Slaa ang’ang’ania nyaraka za siri

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Slaa ang'ang'ania nyaraka za siri
Basil Msongo
Daily News; Sunday,June 29, 2008 @00:01

Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa (Chadema) yupo tayari kufungwa miaka 20 jela na anaamini kuwa serikali ikificha nyaraka kwa lengo la kuficha maovu ni dhambi kwa Mungu na si haki kwa Watanzania. Ijumaa jioni Dk Slaa alitangaza bungeni kuwa ana nyaraka za serikali na yupo tayari kukamatwa.

Mbunge huyo aliwaonyesha wabunge nyaraka alizonazo na akasema Sheria inayozuia watu kutokuwa na nyaraka hizo haihalalishi wizi, ubadhirifu wa mali ya umma, mikataba mibovu, na maovu mengine yanayodaiwa kuwapo serikalini. Dk alilieleza Bunge kuwa anaifahamu sheria hiyo lakini anazitafuta nyaraka hizo ili kutetea maslahi ya Watanzania.

Aliyasema hayo wakati Bunge lilipokaa kama kamati ya matumizi kupitia vifungu kwa vifungu bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na taasisi zilizo chini ya Mamlaka hizo kwa mwaka wa fedha 2008/2009. Dk Slaa alilieleza Bunge kuwa anazipata nyaraka hizo kwa Watanzania wenye dhamira safi kwa nchi yao na kwamba usiri wa serikali unaliumiza taifa hivyo hatakaa kimya.

Alieleza Bunge kuwa anazo nyaraka hizo na atakapotakiwa kuzitoa atazitoa kwa viongozi wa Serikali akiwamo Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Dk Slaa alisema kitendo cha yeye kuweza kuzipata nyaraka hizo zikiwamo kutoka Benki Kuu Tanzania (BOT) ni uthibitisho wa kuanguka kwa mfumo wa Serikali na akaiuliza Serikali, ni nyaraka zipi anazoweza kuzisoma bungeni na zipi zisizoruhusiwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge, Sera na Uratibu, Philip Marmo, alimjibu kwa kusema kuwa, hakuna kanuni ya Bunge inayoweka mipaka ya nyaraka hizo hivyo inahitajika busara ya Spika wa Bunge kuhusu suala hilo kwa kuzingatia mila na desturi ya mabunge mbalimbali duniani.

Kwa mujibu wa Marmo kanuni haziko wazi lakini Dk Slaa anafahamu kuwa anavunja sheria kwa kuwa anaifahamu sheria inayomzuia kuwa na nyaraka za serikali. Waziri Marmo alitoa mfano kuwa, Dk Slaa ana nyaraka za kikao cha bodi ya wakurugenzi wa BOT cha Juni 6 mwaka huu na sehemu ya muhuri imekatwa ili kuficha ushahidi.

Alisema nyaraka hiyo ya BOT imeandikwa ' Mp tafadhali nimeondoa muhuri kwa usalama wa maofisa wetu." "Kwa hiyo mheshimiwa Spika Mheshimiwa Slaa hahitaji kufundishwa maana ya siri…….mheshimiwa Slaa hahitaji kufundishwa nini nyaraka za Serikali au la" alisema Marmo na kusema kuwa kuwa nyaraka kama hiyo ni kosa la jinai.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Matumizi ya Bunge iliyopitia vifungu vya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Anne Makinda, alisema nyaraka za Serikali zinaaweza kupatikana kwa utaratibu halali na kwamba, hali ya sasa ya nyaraka hizo kupatika ovyo ni uthibitisho kuwa ndani ya Serikali kuna tatizo. "Nchi yoyote heshima yake ni siri zake zinazotolewa ndani ya utaratibu husika" alisema Makinda.

Alhamisi wiki hii Bunge lilitangaza kuwa wabunge wakikamatwa mitaani kwa kuwa na nyaraka za Serikali watashitakiwa kama wananchi wengine kwa kuwa ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuwa na nyaraka hizo. Naibu Spika wa Bunge Anna Makinda alitoa msimamo huo baada ya Waziri Marmo kuomba muongozo wa Spika baada ya wabunge kusema wana nyaraka za Serikali.

"Ukikutwa na kitu cha namna hiyo mitaani ni shauri yako wewe" alisema Naibu Spika bungeni wakati wabunge wakichangia hoja ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2008/2009. Marmo alisema kuwa na nyaraka za Serikali ni kosa la jinai, na kwamba anayepatikana na hatia hiyo anaweza kufungwa miaka 20 jela.

"Na duniani kote nyaraka hizi hazijadiliwi bungeni katika mijadala ya wazi"alisema Marmo na kuhoji itakuwaje kama wabunge hao wakikutwa nazo mitaani. Marmo aliuliza kama wabunge wanazipata nyaraka hizo bungeni au zinawafikia kimiujiza na akataka Spika aeleze itakuwaje kama vyombo vya dola vikiwachukulia sheria.

Waziri huyo aliuliza hivyo baada ya Mbunge wa Viti Maalum (CUF) Mkiwa Kimwanga kutangaza bungeni kuwa ana nyaraka aliyoiandika Katibu Mkuu Ofisi ya Rais kwenda kwa mwekezaji akimuagiza jambo linaliowahusu wafanyakazi wa kiwanda.
Marmo alisema kitendo cha wabunge kutangaza kuwa wana nyaraka za serikali ni makosa ya wazi ya jinai na wakikutwa nazo mitaani pia ni kosa na wanaweza kufungwa jela.

Makinda alisema kwa kuwa wabunge hao hawakuziweka mezani, na walizisoma bila ruhusa ya Spika, Bunge halizitambui kwa kuwa hazikuwa rasmi na kwamba, hata wabunge wanapotaka kusoma hotuba za mawaziri inabidi waweke mezani na wapate ruhusa ya Spika wa Bunge. Naibu Spika wa Bunge, alisema, endapo Mbunge anataka kusoma kitu chochote wakati akizungumza bungeni anapaswa kuweka maandishi hayo mezani na aombe ruhusa ya Spika ndipo asome.
 
Tofauti kati ya ZANU PF na serikali ya Mugabe ukilinganisha na CCM na serikali ya Kikwete inazidi kuwa finyu kila kukicha.
 
...atakapotakiwa kuzitoa atazitoa kwa viongozi wa Serikali akiwamo Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Dk Slaa alisema kitendo cha yeye kuweza kuzipata nyaraka hizo zikiwamo kutoka Benki Kuu Tanzania (BOT) ni uthibitisho wa kuanguka kwa mfumo wa Serikali na akaiuliza Serikali, ni nyaraka zipi anazoweza kuzisoma bungeni na zipi zisizoruhusiwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge, Sera na Uratibu, Philip Marmo, alimjibu kwa kusema kuwa, hakuna kanuni ya Bunge inayoweka mipaka ya nyaraka hizo hivyo inahitajika busara ya Spika wa Bunge kuhusu suala hilo kwa kuzingatia mila na desturi ya mabunge mbalimbali duniani.

Kwa mujibu wa Marmo kanuni haziko wazi lakini Dk Slaa anafahamu kuwa anavunja sheria kwa kuwa anaifahamu sheria inayomzuia kuwa na nyaraka za serikali. Waziri Marmo alitoa mfano kuwa, Dk Slaa ana nyaraka za kikao cha bodi ya wakurugenzi wa BOT cha Juni 6 mwaka huu na sehemu ya muhuri imekatwa ili kuficha ushahidi.
Bubu thank you for the info.
Hawa jamaa lazima wawe smart; hakuna haja ya kumfatilia Dr. kwa sababu kama hizo docs zingekuwa safi hayo mabomu yangekuwa yanamlipukia Slaa mwenyewe.
 
Dr Slaa ni msafi na Marmo ni mchafu. Sasa hata wakizikataa hizo nyaraka Bungeni na sisi huku tukazikubali si wamecheza faulo?
Wasubiri kama hawakukuta zimetundikwa baa, na kwenye vyoo vya vijiji vya jumuiya ambako kila mtu anaweza kusoma bila kuwa nayo. Hapo watajua.
Si tunazo hapa jf? kwani hawajui?
 
Hizo ziondolewe katika kundi la Nyaraka za siri ,maana sio siri tena ,ziachwe zisomwe ,ila nafikiri katika kipindi hiki cha kukulu kakara zipo Nyaraka mpya za siri hizo walizo nazo akina Slaa zimeshaexpire zinafaa kuandikwa hata kama kwenye magazeti ili wananchi wazipime kama zi za siri na zilikuwa zikifichwa kwa sababu zina siri..
 
Mkuu Bubu,

Ahsante sana kwa tarifa hii makini ambayo imenifungua macho husiana na hizi ziitwazo nyaraka za siri za Serikali.

Kweli na Hakika kwamba safari hii Serikali ya CCM imedhamiria kufukia maovu na mabaya yao...kwa gharama na njia yoyote.
Kama Dr. Slaa alivyoongea ya kwamba anapata nyaraka hizo za siri za serikali kutoka kwa Wazalendo, wenye Uchungu na Tz...

Hizo nyaraka za siri huw
zinakuwa zinamlenga nani, zinamuhusu nani na ni kwa manufaa ya nani? Je serikali ipo kwa ajili wa umma wa Watanzania ama?

kuna nyaraka za siri ambazo serikali inatakiwz kuzilinda kwa maslahi ya umma lakIni unapofikia kuziita nyaraka ambazo zinafichua uozo wa viongozi waliopewa dhamana na wananchi kuwaongoza badala yake wanajinufaisha wao za siri na Bunge linatetea kwanGu sintokubaliana nalo.

Ningeshangilia sana kama kauli toka bungeni ingesema kwamba Watuhumiwa wa Ufisadi watachukuliwa hatua kali ambazo zinalengwa kuwachukulia wanaowafichua mafisadi...

Godspeed Slaa et al...
 
Hizi kauli za viongozi wetu ni bonge la promotion kwenye vitendo vya uvujaji wa hizo wanazoziita 'siri', yaani ni kama wanamwagia petroli kwenye moto kwa kuwa naamini sasa hata wale wafanyakazi wenye access na hizo 'siri' na walikuwa hawako aware kwamba ni big deal kiasi hiki wataanza kuzivujisha either kwa pesa au kwa uchungu tu walikuwa nao kwa nchi yao. Expect more embarassments!
 
Serikali inabidi iweke bayana kuwa siri zake ni siri kwa nani na ni kwa nini ni siri. Sioni mantiki ya serikali kuwaficha wabunge habari za mikataba ya kibishara eti ni siri. Siri pekee nionazo ambazo zinahitaji kufichwa ni zile za usalama wa taifa ambazo hata hivyo haziwezi kuwa siri kwa wabunge wote: Spika, Katibu wa Bunge, Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama pamoja na makamu wake wana haki ya kuzipata siri hizo.
 
Hawa viongozi wa Tanzania naona wanamwelekeo ambao hautaleta mambo mazuri kwa Taifa letu. Iweje nyaraka zenye mwelekeo wa kuangamiza Taifa letu, kuwalinda mafisadi na kutoa baraka na kinga kwa wakwapuaji wa uchumi wetu zionekane siri kwa wazalendo wa nchi yetu?. Mbona ripoti nyeti ambazo zimebeba maelezo na ushauri nyeti kwa Serikali zinatolewa na viongozi wa juu kwa wageni kama Sinclair, ambao hawana uchungu wala mchango wowote kwa Taifa letu bali kutuibia tu. Nyaraka akiwa nayo raia kama Dr. Slaa inaoneka ni kosa kisheria lakini wageni pamoja na mafisadi kuwa nazo sio kosa, hii sio sawa naona kunahitajika nguvu mbadala kupambana na mafisadi kwani hata PM ameshalegea kabla ya kuanza shughuli anayotakiwa kuwafanyia wananchi.
 
Guys lets agree in this, kwamba katika kila sirikali duniani kuna siri za sirikali husika (tusibishe hili). Tatizo lipo kwenye siri za sirikali yetu. Mataifa mengine yana siri za kulinda taifa, technolojia mpya, ugunduzi wa natural resources mahali fulani (espc out of their country) Siri za sirikali yetu ni vijisenti vya chenge, Richmonduli EPA ... Nimechoka kutype. Kazi kweli kweli. We need to re-difine the term SIRI
 
nyaraka za siri ?hizo hatuzitaki, nyaraka za siri kuhusu wizi na ufisadi wa rasilimali za watanzania ? HIZO NI HALAI YETU! BRAVO SLAA!
 
Serikali inabidi iweke bayana kuwa siri zake ni siri kwa nani na ni kwa nini ni siri. Sioni mantiki ya serikali kuwaficha wabunge habari za mikataba ya kibishara eti ni siri. Siri pekee nionazo ambazo zinahitaji kufichwa ni zile za usalama wa taifa ambazo hata hivyo haziwezi kuwa siri kwa wabunge wote: Spika, Katibu wa Bunge, Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama pamoja na makamu wake wana haki ya kuzipata siri hizo.

Ukweli ni kwamba, hakuna siri duniani kwani hata siri inayohusu usalaama wa taifa lolote huwa inabadilika kuwa siyo siri baada ya muda na katika mazingira fulani. Kila siri ina mwisho wake isipokuwa siri ya Mungu inayohusu kifo.

Na siri ikijulikana kwa waliofichwa, inakuwa siyo siri tena. Kama kuna sheria inayohusu siri za nyaraka za serikali naomba ifutwe kwani hizo siri zote za serikali ya ccm ni uovu mtupu na hazina maslahi kwa taifa letu.
 
Guys lets agree in this, kwamba katika kila sirikali duniani kuna siri za sirikali husika (tusibishe hili). Tatizo lipo kwenye siri za sirikali yetu. Mataifa mengine yana siri za kulinda taifa, technolojia mpya, ugunduzi wa natural resources mahali fulani (espc out of their country) Siri za sirikali yetu ni vijisenti vya chenge, Richmonduli EPA ... Nimechoka kutype. Kazi kweli kweli. We need to re-difine the term SIRI

Hakuna anayekataa, lakini ni siri ya aina gani nakwa nani.Kila kitu kinakuwa halali kutokana na uhalali wake. Kama wizi ni halali then nitakubaliana nawe( ambapo wizi sio kitu halali) upande mmoja. Sasa je kama wizi ni halali na then ni siri, basi haiwezi kuwa siri kwa chombo kinachokusimamia, Bunge.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom