Sokoine angefaa kuongoza kizazi cha sasa?

LE GAGNANT

JF-Expert Member
Jan 20, 2011
1,241
251
Edward Moringe Sokoine ansifika kuwa alikuwa mmoja wa viongozi wapenda haki na uwajibikaji. Lakini alikuwa pia na silka ya utawala wa ki-imla, nakumbuka jinsi alivyolishughulikia suala la wahujumu uchumi, kipindi kile badala ya kutatua tatizo la uhaba wa bidhaa ndiyo ikawa bidhaa zinafichwa na kuuzwa kwa bei za kuruka. Kwa maoni yangu ni kiongozi wa kutumia mamlaka zaidi kuliko kutafuta suluhisho la matatizo ya nchi. Kwa kizazi cha siasa za sasa sidhani kama angefika mbali.
 
Edward Moringe Sokoine ansifika kuwa alikuwa mmoja wa viongozi wapenda haki na uwajibikaji. Lakini alikuwa pia na silka ya utawala wa ki-imla, nakumbuka jinsi alivyolishughulikia suala la wahujumu uchumi, kipindi kile badala ya kutatua tatizo la uhaba wa bidhaa ndiyo ikawa bidhaa zinafichwa na kuuzwa kwa bei za kuruka. Kwa maoni yangu ni kiongozi wa kutumia mamlaka zaidi kuliko kutafuta suluhisho la matatizo ya nchi. Kwa kizazi cha siasa za sasa sidhani kama angefika mbali.

Mh. Edward Moringe Sokoine (RIP) alishatangulia mbele ya haki. Kwamba angekuwepo angefaa kuongoza kizazi cha sasa au la kwa ufupi ni kwamba haiwezekani awepo tena. Labda umjadili kwa mengine lakini sio kwa hilo; halafu hii hoja yako inaonekana ina hila ndani yake tena hila mbaya. Mkakati maalumu kwa malengo maalumu mkianzia na Mzee Nyerere hapa: https://www.jamiiforums.com/habari-...tulikwenda-kupigana-msumbiji-kama-nani-2.html. Tena post zote za leo leo. Achana na hizo hadithi. Au ndio maandalizi ya "zamu yetu"?
 
Edward Moringe Sokoine ansifika kuwa alikuwa mmoja wa viongozi wapenda haki na uwajibikaji. Lakini alikuwa pia na silka ya utawala wa ki-imla, nakumbuka jinsi alivyolishughulikia suala la wahujumu uchumi, kipindi kile badala ya kutatua tatizo la uhaba wa bidhaa ndiyo ikawa bidhaa zinafichwa na kuuzwa kwa bei za kuruka. Kwa maoni yangu ni kiongozi wa kutumia mamlaka zaidi kuliko kutafuta suluhisho la matatizo ya nchi. Kwa kizazi cha siasa za sasa sidhani kama angefika mbali.

Jamani, haya maneno kama "haki" na "uwajibikaji" wengine, (ijapokuwa siyo mtoa mada), tunayatumia tu ovyo ovyo bila kujali kama hapo yanapo-apply yana ukweli? Ama ni ule utumwa wa fikra na mawazo tuliofugwa wakati huo na wengi wetu bado wanashindwa "kujivua gamba" hilo? Sokoine alibobea kwa kunyang'anya watu mali zao, kinyume cha haki, kuwasweka watu wasio na hatia jela, kinyume cha haki, na kutunga sheria batili za kufanya mambo yaliyotendeka kabla ya hiyo sheria kuweko kuwa ni makosa, kinyume cha haki. Kama ni kuwajibika, Sokoine akiwajibika kwa Nyerere tu; siyo kwa haki, wala kwa sheria wala kwa wananchi. Na Nyerere alikuwa hawajibiki kwa mtu yeyote !

Kama huyo ni mmoja wa viongozi "wapenda haki na wawajibikaji" basi ukweli ni kwamba tunatumia hayo maneno ovyo ovyo tu bila kujali maana yake. Tuwe makini katika kufikiri.
 
Back
Top Bottom