Kivumah
JF-Expert Member
- Jan 7, 2008
- 2,428
- 1,050
asante sana kaka. nitazipitia but ishu ni kwamba maswali yangu huku hakuna wa kuyajibu.
btw ukiwa umenunua hisa ndogo ina maana wewe ndo unakuwa kibaraka wa wenye hisa nyingi??
Sio kibaraka, ktk lugha rahisi tunasema utakula kwa urefu wa kamba yako, kwamba endapo kampuni ambayo umenunua hisa kwayo ikipata faida na kuamua kutoa gawio kwa wanahisa wake, basi kama wewe ni mmoja wao kiwango cha gawio utakachopata kitatokana na ukokotoaji unaotokana na hisa unazomiliki katika kampuni hio, kama ambavyo mchangiaji mmoja ameeleza hapo juu.
All in all biashara ya hisa hapa kwetu bado haina mwamko sana kama ilivo kwa wenzetu nchi zilizoendelea, na ndio maana wenzetu Marekani na Ulaya endapo soko la hisa likiyumba basi inapelekea pia kudorora kwa uchumi zao