Elections 2010 Sms za uchochezi wa kisiasa wakulaumiwa ni tcra?

payuka

JF-Expert Member
Jun 17, 2010
829
127
Wadau Kwanza habarini!

Poleni sana na harakati za kumsapoti Raisi wa watanzania kuingia Ikulu, Raisi Mwenye PHD ya ukweli ( siyo fekifeki za kuchakachuliwa).

MADA:
Kwa mtizamo wangu mimi...kuhusu hizi SMS za Uchochezi ambazo watu wanazipata kila kukicha, wa Kulaumiwa hapa ni Tume ya Mawasiliano ( TCRA) kwa kushindwa kudhibiti haraka iwezekanayo.

Huenda wanaachia hali hii wakiwa na sababu zao, either kutokana na kushabikia chama kile cha kijani! lakini ninyi mnao fanya kazi TCRA hasa walioko kwenye position ya kuweza kudhibiti hali hii lakini kwa makusudi au kwa benefits fulanifulani Mmeamua kuakaa kimya....Jueni consequences zake kama nilivoainisha hapo chini:-

  1. Inaashiria watu wanaokaimu position za juu TCRA ambao mngeweza dhibiti vitu vidogovidogo kama hivi ni watu wenye uwezo mdogo kitaaluma......swali ni Je, inakuwaje watu kama ninyi mpate nyadhifa hizo huku kuna watu ambayo performance yao iko juu na wako mtaani?
  2. Ninyi ni watu mnao onesha dhahiri ya kwamba mnasupport chama fulani huku mkitumia rasilimali za watanzania. Je, Mnastahili kuendelea kushikilia nyadhifa hizo endapo Dr Wilbroad Slaa atachaguliwa kuingia ikulu? mana uchaguzi bado!
  3. Kwanini mliwadanganya watanzania kuhusu registration ya sim cards, huku mkitoa sababu moja wapo ni Kudhibiti matumizi mabaya ya sim cards? Je kwa mwendo huu, kile mlichokitaja kwmba ni KYC - Know Your Customer kina ukweli ndani yake?
  4. Mnafahamu ya kwamba mnaondoa trust ya wananchi kwenye huu mfumo mpya wa " Mobile payments" nasikitika kusema huduma kama vile ZAP, M-PESA, Tigo PESA zinaweza kufacilitate Money Laundering kama mwendo wenyewe ndo huu. Inakuwaje mtu anatumia namba ya hapahapa nchini ila anawafool watanzania kwa kutumia country code ya nchi nyingine afu bosi mzima unakwenda TBC1 kwenye mahojiano ya mwandishi wa habari ...huku hunajibu la uhakika!
Wadau ni hayo kwa leo, lakini nimepoteza imani kabisa na TCRA kabisa!
 
Back
Top Bottom