Snow inavyofunika magari ulaya siku hizi

Hahahaaaa, hii naikumbuka sana miaka ileee.....

Ilinyesha snow halafu ikanyesha mvua kidogo na temperature ikashuka na yale majimaji yakaganda kama usiku wa saa sita.

Asubihi yake, Madokta wote wa mifupa waliitwa kazini na unga wa gypsy hadi ukaisha baadhi ya hospital. Magongo ya kutembelea bei ikapanda. Watu kibao wakawa na POP mikononi, miguuni na sijui hata kiunoni (Mkimbili?).

Hiyo inaonekana na kungaa kama KIOO. Achana na kioo barabarani au kwenye pavements. Watu walicheza breakdance bila kutaka na unasikia tu puu, ukigeuka nyuma, mtu anagaa gaa kusimama au "Yalaa" basi ujuwe kavunjika au kuteguka.
Inyeshe snow wakati temperature imedrop halafu mvua inyeshe, afadhali kuendesha gari kwenye tope linaloteleza kuliko barafu iliyoganda barabarani.

Nchi inavyochafuka huna hamu na unakumbuka bora Afrika kwetu pamoja na umaskini kuna unafuu. Nchi haipendezi, watu wanaonekana macho tu kwani hata midomo na ua zimefunikwa. Unaonja kama uko mwisho wa dunia vile.

Hawa jamaa matatizo yamewafanya waendelee, maana kabla ya maendeleo sijui walikuwa wanaishije. Ndio maana Ulaya hakuna miti ya asili kwa vile yote waliimaliza kukoka moto kipindi cha winter.
 
Hahahaaaa, hii naikumbuka sana miaka ileee.....

Ilinyesha snow halafu ikanyesha mvua kidogo na temperature ikashuka na yale majimaji yakaganda kama usiku wa saa sita.

Asubihi yake, Madokta wote wa mifupa waliitwa kazini na unga wa gypsy hadi ukaisha baadhi ya hospital. Magongo ya kutembelea bei ikapanda. Watu kibao wakawa na POP mikononi, miguuni na sijui hata kiunoni (Mkimbili?).

Hiyo inaonekana na kungaa kama KIOO. Achana na kioo barabarani au kwenye pavements. Watu walicheza breakdance bila kutaka na unasikia tu puu, ukigeuka nyuma, mtu anagaa gaa kusimama au "Yalaa" basi ujuwe kavunjika au kuteguka.

We usinikumbushe, maana hali kama hiyo ilinipata kidogo nigonge mlingoti wa utility. No control at all. Akaja mzungu naye yale yale, akanishauri niache kuendesha vinginevyo nitaumiza kakorolla kangu na mimi mwenyewe na yeye akafanya viyvo hivyo. Akaniulia na muda gani nchini nikamwambia miezi 4, kanitazama kwa huruma na kunipa pole baada ya kumbwambia natoka Afrika. Kwa kuwa wao walikuwa wenyeji na mimi ndo winter ya kwanza kuona. Akaita polisi, basi wakaja na wakaita lile karandika la kumwagia chumvi just 20 minutes hali ikawa nzuri kupita barafu yote iliyeyuka na kubaki majimaji. Kesho yake nikaenda kuangalia sehemu ile ikoje nikaona tu pavement imekuwa nyeupe kama vila wamemwagia majivu kumbe ni ile chumvi waliyomwaga tulipokwama.

Pavement kwenye barafu balaa tupu. Bora barabara za kwetu za kushindiliwa na kokoto mawe yale yanasaidia kidogo.
 
aiseeeeee........arifu na mko yupo bongo eeeeh? aiseeee goood sana
Yoyo karibu uje ugande huku kama una ngiri ya tumbo au pumu usije ukaje kufa huku.

Mzee ulikuwa pande za wapi na College gani uliyosoma, maana inawezekana ulisoma na mbeba Box mmoja maarufu sana siku hizi amekuwa ni Rais wa wabeba mabox!!
Mkuu mbona unapenda kumtania Rais wako? mbona hujiheshimu ?
 
Hii ndiyo hali halisi ya majuu siku hizi, hakinogi kitu, ukihitaji kutoka nje unajiuliza kwanza kama ni lazima unachoenda kufanya ukifanye leo au la.
Mie sijatoka siku ya 3 nimesingizia kazini naumwa na ngiri wamekubali nimeomba mapumziko ya wiki moja maana hali mbaya Mkuu hata dukani siendi napiga simu wanaleta chakula nyumbani kwangu si unajuwa huku kila kitu unapiga simu? kuita Gesi maji ya kunywa vitu vya dukani ni simu tu sitoki nje mpaka kuwe hali shwari nagopa baridi nipo na heater karibu nalikumbatia sana nakumbuka sana nyumbani bongo.
 
<label class="txtClrDef" style="display: block;"> </label>
DSC00037.jpg




IMG_0033_1.jpg



9c35.jpg






7fa4.jpg







20ca.jpg






c110.jpg





fc0e.jpg
 
Mzizi Mkavu basi siku hizi nakuonea huruma bili ya umeme, maana ndani hakukaliki bila hita, na masharti ya nyumba siku hizi lazima hita iwe on vinginevyo mabomba ya maji yanapasuka. Nakumbuka nilivyowekewa mashari na Landlord na kukumbushwa kipindi cha winter kinapoingia. Anayway ni kipindi cha kukomaa sana usoni ka uko Kusini nyanda za juu au lushoto vile.
Bili ya umeme kwa mwezi unaweza kujikuta unalipa Dola 100 au Dola 150 kwa mwezi na umeme haukatiki ovyo ovyo bila ya sababu muhimu ukikatika basi unarudi baada ya haizidi nusu saa na hivyo hivyo inaweza kutokea labda kwa mwezi mara moja au mbili aghalabu kusikia umeme umekatika huku sio sawa na huko kwetu Bongo Giza totoro utafikiri tupo makaburini.
 
By the way suala la umeme kwa wazungu its not an issue hata siku moja, mimi nimemaliza mwaka umeme haujawahi kukatika na kwa jinsi ambavyo kila kitu kwao kina tumia umeme sijui huko kukatika kutatoka wapi, vyao vya umeme kila kona.Hwa jamaa mimi sidhani kama itatokea siku tukafika walipofika milele amina.
 
Na mpaka leo ni zaidi ya watu 300 tayari wamekufa kwa baridi. Ukraine ikiongoza, na nchi zingine ni Luthenia, poland, n,k. Hakika hali ni mbaya na tunashukuru tu umeme upo na hita kila wakati hasa ktk hizi nchi za ulaya zenye maendeleo makubwa. kwa kweli hali ni mbaya sana kwa homeless kwasasa, kwani ndiyo wengi wao wanakufa kutokana na baridi.
 
Na mpaka leo ni zaidi ya watu 300 tayari wamekufa kwa baridi. Ukraine ikiongoza, na nchi zingine ni Luthenia, poland, n,k. Hakika hali ni mbaya na tunashukuru tu umeme upo na hita kila wakati hasa ktk hizi nchi za ulaya zenye maendeleo makubwa. kwa kweli hali ni mbaya sana kwa homeless kwasasa, kwani ndiyo wengi wao wanakufa kutokana na baridi.

Umegusa pabaya kuhusu homeless katika nchi za magharibi. Ninachoshangaa kwa nini serikali haifanyi tijihada kusaidia watu hawa, Mambo yakishakuendea vibaya nchi tajiri maskini ni ombaomba na wa kulala chini ya madaraja yanayocross haighway au express ways, na wengine kando ya makontaina. Kipindi hiki cha baridi inatia huruma sana. Wanaoweza kuwasaidia ni nyumba za mashirika ya makanisa hasa ya kilokole, lakini masharti huko ni kama unavyojua wanaishia kufukuzwa.
 
chicago_il.jpg


Hii picha imenikumbusha mbaoi siku nilipochelewa kwenda darasani college huko baada ya kukwamba njiani nilipotoka kazini usiku sababu ya snow kunyesha futi tatu sawa na karibu meter moja

Hongera mkuu naona umekaa sana ulaya mpaka umesahau kuandika vizuri kiswahili
 
Bili ya umeme kwa mwezi unaweza kujikuta unalipa Dola 100 au Dola 150 kwa mwezi na umeme haukatiki ovyo ovyo bila ya sababu muhimu ukikatika basi unarudi baada ya haizidi nusu saa na hivyo hivyo inaweza kutokea labda kwa mwezi mara moja au mbili aghalabu kusikia umeme umekatika huku sio sawa na huko kwetu Bongo Giza totoro utafikiri tupo makaburini.

Mbona wengine na vijizungu vikija huku vinajifanya kushangaa pindi ngereja akikasiriaka
 
Mie sijatoka siku ya 3 nimesingizia kazini naumwa na ngiri wamekubali nimeomba mapumziko ya wiki moja maana hali mbaya Mkuu hata dukani siendi napiga simu wanaleta chakula nyumbani kwangu si unajuwa huku kila kitu unapiga simu? kuita Gesi maji ya kunywa vitu vya dukani ni simu tu sitoki nje mpaka kuwe hali shwari nagopa baridi nipo na heater karibu nalikumbatia sana nakumbuka sana nyumbani bongo.

Pole sana Mzizimkavu..Jamani hili baridi si mchezo! sasa huko ndani huwi mpweke zaidi mana unalala na kuamka ila kuboreka kunazidi mkuu. Nahisi masikio yatakatika hapa Russia kwa hali hii next week nimeamua niende nyumbani kwa wiki 3. Nashangaa hawa watu wamezaliwaje na kuzeekea huku, kama wanaishi kwenye friza daily..!
 
Hivi nimebakia mimi tu sijaenda ulaya?? haki ya nani nazamia!!!

Uchumi ulivyoyumba huko majuu balaa, makampuni makubwa yanafunga biashara kila kukicha kama wamepagawa vile, gharama za uendeshaji haziwiani na gharama za mapato. Watu nasikia wanabana matumizi sasa hivi ile mbaya.
 
mimi juzi kati hapa, niliamua kukata mzizi wa fitina,............... nikasonga bonge la ugali nikauangamiza kwa samaki wa kufa mtu................. sasa kilichofuatia, sufuria liliungulia ukoko.................... nikaliloweka na kuliegesha kwenye balcony................ nilipoenda kutaka kulijulia hali (kuliosha), nikakuta maji niliyolowekea yameganda kama jiwe!................ imagine nyumba za huku, balcony nayo huwa imefungwa pande zote na si za wazi kama za kwetu bongo, ...................lakini wapi, baridi inapiga kama kwenye friza!!!.................. ilibidi kutafuta msaada wa maji ya moto kabla ya kuendelea zaidi....................

siku moja tena wiki moja iliyopita,...............bwana mkubwa mmoja akaniitia box linalolipa vizuri nibebe japo kwa siku moja hivi kumshikia kuwa yeye hajisikii vizuri siku hiyo.................. sehemu yenyewe ya kupigia box unabadili tram mbili na basi moja ............... duh! kufika huko ikawa viroja...................... barabara zimejaa matope ya snow, zimechafuka zimekuwa nyeusiiii tiiiii ............... na watu wanakula mieleka barabarani kama WWE vile................ mi mwenyewe nililamba snow down mara moja hivi................ ngoma ilikuwa wakati wa kurudi baada ya box!!................. kituoni watu wamejazana kila mtu kimya haongei ............... gubigubi kama maninja wa boko haram................. basi likifika limejaa, kuteremka hateremki mtu................. na kila mtu anataka kuingia kwanza, hata utaratibu wa foleni ulivurugika................ nikapata basi baada ya saa moja na nusu................. kumbuka mbele kuna tram mbili zinanuisubiri........................ dah!! hawa watu kabla "hawajaendelea" sijui walikuwa na maisha gani???................ kwa kweli sipati picha!!.......................

kwa kweli pamoja na kutengeneza dolari fresh, .................. lakini nilikoma ubishi!!......................
 
Sisi ambao hatujawahi kufika europe hatuna cha kuchangia hapa!!!!

Tiba
 
Back
Top Bottom