Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Frederick Katulanda na Israel Mgussi, Dodoma
BUNGE limepitisha Muswada wa Sheria ya watu wenye ulemavu wa 2010, huku Mbunge wa Karatu Dk Willibrod Slaa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Frederick Werema wakivutana kuhusu masuala ya wenye ulemavu kushughulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mvutano huo ulizuka jana wakati bunge likiwa limekaa kama kamati kwa ajili ya kuupitisha muswada huo.
Dk Slaa alitaka muswada huo ubainishe katika kifungu cha 16 kuwa masuala ya watu wenye ulemavu yatakuwa chini ya ofisi ya waziri mkuu badala ya sasa ambapo inaelekezwa kuwa yatakuwa chini ya wizara katika idara ya maendeleo ya jamii.
Kutokana na hoja hiyo ya Dk Slaa, Werema alisimama na kulieleza bunge kuwa kifungu hicho hakina shaka kwa vile kinaposema itakuwa chini ya waziri anayehusika na masuala ya maendeleo ya jamii, kinamaanisha pia kuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Majibu hayo hayakumridhisha Dk Slaa ambaye alisimama tena na kusisitiza kuwa muswada huo unapaswa kutamka wazi kwa vile dhana ya maendeleo ya jamii ni pana hivyo kutokana na umuhimu wa masuala hayo, jambo hilo liwekwe wazi na siyo kwa kificho.
"Katika nchi nyingine walemavu wanawekwa katika ofisi ya Rais ama ofisi ya waziri mkuu, sasa tungependa waziri mkuu atoe tamko lake hapa ama itamke wazi kwa vile ikiachiwa hivyo inaonyesha kuwa inaweza kuwa na tatizo katika utekelezaji," alizidi kufafanua Dk Slaa.
Baada ya mvutano wa muda mrefu, Werema alikubaliana naye hivyo kuuhitimisha mjadala huo na kifungu hicho kubadilishwa.
Wakati wa upitishaji muswada huo kwa kutamka ndiyo ama siyo wakiwa katika ibara ya 37, wabunge walikaa kimya kwa muda hatua ambayo Spika Sitta aliamua kuwaeleza wabunge kuwa wanapaswa kuchangia licha ya kuwa mawazo yao kuwa majimboni kwa sasa.
"Waheshimiwa wabunge, muswada upo mbele yetu, naelewa kuwa kwa sasa mawazo yetu yapo majimboni, lakini tunapaswa kuwa makini katika kuupitisha muswada huu," alieleza Spika.
Akihitimisha katika muswada huo Spika Samwel Sitta naye alirejea kuiomba serikali kuhakikisha kanuni zinapitishwa mapema ili muswada huo uanze kutumika.
Aliasa serikali kuhakikisha inashughulikia mabadiliko ambayo yametolea na mbunge wa Karatu ili kuboresha muswada huo na hasa kwa kuzingatia katika kumbukumbu za bunge, badiliko hilo limezingatiwa.
Awali wakati wabunge wakijadili muswada huo, waliomba baada ya muswada huo kupitishwa usainiwe mapema na kanuni zake ziandaliwe kama ilivyokuwa kwa muswada wa sheria wa fedha za uchaguzi ambao baada ya kupitishwa na bunge ulisainiwa haraka kwa mbwembwe na Rais Jakaya Kikwete na kanuni zake kuandaliwa haraka.
Baadhi ya wabunge waliiomba serikali kuhakikisha kanuni za muswada huo zinaandaliwa haraka ili baada ya kusainiwa na rais iweze kutumika na kuwasaidia watu wenye ulemavu.
Aliyeanza kuomba kanuni za muswada huo kuandalia mapema alikuwa ni mbunge wa viti maalum Magreth Mkanga ambaye alisema haoni tatizo katika muswada huo.
âMie sioni shaka ya Muswada huu kupitishwa lakini shaka yangu ipo katika uandaaji wa kanuni zake. Naomba ukishaandaliwa mapema na kanuni zake pia ziandaliwe mapema ili uanze kutumika mara moja,"alisisitiza.
Hoja hiyo ya Mkanga iliungwa na Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi ambaye aliieleza serikali kuwa kutoandaliwa kwa kanuni za sheria mapema mara baada ya kupitishwa ni ukosefu wa utawala bora.
Hii ni mara ya pili kwa Dk Slaa kuvutana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu vifungu vya sheria. Hivi karibuni walikuwa wamevutana kuhusu kifungu namba 7(3) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi baada ya Dk Slaa kusema kifungu hicho kiliingizwa kinyemela.
Source: Mwananchi
BUNGE limepitisha Muswada wa Sheria ya watu wenye ulemavu wa 2010, huku Mbunge wa Karatu Dk Willibrod Slaa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Frederick Werema wakivutana kuhusu masuala ya wenye ulemavu kushughulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mvutano huo ulizuka jana wakati bunge likiwa limekaa kama kamati kwa ajili ya kuupitisha muswada huo.
Dk Slaa alitaka muswada huo ubainishe katika kifungu cha 16 kuwa masuala ya watu wenye ulemavu yatakuwa chini ya ofisi ya waziri mkuu badala ya sasa ambapo inaelekezwa kuwa yatakuwa chini ya wizara katika idara ya maendeleo ya jamii.
Kutokana na hoja hiyo ya Dk Slaa, Werema alisimama na kulieleza bunge kuwa kifungu hicho hakina shaka kwa vile kinaposema itakuwa chini ya waziri anayehusika na masuala ya maendeleo ya jamii, kinamaanisha pia kuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Majibu hayo hayakumridhisha Dk Slaa ambaye alisimama tena na kusisitiza kuwa muswada huo unapaswa kutamka wazi kwa vile dhana ya maendeleo ya jamii ni pana hivyo kutokana na umuhimu wa masuala hayo, jambo hilo liwekwe wazi na siyo kwa kificho.
"Katika nchi nyingine walemavu wanawekwa katika ofisi ya Rais ama ofisi ya waziri mkuu, sasa tungependa waziri mkuu atoe tamko lake hapa ama itamke wazi kwa vile ikiachiwa hivyo inaonyesha kuwa inaweza kuwa na tatizo katika utekelezaji," alizidi kufafanua Dk Slaa.
Baada ya mvutano wa muda mrefu, Werema alikubaliana naye hivyo kuuhitimisha mjadala huo na kifungu hicho kubadilishwa.
Wakati wa upitishaji muswada huo kwa kutamka ndiyo ama siyo wakiwa katika ibara ya 37, wabunge walikaa kimya kwa muda hatua ambayo Spika Sitta aliamua kuwaeleza wabunge kuwa wanapaswa kuchangia licha ya kuwa mawazo yao kuwa majimboni kwa sasa.
"Waheshimiwa wabunge, muswada upo mbele yetu, naelewa kuwa kwa sasa mawazo yetu yapo majimboni, lakini tunapaswa kuwa makini katika kuupitisha muswada huu," alieleza Spika.
Akihitimisha katika muswada huo Spika Samwel Sitta naye alirejea kuiomba serikali kuhakikisha kanuni zinapitishwa mapema ili muswada huo uanze kutumika.
Aliasa serikali kuhakikisha inashughulikia mabadiliko ambayo yametolea na mbunge wa Karatu ili kuboresha muswada huo na hasa kwa kuzingatia katika kumbukumbu za bunge, badiliko hilo limezingatiwa.
Awali wakati wabunge wakijadili muswada huo, waliomba baada ya muswada huo kupitishwa usainiwe mapema na kanuni zake ziandaliwe kama ilivyokuwa kwa muswada wa sheria wa fedha za uchaguzi ambao baada ya kupitishwa na bunge ulisainiwa haraka kwa mbwembwe na Rais Jakaya Kikwete na kanuni zake kuandaliwa haraka.
Baadhi ya wabunge waliiomba serikali kuhakikisha kanuni za muswada huo zinaandaliwa haraka ili baada ya kusainiwa na rais iweze kutumika na kuwasaidia watu wenye ulemavu.
Aliyeanza kuomba kanuni za muswada huo kuandalia mapema alikuwa ni mbunge wa viti maalum Magreth Mkanga ambaye alisema haoni tatizo katika muswada huo.
âMie sioni shaka ya Muswada huu kupitishwa lakini shaka yangu ipo katika uandaaji wa kanuni zake. Naomba ukishaandaliwa mapema na kanuni zake pia ziandaliwe mapema ili uanze kutumika mara moja,"alisisitiza.
Hoja hiyo ya Mkanga iliungwa na Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi ambaye aliieleza serikali kuwa kutoandaliwa kwa kanuni za sheria mapema mara baada ya kupitishwa ni ukosefu wa utawala bora.
Hii ni mara ya pili kwa Dk Slaa kuvutana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu vifungu vya sheria. Hivi karibuni walikuwa wamevutana kuhusu kifungu namba 7(3) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi baada ya Dk Slaa kusema kifungu hicho kiliingizwa kinyemela.
Source: Mwananchi