SLAA na Kauli Tata

Salimia

JF-Expert Member
Feb 14, 2011
665
103
Dr. W.Slaa ana sifa nyingi sana za uongozi,, lakini mojawapo ya sifa za kiongozi ni kutoa kauli zenye uhakika hasa unapokuwa kiongozi mkuu. Slaa anatarajiwa kuwa Rais,, sifa hii ya umakini wa kauli anapungukiwa sana hasa ukizingatia kauli kadha ambazo amewahi kuzitoa katika kipindi kifupi cha nyumba.

Mathalani kuhusu kontena la kura, kifo cha RC shinyanga na nyingine nyingi. Hizi ni kauli nzito ambazo kiongozi makini asingeweza kuzitoa hadharani kabla hajapata uhakika..

Nashauri ikiwa atakuwa Rais basi ajifunze kuwa na subira, ukisikia jambo usifanye pupa na kuropoka hadharani kuuvuruga muamana.

Bado naendelea na uchunguzi kujua kama kweli Mbowe na SLAA ni waadilifu. Isije kuwa ni usanii tu.

Nitarudi

 
duh!!!!!

salimia sasa umeanza kuwachokoza wa chadema shauri yako mi simo maana hawa jamaa wakali sana ili tukuelewe andika mazuri tuu, ukianza hayo utaaribu sasa hivi ngoja tuone majibu yake!

mimi binafsi Slaa alinivutia pale alipolalamika kuwa wabunge wanalipwa pesa nyingi lakini duuh hili halikupata kuungwa mkono na mbunge yeyote yule wa chama chake, upinzani wala sisiemu sijui kwasasa wakati kuna dalili kadhaa kwamba watz tunaweza kumpa ridhaa atuongoze sijui atathubutu kuliendeleza hili?
 
mimi binafsi Slaa alinivutia pale alipolalamika kuwa wabunge wanalipwa pesa nyingi lakini duuh hili halikupata kuungwa mkono na mbunge yeyote yule wa chama chake, upinzani wala sisiemu sijui kwasasa wakati kuna dalili kadhaa kwamba watz tunaweza kumpa ridhaa atuongoze sijui atathubutu kuliendeleza hili?

Usisahau pia yeye analipwa na Chama chake sh. milioni 13 kila mwezi kwa mkataba waliokubaliana kabla ya uchaguzi hivyo angeanza kwanza na kupunguza mshahara wake ndipo ageukie wa Wabunge!!!
 
Dr Slaa alisema kuwa tarifa alizopata ni kwamba mkuu wa mkoa wa Shy amefariki lakini akaongeza kusema kuwa kama hizo taarifa ni za kweli basi alale mahali pema maana jana yake alikuwa amemsema kwenye mkutano wake.. Mbona CCM mnapenda kuzusha upuuzi hoja zilishawaishia mnabakia propaganda,
 
Dr. W.Slaa ana sifa nyingi sana za uongozi,, lakini mojawapo ya sifa za kiongozi ni kutoa kauli zenye uhakika hasa unapokuwa kiongozi mkuu. Slaa anatarajiwa kuwa Rais,, sifa hii ya umakini wa kauli anapungukiwa sana hasa ukizingatia kauli kadha ambazo amewahi kuzitoa katika kipindi kifupi cha nyumba.

Mathalani kuhusu kontena la kura, kifo cha RC shinyanga na nyingine nyingi. Hizi ni kauli nzito ambazo kiongozi makini asingeweza kuzitoa hadharani kabla hajapata uhakika..

Nashauri ikiwa atakuwa Rais basi ajifunze kuwa na subira, ukisikia jambo usifanye pupa na kuropoka hadharani kuuvuruga muamana.

Bado naendelea na uchunguzi kujua kama kweli Mbowe na SLAA ni waadilifu. Isije kuwa ni usanii tu.

Nitarudi
Dirty POLITICS!

Hilo la contena ni la ukweli kwa asilimia 100!

Ulitegemea polisi wamdhalilishe mkwere na ile mbinu yake chafu hadharani, wakati bado wanamtegemea awalipe madeni ya fedha za uhamisho wanazomdai?

Hilo la pili, mimi binafsi nina mashaka sana na jinsi inavyosemekana alitangaza!...Binafsi sikuona, ila kuna aina nyingi za usemaji, na watafsiri wako wa aina nyingi!

Nawasilisha!
 
Kweli Dr. kiboko bado tu na kampeni zenu kumhusu? Watu hawana naji safi, mfumuko wa bei juu, barabara mbovu, shule ni magofu.

Embu badilikeni wakumbukeni wananchi maskini waliowapa kura..wanataabika
 
Huyu jama vipi? Haya tuambie RC wa Shinyanga yuko hospitali gani na nani kiongozi gani alyeenda kumjulia hali? Yule kafa we sema wanamficha. Swali watamficha hadi lini?

Kuhusu kura feki, je wewe ulienda kuhakikisha au kwa vile wamezificha, ukweli ni kwamba anayoyasema slaa ni ya kweli na ndio maana wanaogopa kumpeleka mahakamani.

Tokea Slaa aanze kuongea umeshasikia kuna mtu kamfungulia kesi kwa kusema uwongo? Wote hao wanajulikana na ni ukweli mtupu.

Jipange, kalete hoja mpya tena
 
Mzushi tu hana lolote na hafai kupewa nchi sababu yeye na wasaidizi wake hawako makini katika kupokea na kutoa habari
 
Usisahau pia yeye analipwa na Chama chake sh. milioni 13 kila mwezi kwa mkataba waliokubaliana kabla ya uchaguzi hivyo angeanza kwanza na kupunguza mshahara wake ndipo ageukie wa Wabunge!!!

Una uhakika na unachokisema, CDM, wanaolipwa ni waajiriwa tu, David Kafulila alikuwa analipwa pamoja na waajiriwa wenzake, lakini viongozi wa juu including Zitto Kabwe wanafanya kazi za kujitolea mkuu.

Mishahara hiyo CDM haipo labda Utuambie tambwe Hizza analipwa shillingi ngapi tena ana cheo ambacho hata kwenye katiba ya CCM hakipo.

Aacha KUKURUPUKA tu from no where unasema upupu.
 
Dr Slaa ni member hapa....anachangia sana na anachukua mawazo pia kwa uangalifu mkubwa na anaiamini JF kama credible source yake ya hoja (from credible members of course sio wakina JeyKeywaUkweli,MS,Kishaga etc)....sasa anapotoa hoja hadharani anaumakini wake...mathalan:
  1. Issue ya CONATINER LA KURA TUNDUMA ilianzia hapa...thread yake ipo ni kubwa tu
  2. Suala la RC Shinyanga lilianzia hapa na thread yake ipo
  3. EPA ilianzia hapa na thread ziko kibao
  4. MEREMETA pia imo humu
  5. RICHMOND, DOWANS zote zilianzia hapa
 
Kama julius mtatiro aliomba gari na nyumba tukamkataa akakimbilia mskitini, bado CDM haijawa na hela ya kulipa kila mtu wengine tunatumia pesa zetu mfukoni
 
Mpuuzi kweli wewe,we slaa si alisha kujibu upuuzi wako huo kwenye thread ya liberia?
Bahati yako hamna mods wakatili kama mimi,ungekuwa ukirudia thread moja mara nyingi nakufungia kuanzisha thread
 
Umeomba utukanwe? Jamani.... we haya tu.

Ngoja nimuachie Mkuu hapa chini afanye kazi...... Mie simo, ni mjumbe tu.

 
Last edited by a moderator:
Una uhakika na unachokisema , CDM, wanaolipwa ni waajiriwa tu , david kafulila alikuwa analipwa pamoaja na waajiriwa wenzake, lakini viongozi wa juu including Zitto kabwe wanafanya kazi za kujitolea mkuu,
mishahara hiyo CDM haipo labda Utuambie tambwe Hizza analipwa shillingi ngapi tena ana cheo ambacho hata kwenye katiba ya CCM hakipo
acha KUKURUPUKA tu from no where unasema upupu,
crap
sasa mkuu kama wanaolipwa ni waajiriwa tuu ambao kimsingi ni wachache sana sasa haya mamilioni ya SABODO na mabilioni kutoka nje ya nchi wanayopewa CDM yanatumika kwenye nini? maana ofisi za kuhesabu,tungesema wanalipia pango,umeme maji nk! pesa zinaenda wapi? tunaomba tupewe mchanguo la sivyo kuna ufisadi hapo
 
Usisahau pia yeye analipwa na Chama chake sh. milioni 13 kila mwezi kwa mkataba waliokubaliana kabla ya uchaguzi hivyo angeanza kwanza na kupunguza mshahara wake ndipo ageukie wa Wabunge!!!
Tell me about it!1 Nakwambia hawa wote ni power struggle tu ndiyo inawasumbua. Leo hii na anyoshe mkono mbunge wa CDM au chama kingene chochite aliyekataa Mil 90 za gari? Yu wapi mwenye uchungu wa kweli wa nchi Tanzania? Nani aliyemuunga mkono Slaa juu ya mshahara wa wabunge? Wenzetu wanakula bata sisi huku ndiyo tunatukanana. Ndiyo maana niliacha ushabiki hata wa mpira,, timu ifungwe eti na chakula ususe? Kocha na hata wachezaji hawakujui na wanakula pesa yao kama kawaida!! Acha nikanunulie dagaa wanangu hapa tunadanganyana tu hakuna CHADEMA wala nini,, wote walaji tu.
 
Kweli Dr. kiboko bado tu na kampeni zenu kumhusu.watu hawana naji safi,mfumuko wa bei juu,barabara mbovu,shule ni magofu.Embu badilikeni wakumbukeni wananchi maskini waliowapa kura..wanataabika

Mkuu,
Mtu hujikuna pale panapowasha. Ni lazima wamseme Dr. kwa saaaana kwa sababu huyo ndiye anayewawasha sana mpaka wanakosa usingizi.
 
Dr. W.Slaa ana sifa nyingi sana za uongozi,, lakini mojawapo ya sifa za kiongozi ni kutoa kauli zenye uhakika hasa unapokuwa kiongozi mkuu. Slaa anatarajiwa kuwa Rais,, sifa hii ya umakini wa kauli anapungukiwa sana hasa ukizingatia kauli kadha ambazo amewahi kuzitoa katika kipindi kifupi cha nyumba.
Mathalani kuhusu kontena la kura, kifo cha RC shinyanga na nyingine nyingi. Hizi ni kauli nzito ambazo kiongozi makini asingeweza kuzitoa hadharani kabla hajapata uhakika.
Nashauri ikiwa atakuwa Rais basi ajifunze kuwa na subira,, ukisikia jambo usifanye pupa na kuropoka hadharani kuuvuruga muamana.
Bado naendelea na uchunguzi kujua kama kweli Mbowe na SLAA ni waadilifu. Isije kuwa ni usanii tu. Nakaribisha matusi.
Nitarudi


uko sahihi mkuu,nakumbuka aliropoka kwa kuwataja mafisadi papa pale mwembe yanga,yan list of shame,akiwemo jk,baadae ikathibitika kuwa ni uongo ivo serikali ilimpeleka Dr.slaa mahakamani,nlisikia yuko jela mpaka leo. Pia alisema kuna makampuni ya kitapeli kama Meremeta,iptl na Dowans,kagoda na tangold,kumbe ulikuwa uongo hata kampuni izo hazijawahi kuwepo Tanzania. Cha ajabu akadai kuna ufisadi benki kuu kwenye EPA,serikali ilichunguza ikakuta hamna tatizo na dr.balali hakufichwa mpaka leo anaendelea na kazi wala hakufa wala kuuawa,pia Jk alisema kuwa waliodhaniwa kuiba ela aliwaambia wazirejeshe haraka aliwaomba samahani na kuwaambia wakachukue ela yao kwa sababu alimuelewa vibaya dr.slaa aliyeongopa kuwa kuna ufisadi epa kumbe hakuna. Kweli mleta mada ni mkweli zaidi ya dr.slaa anayedai kuna ufisadi Tanzania wakati Tanzania hamna ufisadi iko shwari wala hamna mtanzania mwenye maisha magumu. Kweli mleta mada we jiniasi kwa kuona uongo wa dr.wa ukweli ukiachana na ukweli wa dr.dr.dr.dr rais ambaye hata izo dr.s ni za kwenye gift pepa.
 
Mpuuzi kweli wewe,we slaa si alisha kujibu upuuzi wako huo kwenye thread ya liberia?
Bahati yako hamna mods wakatili kama mimi,ungekuwa ukirudia thread moja mara nyingi nakufungia kuanzisha thread

Hewala, miye mpuuzi,, lakini hapa chini nanukuu alichonijibu Slaa kwenye thread ya Liberia,, bahati njema ingalipo hai. Soma halafu unijibu swali langu chini yake:
Salimia,

Salamu toka Monrovia. Kama sikosei nilikwisha kufanya posting kwenye Jamvi hili kutoka hapa Monrovia tulipokuwa tu tumewasili hapa tarehe 9 Machi, 2011. Nilieleza kuwa tuko hapa na Mheshimiwa Mwenyekiti wa Taifa kuhudhuria Mkutano wa Mwaka wa Democratic Union of Africa, (DUA) ambayo wengi wenu watakumbuka hadi 2009 Chadema ilikuwa Secretariat, na NPP ya Ghana ilikuwa mwenyekiti.


DUA ni Chapter ya Africa ya vyama vya mrengo wa "Centre Centre Parties" katika mfumo wa vyama vya siasa Duniani na wote tunaunganika katika International Democratic Union kwa Dunia nzuri. Wanachama ni pamoja na vyama tawala katika nchi zao na au vyama vya upinzani ikikumbukwa kuwa kutawala au kutokutawala kwa wanaoelewa demokrasia ni swala la kupokezana vijiti. Hivyo kinachotuunganisha ni "values" au mambo tunayosimamia katika jamii.


Kama nilivyosema huu ni mkutano wa Mwaka yaani Annual General meeting, na wajumbe ni wenyeviti na Makatibu wakuu. Si kosa lako inawezekana umechangia bila kufahamu Katiba ya umoja huo. Mkutano una sehemu kubwa mbili, Deliberative Session, ambayo theme yake ni "Re-bilding the blocks of Democracy in Africa". Mhe. Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinani Bungeni alitoa Mada kuhusu "Consolidating Democracy -Tanzania Election and Aftermath".


Mkutano pia umejadili Trends zinaziojitokeza katika Demokrasia Afrika mifano ya Afrika Kaskazini, Ivory Cost,Kenya na Zimbabwe. Hakuna siri katika Democrasia na kesho Mkutanpo utatoa Tamko rasmi kutokana na mambo yaliyojitokeza katika deliberative Session. Sehemu ya pili na maswala zaidi ya uongozi wa umoja wenyewe Dua. Nadhani ulinganisho na upande mwingine ungelikuwa na maana iwapo "wakubwa" hao wangelikuwa wanahudhuria tu semina ambayo hata mtu mwingine angeliweza kuhudhuria.

Sasa wewe Speaker, nionyeshe ni wapi Slaa ameongelea suala la kontena la kura hapo juu?? Au ni wapi amezungumzia kifo cha RC wa Shinyanga kwenye majibu yake hapo juu?
Hapo sasa wenye hekima watachambua mpuuzi kati yangu na wewe nani?
 
Salimia, hatudanganyiki mtasema tutaendelea kumuamini tu.

Na mtabaki kusalimiana.
 
Mzushi tu hana lolote na hafai kupewa nchi sababu yeye na wasaidizi wake hawako makini katika kupokea na kutoa habari

Hivi hafif, wewe hukwepo kwenye ile opinion polls ya hapa JF na kwingineko? Mbona Dr Slaa alishinda au kwa vile mechakachua?

Na mzimu wa uchakachuaji bado unawasumbua mtakoma, na kama hamkuchakachua kwa nini mnahofia nguvu ya uma? wakati ni juzi tu tulifanya uchaguzi?
 
Back
Top Bottom