BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Slaa, Mbowe wamkaanga JK
Wamshangaa kwenda nje wakati wa matatizo
na Mwandishi wetu
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, wamemrushia kombora Rais Jakaya Kikwete kuwa analea nyufa za udini, ukabila pamoja na kukataa kutoa fedha za kuharibu mabomu yaliyozua balaa kwa wakazi wa Gongo la Mboto.
Viongozi hao walisema Rais Kikwete anashindwa kudhibiti nyufa za udini na ukabila kwa sababu ni mkakati wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuidhoofisha CHADEMA ambayo hivi sasa imejizolea sifa na wanachama wengi, kwa sababu ya uimara wake wa kukiwajibisha chama tawala na serikali yake.
Wakizungumza kwa wakati tofauti katika viwanja wa Shule ya Mkendo mjini Musoma jana, viongozi hao walisema kwa hali ilivyo, Rais Kikwete, amekosa sifa za kuwa kiongozi imara.
Mbowe alisema Rais Kikwete ameshindwa kudhibiti nyufa za udini na ukabila ambao umeonekana dhahiri kuanza kuota mizizi hapa nchini, hivyo zinahitajika juhudi za haraka na makusudi kuuwajibisha utawala wake ili kuinusuru nchi.
Taifa limeingia kwenye udini na ukabila ambao rais wa nchi ameshindwa kuudhibiti...sisi tunafahamu ajenda ya udini na ukabila ni mkakati wa CCM wa kutaka kuimaliza CHADEMA, jambo ambalo kamwe hatulikubali, alisema.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Waziri Mkuu Kivuli, aliwataka Watanzania kuunganisha nguvu zao kwa pamoja katika kulikomboa taifa hasa katika kipindi hiki ambacho umasikini unazidi kushamiri siku hadi siku.
Tukiwaachia hawa CCM waendelee kututawala kama wanavyotaka kamwe umaskini hauwezi kutoweka miongoni mwetu, uwezo wa kubadilisha uongozi na hali zetu za kimaisha tunao, kwanini tunashindwa kuutumia? alihoji.
Kuhusu uundwaji wa Katiba, Mbowe aliionya serikali kuwa ni vema isifanye hila mara baada ya wananchi kutoa maoni yao, kwani mchezo wowote utakaofanywa kwa lengo la kupinga maamuzi ya umma hukumu yake itakuwa kubwa kama ile inayoonekana hivi sasa nchini Libya au ile iliyotokea Misri.
Naye Dk. Slaa, alisema kuwa amesikitishwa na milipuko ya mabomu iliyotokea Gongo la Mboto ambayo kwa kiasi kikubwa imesababishwa na uzembe wa serikali ambayo iligoma kutoa fedha kwa ajili ya kuyaharibu mabomu hayo.
Alibainisha kuwa anazo taarifa kuwa Rais Kikwete alilinyima jeshi hilo fedha za kuharibu mabomu hayo ambayo yalionekana kwisha muda wake miaka miwili iyopita.
Ninayo taarifa kwamba serikali ya Rais Kikwete iliombwa fedha mara mbili za kuharibu mabomu lakini ilishindwa kufanya hivyo...hali hiyo ndiyo iliyosababisha vifo vya Watanzania Mbagala na sasa Gongo la Mboto, alisema Dk. Slaa.
Aliongeza kuwa, kutokana na uzembe huo, anamtaka Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, pamoja na Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Davis Mwamnyange, kujiuzulu mara moja nyadhifa zao na iwapo watashindwa, basi Rais Kikwete awafukuze.
Alisema Watanzania hawawezi kuendelea kuvumilia viongozi kama hao wazembe wa kazi na kwamba ni vema Waziri Mwinyi akaiga mfano wa baba yake, Ali Hassan Mwinyi, aliyeachia ngazi kutokana na mauaji yaliyotokea wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani.
Tunamtaka Waziri Mwinyi ajiuzulu, na akishindwa basi Rais Kikwete amfukuze kazi huyu mtu pamoja na Mkuu wa Majeshi...wananchi wameshachoka kuona usanii wa uongozi, alisema.
Mbowe na Slaa waliongeza kuwa wamemshangaa Rais Jakaya Kikwete kwa kuacha msiba wa Watanzania waliokufa kwa mabomu ya Gongo la Mboto, kisha kwenda nchini Mauritania kusuluhisha mgogoro wa kisiasa wa Ivory Coast.
Walisema ni aibu kwa kiongozi wa wananchi kuacha msiba mkubwa nchini kwake na kukimbilia nje ya nchi kwenda kusuluhisha mambo ya nchi nyingine.
Kwenda Mauritania kwa Rais kikwete ni kuwadhalilisha Watanzania ...ni sawasawa na baba mwenye familia kuacha watoto wake wanakufa njaa, yeye anakwenda kutoa chakula nyumba ya jirani, alisema Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.
Katika hotuba yake, Dk. Slaa alisema kamwe Watanzania hawawezi kuvumilia kuona usaliti wa namna hiyo unafanywa na mtu mkubwa kama Rais Kikwete, ambaye ndiye Amiri Jeshi Muu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Katika hatua nyingine, alimtaka Rais Kikwete na serikali yake kuitaifisha mitambo ya Dowans, kwani mitambo hiyo imeingizwa nchini kwa njia za kitapeli na ujanja ujanja, kinyume cha sheria za nchi.
Wamshangaa kwenda nje wakati wa matatizo
na Mwandishi wetu
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, wamemrushia kombora Rais Jakaya Kikwete kuwa analea nyufa za udini, ukabila pamoja na kukataa kutoa fedha za kuharibu mabomu yaliyozua balaa kwa wakazi wa Gongo la Mboto.
Viongozi hao walisema Rais Kikwete anashindwa kudhibiti nyufa za udini na ukabila kwa sababu ni mkakati wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuidhoofisha CHADEMA ambayo hivi sasa imejizolea sifa na wanachama wengi, kwa sababu ya uimara wake wa kukiwajibisha chama tawala na serikali yake.
Wakizungumza kwa wakati tofauti katika viwanja wa Shule ya Mkendo mjini Musoma jana, viongozi hao walisema kwa hali ilivyo, Rais Kikwete, amekosa sifa za kuwa kiongozi imara.
Mbowe alisema Rais Kikwete ameshindwa kudhibiti nyufa za udini na ukabila ambao umeonekana dhahiri kuanza kuota mizizi hapa nchini, hivyo zinahitajika juhudi za haraka na makusudi kuuwajibisha utawala wake ili kuinusuru nchi.
Taifa limeingia kwenye udini na ukabila ambao rais wa nchi ameshindwa kuudhibiti...sisi tunafahamu ajenda ya udini na ukabila ni mkakati wa CCM wa kutaka kuimaliza CHADEMA, jambo ambalo kamwe hatulikubali, alisema.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Waziri Mkuu Kivuli, aliwataka Watanzania kuunganisha nguvu zao kwa pamoja katika kulikomboa taifa hasa katika kipindi hiki ambacho umasikini unazidi kushamiri siku hadi siku.
Tukiwaachia hawa CCM waendelee kututawala kama wanavyotaka kamwe umaskini hauwezi kutoweka miongoni mwetu, uwezo wa kubadilisha uongozi na hali zetu za kimaisha tunao, kwanini tunashindwa kuutumia? alihoji.
Kuhusu uundwaji wa Katiba, Mbowe aliionya serikali kuwa ni vema isifanye hila mara baada ya wananchi kutoa maoni yao, kwani mchezo wowote utakaofanywa kwa lengo la kupinga maamuzi ya umma hukumu yake itakuwa kubwa kama ile inayoonekana hivi sasa nchini Libya au ile iliyotokea Misri.
Naye Dk. Slaa, alisema kuwa amesikitishwa na milipuko ya mabomu iliyotokea Gongo la Mboto ambayo kwa kiasi kikubwa imesababishwa na uzembe wa serikali ambayo iligoma kutoa fedha kwa ajili ya kuyaharibu mabomu hayo.
Alibainisha kuwa anazo taarifa kuwa Rais Kikwete alilinyima jeshi hilo fedha za kuharibu mabomu hayo ambayo yalionekana kwisha muda wake miaka miwili iyopita.
Ninayo taarifa kwamba serikali ya Rais Kikwete iliombwa fedha mara mbili za kuharibu mabomu lakini ilishindwa kufanya hivyo...hali hiyo ndiyo iliyosababisha vifo vya Watanzania Mbagala na sasa Gongo la Mboto, alisema Dk. Slaa.
Aliongeza kuwa, kutokana na uzembe huo, anamtaka Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, pamoja na Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Davis Mwamnyange, kujiuzulu mara moja nyadhifa zao na iwapo watashindwa, basi Rais Kikwete awafukuze.
Alisema Watanzania hawawezi kuendelea kuvumilia viongozi kama hao wazembe wa kazi na kwamba ni vema Waziri Mwinyi akaiga mfano wa baba yake, Ali Hassan Mwinyi, aliyeachia ngazi kutokana na mauaji yaliyotokea wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani.
Tunamtaka Waziri Mwinyi ajiuzulu, na akishindwa basi Rais Kikwete amfukuze kazi huyu mtu pamoja na Mkuu wa Majeshi...wananchi wameshachoka kuona usanii wa uongozi, alisema.
Mbowe na Slaa waliongeza kuwa wamemshangaa Rais Jakaya Kikwete kwa kuacha msiba wa Watanzania waliokufa kwa mabomu ya Gongo la Mboto, kisha kwenda nchini Mauritania kusuluhisha mgogoro wa kisiasa wa Ivory Coast.
Walisema ni aibu kwa kiongozi wa wananchi kuacha msiba mkubwa nchini kwake na kukimbilia nje ya nchi kwenda kusuluhisha mambo ya nchi nyingine.
Kwenda Mauritania kwa Rais kikwete ni kuwadhalilisha Watanzania ...ni sawasawa na baba mwenye familia kuacha watoto wake wanakufa njaa, yeye anakwenda kutoa chakula nyumba ya jirani, alisema Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.
Katika hotuba yake, Dk. Slaa alisema kamwe Watanzania hawawezi kuvumilia kuona usaliti wa namna hiyo unafanywa na mtu mkubwa kama Rais Kikwete, ambaye ndiye Amiri Jeshi Muu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Katika hatua nyingine, alimtaka Rais Kikwete na serikali yake kuitaifisha mitambo ya Dowans, kwani mitambo hiyo imeingizwa nchini kwa njia za kitapeli na ujanja ujanja, kinyume cha sheria za nchi.