SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Haloo Nai, Natumaini hujambo. Kule chitchat uliniomba nikufundishe Kichaga cha Mkuu Rombo. Bila shaka ulikuwa serious, ulikuwa hutanii. Nakuletea somo hilo kwenye hili jukwaa maalum kwa ajili hiyo. Tuanze.
Kwanza, jambo ambalo huenda likakushangaza sana ni kwamba kuna vilugha vingi vya kichaga kutegemeana na sehemu. Hii ina maana kwamba kichaga kinachozungumzwa Machame ni tofauti sana na kile cha, tuseme, Kibosho. Hali kadhalika kinachozungumzwa Uru ni tofauti na kile cha Kirua au Kilema. Ila cha Kirua, Kilema,Marangu na Mwika vinafanana kwa kila kitu: Kiimbo(intonation), msamiati nk. Cha Rombo kinaogopwa na wakazi wengi wa Kilimanjaro kwa sababu eti ni kigumu sana. Sina uhakikana hilo labda kwa sababu mimi ni mzungumzaji wa kirombo. Halafu basi kwenye kirombo kuna maajabu yake! Kirombo kinachozungumzwa sehemu iitwayo Mamsera(karibu na Mwika) ni tofauti na kile cha Mashati au Useri na Tarakea.Lakini kijiografia, Mamsera mpaka Tarakea yote hiyo ni Rombo.Unaona hapo? Leo nitakufundisha Kiorombo kinachozungumzwa Mkuu-Kwa Maangulwa na sijui kama kitakufaa kwa shughuli zako ukiwa na yule mtu uliyenieleza kule chit-chat.
Leo tutaanza na (1)Nafsi (Persons) na tutatazama (2) vitendo(verbs)
(1)Nafsi:
Nafsi za Kiorombo ni kama zilezile za Kiswahili yaani
Kiswahili Kiorombo
Mimi Nyihany
.............................................
Wewe Vehave
..............................................
Yeye Ve
................................................
Sisi Sohaso
.................................................
Ninyi Nyohanyo
.................................................
Wao Vo
...................................................
Kila nafsi hapo juu ina kiambishi(subject prefix) yake. Tazama kiambishi kwa kila nafsi hapo chini.
Kiswahili Kiambishi (Subject Prefix) Kirombo Kiambishi .....................................................................................
Nafsi Mimi ni.... Nyihany ng....
.....................................................................................
Nafsi wewe u...... vehave u.....
......................................................................................
Nafsi yeye a..... ve ne....
........................................................................................
Nafsi sisi tu..... sohaso du.....
........................................................................................
Nafsi Ninyi m...... nyohanyo m........
.........................................................................................
Nafsi Wao wa..... Vo ve........
Baada ya hizo nafsi na viambishi vyake tutazame verbs
Common everyday verbs:
ku_la = i_la
Ku_lala = i_laa
Ku_cheka = i_seka
ku_tazama =i_sakwa
ku_ona = i_lolya
Hapa waweza kuona mara moja kwamba infinitive ya vitendo kiorombo ni i.. na kiswahili ni ku..
Kuunganisha nafsi na vitendo:
Kuunganisha nafsi na kitendo kuelezea ulichofanya kunategemea wakati (tense)
Present tense ya kiswahili ni _na_, ya kiorombo ni _i_. Tazama mifano ifuatayo:
Kiswahili: Ni na kwenda
Kiorombo Ng i enda
Tunacheka = Duiseka
Unaelewa siyo Nai? Naomba kwa leo tuishie hapo ila nakuachia mazoezi yafuatayo:
1. Tafsiri kwa kiorombo sentenso zifuatazo:
(a) Tunakula
(b)Wanacheka
(c)Unatazama
Sasa sijui kama approach hii umeipenda. Toa dukuduku zako uleze unavyotaka kujifunza.
Asante, Nyihany Hygeia
Kwanza, jambo ambalo huenda likakushangaza sana ni kwamba kuna vilugha vingi vya kichaga kutegemeana na sehemu. Hii ina maana kwamba kichaga kinachozungumzwa Machame ni tofauti sana na kile cha, tuseme, Kibosho. Hali kadhalika kinachozungumzwa Uru ni tofauti na kile cha Kirua au Kilema. Ila cha Kirua, Kilema,Marangu na Mwika vinafanana kwa kila kitu: Kiimbo(intonation), msamiati nk. Cha Rombo kinaogopwa na wakazi wengi wa Kilimanjaro kwa sababu eti ni kigumu sana. Sina uhakikana hilo labda kwa sababu mimi ni mzungumzaji wa kirombo. Halafu basi kwenye kirombo kuna maajabu yake! Kirombo kinachozungumzwa sehemu iitwayo Mamsera(karibu na Mwika) ni tofauti na kile cha Mashati au Useri na Tarakea.Lakini kijiografia, Mamsera mpaka Tarakea yote hiyo ni Rombo.Unaona hapo? Leo nitakufundisha Kiorombo kinachozungumzwa Mkuu-Kwa Maangulwa na sijui kama kitakufaa kwa shughuli zako ukiwa na yule mtu uliyenieleza kule chit-chat.
Leo tutaanza na (1)Nafsi (Persons) na tutatazama (2) vitendo(verbs)
(1)Nafsi:
Nafsi za Kiorombo ni kama zilezile za Kiswahili yaani
Kiswahili Kiorombo
Mimi Nyihany
.............................................
Wewe Vehave
..............................................
Yeye Ve
................................................
Sisi Sohaso
.................................................
Ninyi Nyohanyo
.................................................
Wao Vo
...................................................
Kila nafsi hapo juu ina kiambishi(subject prefix) yake. Tazama kiambishi kwa kila nafsi hapo chini.
Kiswahili Kiambishi (Subject Prefix) Kirombo Kiambishi .....................................................................................
Nafsi Mimi ni.... Nyihany ng....
.....................................................................................
Nafsi wewe u...... vehave u.....
......................................................................................
Nafsi yeye a..... ve ne....
........................................................................................
Nafsi sisi tu..... sohaso du.....
........................................................................................
Nafsi Ninyi m...... nyohanyo m........
.........................................................................................
Nafsi Wao wa..... Vo ve........
Baada ya hizo nafsi na viambishi vyake tutazame verbs
Common everyday verbs:
ku_la = i_la
Ku_lala = i_laa
Ku_cheka = i_seka
ku_tazama =i_sakwa
ku_ona = i_lolya
Hapa waweza kuona mara moja kwamba infinitive ya vitendo kiorombo ni i.. na kiswahili ni ku..
Kuunganisha nafsi na vitendo:
Kuunganisha nafsi na kitendo kuelezea ulichofanya kunategemea wakati (tense)
Present tense ya kiswahili ni _na_, ya kiorombo ni _i_. Tazama mifano ifuatayo:
Kiswahili: Ni na kwenda
Kiorombo Ng i enda
Tunacheka = Duiseka
Unaelewa siyo Nai? Naomba kwa leo tuishie hapo ila nakuachia mazoezi yafuatayo:
1. Tafsiri kwa kiorombo sentenso zifuatazo:
(a) Tunakula
(b)Wanacheka
(c)Unatazama
Sasa sijui kama approach hii umeipenda. Toa dukuduku zako uleze unavyotaka kujifunza.
Asante, Nyihany Hygeia