Soko la Tandika Lauzwa

Serikali ya JK imekuwa ikitoa tamko baada ya tamko kuhusu kupunguza umasikini. Kuanzia kukubali kwa MDGs mpaka maisha bora kwa kila mtanzania, kinacho nishangaza ni kwamba utapunguza vipi umasikini wakati unmployment rate yako ni 40%. Kingine kinacho nishangaza ni kwamba wakati wa Mkapa hadisi ilikuwa ni kujiajiri, then watu wakajitahidi kujiajiri. Sasa leo unakuja kufunga soko ukidhani unafukuza wauzaji 1000+, unachosahu ni kwamba kuna support industry ambayo ni kubwa sana, which includes waendesha mikokoteni, wauza mazao na wengine wengi. Industry hiyo imeajiri work force kubwa kuliko Vodacom ambayo ina wafanyakazi 600.

Maamuzi ya kisiasa ni maamuzi ya kishenzi more than anything. Majority ya wanasiasa wa Tanzania ni Maboga, yaani empty head haijalishi wana PhD au std seven wote ni same. Wanaweza kusucrifise industry iliyo ajiri 1000+ people sababu ya kujenga fremu 15 za maduka ambazo zitajiri watu 50 or less. What a non sense.
 
Hap kuna vitu vingi sana vinatakiwa kurekebishwa na manispaha ya temeke mfano
  1. Wafanyabiashara waliokuwepo wanapelekwa wapi na kwa gharama za nani? maana inawezekana hawajafikiria hawa watu watafanya nini, kuwaacha tu ni kuongeza majambazi kwa maana lazima wale hata kama ni kuua mtu.
  2. Je kwanini hawakuwashirikisha wakati wa kutafuta mwekezaji ili na wao watoe maoni yao kabla maamuzi, utawara wa kulazimishana maamuzi matokea yake ndio hayo ambayo lazima yataleta ugomvi kwani ukimpa mtu binafsi hatajali masirahi ya wananchi wa kawaida
  3. Tenda ya kubinfisisha hilo soko ilitangazwa lini au mwekezaji kateuliwa na viongozi tu bila kufuata taratibu, maana angefuata taratibu wafanyabiashara wangejua kabla hata hajaleta mchanga sokoni.
  4. Je manispaa itafaidika na nini kwa kubinafisisha hilo soko, mapato yataongezeka kwa asilimia ngapi na nani atakuwa na responsibility ya kukalabati soko na miundo mbinu yake.

Sio swala la kuwaambia kuwa soko limebinafishwa wakati wanajua kuwa hata wao ni stakeholders wa hilo soko, mimi nawaunga mkono kabisa kwa kugoma utawara wa mabavu imepitwa na wakati.
 
366.jpg
... na kutokana na kutoa pesa zake itachukua muda wa miaka 8 kabla ya mkataba wake kuisha.
Tatizo kubwa ni pale tulipojibana kwamba Serikali haiwezi kufanya biashara; hii kitu itatuumiza sana kama tusipoibadili maana ni wazi haina maana yoyote kama tutaweka misingi imara ya "accountability". Hata hao waliokuwa wanalazimisha tuamini kuwa Serikali haiwezi kufanya biashara wanaanza kujirudi kwa ku'nationalize' mali zilizopo nchini kwao baada ya kupata somo toka China (usiniambia ni sababu ya 'financial crisis' ilhali chanzo chake ni China kuzalisha mali zilizoua soko la bidhaa za Magharibi).

Nasema hivi kwa sababu lengo kuu la Manispaa ya Temeke ni kutaka mwekezaji ajenge na baada ya hiyo miaka 8 wabaki na miliki ya maduka hayo. Wanajua kwamba baada ya miaka 8 wataanza kutengeneza faida kupitia maduka hayo kwa manufaa ya Manispaa. Ninachojiuliza ni mbinu gani wataitumia tofauti na kuyakodisha kwa wapangaji kama ambavyo atafanya huyo mwekezaji? Kama itakuwa kuyakodisha (pengine kwa kutumia kampuni binafsi kukusanya mapato toka kwa wapangaji), ni kweli kwamba Manispaa ya Temeke imeshindwa kujenga maduka hayo sasa hivi hata kupitia mkopo Benki? Je, si kweli kwamba mbinu kama hii ndio iliyotumika kujenga Machinga Complex? Uko wapi ubunifu wa madiwani wa manispaa ya Temeke?

Nadhani suruhisho ni kwa Manispaa kuchukua jukumu la kujenga hayo maduka na kisha kuweka kampuni ambayo kazi yake itakuwa kukusanya mapato na kuyakilisha kwenye vikao husika. Tuhachane na dhana ya kwamba hatuwezi kufanya biashara hata katika mazingira kama haya ambayo lengo ni kumpatia mwananchi wa chini unafuu na kuwaondolea urasimu wa watu binafsi. Wananchi wamechoka na mizigo wanayotwishwa kila kukicha, wanategemea kuona viongozi wakija na ubunifu utaosaidia kuinua hali za maisha yao.
 
kama ni chafu, uza. uza hata masoko mengine yaliyobaki kama tandare,buguruni, magomeni, kimala na mengine. tunahitaji majengo mazuri, mapya, yenye usafi, vyoo vizuri, na wauzaji wazuri. sio unanunua kitu anayekuuzia ameenda ****** hajanawa mikono, anatoka jasho, nguo chafu, chini tope hajafanya usafi hopeless. ni bora tuuze na ikiwezekana wenye uwezo wajenge majengo mazuri ya kisasa ya masoko. hatuwezi kubakia na mambo ya kizamani ili kuwafurahisha machinga!
 
Kama nimeelewa vizuri, barua iliyoandikwa na manucipal ya Temeke imeweka wazi kuwa M/s Technical Developer alishinda zabuni ya kuendesha soko hilo. Hii ina maanisha kuwa, mwekezaji huyo alishindanishwa na wengine na akashinda zabuni hiyo. Vile vile, mwekezaji atatakiwa kujenga maduka kuzunguka soko kwa gharama zake mwenyewe na atalikodi soko hilo kwa wafanya biashara kwa kipindi cha miaka 8.

Kwa mtazamo wangu, hatua hiyo inaashiria kuwa;

1. Manucipal ya Temeke imeona ni rahisi kwao kutumia kampuni binafsi kuendesha soko, na wao kupata kodi kutoka kwake badala ya kulisimamia yenyewe. Hii ni njia mbadala ya kuendesha soko, na inakubalika endapo taratibu za kufanya hivyo zimetumika vizuri
2. Manucipal haina/haitaki kutumia pesa zake kujenga soko hilo (200mil). Nadhani ni uamuzi mzuri, hasa kama Manucipal ina lengo la kutumia pesa zake kuendeleza miundombinu mingine kama barabara, hospitali, n.k. badala ya kuziweka katika ujenzi wa soko
3. Muda wa miaka 8 uliotolewa si mwingi kiasi cha kuzua wasiwasi. Ni muda mfupi ambapo mwekezaji anatarajiwa kuwa amemaliza shughuli zake katika soko hilo. Inawezekana baada ya muda huo, mwekezaji mwingine au yule yule akapewa tena muda wa ziada wa kuendesha soko hilo (endapo atakuwa amefanya hivyo kwa ufanisi katika kipindi cha kwanza). Fursa hii inaipa Manucipal uwezo wa kuendelea kusimamia soko endapo itathibitika kuwa mwekezaji aliemaliza muda wake, hakuweza kufikia malengo yaliyotarajiwa na Manucipal
4. Ni namna ya serikali za mitaa kushirikiana na wananchi katika shughuli za maendeleo. Mwendelezaji wa soko ataisaidia Manucipal kuendeleza na kusimamia shughuli zake
5. Sioni madhara makubwa yanayoweza kuwakumba wafanya biashara katika soko hilo. Usumbufu utakaotokea unaweza ukawa katika kipindi cha ujenzi tu. Ila mwekezaji atawahitaji wafanya biashara hao kwa kuwa ndio wateja alionao sasa, kuliko kutafuta wengine wapya. Utaratibu atakaoutumia katika kuwapangishia sehemu za biashara upya unaweza kuwa suala la mjadala.

Nadhani serikali ikiwa inatumia njia kama hizi itaongeza ufanisi kwa kiasi kikubwa. Kwa sasa serikali inajaribu kufanya kila kitu bila kushirikiana na wadau wengine. MAdhara yake ni kushindwa kwa miradi mingi (hata iliyo mizuri)
 
kama ni chafu, uza. uza hata masoko mengine yaliyobaki kama tandare,buguruni, magomeni, kimala na mengine. tunahitaji majengo mazuri, mapya, yenye usafi, vyoo vizuri, na wauzaji wazuri. sio unanunua kitu anayekuuzia ameenda ****** hajanawa mikono, anatoka jasho, nguo chafu, chini tope hajafanya usafi hopeless. ni bora tuuze na ikiwezekana wenye uwezo wajenge majengo mazuri ya kisasa ya masoko. hatuwezi kubakia na mambo ya kizamani ili kuwafurahisha machinga!

Aaaah Aaah Aaah!! Wewe kweli ni Mwana wa Mungu
 
Kama nimeelewa vizuri, barua iliyoandikwa na manucipal ya Temeke imeweka wazi kuwa M/s Technical Developer alishinda zabuni ya kuendesha soko hilo. Hii ina maanisha kuwa, mwekezaji huyo alishindanishwa na wengine na akashinda zabuni hiyo. Vile vile, mwekezaji atatakiwa kujenga maduka kuzunguka soko kwa gharama zake mwenyewe na atalikodi soko hilo kwa wafanya biashara kwa kipindi cha miaka 8.

Kwa mtazamo wangu, hatua hiyo inaashiria kuwa;

1. Manucipal ya Temeke imeona ni rahisi kwao kutumia kampuni binafsi kuendesha soko, na wao kupata kodi kutoka kwake badala ya kulisimamia yenyewe. Hii ni njia mbadala ya kuendesha soko, na inakubalika endapo taratibu za kufanya hivyo zimetumika vizuri
2. Manucipal haina/haitaki kutumia pesa zake kujenga soko hilo (200mil). Nadhani ni uamuzi mzuri, hasa kama Manucipal ina lengo la kutumia pesa zake kuendeleza miundombinu mingine kama barabara, hospitali, n.k. badala ya kuziweka katika ujenzi wa soko
3. Muda wa miaka 8 uliotolewa si mwingi kiasi cha kuzua wasiwasi. Ni muda mfupi ambapo mwekezaji anatarajiwa kuwa amemaliza shughuli zake katika soko hilo. Inawezekana baada ya muda huo, mwekezaji mwingine au yule yule akapewa tena muda wa ziada wa kuendesha soko hilo (endapo atakuwa amefanya hivyo kwa ufanisi katika kipindi cha kwanza). Fursa hii inaipa Manucipal uwezo wa kuendelea kusimamia soko endapo itathibitika kuwa mwekezaji aliemaliza muda wake, hakuweza kufikia malengo yaliyotarajiwa na Manucipal
4. Ni namna ya serikali za mitaa kushirikiana na wananchi katika shughuli za maendeleo. Mwendelezaji wa soko ataisaidia Manucipal kuendeleza na kusimamia shughuli zake
5. Sioni madhara makubwa yanayoweza kuwakumba wafanya biashara katika soko hilo. Usumbufu utakaotokea unaweza ukawa katika kipindi cha ujenzi tu. Ila mwekezaji atawahitaji wafanya biashara hao kwa kuwa ndio wateja alionao sasa, kuliko kutafuta wengine wapya. Utaratibu atakaoutumia katika kuwapangishia sehemu za biashara upya unaweza kuwa suala la mjadala.

Nadhani serikali ikiwa inatumia njia kama hizi itaongeza ufanisi kwa kiasi kikubwa. Kwa sasa serikali inajaribu kufanya kila kitu bila kushirikiana na wadau wengine. MAdhara yake ni kushindwa kwa miradi mingi (hata iliyo mizuri)

Well said Recta,

....sijui hata kwa nini mwanzilishi wa hii mada anasema "limeuzwa"........
 
".....tz bwana........kama tumerogwa"

Ndiyo bongo hiyo, turogwe mara ngapi?, ....huko si kurogwa kwani mara nyingi akulogaye unakuwa humfahamu au anakuwa anakuvizia usiku.....Huku mi nionavyo ni kama kulaaniwa vile, kwani ni bora urogwe kuliko ulaaniwe!...Mazingaombwe ninayoyaona Tanzania yamekaaa kilaana laana tu!

nilikuwepo!
 
Hivi Mhe. Raisi anajua hili au kama kawaida funika kombe? Na hiyo bajeti waliyoweka ya soko imeenda wapi? Hivi Kikwete yupo kweli na anajali wa-Tanzania?

Lusajo, Kikwete hahusiki na kuuzwa kwa soko la Tandika na sidhani kama anahusika na chochote kinachoendelea ndani ya nchi yetu. Amewekwa pale Ikulu kama picha tu wakati mafisadi wakifanya mavitu yao. Wanauza soko hata kumtaja ni nani aliyeuziwa wanaogopa wanaitaja kampuni!!! Sasa hiyi kampuni si ina wamiliki? Kwa nini majina yao yasianikwe hadharani!? Kazi kweli kweli!!! :(
 
Lusajo, Kikwete hahusiki na kuuzwa kwa soko la Tandika na sidhani kama anahusika na chochote kinachoendelea ndani ya nchi yetu. Amewekwa pale Ikulu kama picha tu wakati mafisadi wakifanya mavitu yao. Wanauza soko hata kumtaja ni nani aliyeuziwa wanaogopa wanaitaja kampuni!!! Sasa hiyi kampuni si ina wamiliki? Kwa nini majina yao yasianikwe hadharani!? Kazi kweli kweli!!! :(
Msalie Mtume, Duh! kamanda kauli zingine zinatisha kwani hazina ukweli wowote na zinaashiria chuki...
 
Lusajo, Kikwete hahusiki na kuuzwa kwa soko la Tandika na sidhani kama anahusika na chochote kinachoendelea ndani ya nchi yetu. Amewekwa pale Ikulu kama picha tu wakati mafisadi wakifanya mavitu yao. Wanauza soko hata kumtaja ni nani aliyeuziwa wanaogopa wanaitaja kampuni!!! Sasa hiyi kampuni si ina wamiliki? Kwa nini majina yao yasianikwe hadharani!? Kazi kweli kweli!!! :(

Tafadhali mpe rais heshima yake. Hizo kejeli na dharau haisaidii kitu, kubali hali halisi tu kwamba JK ni rais hadi 2015.

Unajua fika kuwa Mbowe hawezi, Lipumba porojo, Mrema kaachia mchuma, Cheyo kwishne, Mvungi ntoke vipi, Prof Shayo RIP, Mtikila salalee yuko busy na kesi, Zitto siasa basi anaenda kutunga vitabu.
 
Naunga mkono huu mradi wa BOT (Build, Operate and Transfer). Kuna principle hapa. Serikali za Mitaa lazima ziweze kuendeleza maeneo yao kwa kutumia BOT.

Kwa upande wa Tandika, mwekezaji atajenga (Build) atumie kwa miaka 8 (Operate) kisha arudishe (Transfer) soko kwa Serikali ya Mtaa. Hizo shilingi milioni 200 ni kiduchu, lakini principle iliyotumka ni sahihi.

Wachuuzi waliopo Tandika wamedhani soko ni lao? Wao ni wapangaji tu, na mwenye mali ana haki ya kukataa kurenew mkataba.

Let us be independent thinkers. Si lazima wote tushabikie huu ukumbatiaji wa umasikini ambao umejaa kwenye mitaa yetu ya Kiswahili.
 
Lusajo, Kikwete hahusiki na kuuzwa kwa soko la Tandika na sidhani kama anahusika na chochote kinachoendelea ndani ya nchi yetu. Amewekwa pale Ikulu kama picha tu wakati mafisadi wakifanya mavitu yao. Wanauza soko hata kumtaja ni nani aliyeuziwa wanaogopa wanaitaja kampuni!!! Sasa hiyi kampuni si ina wamiliki? Kwa nini majina yao yasianikwe hadharani!? Kazi kweli kweli!!! :(


Hapo dnipo wanapo nfurahisha hawa jamaa, yaani pamoja na wananchi kuchachamaa na ufisadi kiasi hiki bado wanaendeleza dili zao feki. Nikwamba hawawezi kubuni miradi yakuwaingizia pesa au wanakuwa kaa mateja, maana teja anachojua ni kuuza chochote anachokiona apate pesa ya unga wa kubwia
 
Back
Top Bottom