Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Safari ya kujenga umoja katika vyama vya siasa sasa inaelekea kushika njia kwa kuonyesha ushirikiano katika masuala yenye kuleta manufaa kitaifa na kuweka kando tofauti za kiitikadi.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dr. Slaa kujumuika na WanaCUF ni dalili tosha kuleta mvuto pekee na kuibua minong'ono ya kiu ya wengi kwa siku nyingi kwamba wapinzani waunganishe nguvu pamoja kuitoa CCM madarakani.
Nawapongeza Chadema kwa uamuzi wa busara wa kuonyesha mshikamano na kuwa mfano wa kuigwa na baadhi ya vyama vya upinzani kuwa kitu kimoja katika kujenga demokrasia ya kweli nchini. Licha ya tukio zito la uzinduzi wa kampeni Arumeru Mashariki, lakini wameweza kugawana majukumu na halikuaharika neno, kila kitu kimekwenda kama walivyokusudia.