Slaa, Lissu na wafuasi wao wafikishwa mahakamani Arusha

BigMan

JF-Expert Member
Feb 19, 2007
1,096
135


Katibu mkuu wa CHADEMA, Wilbrod Slaa na mkurugenzi wa sheria wa chama hicho Tundu Lissu na wafuasi wengine kumi wa chama hicho wanafikishwa mahakamani muda mfupi ujao jijini Arusha.

Kuna hatari ya kunyimwa dhamana kutokana na vurugu ambazo zinaendelea kwani vijana wa chama hicho wanavunja vioo vya magari na muda mfupi uliopita wamefanya hivyo katika mitaa ya Sabena iliyoko karibu na stand kuu ya Arusha
Katika mahakama ya hakimu mkazi ya mkoa wa Arusha leo mpaka muda huu ambao ni majira ya saa 10:29 (kumi na dk 29 jioni) Dr.Slaa na Lissu na wananchi wengine 27 wamesomewa mashtaka na yako kama ifuatavyo;

1. Kukusanyika kinyume cha sheria .
2. Kukataa kutii amri halali ya polisi

Ila Slaa kasomewa shitaka la tatu peke yake nalo ni la uchochezi, ila maneno yaliyosemwa na polisi kjuwa yalitamkwa sijui yatakuwa yalitamkwa wapi ila sio kwenye mkutano wa hadhara wa jana kama ambavyo mwendesha mashitaka anataka kuiaminisha mahakama .

Taratibu za dhamana zinaendelea kwenye mahakama hiyo , ila ntawajulisha nini kiuitatokea kwani taarifa ni kuwa Lissu na Dr.Slaa wao wataenda Kisongo kuonana na LEMA na kupafanya kuwa ni makazi ya kudumu kama ambavyo polisi na serikali wanataka .
 
Last edited by a moderator:
Alfajiri ya mapambazuko naiona kwa mbaaali..kitaeleweka tu, hata wakitujaza sote selo zao, tutaimba piipoooz pawaaaa kama paulo na sila gerezani, ukandamizaji una mwisho
 
Kuwasweka viongozi wa wananchi ndani kwa sababu eti wameamua kulala pale NMC bila kumfanyia mtu yeyote vurugu ni uvunjifu wa Amani. Hivi mbona wale watoto wa mitaani huwa wanalala mabarazani na hawakamatwi iweje polisi watumike kama majembe
 
Kosa kubwa sana hilo.. Wakikosea akanyimwa dhamana basi hali haitakuwa tete tena bali itakuwa ni mbovu kabisa.
 
Hayo magari waliovunja vioo ni magari ya polisi au ya raia?
 
Jamani we mbundi wa balaa kwanini hautui mikoa yote uonyeshe kila kilichokuwa kinatafutwa na CCM muda mrefu?itakuwa ni vema na haki likinuka nchi nzima maana hapa ni ubabe unatumika sasa kama kweli serikali hii inawekwa na watu na watu wenyewe ni pamoja walioko Arusha basi kuna haja ya kukataa uonevu.

Tupeni habari kama wameshampeleka gerezani hao viongozi na wanachadema wengine.

Ila kama hawatatumia akili na busara wajiulize ni kwa nini mshabiki wa mpira alijinyonga Kenya baada ya Arsenal kufungwa?ni kwa nini kuna watu wanajilipua,ni kwa nini Libya na kwingineko?ni kwanini mkaburu kule Afrika kusini aling'olewa?

Haya bwana dola mnayo ninyi lakini panueni Magereza,hayatoshi kabisa.
 
Back
Top Bottom