SONGEA: Maandamano yameanza upyaaa, mabomu yanarindima!

Polis wa songea wameamua kuonyesha uma wa watz kuwa serikal ya tz sio legelege kama wengi wanavyoisema. Askar wanaonyesha ukakamavu na uimara wa serikali iliyopo madarakan. Nguvu wanayo, uwezo wanao vitendea kazi wanavyo na kizuri zaidi amri wanayo. Semeni tena serikali legelege muone uimara wake.

Hii post inanikumbusha mpuuzi mmoja alikuwa akijisivu kuwa yeye ni mwanaume wa shoka ana nguvu na sababu kubwa ni kuwa na uwezo wa kumpiga mkewe. Ila likija suala la kumhudumia kama chakula bora mavazi malazi na unyumba alikuwa hana uwezo huo.

Watu husema uimara si kupiga bali kuwa na uwezo wa kumridhisha mkeo. Tukija kwenye serikali, uimara wake si kuua au kuonesha kuwa una nguvu, hilo tunalijua kuwa lipo kwenye katiba, ulegelege unaoongelewa ni wa kuendeleza nchi na kukomboa na kukabiliana na changamoto zinazorudisha nyuma uchumi.
 
mkuu wa mkoa nina mashaka naye..anashidwaje kuweka hali sawa? ingekuwa mbeya ingebidi wamtafute sugu
hawa watu bado sielewi kabisa kazi yao inasemekana kuwa wao ni wenyeviti wa kamati ulinzi na usalama wa mkoa husika lakini fuatilia ni mkoa gani mkuu wake akatekeleza majukumu yake ipasavyo

tatizo ninalo liona hawa watu ni wale walio shindwa kwenye chaguzi za ubungeni kimsingi hawana kitu cha kufanya zaidi ya kuchanganya kazi zao na siasa za chama kisha kupoteza mwelekeo
 
ni kawaida kwa askari wa kibongo kuyapa kipaumbele matumizi ya nguvu kuliko akili ktk kusolv issues. ili ni tatizo kubwa na kamwe hatutawavumilia polisi kwa uzembe na ubabe wao wa kitoto. KUTUPIGA RISASI TUPIGEN ILA HAKI YETU TUPENI
 
hivi Baba MwanaAsha akiwa kama Amiri Jeshi mkuu, anatoa maagizo gani kwa hawa askari ambao wanakua wanaua na kunyanyasa raia ambao wapo katika harakati za kudai haki zao???[/
QUOTE]

Polisi wa Tanzania 95% matokeo yao ya form four ni sawa na ya Mwanaasha Jakaya Kikwete...so what do you expect toka kwa mkuu wa kaya!!!!?

Wewe ulipata Div. gani kama siyo 0 wacha kusema Polisi wengi ni Div IV
 
Revolution inaanzia Mikoa ya juu na kuja kumalizika Magogoni, Kazi ianze kuwafukuza hawa wapumbavu

mimi niko hapa Dar najiuliza hawa wanaojiita masharobalo tutawahamasisha vipi kuondoa kuondoa majizi magogoni,kwani nchi nzima wako tayari isipokua hawa midebwedo.
 
Hii post inanikumbusha mpuuzi mmoja alikuwa akijisivu kuwa yeye ni mwanaume wa shoka ana nguvu na sababu kubwa ni kuwa na uwezo wa kumpiga mkewe. Ila likija suala la kumhudumia kama chakula bora mavazi malazi na unyumba alikuwa hana uwezo huo.

Watu husema uimara si kupiga bali kuwa na uwezo wa kumridhisha mkeo. Tukija kwenye serikali, uimara wake si kuua au kuonesha kuwa una nguvu, hilo tunalijua kuwa lipo kwenye katiba, ulegelege unaoongelewa ni wa kuendeleza nchi na kukomboa na kukabiliana na changamoto zinazorudisha nyuma uchumi.

Kweli mkuu!hiyo post kuifananisha na ya mpuuzi fulani haujakosea kabisa!maana imejaa mifano ya kipuuzi tupu!mtu anapost ili mradi nae kapost tu,haelewi hata maana ya ulegelege wa serikali
 
Mkuu, usisahau lindi, mtwara, tabora,.
Tabora unataka tuamke marangapi mdau?Si mwaka jana tu wametupiga risasi hao hao polisi huku Urambo na wakamuweka ndani muheshimiwa Sakaya na wenzake kwenye ile ishu ya wizi wa ng'ombe unaofanywa na maliasili?Au mpaka tufe kumi ndiyo mtajua tumeamka?
 
Akihojiwa na radio moja inayorusha matangazo yake hapa Songea kiongozi mmoja wa ngazi ya juu katika jeshi la polisi hapa mkoani alisema maandamano yaliyofanyika jana hapa mjini yameshinikizwa na vyama vya siasa na wanaharakati. Huku akishindwa kusema ni chama gani kilichoshinikiza maandamano hayo ambayo yeye anayaita vurugu.

Aliongeza kusema kuwa wanasiasa na wanaharakati hao waliwahonga watu pesa ili waandamane. Alipoulizwa anauhakika gani na hilo akasema hizo ni taarifa za kiinterejensi. Alipoulizwa kuhusu polisi kutumia nguvu zaidi katika kupambana na waandamanaji yeye alisema inapobidi nguvu lazima zitumike, lakini itaundwa tume ya kuchunguza mauaji hayo.


Kama kawaida yao, JEshi la Polisi linashindwa kufanya kazi kisha wanasema kuna mkono wa chama cha Siasa. Wananchi walipompelekea taarifa kuhusu mauaji ya kinyama, Kamanda alinyamaza na kutoa majibu ya kishezi kuwa "wanagombea mapenzi ndio maana wameuana" mbona hakusema siku ile kuwa ni wanasiasa hao wameuana

Leo hii hali imekuwa mbaya anatafuta kisingizio ni Siasa.

Na bila aibu anataka kuihusisha CHADEMA katika maandamano hayo, naona amesahau kuwa CHADEMA AKILI ZAO ZOTE ZIPO ARUMERU MUDA HUU.

"HUYU KAMANDA ANATAKIWA AJIUZULU KWA MANUFAA YA UMMA" KWA KUUDANGANYA UMMA WA WATANZANIA


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Serikali ya mkoa iingilie kati na kuzima matumizi ya nguvu. Busara itumike zaidi.


Kawaida mkuu wa Mkoa ana madaraka makubwa sana ndani ya mkoa wake. Hivyo hata hawa Polisi na kamanda wa Polisi mkoa lazima aliwasiliana na Mkuu wa Mkoa naye ndiye anayeruhusu nguvu itumike.

mfano miaka ya awali pale DSM maeneo ya Mwembechai wakati wa vurugu za Waislamu ni kwamba baada ya Polisi kufika pale Waandamanaji waliingia Msikitini kwa Mtoro, na kutumia vipaza sauti vya msikiti kuwatukana Polisi ambao kisheria hawaruhusiwi kuingia na kumkamata mtu ndani nyumba za ibada. Hivyo Kamanda wa Mkoa aiwasiliana na Mkuu wa Mkoa (Yusufu Makamba) ambaye alitoa ruhusa kwa askari kuingia msikitini na kutembeleza virungu.

Hivyo hata Songea ni kwamba Serikali ya Mkoa ndiyo iliyotoa ruhusa kwa askari kuua, hizi lawama haziishii kwa kamanda wa polisi tu bali na mkuu wa Mkoa anahusika.

TAHADHARI: SERIKALI ITAFUTE NJIA NYINGINE YA KUTULIZA GHASIA NA SIYO KUTUMIA NGUVU, KISHA KUSINGIZIA MAMBOP YA SIASA. TUSICHANGANYE SIASA NA UHALISIA WA JAMBO. POLISI IJIFUNZE KUTOKANA NA MAUAJI YA ZANZBAR NA ARUSHA.

MNADHALILISHA JESHI LA POLISI NA KUJENGA UADUI KATI YA POLISI NA RAIA.

JUKUMU LENU NI KULINDA RAIA NA MALI ZAO NA SIYO KUUA RAIA NA KUIBA MALI ZAO



MIZAMBWA
IANNIUMA SANA!!!
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom