Waziri Lukuvi: Mtu anayetaka kujenga Kiwanda popote nchini aje kwangu, atapata ardhi ndani ya siku 7

Jay Milionea

JF-Expert Member
Apr 19, 2015
1,185
154
WAZIRI WILLIAM LUKUVI ABAINISHA MASUALA MUHIMU SEKTA YA ARDHI KATIKA "TUNATEKELEZA" TBC1 27/08/2016

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Serikali ya Awamu ya Tano imeanza kutekeleza program kabambe ya kupima ardhi yote ya Tanzania;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Utekelezaji umeanza mkoani Morogoro kwa kushirikiana na kampuni binafsi zilizosajiliwa ili kila mwananchi awe mkulima, mfugaji, mwenye kiwanda, shamba na kila aina ya shughuli atapimiwa eneo lake kuliongezea thamani;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Nakuhakikishia katika miaka 10 kila kipande cha ardhi Tanzania kitakuwa kimepangwa na kupimwa;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Serikali imeanza kudhibiti bei ya kupima ardhi kwa kushirikiana na wapimaji binafsi;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Serikali itaweka ukomo wa kumiliki ardhi.Haiwezekani mtu anamiliki ardhi kubwa ambayo hata haitumii;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Ni marufuku wageni na wawekezaji kwenda vijijini moja kwa moja kununua ardhi.Waje kwangu au wapitie TIC tutawapa ardhi haraka wawekeze;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Mtu anayetaka kujenga kiwanda popote aje kwangu nitampatia ardhi ndani ya siku 7;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wizara imeshatenga viwanja 240 kwa ajili ya Viwanda Kigamboni.Anayetaka aje hakutakuwa na rushwa wala ubabaishaji;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wawekezaji wanaohodhi tu ardhi bila kuitumia muda wao umekwisha.Rais kashaagiza na tunafanyiakazi.Wasiotumia ardhi tutawapatia wengine;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wananchi wote waliodhulumiwa viwanja Dar es Salaam kwa makosa ya watendaji wa Serikali tumeanza kuwapa fursa na heshima ya kuwapa viwanja vingine mbadala;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Naagiza Halmashauri zote ziwapatie viwanja mbadala wananchi ambao walidhulimiwa viwanja vyao kwa makosa ya watendaji;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wananchi wote walioko kwenye makazi holela tutawapa heshima ya kushirikiana nao na kuwapimia ili wafaidike na makazi yao na kulipa kodi;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Mji mpya wa Kigamboni...nimeona wamekuja wadau wana mawazo mapya baads ya kuwa Manispaa.Tutazungumza nao zaidi. Hatutashindwana.

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: NHC inajiendesha kibiashara lakini nimezuia kupandisha kodi mpya hadi niridhie;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Ni ndoto yangu kuifanya sekta ya ardhi ichangie zaidi katika pato la Taifa

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Nataka pia kutimiza ndoto ya Rais Magufuli ya kuondokana na migogoro isiyo na tija ya ardhi;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Muda wa watendaji kusababisha migogoro umekwisha...muda wa watu kuhodhi ardhi kubwa bila kuitumia nao umekwisha;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wapo wananchi wameanza kunisifu na wapo wanaonilaumu wakitamani nifike kila mahali kuwasaidia lakini nashindwa. Lakini bado ninasafari ndefu kuwafikia; Nitafurahi kuona siku moja nchi hii haina migogoro ya ardhi.
 
Lukuvi ninakukubali sana,,Mungu awe Nawe katika kazi ngumu ya Ardhi iliyojaa Rushwa miaka nenda rudi...
 
cc. Lizaboni.
naona umefukia kichwa kwenye mchanga kwa aibu jinsi ulivyokuwa umemsema vibaya huyu Mheshimiwa.ulilenga kumharibia tukose mchapakazi makini lakini fitina zako hewa zimeshindwa.
 
WAZIRI WILLIAM LUKUVI ABAINISHA MASUALA MUHIMU SEKTA YA ARDHI KATIKA "TUNATEKELEZA" TBC1 27/08/2016

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Serikali ya Awamu ya Tano imeanza kutekeleza program kabambe ya kupima ardhi yote ya Tanzania;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Utekelezaji umeanza mkoani Morogoro kwa kushirikiana na kampuni binafsi zilizosajiliwa ili kila mwananchi awe mkulima, mfugaji, mwenye kiwanda, shamba na kila aina ya shughuli atapimiwa eneo lake kuliongezea thamani;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Nakuhakikishia katika miaka 10 kila kipande cha ardhi Tanzania kitakuwa kimepangwa na kupimwa;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Serikali imeanza kudhibiti bei ya kupima ardhi kwa kushirikiana na wapimaji binafsi;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Serikali itaweka ukomo wa kumiliki ardhi.Haiwezekani mtu anamiliki ardhi kubwa ambayo hata haitumii;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Ni marufuku wageni na wawekezaji kwenda vijijini moja kwa moja kununua ardhi.Waje kwangu au wapitie TIC tutawapa ardhi haraka wawekeze;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Mtu anayetaka kujenga kiwanda popote aje kwangu nitampatia ardhi ndani ya siku 7;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wizara imeshatenga viwanja 240 kwa ajili ya Viwanda Kigamboni.Anayetaka aje hakutakuwa na rushwa wala ubabaishaji;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wawekezaji wanaohodhi tu ardhi bila kuitumia muda wao umekwisha.Rais kashaagiza na tunafanyiakazi.Wasiotumia ardhi tutawapatia wengine;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wananchi wote waliodhulumiwa viwanja Dar es Salaam kwa makosa ya watendaji wa Serikali tumeanza kuwapa fursa na heshima ya kuwapa viwanja vingine mbadala;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Naagiza Halmashauri zote ziwapatie viwanja mbadala wananchi ambao walidhulimiwa viwanja vyao kwa makosa ya watendaji;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wananchi wote walioko kwenye makazi holela tutawapa heshima ya kushirikiana nao na kuwapimia ili wafaidike na makazi yao na kulipa kodi;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Mji mpya wa Kigamboni...nimeona wamekuja wadau wana mawazo mapya baads ya kuwa Manispaa.Tutazungumza nao zaidi. Hatutashindwana.

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: NHC inajiendesha kibiashara lakini nimezuia kupandisha kodi mpya hadi niridhie;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Ni ndoto yangu kuifanya sekta ya ardhi ichangie zaidi katika pato la Taifa

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Nataka pia kutimiza ndoto ya Rais Magufuli ya kuondokana na migogoro isiyo na tija ya ardhi;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Muda wa watendaji kusababisha migogoro umekwisha...muda wa watu kuhodhi ardhi kubwa bila kuitumia nao umekwisha;

[HASHTAG]#LUKUVI[/HASHTAG]: Wapo wananchi wameanza kunisifu na wapo wanaonilaumu wakitamani nifike kila mahali kuwasaidia lakini nashindwa. Lakini bado ninasafari ndefu kuwafikia; Nitafurahi kuona siku moja nchi hii haina migogoro ya ardhi.
Ngoja lizaboni aje aisome hii habari, atasema Lukuvi anaendesha hujuma,
 
Nani aje kufanya uwekezaji kwenye nchi isiyoheshimu katiba yake, isiyokuwa na dira ya kitaifa kwa maandishi? Yeyote anaamua atakalo, hata wazawa wanabughuziwa, itakuwaje kwa wawekezaji wageni? Siku roho ya Idd Amini ikitua Tanzania si watafukuzwa tu hao wawekezaji?
Weka mpango mkakati kwenye maandishi na uhakikishe yanafanyiwa kazi.
 
Back
Top Bottom