kutoka Libya na kuwaita ma ******,south America ameivuruga kwa pesa zake , karibia vita zote huko sponsor yeye
 
Rais wa Sudan, Omar Al Bashir amesema nchi yake ilitoa msaada wa wapinzani wa Libya waliomuondoa madarakani Kanali Muammar Gaddafi.

Katika hotuba kupitia televisheni, Bashir alisema hatua hiyo ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa Gaddafi kutokana na yeye kuwaunga mkono waasi wa sudan miaka mitatu iliyopita.

Sudan na Libya hawajawa na uhusiano mzuri kwa miaka mingi. Rais Al Bashir alisema kundi la JUSTICE AND EQUALITY MOVEMENT (JEM) ambalo ni la waasi kutoka Dafur lilivamia Khartoum miaka mitatu iliyopita wakitumia magari ya jeshi la libya, vifaa, silaha, na pesa kutoka serikali ya Muammar Gaddafi. Alisema Mungu amewapa Sudan fursa ya kulipiza mashambul;io kwa kutuma silaha na msaada kwa raia kwa utawala uliofanya mapinduzi.

Tafsiri yangu:

Kumekuwa na takwimu nyingi zisemazo Gaddafi alikuwa mtu mwema na kutolewa mtiririko wa mengi aliyowafanyia raia wake na wengine kujaribu kukataa maovu yake wakisema kuwa ni propaganda za kimagharibi lakini wanasahau kuwa Gaddafi alileta jeshi lake kupigana na Tanzania katika vita isiyomuhusu ambayo inasemekana wanajeshi wake wapatao 600 walikufa leo unasema alipenda raia wake.

Ikumbukwe Gaddafi amewahi kuwasaidia waasi Chad na Sudan miaka ya nyuma, alihusika na kupotea kwa mwandishi wa habari wa Lebanon Shia imam Musa al-Sadr , ni huyu huyu Gaddafi aliyekuwa na shule ya kijeshi na moja ya graduates wake na ambao waliokuwa wanasapotiwa na Gaddafi ni hawa hapa Charles Taylor - Liberia, Foday Sankoh - mwanzilishi wa Revolutioneray United Front, Jean Bedel Bokassa dictactor wa Afrika ya kati, Blaise Compaore wa Burkina Faso aliyechukua nchi kwa kumuua Rais Thomas Sankara, Ni Gaddafi huyuhuyu aliye kuwa akilifinance kikundi cha waasi wa Ethiopia cha Mengistu Haile Mariam moja ya vikosi vibaya kuwahi kutokea Afrika katika mauaji.

Kifupi Gaddafi aliwafadhiri waasi wa nchi nyingine ili tawala za nchi hizo zianguke alifanikiwa kwa kiwango chake na kwa kuwa aliishi kwa upanga na yeye kaondoka kwa upanga GAME ON NGOMA DRAW, Aliwafadhili waasi na waasi waliomuondoa walifadhiliwa na wengine kumbe mpaka Sudan labda na T+Z maana mauaji ya Gadafi yanapingwa kwa nguvu

Hapo kwenye red; ongezea na tukio baya la ulipuaji wa ndege ya Pan Am huko Lockerbie, Scotland 1988 ambapo mamia ya raia wasio na hatia waliuawa. Halafu baadaye kwa kiburi kabisa kaja kumpokea kwa mbwembwe kama shujaa gaidi alilolituma kulipua ndege hiyo. Baada ya matukio mengi ya kushangaza ya Ghadafi, kama kuna tukio ambalo liliwaudhi mataifa ya magharibi ni hili la kumpokea gaidi kama shujaa. Kwa kituko hiki hata mimi "nilitabiri" mwisho wa Gadafi ulikuwa umewadia.

Huyo Al-Bashiri wa Sudan naye asitake kujipatia "ujiko" hapa hana lolote huyo. Kwanza anatakiwa sasa hizi awe kwenye vizimba vya ICC huko The Hague akihojiwa na o'Campo. Alivyowafanyia weusi wa Sudan ya Kusini na Darfur, ni heri hata ya Gadafi.
 
Mtoa mada hueleweki sijui kama unamsupport al bashir na mauaji yake ya watu weusi huko Dafur na South sudan? Kama gadaf alitoa msaada wa kusaidia watu wa dafur wanaouawa na serkali yao wenyewe basi alifanya vyema hata sisi tanzania tuna wanajeshi wetu huko dafur ili kumzuia al bashir kuua zaidi? Serkali nyingi za kiafrika ni kama hii ya ccm hapa kwetu, hazina haki wala demokrasia ndiyo sababu kuna waasi wengi afrika. watanzania kama tusingekuwa waoga na wajinga lazima tu waasi wangekuwepo hapa nchini kwetu. Waasi wanadai haki na lugha ambayo wakandamijazi kama ccm wanaoielewa ni vita na mauaji.
 
Mtoa mada hueleweki sijui kama unamsupport al bashir na mauaji yake ya watu weusi huko Dafur na South sudan? Kama gadaf alitoa msaada wa kusaidia watu wa dafur wanaouawa na serkali yao wenyewe basi alifanya vyema hata sisi tanzania tuna wanajeshi wetu huko dafur ili kumzuia al bashir kuua zaidi? Serkali nyingi za kiafrika ni kama hii ya ccm hapa kwetu, hazina haki wala demokrasia ndiyo sababu kuna waasi wengi afrika. watanzania kama tusingekuwa waoga na wajinga lazima tu waasi wangekuwepo hapa nchini kwetu. Waasi wanadai haki na lugha ambayo wakandamijazi kama ccm wanaoielewa ni vita na mauaji.

Mkuu, umemaliza kila kitu kwenye hii post yako
 
Mtoa mada hueleweki sijui kama unamsupport al bashir na mauaji yake ya watu weusi huko Dafur na South sudan? Kama gadaf alitoa msaada wa kusaidia watu wa dafur wanaouawa na serkali yao wenyewe basi alifanya vyema hata sisi tanzania tuna wanajeshi wetu huko dafur ili kumzuia al bashir kuua zaidi? Serkali nyingi za kiafrika ni kama hii ya ccm hapa kwetu, hazina haki wala demokrasia ndiyo sababu kuna waasi wengi afrika. watanzania kama tusingekuwa waoga na wajinga lazima tu waasi wangekuwepo hapa nchini kwetu. Waasi wanadai haki na lugha ambayo wakandamijazi kama ccm wanaoielewa ni vita na mauaji.



Mkuu simsampoti Gaddafi najaribu kuonyesha kilichompata ni matokeo ya ya ukauzu wake
 
Back
Top Bottom