Mimi nawashangaa mnaopinga sofia simba kusema anapambana na mafisadi. kwani hao waliojibatiza mgambo wa kupambana na ufisadi wamepata wapi uhalali wa kusema wanachukia ufisadi?....unahoji kwanini sofia simba aseme leo, alikuwa wapi? kwani akina Mwakyembe, Annae Killango, Olesendeka, Mengi na wenzao walikuwa wapi nchi yetu ikiuzwa na mkapa waone leo?
Huyu mama ni m-pambanaji na amedhamiria kupinga ufisadi kwa msio mjua mama Simba hanunuliki ni mtu wa msimamo na hateteleki.
Tatizo ili mtu awe mpinga ufisadi lazima awe na surname Mwakyembe, Selelii, Kilango, sendeka, kimaro et al. Mnaibinafsisha vita ya ufisadi kalabagho!
Kaazi kweli kweli.
Hii inakera na inatia hasira. Kwa mtaji huu wanatupoteza lengo, ni sawa na ujanja wa mijizi ambayo nasikia ikikimbizwa, akiona kafika kona na amepata upenyo mzuri, yeye pia huungana na wakimbizaji mwizi na kupiga kelele za 'mwizi, mwizi'.
Kama wamekosa la kusema bora wanyamaze.
Imepotezwa muelekeo wake, na CCM ndio wahusika wakubwa wa Ufisadi na wao tunashindwa kujua ni nani fisadi wa CCMau vita ya ufisadi inaanza kufanikiwa?