Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imedai fujo zinazoendelea hivi sasa kisiwani Pemba ni mpango maalumu na wa muda mrefu wa serikali ya Marekani.
Kauli hiyo ya kulishutumu taifa kubwa duniani imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana nje ya kituo cha uandikishaji cha shule ya Sizini mkoami Kaskazini Pemba.
Mwishoni mwa mwezi uliopita, Marekani ilitoa taarifa kwa raia wake ikiwataka kuwa makini na safari za kisiwani Pemba ambako ilisema kuna vurugu zinazohusiana na uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Marekani, ambayo ina tabia ya kutahadharisha raia wake kufanya ziara sehemu ambazo kuna ama kunaweza kutokea vurugu, ilieleza kuwa tangu kuanza kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura, kumekuwa na vurugu kubwa kisiwani Pemba na kuwaonya raia wake kuwa makini na mikusanyiko wawapo visiwani Zanzibar, huku ikiwataka wajiandikishe kwenye ubalozi wake mara watakapowasili Tanzania.
Lakini SMZ ilijibu vikali taarifa hiyo ya tahadhari kwa raia wa Marekani na jana Waziri Juma alieleza msimamo wa serikali yake kuhusu kitendo hicho cha Marekani.
"SMZ inaamini kwamba Marekani ilikuwa inajua nini kitatendeka katika kisiwa cha Pemba na ndio maana ikaanza kutoa tahadhari kwa wananchi wake mapema," alisema Waziri Juma ambaye alisema ametumwa na serikali kwenda Pemba kuangalia hali ya usalama.
"Haiwezekani Marekani iwatake wananchi wake wasitembelee kisiwa cha Pemba halafu iwe haijui nini kitatokea katika kisiwa hicho.
"Sisi serikali ya Zanzibar tunaamini kwamba Marekani ndio iliyopanga mpango huu maalumu wa kufanyika vurugu huku Pemba na ndio maana wakawatahadharisha raia wake mapema wasitembelee Pemba. Kama walikuwa hawajui kwa nini watoe tahadhari? Wanajua na ndio waliopanga mpango huu kwa kutafuta sababu wanazozijua wao."
Zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura kisiwani Zanzibar limekumbwa na vurugu kubwa na awali serikali ililazimika kulisimamisha baada ya wananchi kurushiana mawe na polisi. Juzi polisi walilazimika kutumia silaha za moto kutawanya wananchi ambao walijikusanya nje ya vituo vya kujiandikishia kwa lengo la kuzuia wenzao kujiandikisha.
Tayari nchi 14 wanachama wa Umoja wa Ulaya (EU) na Marekani zimeshaitaka SMZ kushughulikia matatizo yaliyojitokeza kwenye zoezi la uandikishaji wapigakura ili kuufanya uchaguzi ujao kuwa huru na wa haki. Tatizo kubwa linalopingwa na wananchi wa Zanzibar ni matumizi ya kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi kama ndio sifa kuu ya mtu kuandikishwa.
Wananchi wengi visiwani Zanzibar, ambako mkaazi ni yule aliyeishi kwa miaka mitatu mfululizo, wanadai wamenyimwa vitambulisho vya ukaazi na hivyo hawawezi kuandikishwa kupiga kura.
Waziri huyo pia alisema ili kuondokana na masharti ya nchi wahisani, SMZ itaanza kusimamia uchaguzi wake na kuachana na ufadhili wa wahisani kwa madai kuwa uzoefu unaonyesha kuwa ufadhili huambatana na masharti, jambo ambalo alisema si jema.
Kwa mujibu wa Waziri Juma, pamoja na kuwa nchi wahisani wanatoa fedha kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali, hakuna sababu ya nchi hizo kuingilia mambo ya ndani kwa kuwa kila nchi ina uhuru wake na inajiendesha.
Alisema fedha zinazochangwa na wafadhili ndio zinazosababisha matatizo yanayototokea Pemba sasa kwa kuwa wafadhili huwa wana masharti yao, hivyo SMZ itaanza kusimamia uchaguzi wake hata kama italazimika kuchangishana shilingi moja moja.
"Mtu akikufadhili ndio anakuwekea masharti anayotaka yeye lakini sisi wenyewe tutaanza kuchanga fedha wenyewe ili kusimamia uchaguzi wetu wenyewe maana tushaona hawa wanataka kutuletea maneno mengi," alisema Juma.
Waziri Juma alisema SMZ haitaki kuona fedha za wafadhili zinatumika kuvuruga amani na kwamba itatumia nguvu zake zote kurudisha amani iliyoanza kutoweka katika kisiwa cha Pemba.
"Sisi ni wasimamizi wa sheria… Marekani walikuwa wanajua nini kitatokea lakini tunasema tutatumia nguvu zote katika kurejesha hali ya amani kwa sababu tunajua hii ni mbinu tu na hatutaivumilia hali hii," alisisitiza waziri huyo.
Alisema pamoja na matatizo yote yaliyotokea, uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 utafanyika kama ulivyopangwa hata kama Zanzibar nzima wataandikishwa watu 100.
"Tunasema uchaguzi utafanyika na upo pale pale hata kama ni watu 100 wataandikishwa, hatutaacha kufanya uchaguzi kwa visingizio kama hivi kwa sababu hatutaki kufadhiliwa; uchaguzi ni wetu wenyewe," alisema Waziri Juma.
Alisema kuanzia sasa mtu yeyote au kiongozi atakayehamasisha wananchi kufanya fujo ili kuharibu zoezi hilo, atachukuliwa hatua za kisheria.
"Haiwezekani mwananchi anataka kutumia haki yake, halafu mwingine anamkataza kufanya hivyo. Kwa kweli kama tukimgundua kiongozi au mtu yeyote tutamchukulia hatua za kisheri kwa kuwa anachochea vurugu," alisema Hamza.
Alisema kuwa wananchi ambao bado hawajapata fursa ya kujiandikisha, watapata fursa wakati mwingine kwa kuwa zoezi hilo litafanywa kwa awamu tatu.
Kuhusu tatizo la vitambulisho vya ukaazi, Waziri Juma alikanusha kuwa ndilo lililosababisha kutokea kwa mvutano kati ya wananchi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) na kusababisha zoezi hilo la uandikishaji kugomewa.
"Vitambulisho ni propaganda za kisiasa tu ambazo zinafanywa na wafuasi na viongozi wa upinzani, lakini sisi tunasema tunatumia nguvu zote katika kuhakikisha tunamaliza suala hili. Wacha wao wagome lakini tutawaandikisha wanaotaka kujiandikisha," alisema.
Alisema hali hairidhishi lakini ameahidi kutumia nguvu za ulinzi katika kurejesha amani, na kudokeza kuwa fedha nyingi zimetumika katika kuimarisha ulinzi na usalama katika kipindi cha siku tatu zilizopita.
"Sitaki kusema ni kiasi gani tumetumia lakini nakwambia ni fedha nyingi sana tumeshatumia na tunaendelea kutumia kw akuwa hilo si tatizo kubwa," aliwaambia waandishi wa habari..........
SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG
Kauli hiyo ya kulishutumu taifa kubwa duniani imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana nje ya kituo cha uandikishaji cha shule ya Sizini mkoami Kaskazini Pemba.
Mwishoni mwa mwezi uliopita, Marekani ilitoa taarifa kwa raia wake ikiwataka kuwa makini na safari za kisiwani Pemba ambako ilisema kuna vurugu zinazohusiana na uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Marekani, ambayo ina tabia ya kutahadharisha raia wake kufanya ziara sehemu ambazo kuna ama kunaweza kutokea vurugu, ilieleza kuwa tangu kuanza kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura, kumekuwa na vurugu kubwa kisiwani Pemba na kuwaonya raia wake kuwa makini na mikusanyiko wawapo visiwani Zanzibar, huku ikiwataka wajiandikishe kwenye ubalozi wake mara watakapowasili Tanzania.
Lakini SMZ ilijibu vikali taarifa hiyo ya tahadhari kwa raia wa Marekani na jana Waziri Juma alieleza msimamo wa serikali yake kuhusu kitendo hicho cha Marekani.
"SMZ inaamini kwamba Marekani ilikuwa inajua nini kitatendeka katika kisiwa cha Pemba na ndio maana ikaanza kutoa tahadhari kwa wananchi wake mapema," alisema Waziri Juma ambaye alisema ametumwa na serikali kwenda Pemba kuangalia hali ya usalama.
"Haiwezekani Marekani iwatake wananchi wake wasitembelee kisiwa cha Pemba halafu iwe haijui nini kitatokea katika kisiwa hicho.
"Sisi serikali ya Zanzibar tunaamini kwamba Marekani ndio iliyopanga mpango huu maalumu wa kufanyika vurugu huku Pemba na ndio maana wakawatahadharisha raia wake mapema wasitembelee Pemba. Kama walikuwa hawajui kwa nini watoe tahadhari? Wanajua na ndio waliopanga mpango huu kwa kutafuta sababu wanazozijua wao."
Zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura kisiwani Zanzibar limekumbwa na vurugu kubwa na awali serikali ililazimika kulisimamisha baada ya wananchi kurushiana mawe na polisi. Juzi polisi walilazimika kutumia silaha za moto kutawanya wananchi ambao walijikusanya nje ya vituo vya kujiandikishia kwa lengo la kuzuia wenzao kujiandikisha.
Tayari nchi 14 wanachama wa Umoja wa Ulaya (EU) na Marekani zimeshaitaka SMZ kushughulikia matatizo yaliyojitokeza kwenye zoezi la uandikishaji wapigakura ili kuufanya uchaguzi ujao kuwa huru na wa haki. Tatizo kubwa linalopingwa na wananchi wa Zanzibar ni matumizi ya kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi kama ndio sifa kuu ya mtu kuandikishwa.
Wananchi wengi visiwani Zanzibar, ambako mkaazi ni yule aliyeishi kwa miaka mitatu mfululizo, wanadai wamenyimwa vitambulisho vya ukaazi na hivyo hawawezi kuandikishwa kupiga kura.
Waziri huyo pia alisema ili kuondokana na masharti ya nchi wahisani, SMZ itaanza kusimamia uchaguzi wake na kuachana na ufadhili wa wahisani kwa madai kuwa uzoefu unaonyesha kuwa ufadhili huambatana na masharti, jambo ambalo alisema si jema.
Kwa mujibu wa Waziri Juma, pamoja na kuwa nchi wahisani wanatoa fedha kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali, hakuna sababu ya nchi hizo kuingilia mambo ya ndani kwa kuwa kila nchi ina uhuru wake na inajiendesha.
Alisema fedha zinazochangwa na wafadhili ndio zinazosababisha matatizo yanayototokea Pemba sasa kwa kuwa wafadhili huwa wana masharti yao, hivyo SMZ itaanza kusimamia uchaguzi wake hata kama italazimika kuchangishana shilingi moja moja.
"Mtu akikufadhili ndio anakuwekea masharti anayotaka yeye lakini sisi wenyewe tutaanza kuchanga fedha wenyewe ili kusimamia uchaguzi wetu wenyewe maana tushaona hawa wanataka kutuletea maneno mengi," alisema Juma.
Waziri Juma alisema SMZ haitaki kuona fedha za wafadhili zinatumika kuvuruga amani na kwamba itatumia nguvu zake zote kurudisha amani iliyoanza kutoweka katika kisiwa cha Pemba.
"Sisi ni wasimamizi wa sheria… Marekani walikuwa wanajua nini kitatokea lakini tunasema tutatumia nguvu zote katika kurejesha hali ya amani kwa sababu tunajua hii ni mbinu tu na hatutaivumilia hali hii," alisisitiza waziri huyo.
Alisema pamoja na matatizo yote yaliyotokea, uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 utafanyika kama ulivyopangwa hata kama Zanzibar nzima wataandikishwa watu 100.
"Tunasema uchaguzi utafanyika na upo pale pale hata kama ni watu 100 wataandikishwa, hatutaacha kufanya uchaguzi kwa visingizio kama hivi kwa sababu hatutaki kufadhiliwa; uchaguzi ni wetu wenyewe," alisema Waziri Juma.
Alisema kuanzia sasa mtu yeyote au kiongozi atakayehamasisha wananchi kufanya fujo ili kuharibu zoezi hilo, atachukuliwa hatua za kisheria.
"Haiwezekani mwananchi anataka kutumia haki yake, halafu mwingine anamkataza kufanya hivyo. Kwa kweli kama tukimgundua kiongozi au mtu yeyote tutamchukulia hatua za kisheri kwa kuwa anachochea vurugu," alisema Hamza.
Alisema kuwa wananchi ambao bado hawajapata fursa ya kujiandikisha, watapata fursa wakati mwingine kwa kuwa zoezi hilo litafanywa kwa awamu tatu.
Kuhusu tatizo la vitambulisho vya ukaazi, Waziri Juma alikanusha kuwa ndilo lililosababisha kutokea kwa mvutano kati ya wananchi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) na kusababisha zoezi hilo la uandikishaji kugomewa.
"Vitambulisho ni propaganda za kisiasa tu ambazo zinafanywa na wafuasi na viongozi wa upinzani, lakini sisi tunasema tunatumia nguvu zote katika kuhakikisha tunamaliza suala hili. Wacha wao wagome lakini tutawaandikisha wanaotaka kujiandikisha," alisema.
Alisema hali hairidhishi lakini ameahidi kutumia nguvu za ulinzi katika kurejesha amani, na kudokeza kuwa fedha nyingi zimetumika katika kuimarisha ulinzi na usalama katika kipindi cha siku tatu zilizopita.
"Sitaki kusema ni kiasi gani tumetumia lakini nakwambia ni fedha nyingi sana tumeshatumia na tunaendelea kutumia kw akuwa hilo si tatizo kubwa," aliwaambia waandishi wa habari..........
SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG