IshaLubuva
JF-Expert Member
- Dec 4, 2008
- 250
- 11
Nina tatizo na Camera yangu aina ya Sony Cyber-shot 8.1 Megerpixels. Kuna siku nilimpa Mtumishi mwenzangu baada ya kuniomba ili aione. Mimi nikawa nimeende pembeni kidogo, baada ya mda kidogo alikuja huku Camera ikiwa inatetemeka. Maelezo aliyonipa ni kwamba yeye alipiga picha na baadaye kubonyeza kitufe cha kumwezesha kuona picha alizopiga na ndipo ilipoanza kutetemeka. Baada ya muda ilitulia lakini hali hiyo iliendelea kujitokeza kila nilipoiwasha Camera na kuchukua muda kadhaa kabla ya kutulia. Majuzi utetemekaji huo ulifikia kuwango kibaya zaidi ambapo kila nilipoiwasha Camera ilitetemeka huku ikipata joto na baadaye kujizima.
Nilijasribu kumdadisi kujua iwapo aliidondosha lakini alisema kuwa hakuidodosha.
Naomba mwenye kuweza kujua sababu au kujua mtaalamu Muungwana aliyeko Dar es Salaam ambaye anaweza kuihudumia Camara yangu tafadhal.
Nilijasribu kumdadisi kujua iwapo aliidondosha lakini alisema kuwa hakuidodosha.
Naomba mwenye kuweza kujua sababu au kujua mtaalamu Muungwana aliyeko Dar es Salaam ambaye anaweza kuihudumia Camara yangu tafadhal.