GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Nilikuwa nasikiliza juzi mjadala wa uchumi kwenye Radio Free Africa kuhusiana na sababu za mfumuko wa bei. Wakasema , mojawapo ya sababu za mfumuko wa bei ni kupanda kwa ajira ambapo kunasababisha mzunguko wa pesa kuwa mkubwa (kwani kila mtu anakuwa na pesa) hivyo basi kusababisha mfumuko wa bei kwani kila mtu anakuwa anahitaji kutumia. Mie nikajiuliza kama ni hivyo, mbona sababu hii mtu kama Dr. Slaa haisemi ? au ndio maimuna wa mambo ya uchumi?.