Sony Cyber-shot

IshaLubuva

JF-Expert Member
Dec 4, 2008
250
11
Nina tatizo na Camera yangu aina ya Sony Cyber-shot 8.1 Megerpixels. Kuna siku nilimpa Mtumishi mwenzangu baada ya kuniomba ili aione. Mimi nikawa nimeende pembeni kidogo, baada ya mda kidogo alikuja huku Camera ikiwa inatetemeka. Maelezo aliyonipa ni kwamba yeye alipiga picha na baadaye kubonyeza kitufe cha kumwezesha kuona picha alizopiga na ndipo ilipoanza kutetemeka. Baada ya muda ilitulia lakini hali hiyo iliendelea kujitokeza kila nilipoiwasha Camera na kuchukua muda kadhaa kabla ya kutulia. Majuzi utetemekaji huo ulifikia kuwango kibaya zaidi ambapo kila nilipoiwasha Camera ilitetemeka huku ikipata joto na baadaye kujizima.

Nilijasribu kumdadisi kujua iwapo aliidondosha lakini alisema kuwa hakuidodosha.

Naomba mwenye kuweza kujua sababu au kujua mtaalamu Muungwana aliyeko Dar es Salaam ambaye anaweza kuihudumia Camara yangu tafadhal.
 
JAribu kubadilisha battery...weka Lithium battery kisha angalia kama bado ina tetemeka au vipi...
 
Kuna uwezekano mkubwa kamera yako ilipata mtikisiko mkubwa uliosababishwa na kishindo.
Kama bado kamera yako ina waranti basi fanya hima uirudishe kwa mtengenezaji au wakala wake kwa usaidizi zaidi.
Or elese kwa haraka-haraka ingia kwenye website ya Sony tafuta aina ya kamera yako then tafuta kitatuatatizo (troubleshoot)
 
Camera hiyo iliangushwa ni tatizo la kamera za sony very delicate to handle...na ni nzuri kwa kweli haina tofauti na laptop zao plus simu.

Mfanyakazi mwenzako kakuficha ukweli camera haiwezi kusisimka tu na kuanza kutetemeka..kwanza ingekuwa mie labda ningeiangusha mara ya pili kufikiri labda bomu.Ila ukweli kwamba iliangushwa na ukienda kwa mafundi ndio itaharibika kabisa.

Check na website yao lakini kupata suluhisho la camera vibrating ni very rare sana kwenye mtandao wa camera..
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom