Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Yona Fares Maro
The ICT Pub
SOMO KUHUSU PROGRAMU/SOFTWARE BANDIA
Kumekuwa na ulanguzi wa programu/software haswa za kompyuta zinazofanywa na watu mbalimbali haswa kwenye nchi ambazo hazina sheria kali zinazohusiana na masuala haya , Ulanguzi huu umesababisha Serikali kupoteza mapato makubwa , waingizaji wa programu hizi nao kuingia hasara pamoja na hasara za kiusalama kwa watu wanaopatiwa programu hizo .
Mfano unaweza kupatia programu ya antivirus kwa ajili ya ulinzi wa komputa yako na vifaa vyake , unapounganisha komputa kwenye mtandao ili uweze kufanya updates kadhaa unaambiwa leseni ya antivirus hiyo sio yake labda imeshatumika au ni batili unatakiwa utumie leseni halali .
Kitu kama hicho kikitokea antivirus hiyo inaweza kuacha kabisa kufanya updates na kuruhusu virus kuingia kwenye komputa yako , nyingine zitaendelea kukukumbusha kuhusu leseni unayotumia si yake au batili lakini itaendelea kukulinda kwa muda fulani tu kisha itaacha kufanya hivyo .
Tofauti na vitu vingine vinavyouzwa kwenye maduka na sehemu zingine duniani programu zinazoendesha mashine kama komputa na vifaa vyake sio zako wewe unanunua leseni ya kukusaidia kutumia programu hiyo kwa muda fulani kisha unatakiwa kununua leseni nyingine .
NJIA ZINAZOTUMIWA NA WAHALIFU
1 - Kama umenunua leseni ya kompyuta moja ni kosa kutumia leseni hiyo kwenye kompyuta nyingine kosa hilo linaweza kukusababishia kifungo au faini kubwa kulingana na ulichofanya na bei za programu hizo na sheria za nchi husika au za kimataifa , unaponunua leseni ya kompyuta moja tumia kwenye kompyuta hiyo hiyo labda kama umenunua leseni ya komputa au kifaa zaidi ya kimoja na unaponunua leseni hiyo unatakiwa usome mkataba wako na mtengenezaji wa programu hiyo itaeleza kwa wazi aina ya leseni na jinsi unavyotakiwa kuitumia .
Hii ya kuweka leseni moja ya programu kwa komputa nyingi mara nyingi inafanyika kwenye komputa ambazo hazijaunganishwa kwenye mtandao haswa za watu wanaofanya huduma za steshenali mijini wanawekewa antivirus sana , programu za kutengeneza maumbo na aina nyingine ya programu hili ni kosa .
Hata kama ulinunua programu ukamuuzia rafiki yako , jirani yako au jamaa yako yoyote leseni hiyo hiyo hili pia ni kosa kuna watu wengi sana wanaotumiana au kupeana programu kwa njia hizi kwa kufikiri ni halali .
2 Angalia sana unavyoshusha programu na leseni kwa njia ya mtandao , ni vizuri ukanunua programu hiyo kwenye mtandao na kampuni husika mfano kama ni windows nunua toka Microsoft , kama ni autocad nunua toka autodesk kama ni adobe Photoshop fuata tovuti ya Kampuni husika ingawa kuna Tovuti zinazouza Pia programu hizi angalia sana masuala ya bei na kama kweli wanaushirikiano wowote na kampuni kuu , Na zaidi tembelea maduka ya programu Mji wako wa karibu unaweza kupata kwa urahisi zaidi .
La Mwisho ni kuangalia tovuti unazotembelea kudownload programu husika kuna tovuti kibao ambazo zinasambaza programu ambazo ni bandia au zimebadilishwa ili zionekane halali wakati sio kweli lakini ni kweli kwamba kuna programu ambazo ni za bure kabisa zinazotolewa kwa sababu maalumu .
Mfano kumekuwa na watu wanaouza programu ambazo zinatolewa bure na kampuni zilizotengeneza programu hizo lakini wanauza bila maelezo ni vizuri ukawa na mazoea ya kutembelea tovuti za programu husika kujua uhalali wa programu hiyo .
3 Kuna kampuni zinazouza au kutoa baadhi ya programu zao kwa ajili ya masoko maalumu haswa ya wanafunzi na kwa bei ndogo kwa ajili ya makundi hayo lakini unaweza kukuta programu hizi zinauzwa kwa bei ghali kuliko yake halisi au zinazuzwa kwa maelezo tofauti mara nyingi angalia makubaliano ya leseni hiyo utaelezwa kila kitu
4 Watu wengi sana wanaonunua komputa ambazo zimeshawekwa programu haswa operating system za Microsoft windows , au programu za office kama Office 2003 mpaka 2010 au antivirus wanapoenda kuunganisha kwenye mtandao ndio wanagundua hili haswa wanapotakiwa kuupdate programu hizo au kuzisajili kwa njia ya mtandao , wengi wetu tumezoea kutumia programu zingine kuondoa maonyo tunayopewa kwa programu hii ni bandia unatakiwa kununua na mambo mengine kama hayo .
MADHARA YA KUTUMIA/WEKA LESENI BANDIA
1 - Unapofanya mambo hayo hapo juu niliyoyataja unahatarisha usalama wa komputa yako na programu zingine zilizokuwa ndani ya computer hiyo kwa kushambuliwa Na kupata aina nyingine ya matishio kwenye mtandao au yanayoletwa kwa njia ya kuhamisha .
2 Hautoweza kuisajili programu hiyo kwahiyo haitoweza kufanya kazi vizuri kama inavyotakiwa mfano mzuri ni programu za ulinzi kama antivirus , internet security na zingine zinazotumika kwa shuguli maalumu .
3 Unakosesha Serikali mapato yake kwa njia fulani na unasaidia kupunguza ajira za watu ambao wametumia muda mwingi kutengeneza programu hizo ili kukufanya wewe uweze kufanya kazi zako kwa urahisi zaidi .
4 Ni njia nyingine ya Wizi ( Uhalifu ) wewe unayetumia na aliyekuuzia akikamatwa anaweza kufunguliwa mashitaka akafungwa au kulipishwa faini kubwa .
5 Kama umenunua programu kutoka kwenye tovuti ambayo ni bandia inawezekana ukatoa taarifa kuhusu kadi yako ya benki , wahalifu wanaweza kutumia kadi hiyo kwa ajili ya uhalifu mwingine au kuhamisha hela toka kwenye kadi hiyo , uwe unaangalia taarifa kuhusu anuani ya tovuti hiyo kabla ya kuamua kufanyanao biashara .
ONYO KWA WAFANYAKAZI
Kampuni na mashirika mengi hayana miongozo kuhusu Matumizi ya programu haswa na kompyuta na vifaa vingine vya mawasiliano na hata kama zipo basi hawaweki miongozo inayohusu programu kwahiyo ni rahisi kukuta wafanyakazi wakichukuwa programu za nje kwenda nazo makazini na kupeana na wafanyakazi wengine au kuingiza kwenye kompyuta zao kwa ajili ya kazi , Ni vizuri kampuni na mashirika kuwa na miongozo na sheria zingine zinazohusu programu na matumizi yake kwa ajili ya ulinzi na usalama wa masuala yao huko mbeleni .
ONYO KWA WAZAZI
Watoto wenu na vijana wenu wengine wanapenda kupeana programu hizi kwa njia nyingi tu mnatakiwa muwe makini haswa na komputa zenu za nyumbani zenye taarifa na vitu vyenu vingine endapo mtoto akaja kuweka programu kama hizi ambazo zinaweza kumwezesha mhalifu kuingilia komputa yako na kuhamisha taarifa au kupandikiza programu zingine , kumbuka kuweka programu za kudhibiti matumizi ya komputa kwa watoto wadogo .
Yona Fares Maro
The ICT Pub
The ICT Pub
SOMO KUHUSU PROGRAMU/SOFTWARE BANDIA
Kumekuwa na ulanguzi wa programu/software haswa za kompyuta zinazofanywa na watu mbalimbali haswa kwenye nchi ambazo hazina sheria kali zinazohusiana na masuala haya , Ulanguzi huu umesababisha Serikali kupoteza mapato makubwa , waingizaji wa programu hizi nao kuingia hasara pamoja na hasara za kiusalama kwa watu wanaopatiwa programu hizo .
Mfano unaweza kupatia programu ya antivirus kwa ajili ya ulinzi wa komputa yako na vifaa vyake , unapounganisha komputa kwenye mtandao ili uweze kufanya updates kadhaa unaambiwa leseni ya antivirus hiyo sio yake labda imeshatumika au ni batili unatakiwa utumie leseni halali .
Kitu kama hicho kikitokea antivirus hiyo inaweza kuacha kabisa kufanya updates na kuruhusu virus kuingia kwenye komputa yako , nyingine zitaendelea kukukumbusha kuhusu leseni unayotumia si yake au batili lakini itaendelea kukulinda kwa muda fulani tu kisha itaacha kufanya hivyo .
Tofauti na vitu vingine vinavyouzwa kwenye maduka na sehemu zingine duniani programu zinazoendesha mashine kama komputa na vifaa vyake sio zako wewe unanunua leseni ya kukusaidia kutumia programu hiyo kwa muda fulani kisha unatakiwa kununua leseni nyingine .
NJIA ZINAZOTUMIWA NA WAHALIFU
1 - Kama umenunua leseni ya kompyuta moja ni kosa kutumia leseni hiyo kwenye kompyuta nyingine kosa hilo linaweza kukusababishia kifungo au faini kubwa kulingana na ulichofanya na bei za programu hizo na sheria za nchi husika au za kimataifa , unaponunua leseni ya kompyuta moja tumia kwenye kompyuta hiyo hiyo labda kama umenunua leseni ya komputa au kifaa zaidi ya kimoja na unaponunua leseni hiyo unatakiwa usome mkataba wako na mtengenezaji wa programu hiyo itaeleza kwa wazi aina ya leseni na jinsi unavyotakiwa kuitumia .
Hii ya kuweka leseni moja ya programu kwa komputa nyingi mara nyingi inafanyika kwenye komputa ambazo hazijaunganishwa kwenye mtandao haswa za watu wanaofanya huduma za steshenali mijini wanawekewa antivirus sana , programu za kutengeneza maumbo na aina nyingine ya programu hili ni kosa .
Hata kama ulinunua programu ukamuuzia rafiki yako , jirani yako au jamaa yako yoyote leseni hiyo hiyo hili pia ni kosa kuna watu wengi sana wanaotumiana au kupeana programu kwa njia hizi kwa kufikiri ni halali .
2 Angalia sana unavyoshusha programu na leseni kwa njia ya mtandao , ni vizuri ukanunua programu hiyo kwenye mtandao na kampuni husika mfano kama ni windows nunua toka Microsoft , kama ni autocad nunua toka autodesk kama ni adobe Photoshop fuata tovuti ya Kampuni husika ingawa kuna Tovuti zinazouza Pia programu hizi angalia sana masuala ya bei na kama kweli wanaushirikiano wowote na kampuni kuu , Na zaidi tembelea maduka ya programu Mji wako wa karibu unaweza kupata kwa urahisi zaidi .
La Mwisho ni kuangalia tovuti unazotembelea kudownload programu husika kuna tovuti kibao ambazo zinasambaza programu ambazo ni bandia au zimebadilishwa ili zionekane halali wakati sio kweli lakini ni kweli kwamba kuna programu ambazo ni za bure kabisa zinazotolewa kwa sababu maalumu .
Mfano kumekuwa na watu wanaouza programu ambazo zinatolewa bure na kampuni zilizotengeneza programu hizo lakini wanauza bila maelezo ni vizuri ukawa na mazoea ya kutembelea tovuti za programu husika kujua uhalali wa programu hiyo .
3 Kuna kampuni zinazouza au kutoa baadhi ya programu zao kwa ajili ya masoko maalumu haswa ya wanafunzi na kwa bei ndogo kwa ajili ya makundi hayo lakini unaweza kukuta programu hizi zinauzwa kwa bei ghali kuliko yake halisi au zinazuzwa kwa maelezo tofauti mara nyingi angalia makubaliano ya leseni hiyo utaelezwa kila kitu
4 Watu wengi sana wanaonunua komputa ambazo zimeshawekwa programu haswa operating system za Microsoft windows , au programu za office kama Office 2003 mpaka 2010 au antivirus wanapoenda kuunganisha kwenye mtandao ndio wanagundua hili haswa wanapotakiwa kuupdate programu hizo au kuzisajili kwa njia ya mtandao , wengi wetu tumezoea kutumia programu zingine kuondoa maonyo tunayopewa kwa programu hii ni bandia unatakiwa kununua na mambo mengine kama hayo .
MADHARA YA KUTUMIA/WEKA LESENI BANDIA
1 - Unapofanya mambo hayo hapo juu niliyoyataja unahatarisha usalama wa komputa yako na programu zingine zilizokuwa ndani ya computer hiyo kwa kushambuliwa Na kupata aina nyingine ya matishio kwenye mtandao au yanayoletwa kwa njia ya kuhamisha .
2 Hautoweza kuisajili programu hiyo kwahiyo haitoweza kufanya kazi vizuri kama inavyotakiwa mfano mzuri ni programu za ulinzi kama antivirus , internet security na zingine zinazotumika kwa shuguli maalumu .
3 Unakosesha Serikali mapato yake kwa njia fulani na unasaidia kupunguza ajira za watu ambao wametumia muda mwingi kutengeneza programu hizo ili kukufanya wewe uweze kufanya kazi zako kwa urahisi zaidi .
4 Ni njia nyingine ya Wizi ( Uhalifu ) wewe unayetumia na aliyekuuzia akikamatwa anaweza kufunguliwa mashitaka akafungwa au kulipishwa faini kubwa .
5 Kama umenunua programu kutoka kwenye tovuti ambayo ni bandia inawezekana ukatoa taarifa kuhusu kadi yako ya benki , wahalifu wanaweza kutumia kadi hiyo kwa ajili ya uhalifu mwingine au kuhamisha hela toka kwenye kadi hiyo , uwe unaangalia taarifa kuhusu anuani ya tovuti hiyo kabla ya kuamua kufanyanao biashara .
ONYO KWA WAFANYAKAZI
Kampuni na mashirika mengi hayana miongozo kuhusu Matumizi ya programu haswa na kompyuta na vifaa vingine vya mawasiliano na hata kama zipo basi hawaweki miongozo inayohusu programu kwahiyo ni rahisi kukuta wafanyakazi wakichukuwa programu za nje kwenda nazo makazini na kupeana na wafanyakazi wengine au kuingiza kwenye kompyuta zao kwa ajili ya kazi , Ni vizuri kampuni na mashirika kuwa na miongozo na sheria zingine zinazohusu programu na matumizi yake kwa ajili ya ulinzi na usalama wa masuala yao huko mbeleni .
ONYO KWA WAZAZI
Watoto wenu na vijana wenu wengine wanapenda kupeana programu hizi kwa njia nyingi tu mnatakiwa muwe makini haswa na komputa zenu za nyumbani zenye taarifa na vitu vyenu vingine endapo mtoto akaja kuweka programu kama hizi ambazo zinaweza kumwezesha mhalifu kuingilia komputa yako na kuhamisha taarifa au kupandikiza programu zingine , kumbuka kuweka programu za kudhibiti matumizi ya komputa kwa watoto wadogo .
Yona Fares Maro
The ICT Pub