Soma hapa tafadhali

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
kuna mambo mengi sana yanatokea huko vijijini na vyombo vya habari hawaviripoti hata waandishi wa habari hawaripoti mambo haya
Ni dakika chache tu nimeingia kutoka Kaliua na Urambo. Tumekuwa na mikutano mitatu ya hadhara, tumefungua ofisi na matawi ya Chama. Hivyo si kweli kuwa Chadema inalipiza kisasi kwa CCM.

1)Kwanza inaelekea wengi hawafahamu malengo ya mikutano ya vijijini, na hasa kwa kuwa wanapata magazeti, wanatazama TV wanaamini Watanzania wote wanafanana. Lengo la Chadema katika hatua hii siyo kuwaambia CCM mbinu ya kuleta maendeleo wala kuwapa mikakati ya maendeleo. Ikumbukwe kuwa Chadema haikusanyi kodi yeyote ya wananchi na hivyo katika kipindi katika ya Uchaguzi kazi ya Chama cha siasa ni kujijenga kwa uchaguzi ujao,kukosoa Serikali iliyoko madarakani katika sera,Ilani na utekelezaji wa sera na ilani hiyo,kwa lengo la kuwaelimisha wananchi kuelewa udhaifu wa Chama hicho Tawala ili katika uchaguzi ujao tuiondoe. Hii ndiyo kazi yetu ya kikatiba. Chama cha siasa chenye kujua wajibu wake hakiwezi kuwa wasindikizaji tu. Sisi si washauri wa Serikali kwa kuipatia mbinu za kuongoza au mikakati ya kuongza na kuleta maendeleo. Kama yuko anayefikiri hivyo ni vema arejea vizuri majukumu ya vyama vya siasa.

2)Sisi tunaofika vizuri ndio tuko kwenye mazingira ya kutafsiri nini kizungumzwe katika kijiji fulani tofauti na kingine. Hii inatokana na uelewa unaotofautiana. Katika kijiji kingine hata ajenda iliyokwisha kuzoeleka kwa watu wa vijijini kama Listi of Shame iliyotolewa 2007 inabidi itolewe upya kwa kuwa wananchi hawajawahi kujua ni kwanini nchi yeny utajiri mkubwa kama TZ inaweza kuwa maskini, au inakuwaje wako wanaoogelea katika utajiri mkubwa wakati wao hawana zahanati, maji, wanakula mlo mmoja bila kujua kuwa inatokana na rasilimali nyingi kutafunwa na mafisadi. Najua wako ambao wanaumia kwa sababu zao kila tunapowataja mafisadi, lakini katika mazingira kama hayo Mwanasiasa makini ni yule anayejua mahitaji ya wananchi wake. Hivyo, Msishangae wana JF kuona tunayarudia yale yale. Mtakuwa wabinafsi iwapo hamtapenda watanzania wenzenu wayajue mnayoyajua nyie.

3) WanaJF wako katika jamvihili wanaoishi dunia yao wenyewe, au kwa kutaka au kwa bahati mbaya. Mathalan, nimestuka sana, kama niliyoelezwa Kaliua ni ya kweli Tanzania kuna ndugu zetu wanaishi bado Tanganyika ni si mwaka 47. Kaliua mtu mmoja aliyetajwa kama Baraka,mtoto wa Kapuya amekuwa tishio kwa wana Kaliua wote.Wanakaliua wanapigwa,wanachomewa nyumba, wanauawa na wakilalamika polisi nao inafyata kutokana baba Baraka kuwa tishio. Katika mazingira kama hayo usifikirie utazungumzia maendeleo zaidi ya kuwajengea ujasiri,mbinu za ukombozi na hata kuwafafanulia ufisadi mkubwa katika Jimbo kama hilo. Haiingii akilini mwa yeyote, kwa umaskini mkubwa tulioona Kaliua, na bado 72 Millioni zimetafunwa kwa jina la au kupitia kasma ya Mishahara (mishahara hewa, mishahara kulipwa kwa watumishi waliofariki, waliofukuzewa watoro n.k.) Kwa bahati mbaya hata tunapokuwa na Waandishi wa habari katika ziara mazingira na hotuba kama hizo hazipati nafasi kwa sababu yeyote ile, au hata kwa vile tu mwandishi anachagua anayotaka yeye.

Hali inatisha, ndiyo maana Chadema tumedhamiria kutoa elimu katika vijiji mbalimbali kati ya sasa na 2015. Wanaoumia na hiyo waumie tu. Wananchi wengi vijijini ndicho wanachohitaji kwa CCM siku mmoja haitawapa elimu hiyo. Wilaya/Jimbo Maskini kama Kaliua haingii akilini inapotokea Halmashauri inashindwa kutumia Tshs 659,697 Millioni katika mwaka wa Fedha, na hatimaye isionekane katika B/F kwa kuwa mfumo wa uhasibu wa almashauri hauna utaratibu huo. Matokeo yake hakuna anayejua fedha hizo zimeenda wapi. Kama Madfiwani wa Kamati ya Fedha hawajapangia matumizi ni nani anapangia matumizi. Kama Chadema hatutakemea ufisadi wa namna hiyo nani akemee. Ikumbukwe hii ni wilaya iliyokuwa hadi mwaka wa ukaguzi yaani Juni 30, 2010, mawaziri wawili na Spika wa Bunge.

Ndugu zangu wengine kwenye jamvi hili wanazungumza tu nadharia bila kujua hali halisi ya nchi yetu, au kwa makusudi tu wanataka kutuondoa kwenye ajenda zetu. Hatoki mtu hapa "ngo"(kwa lugha ya kina Kombani. Atakuwa mwanasiasa wa ajabu ambaye anahutubia mbele ya Ofisi ya "Spika" iliyojengwa Urambo, wakati Urambo haina Bunge na hivyo haina Spika. Hii ni ofisi iliyojengwa kwa milioni zaidi ya 300 na kuwekewa fenicha ya zaidi ya 170 Millioni, katika jimbo ambalo hakuna zahanati, vituo vya afya n.k. Mwanasiasa atakayeacha kutaja Ufisadi huu kwa kuwa wanaJamvi wachache wadhani wamechoka kusikia habari ya ufisadi atakuwa siyo mwanasiasa Makini. Kafiribigiri,naamini nimeeleweka.

Tushuke chini, tusidhani maisha ndani ya jamvi hili ndivyo yalivyo vijijini. Hata kama sisi tuna maisha mazuri, tuwafikirie wazazi wetu,shangazi zetu,wajomba zetu ambao bado wanaishi nyumba za tembe na majani, ambao mlo wa siku ni shida, ambao wameacha kula nyama kwa kuwa bei haishikiki nakadhalika. Hizi ni ajenda za kudumu na ndiyo namna ya kuondoa umaskini wa wananchi wetu kwa kuikaba serikali ngazio zote iache ufisadi na ielekeze rasilimali zote kuwahudumia wananchi badala ya kujijengea mahekalu, kutembelea mashangingi ya millioni 500. Hii ndiyo ajenda,inaewzerkana wewe huipendi lakini vijijini ndiyo mambo yenye "mshiko"

NB:hii post nimeiquote hapa hapa jamvini . dk. Slaa alikuwa anajibu swali la mtu . tujadili yaliyomo
 
Hii kweli naiunga mkono kwa utaratibu ulioko ni lazima watanzania watambue kwamba vita hii ni yetu sote na aina aja yakuchoshwa na neno ufisadi. kwakweli umesema maneno ya busara kwani umaskini tulio nao 75% uko vijijini na ukiukwaji wa haki za binadamu umekidhiri sana vijijini. kwa ilo tunabidi tuangalie kwa undani jinsi ya kuwafumbua macho watanzania wenzetu waliopo vijijini pamoja na kwaelimisha ili tuweze kukomboa nchi yetu 2015. shime kwa kila mwanaharakati kuchangia mada hii siyo kiushabiki bali kimawazo tena yakina ili tuweze kuangalia jinsi ya kufanya. Mungu ibariki Tabnzania
 
Nashukuru kwa taarifa. Endelea kutujuza. Mapambano mpaka kieleweke!!! Usijari wanaovuruga motion yetu maana wametumwa na CCM baada ya Consultant wao kuwadanganya kuwa Jamiii forum ni tishio kwao. Wamepandikiza magugu humu lakini wenye akili tunayajua magugu na mpunga!!!
 
Wale nyoka-magamba ndio huwa wana sema hakuna jipya lakini wananchi wengi wa vijijini watakuwa wanapata taarifa mpya tena wakiwaona live majukwaani. Hongereni.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Thanks kwa taarifa mkuu! Binafsi nakerwa sana na ubabe wa Kapuya na mwanae Baraka anayejiita "full boss". Mimi ni mkazi wa Kaliua na nimeushuhudia ubabe ma kinyama unaofanywa na watu hawa waliojimilikisha Kaliua as if ni ya baba yao.

Nakumbuka kipindi cha kampeni watu waliouliza maswali ya kumbana Kapuya kwenye mikutano yake walipata kipigo on the sport kutoka kwa mabaunsa walioongozwa na so called Baraka kapuya.

NOTE KW CDM: Kiukweli watu wa Kaliua tumechoshwa na hii hali na tulifikiri CUF wak
uwa wakombozi wetu; but due to on going situation between CCM and CUF tumepoteza matumaini. So ujio wa CDM Kaliua umefufua matumaini ya wengi. Tunawaomba mjipenyeze zaidi hasa maeneo ya Kamsekwa, Igagala hadi Usinge ili kujiimarisha zaidi before election ili finally ukombozi wa kweli upatikane.

THANKS GOD KWA KUILETA CDM KALIUA, THANKS GOD FOR Dr SLAA (Phd) AND HIS TEAM!!!
 
Mimi nilikuwa Tabora pia last wiki ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika Tabora kwa ujumla, nilienda Sikonge, Urambo na hata Kaliua. Kwa Tabora nzima miundo mbinu nu mibovu sana nadhani afadhali ya Kigoma. Barabara toka Tabora hadi urambo ni km 70 na ushee lakini tulisafiri masaa matano hii barabara ndo inaelekea kwa spika mstaafu SS na huyu ndo kajenga ofisi ya bunge urambo badala ya barabara.
Nilivutiwa na ofisi ya spika na mji ulivyo, umeme umekatika mwezi umeisha haujarudi kisa transforma eti iliungua. nawaonea huruma wana urambo na tabora kwa ujumla
 
Nimesikia sauti ya KIONGOZI, mtu anaejua jamii husika inataka nini na anajua namna ya kuwapa....
Ufisadi ndio kukwama kwetu kama ilivyopata kunenwa kuwa adui nambari moja wa maendeleo ya taifa baada ya uhuru ni UFISADI.
Hii ni agenda ya kudumu.....
Kweli kabisa kuna watu wanadhani nchi nzima ipo kama Dar, Arusha na Mwanza kumbe hata hayo maeneo yenyewe ukienda ndani zaidi hali mbaya kuliko unavyoweza kufikiria sasa ndio itakuwa huko kaliua..... hii nchi yote bado sana tofauti na hao wanajf wanaotaka kujidanganya kwa kuangalia mazingira yao binafsi,
Endeleeni kuwamulikia Watanganyika hao Taa mchana!
 
Safi sana wawakomboe na wangu wa Sikonge asanteni Chadema kwa kufika kwangu nadhani mliridhika na maandalizi niliyoyafanya. Keep up the mapinduzi halisi
 
Nawashukuru sana Chadema kwa kuliona hilo. Kimbulu heshima kwako mkuu. Nami nimewahi kukaa Kaliua, Urambo nk. Ni maskini wa kutupa na Baraka na baba yake ndo miungu ya huko. Wanachukua wake za watu waume zao wakija juu mh. anampachika jamaa mwenye mke cheo chochote ktk ofisi yake na mwingine aliwahi hata kupewa udiwani mh alizuia wengine kugombea akidai ni nafasi ya huyo anayemlia mkewe. Hadi leo jamaa anapokuja bungeni mara nyingi anajibebea mke huyo ama vitoto vingine toka kaliua. Pia ana hotel sikumbuki jina humo ndimo anashinda na kukesha akiwashughulikia watoto wa watu awzazi wakireact kesi zao polisi huzimwa.
 
Nawashukuru sana Chadema kwa kuliona hilo. Kimbulu heshima kwako mkuu. Nami nimewahi kukaa Kaliua, Urambo nk. Ni maskini wa kutupa na Baraka na baba yake ndo miungu ya huko. Wanachukua wake za watu waume zao wakija juu mh. anampachika jamaa mwenye mke cheo chochote ktk ofisi yake na mwingine aliwahi hata kupewa udiwani mh alizuia wengine kugombea akidai ni nafasi ya huyo anayemlia mkewe. Hadi leo jamaa anapokuja bungeni mara nyingi anajibebea mke huyo ama vitoto vingine toka kaliua. Pia ana hotel sikumbuki jina humo ndimo anashinda na kukesha akiwashughulikia watoto wa watu awzazi wakireact kesi zao polisi huzimwa.

sasa kwetu bongo haya mambo yanazimwa, na akitaka tu kugombea urais ndio utasikia yanachomolewa, kwa nini lakini tuna ukoloni ndani ya nchi yetu?
 
Kwa kweli hali ya Urambo inasikitisha sana,nilifika pale mwaka 2009 kwa mara ya kwanza sikuamini kama niko Tanzania kwa umaskini ulioko pale,maeneo ya ussinge,km 60 hali ni mbaya by that time Kapuya alikuwa waziri lakini alichowasaidia wakazi wa kaliua hata hakionekani
 
Uchafu wa Baraka Kapuya
1. Alishawahi kumpiga makofi na mateke mzee mmoja ambaye baadaye alipoteza maisha. Kisa mzee huyo alichelewa kutoka barabarani pale
alipopigiwa honi na Baraka.
2. Alishawahi kuongoza mauaji ya manafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Ushokola kwa kisa cha kugombea mwanamke katika ukumbi
wa millenium unaomilikiwa na Kapuya.
3. Alishawahi kumpiga makofi Mh diwani mbele ya kituo cha polisi huku mkuu wa kituo akishuhudia.

Cha kusikitisha, hakuna hatua iliyochukuliwa dhidi yake; mpaka leo yupo tu anakula starehe akiwa kama meneja wa vitegauchumi vya babayake ukiwemo ukumbi wa millenium.

Baba yake, Juma Kapuya hana alifanyalo hapa Kaliua zaidi ya kutembea na wake za watu na kujirusha kwenye kumbi za starehe kama alivyowahi kunaswa na chombo kimoja cha habari..................


kapuya.jpg

kapuya.jpg


kapuya.jpg
 
Kwa kweli hali ya Urambo inasikitisha sana,nilifika pale mwaka 2009 kwa mara ya kwanza sikuamini kama niko Tanzania kwa umaskini ulioko pale,maeneo ya ussinge,km 60 hali ni mbaya by that time Kapuya alikuwa waziri lakini alichowasaidia wakazi wa kaliua hata hakionekani
anachowasaidia bi hiki hapa kura si wanapiga wenyewe bana
Nawashukuru sana Chadema kwa kuliona hilo. Kimbulu heshima kwako mkuu. Nami nimewahi kukaa Kaliua, Urambo nk. Ni maskini wa kutupa na Baraka na baba yake ndo miungu ya huko. Wanachukua wake za watu waume zao wakija juu mh. anampachika jamaa mwenye mke cheo chochote ktk ofisi yake na mwingine aliwahi hata kupewa udiwani mh alizuia wengine kugombea akidai ni nafasi ya huyo anayemlia mkewe. Hadi leo jamaa anapokuja bungeni mara nyingi anajibebea mke huyo ama vitoto vingine toka kaliua. Pia ana hotel sikumbuki jina humo ndimo anashinda na kukesha akiwashughulikia watoto wa watu awzazi wakireact kesi zao polisi huzimwa.
 
Uchafu wa Baraka Kapuya
1. Alishawahi kumpiga makofi na mateke mzee mmoja ambaye baadaye alipoteza maisha. Kisa mzee huyo alichelewa kutoka barabarani pale
alipopigiwa honi na Baraka.
2. Alishawahi kuongoza mauaji ya manafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Ushokola kwa kisa cha kugombea mwanamke katika ukumbi
wa millenium unaomilikiwa na Kapuya.
3. Alishawahi kumpiga makofi Mh diwani mbele ya kituo cha polisi huku mkuu wa kituo akishuhudia.

Cha kusikitisha, hakuna hatua iliyochukuliwa dhidi yake; mpaka leo yupo tu anakula starehe akiwa kama meneja wa vitegauchumi vya babayake ukiwemo ukumbi wa millenium.

Baba yake, Juma Kapuya hana alifanyalo hapa Kaliua zaidi ya kutembea na wake za watu na kujirusha kwenye kumbi za starehe kama alivyowahi kunaswa na chombo kimoja cha habari..................


View attachment 27652

kapuya.jpg


kapuya.jpg

 
Kushiba mali ya kifisadi ni laana inayoharibu hata uwezo wa kawaida wa mtu kufikiri. Mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kukerwa eti kwa sababu watu wanautaja na kuwashutumu mafisadi mara nyingi. Wakati wa ubaguzi kusini mwa Africa, ubaguzi wa rangi ulipigiwa kelele na kila mpenda haki kwa miaka kibao hadi ulipotokomezwa. Mafisadi ktk Tanganyika watapigiwa kelele hadi wakome.
 
Back
Top Bottom