Soko La Mbao!

Dodo18

JF-Expert Member
Feb 26, 2011
315
93
Nilikua naulizia kuhusu soko la biashara ya mbao Dar. Wanasema hii biashara inalipa sana mjini ni kweli na soko kweli kubwa ?
 
mkuu ukitaka kujua uhondo wa ngoma uingie ucheze!taabu ya bness ya mbao ni madalali!wanaharibu kila kitu!pia wafanya biashara hawana cash,wanachukua kwa mkopo!ndio shida yenyewe ilipo.
 
mkuu ukitaka kujua uhondo wa ngoma uingie ucheze!taabu ya bness ya mbao ni madalali!wanaharibu kila kitu!pia wafanya biashara hawana cash,wanachukua kwa mkopo!ndio shida yenyewe ilipo.

Umesema kweli kabisa. Madalali, matapeli na wakopaji wapo wengi sana katika biashara ya mbao.

Ushauri wangu kama unataka kuanza biashara ya kuuza mbao ni kuwa na mtaji wa kutosha has wakati wa kuanza biashara yako ili uweze kumudu gharama mbalimbali kama kununua mbao zenyewe, kuzisafirisha kama lazima na kulipa pango. Ni swala la "working capital".Hii itakuweza kuepukana na matapeli wanaokuja kukwambia uwakiopeshe nusu ya mbao wanazotaka kununua. Uzuri wa biashara ya mbao ni kuwa haziozi. Utakapoanza utapata shida ya kupata wateja lakini wakishalizoea duka lako utapata raha kabisa. Narudia tena, usikopeshe mbao.
 
Ni vema uanze kwa kujiuliza hasa ni nani mlaji/mtumiaji wa hiyo product then uone uta-deal nae vipi.,na hapo utakuwa umekwepa kugongana na madalali. Binafsi nilishawahi kufanya zoezi hili miaka 3 iliyopita. Namna niliyotumia ni kuwafikia haya Makampuni ya Ujenzi ambayo niliona yana Fursa nyingi za miradi ya ujenzi wa magorofa then nikafanya mawasiliano na nikapata oda na wao wanalipa cash,japo kuwapata wahusika hawa huwa ni ngumu kwani nadhani walinzi wa makampuni haya wamedhibitiwa na madalali wasiruhusu hii fursa kwa washindani wao. Hivyo huo ni mfano mmoja wapo ambao kwangu niliufanya kwahiyo waweza chagua aina mbalimbali za watumiaji wa mwisho then ukabuni namna ya kukutana nao.,hapo utafanikiwa kuwaruka madalali. Ishu nyingine ufanye utafiti mzuri wa Working Capital wa kukidhi mzunguko huo.
 
Hey kama kweli kaka unahitaji hii biashara inalipa sana!alafu kama unahitaji kuuza mimi ninafanya shughuri zangu buguruni ndio kunasoko kubwa sana hapa ukihitaji mzigo wowote toka shamba mimi nitausika hapo wewe tu.
 
buguruni ndio kitovu cha hii bness,ila madalali sasa! Kingsimba na wewe ni dalali?mm ni mnunuzi mzuri wa mbao,hebu nipe bei ya 10X1,nahitaji Pc 200 aina ya cyprus!ukitoa bei nzuri ntakua mteja wako!mwaga hapa jamvini.
 
Last edited by a moderator:
Anaetaka mbao za Cyprus ambazo treated ani PM kila size nasafirisha kokote Tanzania na nchi jirani. (Serious Buyers only, no middleman). Nawasiliana na wanunuzi tu dalali apotee na nauza cash tu, hakuna mkopo wala mchupa. Bei yangu ni poa kabisa na bidhaa za ubora wa hali ya juu.
 
buguruni ndio kitovu cha hii bness,ila madalali sasa! Kingsimba na wewe ni dalali?mm ni mnunuzi mzuri wa mbao,hebu nipe bei ya 10X1,nahitaji Pc 200 aina ya cyprus!ukitoa bei nzuri ntakua mteja wako!mwaga hapa jamvini.
1x10 cypres=1500/ft ongea!
 
Last edited by a moderator:
Anaetaka mbao za Cyprus ambazo treated ani PM kila size nasafirisha kokote Tanzania na nchi jirani. (Serious Buyers only, no middleman). Nawasiliana na wanunuzi tu dalali apotee na nauza cash tu, hakuna mkopo wala mchupa. Bei yangu ni poa kabisa na bidhaa za ubora wa hali ya juu.

kaka me nina office na mashamba mafinga kama unahitaji mbao naomba unitafute j3 nikiwa ofisini tutafanikisha bila madalali...nitafute kwa namba hii 0713935738
 
Kwa faida ya jukwaa, ni vizuri tukielimishana vizuri kuhusu aina ya mbao, samahani kama nitakosea, kupata cyprus kwa mkupuo kwa kiwango kikubwa ni kazi ngumu sana. Misitu ya miti hiyo kwa sasa naweza kusema haipo. Iliyopo ni michache sana na kazi sana kupata, labda uende Rombo kule kama bado ipo. Kinyume na hapo ni kuokoteza hapa na pale ili ujaze kafuso kamoja.

Ukienda Malawi unaweza kupata.

Wengi wanachanganya na pinus patula ( pines) wanadhani ni cypruss. Ila ukipata miti 500 ya cypruss na ukachana mbao, fedha ipo. Ni hayo.
 
buguruni ndio kitovu cha hii bness,ila madalali sasa! Kingsimba na wewe ni dalali?mm ni mnunuzi mzuri wa mbao,hebu nipe bei ya 10X1,nahitaji Pc 200 aina ya cyprus!ukitoa bei nzuri ntakua mteja wako!mwaga hapa jamvini.

kaka 1x10@13000kwa ubao wa futi 12 haina udalali.
 
Last edited by a moderator:
Anaetaka mbao za Cyprus ambazo treated ani PM kila size nasafirisha kokote Tanzania na nchi jirani. (Serious Buyers only, no middleman). Nawasiliana na wanunuzi tu dalali apotee na nauza cash tu, hakuna mkopo wala mchupa. Bei yangu ni poa kabisa na bidhaa za ubora wa hali ya juu.

Check inbox I need it
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom