Songwe International Airport

RedDevil

JF-Expert Member
Apr 30, 2009
2,368
1,518
58.jpg

Songwe-International-Airport.jpg


Minister for Infrastructure Development Dr. Shukuru Kawambwa has directed the Tanzania Airports Authority (TAA) to work in partnership with the Tanzania National Roads Agency (Tanroads) to construct good roads surrounding the newly built Songwe International Airport in a bid to reduce congestion of vehicles when it starts to operate.

Kawambwa issued the order last week when he toured the airport to inspect the construction process.

He said he was satisfied with the current construction pace and that he was sure the construction would be completed by the end of this year.

However, he said upon completion and the airport opened there would be congestion of vehicles, people and business in the area. He said it was therefore, important to take urgent measures to build good roads around the a stivedive airport.

"The Tunduma road borders the airport and therefore, urgent measures must be taken to build good roads near the airport in a move to avoid transport obstruction," he said.

Earlier, while briefing the minister on the construction development, TAA director Prosper Tesha said construction of the airport was complete by between 60 and 70 per cent and by the end of next month, runways would be completed.

He further said that the construction of the passengers' lounge was underway and it was expected to be completed by the end of the year. Songwe airport is expected to be among the best airports in the country upon its completion and is said to be bigger that Mwalimu Julius Nyerere international airport in Dar es Salaam. Songwe's runway is 3.5 km long while Mwalimu Julius Nyerere's is only 3.0 Km. Source ippmedia.

Hivi kuna dili gani jamani huko hadi kujenga airport kubwa kama hiyo?

Huenda siko updated na habari zingine. Naomba mwenye taarifa sahihi anihabarishe.
 
Hivi kuna dili gani jamani huko hadi kujenga airport kubwa kama hiyo?
Huenda siko updated na habari zingine. Naomba mwenye taarifa sahihi anihabarishe.

Eneo lote la nyanda za juu kusini linakua kwa kasi sana kiuchumi na tena limechelewa sana kupata huduma hii!Kujibu swali lako huko ndio the next economic giant wa Tanzania anatarajiwa kuibuliwa:becky:
 
Mbona hukuuliza wakati pale Arusha uwanja wa ndege ulikarabatiwa/kujengwa wakati kuna uwanja mkubwa pale KIA,na muda si mreefu Mbeya itakuwa makao makuu ya SADC,leka tujobe

:becky::becky::becky:mweee mweee mweeeeeeee....! mbombongafu :becky::becky::becky:
 
Muulizaji na wachangiaji wake mnajaribu kutuonesha jinsi mlivyo wabinafsi. Mbona yako maeneo economically viable lakini hayana barabara ambayo ni muhimu kwa uchumi kuliko hata huo uwanja wa ndege?
 
Muulizaji na wachangiaji wake mnajaribu kutuonesha jinsi mlivyo wabinafsi. Mbona yako maeneo economically viable lakini hayana barabara ambayo ni muhimu kwa uchumi kuliko hata huo uwanja wa ndege?

Yataje tuendelee na mjadala!



Hivi kuna dili gani jamani huko hadi kujenga airport kubwa kama hiyo?
Huenda siko updated na habari zingine. Naomba mwenye taarifa sahihi anihabarishe.[/QUOTE]

Kwa ujumla, nyanda za juu kusini zina potentials zifuatazo, ambazo ni muhimu sana kwa ukuaji wa uchumi wa nchi.

1) Kilimo (Mazao ya Biashara)
-Chai (Njombe, Mufindi, Rungwe)
-Kahawa (Rungwe, Mbinga, Mbozi
-Pamba (Chunya)
-Kakao (Kyela)
-Tumbaku (Chunya, Kilolo, Sumbawanga)
-Pareto (Mufindi, Mbeya Vijijini)
-Chikichi (Kyela, Ludewa)

2) Madini
-Makaa ya mawe (Ludewa, Rungwe)
-Dhahabu (Chunya)
-Chuma (Ludewa)
-Madini ya vito (Tunduru)

3) Utalii
-Milima mbalimbali
-Mbuga za wanyama (Ruaha, Kipengere, Katavi, Ihefu)
-Maziwa (Nyasa, Ngosi, Tanganyika)
-Barabara Kuu ya TANZAM

4) Mipaka ya Nchi (Inasaidia ongezeko la biashara kati ya nchi hizi)
-Malawi
-Congo
-Zambia


Nitaendelea
 
mi na-support uwanja huu maana ninavyoyajua haya maeneo yana fursa nyingi ambazo zinahitaji hii miundo mbinu yaani kama horticulture ukiachia mbali strategic location, recreation area (mbuga za wanyama), madini, uvuvi na kadhalika
 
Kwani nini wameutelekeza uwanja wa ndege wa Mwanza? Uwanja wa ndege wa Mwanza ungetumika kama hub ya EAC. nchi kama Uganda, rwanda na burundi. Sibishi Kuwa hata Songwe pia inahitajika lakini serikali etu haifanyi miradi yake kwa Priority.

Nakumbuka waziri wa mawasiliano na uchukuzi wakati huo akiwa ni mwenyeji wa mbeya ndo alianzisha move hii. Bungeni akatangaza kuwa Songwe ni Uwanja wa kimataifa. akabanwa na mbunge 1ja kuhusu uwanja wa mwanza hapo hapo akasema na wenyewe ameupa hadhi ya kimataifa.

Teh teh unaweza kuona nchii hii inapelekwa kisiasa siasa. Pili, hizi project za Anga zingekuwa minimised badala yake mapesa hayo yangetumika ku boost ufanisi kwenye project za TAZARA na TRL.
 
Kwani nini wameutelekeza uwanja wa ndege wa Mwanza? Uwanja wa ndege wa Mwanza ungetumika kama hub ya EAC. nchi kama Uganda, rwanda na burundi. Sibishi Kuwa hata Songwe pia inahitajika lakini serikali etu haifanyi miradi yake kwa Priority.

Nakumbuka waziri wa mawasiliano na uchukuzi wakati huo akiwa ni mwenyeji wa mbeya ndo alianzisha move hii. Bungeni akatangaza kuwa Songwe ni Uwanja wa kimataifa. akabanwa na mbunge 1ja kuhusu uwanja wa mwanza hapo hapo akasema na wenyewe ameupa hadhi ya kimataifa.

Teh teh unaweza kuona nchii hii inapelekwa kisiasa siasa. Pili, hizi project za Anga zingekuwa minimised badala yake mapesa hayo yangetumika ku boost ufanisi kwenye project za TAZARA na TRL.
Mbona Mwanza umepanuliwa ndege kubwa za mizigo zinatua! na passengers lounge ilikuwa inajengwa au ni geresha za serikali yetu?
 
Muulizaji na wachangiaji wake mnajaribu kutuonesha jinsi mlivyo wabinafsi. Mbona yako maeneo economically viable lakini hayana barabara ambayo ni muhimu kwa uchumi kuliko hata huo uwanja wa ndege?
Ingekuwa hivyo tayari kungekuwa na barabara na viwanja vya ndege. Kuna maeneo yanasemekana kuwa economically viable lakini sio, na kuna maeneo ni economically viable lakini yanapuuzwa, kuna maeneo ambayo sio economically viable lakini yanapewa umuhimu mkubwa kutokana na sababu za kisiasa na kidini.

It is a fact that given their geagraphical locations Mwanza, Mbeya, Arusha na Mtwara zinatakiwa kupewa msukumo zaidi wa kimaendeleo ili zichangie zaidi maendeleo ya Tanzania, ni uzembe tu katika mipango na utekelezaji.
 
mimi napongeza hatua za kujenga uwanja wa ndege sehemu nyingi iwezekanavyo.... itasaidia sana kufungua mikoa na hatimaye kuongeza fursa za kiuchumi... tuache kuwa na mawazo mgando!!!
 
... hizi project za Anga zingekuwa minimised badala yake mapesa hayo yangetumika ku boost ufanisi kwenye project za TAZARA na TRL.
Nakubaliana na pointi hii kwa 100%. Tungeimarisha usafiri wa treni, nchi yetu ingepiga maendeleo sana, ikichangiwa na uboreshaji wa huduma za bandari. Lakini je, ni nani wa kuipa vipaumbele miundombinu hii baada ya Mzee Mkapa kuondoka?
 
Yaani unakuwa na International airports nne- JK Nyerere(dar), KIA(Arusha/Moshi), Mwanza(?), Songwe(Mbeya) na nasikia kuna ya tano hapo Bagamoyo---HALAFU HUNA HATA NDEGE YAKO MOJA YA KUTUA HAPO! YAANI UNAWAJENGEA NA KUTEGEMEA WATAKUJA! WACHENI!!!!!!! HATA KIA ilikuwa ngumu kukubalika kuwa International Airports, kwa muda mrefu ilikuwa ni KLM tu inatua pale tena kwa sababu moja tu, kuchukua maua kupeleka Europe!

Songwe---mhhhhhhhh potential yes, but we need integrated investments, investments that support each other and therefore ensure sustainability in the long run.
 
Yataje tuendelee na mjadala!


Hivi kuna dili gani jamani huko hadi kujenga airport kubwa kama hiyo?
Huenda siko updated na habari zingine. Naomba mwenye taarifa sahihi anihabarishe.

Kwa ujumla, nyanda za juu kusini zina potentials zifuatazo, ambazo ni muhimu sana kwa ukuaji wa uchumi wa nchi.

1) Kilimo (Mazao ya Biashara)
-Chai (Njombe, Mufindi, Rungwe)
-Kahawa (Rungwe, Mbinga, Mbozi
-Pamba (Chunya)
-Kakao (Kyela)
-Tumbaku (Chunya, Kilolo, Sumbawanga)
-Pareto (Mufindi, Mbeya Vijijini)
-Chikichi (Kyela, Ludewa)

2) Madini
-Makaa ya mawe (Ludewa, Rungwe)
-Dhahabu (Chunya)
-Chuma (Ludewa)
-Madini ya vito (Tunduru)

3) Utalii
-Milima mbalimbali
-Mbuga za wanyama (Ruaha, Kipengere, Katavi, Ihefu)
-Maziwa (Nyasa, Ngosi, Tanganyika)
-Barabara Kuu ya TANZAM

4) Mipaka ya Nchi (Inasaidia ongezeko la biashara kati ya nchi hizi)
-Malawi
-Congo
-Zambia

Nitaendelea[/QUOTE]

Mahindi-ugali chakula kikuu cha tz, ndizi, dhahabu, cor-tan, makaa ya mawe, chuma....
 
mimi napongeza hatua za kujenga uwanja wa ndege sehemu nyingi iwezekanavyo.... itasaidia sana kufungua mikoa na hatimaye kuongeza fursa za kiuchumi... tuache kuwa na mawazo mgando!!!
Naakunga mkono Kanyagio:
Nchi hii inahitaji viwanja vya ndege kwa ajili ya kujenga uchumi imara. Hatujaweza kutumia maliasili zetu alizotupatia Mungu Mwenyezi kwa sababu hazijaweza kufikiwa. Nchi hii inastahili kuwa na viwanja vya ndege vyenye ubora wa kimataifa 4 hivi. Na kiisha kuweka utaratibu wa kuwa na viwanja vidogo vingi ambavyo ndege zinaweza kutua wakati wote. Hatutaweza kuwa katika hali ya ushindani bila ya usafiri huu wa ndege. Malawi ni nchi ndogo lakini ina viwanja viwili vya kimataifa vya ndege na wakati huo ina viwanja vidogo ambavyo hata ndege kubwa zinatua kwa ajili ya watalii.
 
Mimi naunga mkono wachangiaje wote waliotoa mifano ya fursa mbali mbali zilizoko huko nyanda za juu kusini, ni safi kabisa! lakini tuachane na hizo fursa harafu tuone ni vipi serikali yetu imeshawishika kujenga huu uwanja! maana kuna taarifa ambazo si za uhakika kuwa kuna mkono wa Bush huko maeneo fulani kuna madini sasa wanataka dili lichezwe juu kwa juu kama wanavyofanya Geita Mining, na migodi mingine kuwa ndege ikija inaishia huko huko kuchua mzigo na kuondoka. Huo ndo ulikuwa wasiwasi wangu, ndo maana nikaomba taarifa za mina na wanaJF.

Tuna viwanja vingi lakini ndo hivyo kila kitu tunasubiri misaada hata ndege za makampuni yetu ya serikali tunataka misaada.
 
Mimi naunga mkono wachangiaje wote waliotoa mifano ya fursa mbali mbali zilizoko huko nyanda za juu kusini, ni safi kabisa! lakini tuachane na hizo fursa harafu tuone ni vipi serikali yetu imeshawishika kujenga huu uwanja! maana kuna taarifa ambazo si za uhakika kuwa kuna mkono wa Bush huko maeneo fulani kuna madini sasa wanataka dili lichezwe juu kwa juu kama wanavyofanya Geita Mining, na migodi mingine kuwa ndege ikija inaishia huko huko kuchua mzigo na kuondoka. Huo ndo ulikuwa wasiwasi wangu, ndo maana nikaomba taarifa za mina na wanaJF.

Tuna viwanja vingi lakini ndo hivyo kila kitu tunasubiri misaada hata ndege za makampuni yetu ya serikali tunataka misaada.
Hakuna cha Bush wala nini. Mradi huu ulianzishwa enzi za mkapa mwandosya akiwa waziri wa mawasiliano. bahati mbaya sana Pm wa wakati huo hakupenda kwa mtazamo wake ingekuwa threat kwa KIA naye anatoka kanda hiyo hiyo ya KIA na wakati huo yeye mwenyewe na mzee mwandosya walikuwa wanataka urais baada ya mkapa.

Hivyo some political forces corrupted the project, bahati mbaya hata enzi hizi za jk kuna hali isiyo shwari mkoani mbeya-but at least jk ameridhia kujengwa kwake.

Uwanja huu unajegwa na kodi za tz, issues za Bush (as I hear) ziko Ruvuma. Ruvuma na Mbeya kuna distance nako pia kunahitaji uwanja wa level ya kimataifa.
 
ukizungumzia the tz big4 mbeya ndiyo inaongoza kuwa feeder wa country..........hata kibiashara pia kwani ni mkoa unaopakana na nchi nyingi zaidi.......kiukweli hata bidhaa za mbeya zinasoko zaidi kuliko sehemu zingine...nasikia hata bidhaa kama mahindi ,mchelele vikipelekwa nje pia vina soko kutokana na ubora wake .......sio kwasababu watu wa kule ni bora ra hasha ila kwa sababu Mungu kawakirimia kwa hiyo sio lazima kupingana na Mungu tuukubali ukweli...........pamoja na hayo kuna taarifa zisizorasmi kuwa baadhi ya wakubwa waliubania sana kipindi fulani kwa sababu kuwa ungeweza kumpa zaidi umaarufu prof.mwandosya.......tukuze uchumi wa nchi kwa kuboresha mikoa kama Mbeya.....kwanza umechelewa sana
 
Mbona Mwanza umepanuliwa ndege kubwa za mizigo zinatua! na passengers lounge ilikuwa inajengwa au ni geresha za serikali yetu?

Uwanja wa mwanza sio serikali iliyokuwa ya kwanza kuonyesha initive za kuuendeleza. Ni UN na taasisi zake baada ya makashe ya DRC na Rwanda.

Hata huo usanii waliofanya ni mfadhili ndo alikuwa wa kwanza kuona umuhimu na kupendekeza. Ndo maana nasema Serikali yetu haina priority in place. Inakwenda kwenda tu.

Ni vizuri kila sehemu kukawa na kiwanja tena cha kimataifa lakini inabidi twende hatua kwa hatua. Wakati TAZARA na mindombinu yake inazidi kuchoka wanashupalia anga. haya Kwa ndege za shirika gani hizo zitatua songwe? Mizigo tani ngapi ya hayo mazao itasafirishwa kupitia huo uwanja.? Wananchi% ngapi wana uwezo wa gharama za kupaa.

Next Bagamoyo nayo itakuwa bandari ya kimataifa. Hawa hawa wanaoshangilia Songwe kuwa na internationa Airport watakuja kuponda . Kwa nini iswe mtwara au Tanga?????

Nawashauri Great thinkers tuwe tunafanya unbiased analysis kabla ya kukubaliana au kupinga kitu fulani.

Kwa hii ya songwe ni purely politics
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom