Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,111
19th November 2009
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba, amedai kuwa baadhi ya vyama vya upinzani vimekuwa vikitumia baadhi ya vyombo vya habari au taasisi zisizo za kiserikali kama vile Tamwa na tangazo lao la 'Sidanganyiki' ili kukichafua chama hicho na serikali yake ili kionekane hakijafanya kitu.
Alitoa kauli hiyo juzi mjini hapa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza Kuu la UWT na mafunzo kwa viongozi na wajumbe wa baraza hilo.
Simba ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), alidai kuwa baadhi ya vyama vya upinzani vinapokea fedha kutoka nje kwa lengo hilo.
Alitolea mfano tangazo linalotolewa katika vyombo vya habari na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) la 'Sidanganyiki' kwamba linatangazwa kwa ufadhili wa fedha nyingi kutoka nje.
Hata hivyo, hakueleza uhusiano uliopo kati ya Tamwa na vyama vya upinzani.
Tamwa imekuwa ikitumia tangazo hilo kama kampeni ya kuwalinda watoto wa kike dhidi ya vishawishi vya ngono. Kadhalika ilitumia tangazo kama hilo kuwahamasisha Watanzania kuwa macho kwa kuchagua
Waziri huyo wa Utawala Bora alihoji kuwa wapinzani wanaotaka kukiangusha chama chake kwa kupeleka vijisenti siku zote walikuwa wapi.
Wapinzani hawana cha kuonyesha, wamefanya nini ila CCM wana uwezo wa kuonyesha wamefanya nini katika utekelezaji wa ilani yetu ya chama, alisema Sophia, ambaye hivi karibuni anadaiwa kutoa kauli za matusi wakati wabunge wa CCM walipokutana na Kamati ya Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, kueleza kiini cha mpasuko ndani ya Bunge.
Kipindi cha nyuma hapakuwepo shule nyingi na zilizokuwepo zilikuwa mbali lakini sasa zipo nyingi mpaka wanafunzi wanajazana kwenye magari, alisema na kuwataka wanawake wa chama tawala kuwa mstari wa mbele kujibu mapigo ya wapinzani.
Alisema kuwa wanawake hao wawajibu wapinzani kwa kuonyesha ilani ya uchaguzi ya CCM kuwa imetekelezwa. Aidha, Sophia Simba alimtetea Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kuwa anafanyakazi kwa juhudi licha ya kuwepo maneno maneno ya wivu dhidi yake.
Kikao cha UWT kinampongeza kwa kazi nzuri, wale wanaomsema vibaya washindwe na walegee, alisema Waziri Sophia.
CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba, amedai kuwa baadhi ya vyama vya upinzani vimekuwa vikitumia baadhi ya vyombo vya habari au taasisi zisizo za kiserikali kama vile Tamwa na tangazo lao la 'Sidanganyiki' ili kukichafua chama hicho na serikali yake ili kionekane hakijafanya kitu.
Alitoa kauli hiyo juzi mjini hapa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza Kuu la UWT na mafunzo kwa viongozi na wajumbe wa baraza hilo.
Simba ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), alidai kuwa baadhi ya vyama vya upinzani vinapokea fedha kutoka nje kwa lengo hilo.
Alitolea mfano tangazo linalotolewa katika vyombo vya habari na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) la 'Sidanganyiki' kwamba linatangazwa kwa ufadhili wa fedha nyingi kutoka nje.
Hata hivyo, hakueleza uhusiano uliopo kati ya Tamwa na vyama vya upinzani.
Tamwa imekuwa ikitumia tangazo hilo kama kampeni ya kuwalinda watoto wa kike dhidi ya vishawishi vya ngono. Kadhalika ilitumia tangazo kama hilo kuwahamasisha Watanzania kuwa macho kwa kuchagua
Waziri huyo wa Utawala Bora alihoji kuwa wapinzani wanaotaka kukiangusha chama chake kwa kupeleka vijisenti siku zote walikuwa wapi.
Wapinzani hawana cha kuonyesha, wamefanya nini ila CCM wana uwezo wa kuonyesha wamefanya nini katika utekelezaji wa ilani yetu ya chama, alisema Sophia, ambaye hivi karibuni anadaiwa kutoa kauli za matusi wakati wabunge wa CCM walipokutana na Kamati ya Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, kueleza kiini cha mpasuko ndani ya Bunge.
Kipindi cha nyuma hapakuwepo shule nyingi na zilizokuwepo zilikuwa mbali lakini sasa zipo nyingi mpaka wanafunzi wanajazana kwenye magari, alisema na kuwataka wanawake wa chama tawala kuwa mstari wa mbele kujibu mapigo ya wapinzani.
Alisema kuwa wanawake hao wawajibu wapinzani kwa kuonyesha ilani ya uchaguzi ya CCM kuwa imetekelezwa. Aidha, Sophia Simba alimtetea Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kuwa anafanyakazi kwa juhudi licha ya kuwepo maneno maneno ya wivu dhidi yake.
Kikao cha UWT kinampongeza kwa kazi nzuri, wale wanaomsema vibaya washindwe na walegee, alisema Waziri Sophia.
CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni